Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

hapana Mkuu nilishaacha ila Nilikuwa na connection ya hizo mambo sana kuna mishangazi hata huku JF nafikiri wananisoma hapa

Pamoja mkuu, Nimekusoma 🙌

Ila JF bana toka mwanzo umesema hujui kuelezea story vizuri bado linakuja jitu linaponda.

Nimecheka ulivyomsogelea Jeni ukataka kula denda then aliposhtuka ukamwambia tufunge macho tuombe 😂😂😂😂😂
 
Kinyume cha Judi yani nimkopee mwanaume hela tena hawara tu ambae hajawekeza chochote kwangu😀😀😀 ngumu sana, msema kweli mpenzi wa Mungu hiyo roho sina hata wazo tu halijawahi kukatiza kichwani kwangu kwanza nitawehuka nitakimbia kawe nikakanyage mafuta
Kapeace as Kapeace shukuru Mungu wako kwa kutokutukutanisha
Mamaangu mbona ungefanya mengi tu yaani maana daah..
Sijui tu kuna watu tuko na ushetani sana.
Tena ule wa ndani kabisa mwanamke anakuwa haoni yaani..
Kila kitu anafanya kwa mapenzi yake na wivu mwingi
Shida mnakutana wote mshaumizwaga mna kumbukumbu mbaya..
 
EPS 14

N.B Udalali niliacha kuna sehemu nilipata ajira nafanya hapo tangu mwezi wanne mwaka Huu lakini hata hivyo nilikuwa nimeshaacha. Sasa hivi nafanya mara chache sana inapobidi. Nimeweka sawa ili kupunguza maswali.

Kama wewe ni mpangaji au ulishawahi Kununua nyumba kwa watu au kiwanja bila shaka ulishawahi Kukutana na kisa cha Ushirikina hasa Uchawi kwenye Shughuli zako.

Miongoni mwa visa nilivyokutana navyo katika pilikapilika pilika za Udalali ni kazi hii Kuhusishwa na vitendo vya Ushirikina.

Kabla sijaingia kwenye udalali nilikuwa nafikiri kwamba Wenye nyumba ni washirikina sana kumbe visa Vingine vinafanywa na baadhi ya madalali wasiokuwa na maadili.

Kuna visa vingi sana vya watu kufanya Ushirikina asee.

Kisa kimojawapo siku moja Tupo bar na dalali mmoja anaitwa Rama, wakati huo ndio nilikua Nimeshakaa sana kwenye udalali lakini tukawa tuna share Experience za kazi zetu.

Nlimwambia rama Ilivyo ngumu Kumshawishi mteja hadi akubaliane na kazi yako

Rama akaniambia tatizo lako wewe Ni wale wa “MUNGU NISAIDIE” kutoboa ni ngumu sana lazima utembee kidogo kwa wazee.

Aliniambia kwamba madalali wengi wana wa wini wateja kwa sababu ya ushirikina.

Alinisimulia namna ilivyo kwamba ili uweze kupata mteja na hata kumbadilisha akili aache chaguo lake na akubaliane na chagu lako sio kazi rahisi.

Hivyo kuna Bibi ambaye wanamtumia yupo Kihesa Iringa anatoa dawa ya mvuto ambayo ukiitumia ukimshawishi mteja hata nyumba ambayo ipo bondeni anakubali hata kama nyumba aliyokuwa anahitaji yenye sifa Fulani, unaweza kumbadilisha

Huyo bibi wa Kihesa anakupa dawa ambayo ni kama kimzizi ambacho unatakiwa kukiweka mfuko wa nyuma wa suruali yako kila siku unapoenda kwenye mishe mishe zako au kama una kiofisi kuna kidawa anakupa unakiweka kwenye droo unachanganya anhela nyingine zinaitahela tu na watu.

Sikutaka kumbishia maana lengo langu ilikuwa nimsikilize tu ila mimi huwa simaini hayo mambo japo yapo ila sitaki kuyategemea kabisa madhara yake ni makubwa mkuu wala usiyatamani.

Sasa akaniambia kwamba yeye anacho kizizi akiongea na mteja yeyote lazima atakubali tu hata kama alihitaji nyumba Ubungo atampanga atampa ya Kimara au mbezi na atakubali.

Lakini pia unaweza ukawa unahitaji nyumba au kiwanja na mtu akakupeleka abondeni kabisa, au jirani na dampo au sehemu yenye makelele kama bar au kule wanakouza K, unajikuta uekubaliana nae na kulipia ukishalipia ndio akili zinaanza kukufunguka kumbe dawa yenyewe ndio inakuvuta.

Siku ukimkuta mtu amepanga vingunguti machinjoni na ni mtu mwenye akili timamu au amepanga mabondeni mvua ikinyesha tu anaingia ankutoka akiwa anogelea usije kushangaa ujue ni ushirikina unafanya kazi nah ii ni kazi inayofanywa na madalali njaa.

Rama alinaimbia wengine wanachanjiwa dawa kwenye Uume, wanapeleka majina yao kwa waganga kisha wanafanya wanachojua wanakuchanjia dawa kwenye Uboo au shingoni., huyo akikushawishi huchomoki mzee.

Kisa kingine cha Ushirikina hiki nilisimuliwa na Dalali Tumwite Tall wa Tabata Segerea yeye aliniambia sasa hivi dalali mkuu una connection sana na mabosi mpumbaze mmoja uanze kuzifaidi Kodi usikubali kukaa kizembe.

Iko hivi kuna mzee mmoja wa malamba mawili Mwisho, Alikua ndio mtaalam wa hayo mambo ilikuwa ukimkabidhi funguo tu na hauishi hapo anafanya ushirikina wa kukupeperusha anakufanya unasahau kabisa nyumba yako utakumbuka lakini kila ukipanga kwenda unaahirisha, mzee alikuwa anpanga anakula kodi tu kila mwezi na mwenye nyumba hajui chochote kinachoendelea.

Huyu mzee alikuwa an nyumba yake Malamba mawili Alikuwa anaiuza kwa taarifa za watu wa karibu ni kwamba alishawahi kuiuza kwa watu kadhaa alafu wakishalipia anabaki nayo.

Sasa yeye alikuwa na dawa zake alikuwa akishakuuzia nyumba unafanya malipo na anakuambia umpe wiki moja ahamie kwenye nyumba yake nyingine ila ukishalipia hutarudi tena huko na wala hutakumbuka mzee anaendelea kula hela na nyumba anabaki nayo.

Inasemekana yeye watu walikuja kugundua siri kuna jamaa alitaka kununua nyumba hiyo majirani wakamtonya kuhusu hilo swala mnunuzi akasema sasa huu ndio utakuwa mwisho wake. Jamaa akanunua nyumba wakafuata michakato yote kisha akampa hela yake akaondoka mzee akasemaapew siku tatu ahamishe vitu. Usiku akatengeneza dawa zake kama kawaida akafanya ya kufanya, Kesho yake asubuh mnunuzi akarudi akammabia ulichofanya umeshashindwa hama leo leo na ndio ikawa mwisho wa ufalme wa Yule mzee baada ya kuumbuliwa, Kumbe jamaa alikuwa amejipanga sana kiroho alikuwa na kinga zake za kichawi uwezo ukazidiana.

Kwa ambao wanasema uchawi haupo nawashangaa sana, ndio maana tunaomba Mungu kila siku ili atuepushe na hayo mambo.

Tall akaa ananishauri na mimi niitumie hiyo dawa kupeperusha mabosi angalu na mimi nipate nyumba moja niwe nalia kivulini jasho la mtu hiyo siku nilicheka sana nikaona sasa hii kazi sio. Sikuwahi kujaribu kabisa hilo jambo japo alinipa shuhuda nyingi sana.

Kuna mama nyumba moja ilikuwa kibaha ni Apartment nzuri sana, lakini kila wapangaji walikuwa wakikaa pale miezi sita wanaondoka wengine hata hawamalizi hata hiyo sita wanaondoka.

Kuna Familia moja walipanga hapo ilikuwa ikifika kila siku usiku wanasikia watu wanacheka sebuleni wakichungulia ahwaoni mtu.

Kuna watu walikuwa wakilala kuna mapaka yanalia kweli kweli nje ya nyumba yanatoa sauti za ajabu sana, wakati mwingine wakitoka wakirudi wanaona kama matone ya damu mlangoni lakini walikuwa hawaelwi kabisa ni nini kinafanyika.

Mwanzoni walifikiri kwamba labda ni ugeni mawazo na woga ndio unawafanya wanasikia hivyo.

Na aliyekuwa akisikia mara nyingi ilikuwa ni mke wa jamaa sasa siku wamekaa sebuleni TV ikawa inajiwasha na kujizima alafu inatokea kama sauti ya vicheko hivi vya kukera.

Walikuwa wamekaa sebeleni wote woga uliwaingia sasa la mwanaume alikausha kwamba sio uchawi kuna hitilafu baadae kweli ikatulia na wakasahau.

Vile visa vikazidi sasasiku hadi siku nyumba akawa haikaliki kuna wakati walikuwa wanasikia pia kama watu wanarusha mawe kwneye mabati lakini wakauliza majirani wanasema wao hawakusikia.

Majini yakawa yanawavamia usiku yanawanyonga sana jamaa akaona visa vimezidi wakati mwingine wanalala kitandani wakiamka wanajikuta wamelala chini sebuleni tena wakiwa watupu.

Jamaa ilibidi aanze kutafuta ushauri kwa wadau wake wakamwambia atumie dawa za kienyeji mara maji ya upako lakini wapi mateso yakawa ni makubwa sana usiku ni heka heka hakuna kulala. Mwisho wa siku jamaa ikabidi ashauriane na mke wake ahame na stori zikasambaa mtaani mwneye nyumba ni mshirikina na ndani kwake kuna majini.

Ila mwenye nyumba alikuwa ansikia akafikiri majirani wanamzushia au hawampendi kwa hiyo mambo ya Kiswahili wanasambaza kwa watu ili nyumba yake wapangaji wasidumu.

Taarifa zilisambaa sana hivyo akaaamu na yeye kufanya tafiti zake za tiba huko kwa wataalam ndio wapiga Ramli wakamtaji jina la mtu Fulani hivi kumbe ndio alikuwa dalali wake anayemletea wateja.

Kwanini dalali alifanya vile, kwa sababu ile nyumba ilikuwa ni nzuri na watu wanavutiwa nayo na kodi yake ilikuwa sio ndogo na kila akileta mteja anpewa kamisheni yake.

Hivyo kuna madawa alikuwa amesindika huko ili wapangaji wasiwe wana dumu wahame apelike wengine apige hela tu kirahisi, maana unaambiwa kuna wapangaji wengine walikuwa Wanaka hata wiki tu na kodi wanasamehe wanasema wamepata mchongo mkoani wanahama kumbe wamekimbia mbilinge mbilinge za majini.

Baadae waganga walikuja kutoa hayo mazindiko na nyumba kwa sasa sijui ikoje il naamini iko vizuri.

Hivi ni visa ambavyo kwenye udalali nilikutana navyo, Wenye nyumba na wapangaji umakini unahitaji Kama una Sali Sali sana ombea eneo lako kabla ya kuhamia, Wakristo wanafanya maombi yao ya kuteka na kumiliki sijui maombi ya vita n.k ili uweze kuishi vizuri, washirikina wanaweka pia mamlaka zao.

Kwenye uuzaji wa viwanja dalali akifika kwenye uwanja wako ukimpa kazi lakini akigundua unataka kumzunguka au kumpa mtu mwingine unaweza kuuza hicho kiwanja hata laki na kisipate mteja hadi yeye aamue.

Unaweza kuuza kiwanja hicho kwa mwaka mzima kila mteja akija munakubaliana bei anakubali kulipa akiondoka hata simu hapokei tena.

Hiki ni kisa kingine tena kwenye udalali na ni matukio ya kweli sio ya kusadikika. Nitarudi kuhitimisha kesho muda kama huu.
Umenigusia hadi issue yangu duuh kweli hii ni hadithi ya ukweli kabisa.
Maana hapo kwenye nyumba zenye majini..
Hapo ndipo ulipo mkasa huu wa kwangu
Natamani nisimulie lakini nakumbuka nawezà haribu mambo yangu ya pesa..
Ushawahi kuishi nyumba kubwa kwa bei ya kawaida huku baadhi ya nyumba kama hiyo hapo mtaani zinaenda mil 9, 10 hadi 15 kwa mwaka
Ila wewe ukalipa 2.5m?
Na mwenye nayo hayupo mnatumiana pesa kwenye simu hataki hata kuisogelea nyumba yake?
Dunia ina mikasa hii hasa huku kwa Madon.
 
Kapeace as Kapeace shukuru Mungu wako kwa kutokutukutanisha
Mamaangu mbona ungefanya mengi tu yaani maana daah..
Sijui tu kuna watu tuko na ushetani sana.
Tena ule wa ndani kabisa mwanamke anakuwa haoni yaani..
Kila kitu anafanya kwa mapenzi yake na wivu mwingi
Shida mnakutana wote mshaumizwaga mna kumbukumbu mbaya..
Mnakuwa mmewaroga sio bure
 
Umenigusia hadi issue yangu duuh kweli hii ni hadithi ya ukweli kabisa.
Maana hapo kwenye nyumba zenye majini..
Hapo ndipo ulipo mkasa huu wa kwangu
Natamani nisimulie lakini nakumbuka nawezà haribu mambo yangu ya pesa..
Ushawahi kuishi nyumba kubwa kwa bei ya kawaida huku baadhi ya nyumba kama hiyo hapo mtaani zinaenda mil 9, 10 hadi 15 kwa mwaka
Ila wewe ukalipa 2.5m?
Na mwenye nayo hayupo mnatumiana pesa kwenye simu hataki hata kuisogelea nyumba yake?
Dunia ina mikasa hii hasa huku kwa Madon.
Hebu funguka kidogo mkuu
 
Mnakuwa mmewaroga sio bure
Hapana mummy sio ulozi ni mahaba tu wangu..tukikutana nasuuza roho yangu naacha vinyongo vyote vilivyosababishwa na watangulizi wako..
Ujue kama ni nature ya mwanaume kumhandle mwanamke haibadiliki..
Utachange kwa muda mfupi baada ya hapo unarudi kuwa romantic sana..
Na ufundi mwingi tu.
Sasa mtu kama wewe mtandaoni nishajua unachohitaji sembuse nikikaa na wewe wiki tu.
Nakumaliza kabisa kwenu wanabaki kuuliza nimekupa nini?.
 
Hapana mummy sio ulozi ni mahaba tu wangu..tukikutana nasuuza roho yangu naacha vinyongo vyote vilivyosababishwa na watangulizi wako..
Ujue kama ni nature ya mwanaume kumhandle mwanamke haibadiliki..
Utachange kwa muda mfupi baada ya hapo unarudi kuwa romantic sana..
Na ufundi mwingi tu.
Sasa mtu kama wewe mtandaoni nishajua unachohitaji sembuse nikikaa na wewe wiki tu.
Nakumaliza kabisa kwenu wanabaki kuuliza nimekupa nini?.
Hayo yote ili uhongwe?? Braza una safari ndefu mi sio muhonga wanaume na hii itaenda hivi mpaka kufa kwangu, usipoteze muda wako
 
Hebu funguka kidogo mkuu
Mkuu hii house niliyoamkiamo ina mambo mazito mpaka walioijenga waliiuza wakatimua mbio..
Na aliyeinunua akaishi hapa muda kidogo nae akapigwa donda ndugu na hawa viumbe akatimka mpaka wa leo hajarudi..

Sasa mimi kwenye kutafuta nyumba mwaka juzi nilikuwa na rafiki yangu ananitembeza kwa piki piki yake..
Kwakuwa nilikuwa nahitaji nyumba kwa haraka sana kutokana na nilipokuwa
Kuna nyumba niliirekebisha lakini aliyekuwa mke wangu kwa wakati huo alikuwa amehitilafiana na msimamizi wa pale ambae ni mama mmoja hivi.
Nadhani hiyo scenario unaipata ikifikia heating point.
Nikalazimika kutafuta nyumba fasta.
Mwanangu akanishauri,,We ni tajiri acha kukaa kwa masikini ona sasa visa vya kimasikini hivyo mtu anakupandishia kodi na mkataba ndio umeisha na hakukupa taarifa kukuandaa.
Nikamwambia so twende wapi akasema kipande fulani kwa Madon tu.
Nikasema duuh huko nitaweza kweli kupata nyumba ambayo itaifaa familia yangu?

Mwamba kwakuwa yeye ni mzawa kipande hiki akanipakia tukaanza kusaka nyumba ado ado maana huku cha kwanza Madon hawatumii madalali kwa asilimia kubwa hawa wa lege to lege.
Wanatumia kampuni za madalali zilizosajiliwa.
Tulianzia nyumba tatu zote nikapata ni upande mmoja hapo wanataka m4 kwa m5.
Nikamwambia mwamba kuna moja nimeielewa turudi town nikadraw pesa tuje nilipie kabisa.
Tukaondoka tukaeñda town nikavuta mzigo tukawa njiani kurudi sasa tukiwa tumefika mitaa fulani lakini huku huku kwa matajiri,
Jamaa akaniambia nimekumbuka kipande fulani kuna nyumba vipi tupitepo tukaicheki?
Nikamwambia yap twende.
Sasa nashangaa jamaa anachepuka na kanjia kembamba hivi.
Kichwani nikawaza hata nikiikuta ni nzuri namna gani siwezi kuilipia kanjia kenyewe ndio haka ka kunipeleka home mbona hapa kati wanaweza kukaa watu wa kazi wakakupora wakakuua bila mtu yeyote kujua?
Ila kwakuwa jamaa kashashika njia sikutaka kumsumbua mara sijui turudi tu maana hata njia yenyewe hairuhusu boda kugeuza.
TUkaenda hadi hiyo sehemu ambapo ndio humu nimekaa naandika huu mkasa.
Baada ya kufika tulimuona msimamizi maana yeye anakaa nyumba nyingine ya juu kidogo kiwanja tofauti kabisa na hii nyumba.
Yeye alituelekeza tu na kutupatia ufunguo..
Jamaa akamwambia si twende utuonyeshe?
Manzi akagoma kabisa akatupatia mfanyakazi wake wa ndani akampa maelekezo pale kiaina hatukusikia walichozungumza.
Basi tukafungua kigeti kidogo ambacho ndio kinaunganisha hivi viwanja viwili tukashuka mgazi na kuingia kulikagua hili jengo.
Aisee limejengwa kwa mtindo wa kipekee halafu la kitambo sana..
Baada ya kulicheki tu nikaelewa kuwa mwenye jengo hili kama ndie alilijenga basi bila shaka alikuwa kwenye chama cheusi..
Nikawa kimya tu tukazama ndani.
Kitendo cha kuingia tu ndani akili yangu ikabadilika kabisa na kujikuta nishalikubali hili jengo maana niliona upande ambao unapangishwa nikaambiwa bei 2.8m kwa mwaka kwanza nikashangaa inawezekanaje hii?
Jengo lina setup yote hii vyumba vitatu jiko liko full na bonge la sitting room kwa bei hiyo?
Sasa kwakuwa mazingira yangu yalikuwa ni kupata sehemu fasta nikamuambia tusiendelee kukagua sana turudi kwa msimamizi tukaenda akatuunganisha na mwenye nyumba nikajaribu kutikisa bei ikaja kwenye 2.5 nikalipa kabisa yaani sikutaka kupoteza muda na nikampa msimamizi pesa ya kufanya usafi tukasepa.
Jamaa yangu ndio akawa ananiambia pale sasa ndipo penyewe kwanza hapana watu wengi.
Nikasema pia ndio aina ya maisha nayoyapenda sitaki kuchangamana na watu kabisa..
Tukahamia maisha yakaanza lakini nikashangaa nyumba nzima niko peke yangu ule upande mwingine hauna mtu.
Kuja kuchunguza vizuri ndio nagundua kuwa kule niliko ndiko ilikuwa living room ya walioijenga hii nyumba.
Yaani kila kitu ni kama mwenye nyumba karudi tu maana sebule ni vile vile jiko nalo.
Kifupi ni kama nilifanya kufiti.
Siku moja niko kwenye boda narudi nyumbani niko mbali bado nashangaa simu ya wife napokea ananiuliza uko wapi?
Namjibu kuwa niko kwenye boda nakuja nyumbani,, anashangaa kisha anasema sawa wahi haraka..
Nikadhani labda baby mama yuko moto anahitaj spana za kwenda.
Kufika nimekaa nimepoa ananiambia kuna mtu kaja ndani ya uzio hadi kwenye varanda anaongea na kucheka kama mimi.
Nikawaza labda wenge lake..
Nikamchukua nikampiga miti na kuendelea na ratiba zangu.
Siku zikasonga sasa siku moja niko sebuleni mwenyewe nikasikia jikoni kama kuna paka anakwaruza ukuta kwa nguvu.
Nikanyanyuka taratibu na kwenda kufungua mlango ile ghafla kwa haraka. Maana taa ya jikoni ilikuwa inawaka.
Nikashuhudia msitari mwembamba wa kivuli ukiwa unatoka nje. Damu zikasisimka mwilini nikarudi sebuleni kukaa.
Imepita muda kidogo koki ya jikoni ikafunguliwa nikanyanyuka na kwenda kucheki.
Kweli maji yanatoka nikafunga koki nikatikisa kichwa huku machozi yakinilenga lenga hivi.
Kitendo hiki huwa sikifanyi mara nyingi maana hapa nakuwa naamsha ile nguvu yangu ya asili nyeusi iliyomo ndani yangu ili kukabiliana na mazingira ambayo nahisi si salama kwa mwanadamu yeyote yule.

Baada ya kufanya hivyo nilizima taa ya jikoni nikalock na mlango nikachukua pc yangu maana ndio kipindi nilikuwa naandika ile riwaya yangu ya Mabaduni wa Serikali..
Kuingia chumbani hapo ni mida ya saa sita kwenda saa saba namkuta wufe kakaa kitandani ananitumbulia macho tu.
Akaniuliza vipi mbona hauko sawa?
Nikamjibu niko sawa tu lala maana nataka kuwasha mishumaa nifanye ibada.
Nikisemaga hivi tu wife anaelewa kuwa kuna kazi nzito inataka kuanza.
Basi baada ya kufanya ibada inayochukua dakika tatu nikazima vyote nilivyoviwasha na kuviweka mahali pake nikavua na vazi la ibada nikapanda kitandani kulala.
Ngoma zikawa zimetoka vyumbani zikaenda kujishona jikoni.
Sasa mle ndio ikawa makao makuu yaani.
Ukiingia tu jikoni zinaanza mbwembwe.
Mwanamke akafuatilia historia ya pale

Aisee alichokuja kusikia kilinisisimua sana nikamwambia ajitahidi sana watoto wangu wasipate hizi taarifa maana hazitawaacha salama..
Mwanamke akawa ananisisitizia kuhusu kuhama nikawa namuuliza tu kuna mtu kadhurika labda?
Anajibu hapana lakini tuhame.. namwambia hapa nitaondoka kwenda kwangu tu tofauti na hapo sihami.
Wife akawa anashindwa kunielewa,, mpaka ile siku tuliyokuja kutengana. Aliondoka yeye na watoto wakaniacha peke yangu ndani humu mpaka leo hii naishi peke yangu na mbwa wangu tu huko nje.
Kwasasa nawatumia mbwa kujua kama nje pameshazungukwa na hawa viumbe hasa ikifika saa nane au saa tisa..
Mbwa wangu watalalamika sana kama vile wanahitaji msaada wangu.
Na ni majibwa makubwa ya kizungu lakini nikitoka nje muda huo wanakuwa wanaona kama ukombozi umekuja..
Nakaa nao kidogo nawapeti kiaina nazunguka nyumba nzima kukagua mazingira kisha narudi ndani nalala.

Sasa miezi ya hivi karibuni wakaniamshia popo ile mbaya..
Ikifika saa tisa au kumi za usiku unakuta mtu umelala usingizi mzito wanatumia ile sauti ya mke wangu kuniamsha usingizini.
Yaani ni kama mke wangu amesimama mlangoni ananiita anaita hata mara mbili au tatu ukiamka kabisa hivi anagonga mlango kwa nje kisha panakuwa kimya..

Kwakuwa naelewa narudi tena kulala.
Ilitokea mara kama tano hivi wakaacha kisha wakahamia chumba cha pili kutoka hiki nacholala huko ndiko wamekita kambi..
Kuna kabinti nilikapata tukaanza mahusiano hivi karibuni..
Kakadai nikisafiri nikaache hapa kaishi tu nitakakuta nikirudi.
Nikakaambia suwezi kukuacha hapa ni bora nivifungie vitu vyangu vichache nilivyobaki navyo nisafiri mpaka siku nitakayorudi..
Kakakaza fuvu ikabidi nikaambie ukweli wote kuhusu hii nyumba na hapo ilikuwa ni usiku..
Walivyosikia nawazungumzia tu wakamwaga maji mengi sebuleni asubuhi naamka nashangaa maji mengi kishenzi sebuleni.
Sikutaka kujiuliza mara mbili maana nyumba yenyewe naishi peke yangu nikachukua mopa nikaanza kazi..
Kingine ni kuwa kila chumba lazima nikumbuke kufunga vizuri ila siloki milango maana ukiacha mlango loose inakuwa ni mwendo wa kusukuma milango mpaka wanafika wa chumbani inakuwa ni kama unachunguliwa kisha wanafunga fasta..
Wataendelea mpaka uende ukafunge mbona..
Mi nishazoea kabisa
Sasa utajiuliza nimwezaje kuzoea hii hali ya hivi naishi na viumbe ndani ambao siijui hata idadi yao.
Ni kwamba maisha haya sijayaanzia hapa huko kwetu kijijini kuna nyumba tunayo ina viumbe hawa wakorofi vibaya mno.
Kwa hiyo heka heka zote hizi ni kama marudio.
 
Hayo yote ili uhongwe?? Braza una safari ndefu mi sio muhonga wanaume na hii itaenda hivi mpaka kufa kwangu, usipoteze muda wako
Huwezi kunihonga maana nina zangu but hapo unaposema eti huwezi kumpa mwanaume pesa nakataa sana tu
Maana the way nitaishi na wewe nikikwama
Nikakuomba huwezi kuninyima.
Maana siishi na wewe kwa machale,,
Naishi na wewe ile total life shida yako unadhani nakuwa naishi na wewe kibenten sio hivyo.
Nakuwa nimekuhold as my wife kabisa..
Yaani ukichungulia kulia kushoto unajiona wewe.
Najua unapenda security sana tena sana
Nitakupa ulinzi wote..
Huchomoki mama amini tu hivyo..
We unadhani nitakuwa msingi kiuno ili nikuteke?? No nakuconqure ile mazima kabisa.
 
Huwezi kunihonga maana nina zangu but hapo unaposema eti huwezi kumpa mwanaume pesa nakataa sana tu
Maana the way nitaishi na wewe nikikwama
Nikakuomba huwezi kuninyima.
Maana siishi na wewe kwa machale,,
Naishi na wewe ile total life shida yako unadhani nakuwa naishi na wewe kibenten sio hivyo.
Nakuwa nimekuhold as my wife kabisa..
Yaani ukichungulia kulia kushoto unajiona wewe.
Najua unapenda security sana tena sana
Nitakupa ulinzi wote..
Huchomoki mama amini tu hivyo..
We unadhani nitakuwa msingi kiuno ili nikuteke?? No nakuconqure ile mazima kabisa.
Sio mimi rafiki,
 
Back
Top Bottom