EPS 15
Baada ya kumalzia baadhi ya Visa kama nilivyowaambia kwenye Epsd za huko juu nilipewa Kesi ya kutishia Kuua kwa sababu ya Kuwa karibu sana na miongoni mwa wateja wangu wa mwanzo kabisa kwenye Udalali,Jeni.
Kesi nilikuwa naenda lakini wakanishauri nimalizane na mchepuko wa Jeni, ili mambo yasiwe mengi. Nilimtafuta Mchepuko wa Jeni nikaongea nae akakubali ila akaniambia nitafute hela nikafute hiyo kesi polisi. Nilimkubalia lakini sikufanya hivyo ahdi leo.
Jeni baada ya kuona mchepuo anamnganagania sana na anatamani ndoa, walienda kushirikisha marafiki zake wakaongea nae Mwamba ikabidi wakubaliane yaishe ili amruhusu mwenzie aolewe maana yeye hana namna anayoweza kufanya.
Jeni alikuja akapata mimba na alifurahi sana maana kwenye maisha yake hakutegemea kama ingewezekana tena maana kwa maelezo yake alikuwa amehangaika sana bila mafaniko, alinishukuru sana kwa maombi namna ambavyo tulishirikana aliahidi zawadi kubwa sana na kwa wakati huo kuna zawadi alinipa hii haina haja ya kuiandika.
Mwaka alikuja kuolewa akamfuata jamaa yake Huko kilndi Tanga wakaendelea na maisha yao na sasa ana watoto wawili.
Mwaka 2019 mwishoni Nilikuja Kupata pia mtoto nilizaa na Judy lakini hatukuoana, hivyo ilibidi wakati wa ujauzito alipokaribia kujifungua alirudi kwao na hata baada ya kujifungua alikaa sana, mimi nilikuwa naendela kuwasiliana nae kama kawaida na kumpa mahitaji yote Muhimu ya Mtoto.
Na mwaka huo pia niliacha shughuli za udalali kuna Dili ambalo Jeni alinipa kuna Company moja hivi nilikuwa naenda kwa ajili ya Kuandaa Tender Documentes na Ishu nyingine zinazohusiana na Tender mbalimbali lakini pia kwenye masuala ya IT ila jukumu langu kubwa lilikuwa ni
IT nilipiga hapo kazi sana kwa Muda mrefu hivi.
Hadi siku niliyokuja kupata matatizo makubwa kwenye hiyo kazi nikaja nikafukuzwa kuna ishu ilitokea ya udanganyifu na mimi nikahusishwa moja kwa moja nikafukuzwa nakumbuka hicho kisa nilikisumilia huku miaka ya nyuma
Siwezi kusahau siku niliyofukuzwa kazi nikiwa baa
baada ya hapo nikajichanganya kwenye Company nyingine nikapata kazi kwenye Taasisi Fulani nikawa mkuu wa Kitengo cha Masoko nilifanya kazi pale na ilikuwa ni kazi ya Kusafiri sana nah ii ndio iliyonibadilisha kabisa, maana ilikuwa na Hel asana ile kazi.
Wakati huo Judy alisharudi dar tukaamua tusihi hivyo bila ndoa rasmi ya kisheria/kidini na mtoto alishakuwa mkubwa kabisa na hapo matukio ya usaliti asee yalikuwa yananitokea sana.
Alikuwa ananifuma sana na matukio ya usaliti, maana ile akzi ilikuwa inanikutanisha na watu wengi sana na wengi wao ni wanawake warembo na mimi ndio ilikuwa ugonjwa wangu
Ulevi ndio ilikuwa moja ya sifa yangu kuu Kuna bara za kimara huko, mbezi, na Goba hadi leo nimeacha vimeo vya madeni lakini pia nimeacha huko umaarufu wa Totozi na kulewa chakari.
Matukio yalipozidiana Judy yalimshinda maana tulikuwa hatuna hata watu wa maana wa kutusuluhisha, nilikuwa najitetea sana lakini mwisho wa siku aliamua Tuachane akaendelee na maisha yake.
Tuliahana na wala sikujali kabisa lakini mara kwa mara nilikuwa nawasiliana nae kwa ajili ya mtoto.
Ile kazi ilikuja kuingiliwa na mambo mengi biashara ikayumba wateja wakapungua maana mkoani watu walikuwa wameshaishtukia wauzaji wakawa wengi sana hivyo nikaachana nayo.
Baada ya kuachana nay o mwaka 2023 mwezi wa kwanza maisha yakabadilika sana akiba nikaanza kutumia kiba kidogo niliyokuwa nayo hadi zikaisha.
Jamaa yangu alikuwa kasulu akanipa mchongo wa biashara ya kulangua mazao, tulikuwa tunanunua nafaka kasulu na maeneo mengine ya Kigoma huko hadi katavi ile biashara ilikuwa ni ngumu sana maana kuna wateja tulikuwa tunawatumia mzigo huko dar lakini wakishapata mzigo wanaanza kuzingua malipo.
Lakini pia kupata hasara za mara kwa mara jamaa yangu kwa sababu alikuwa mwenyeji alikuwa ananipa sana hela hadi mwisho wa siku mtaji ukakata.
Nikaachana nae nikahamia Kigoma mjini kuna hela niliuza kiwanja Dar kama Million tatu hivi nikawekeza kwenye biashara ya vinywaji, nyie Kigoma iskieni tu mtaji ulikata ndani ya muda mfupi sana.
Umasiki ukaanza kuninyeemelea nilipigwa sana Uchumi Mkuu, ulinipiga kweli kweli nikawa mlevi tu nashinda vijiweni na kupiga dili za fasta hasa za ufundi kwenye IT lakini kipato kilikuwa kidogo sana kutokana na hali ya kigoma hakuna mtu anaweza kukupa hela ya maana sana sana elfu kumi au kumi na tano.
Maisha yakanipa kwlei nikaw amlevi tu sasa wa zile Pombe za Bei rahisi kunaambayo ilikuwa inaitwa Shimwa ndio ilikuwa pombe yangu, nikaacha na kwenda ibadani kabisa hata maombi nikawa sifanyi tena maana niliona kama dunia imeshanielemea.
Watu wangu wa dar ndio nilikuwa nawapiga vizinga na Jeni mara kwa maraa alikuwa ananiwezesha kama nimekwama sana japo nilikuwa naogopa sana maisha yakuomba omba tena hela ndogo ndogo
Ilifika wakati iakwa hata nakaa wiki bila Kuoga yaani wala kubadili nguo mimi ni kunywa tu asubuhi hadi jioni.
Usiombe maisha yakupige utakumbuka kila kitu, niliahidi kupambana kwa kila nguvu lakini niliamua kurudi Dar mwaka huu mwezi wa kwanza
Nilitafuta akzi sana hata huku JF niliomba mchongo sana ila watu wana ku PM unampa na namba unajieleza wee kisha anakupotezea.
Mtu anaandika tangazo la kazi ukimcheki anakumbia nakurudia, ilikuwa inaniumiza san asana.
Wakati huo nikiwa dar natafuta Kazi na wakati huo huo nilikuwa nishanza kurudisha majeshi pia kwa Judy kwa ajili ya kuomba tuyamalize ili Turudiane maana sasa hata hela ya kula ilikuwa ishanza kunipa chenga.
Marafiki wengi ukwa na shida ndio utawajua, jamaa zangu nilikuwa nimeshawapiga vizinga hadi nikaogopa.
Tumaini lilikuwa limebaki kwa Judy tu na niliona nitafute suluhu kwanza bila hivyo naweza kukata moto.
Wakati natafuta suluhu na Judy pia nilikuwa natafuta kazi kwa udi na uvumba.
NITARUDI SAA TISA KUMALIZIA WAKUU, NIMEJITAHIDI KUANDIKA KWA KIFUPI ILI NISIWACHOSHE MAANA NILIJARIBU SANA KUSIMULIA KWA MTIRIKO MZURI NIKASHINDWA