Mkasa: Wema ni akiba, usiache kutenda wema

Mkasa: Wema ni akiba, usiache kutenda wema

Part Five C: In every life we have some trouble.

How this abduction happened.

Yule mzungu alifikia Dar akiwa na familia yake, wakafanya utaratibu wa kupata 'agent', walikuja bila maandalizi, kwa vile mwanaume alikuwa mzoefu Tanzania.

Walikubaliana na 'agent' wao wakutane geti la ngorongoro , walitaka kufanya utalii wa ndani bila buguza.

Walipata gari la kukodi kwa huyo 'agent' wao, prado ya milango mitano, huku wakiahidiwa kupokelewa geti ta ngorongoro kwa ajili ya safari ya mbugani.

Safari yao ilianza bila tatizo, wakiwa wanafurahia mandhari nzuri ya Tanzania.

Hawakuwa na dereva, walisimama sehemu mbali mbali zilozo wavuti kupiga picha bila usumbufu . Yule mwanaume, alikuwa mzoefu maeneo hayo, ilipita mara nyingi kipindi cha nyuma akiwa na wenyeji wake.

Walipofika moshi wakapumzika, pamoja na kupata chakula.

Wakiwa hapo 'restaurant', walikutana na watekaji wao. Mmoja wa wafanyakazi wa pale mgahawani, tumpe jina la mangi, aliwasikia maongezi yao na akabaini ni wageni na hawakuwa na mwenyeji.

Akawasiliana na mwenzake, tumuite jina la komando. Baada ya wale wazungu kuondoka pale mgahawani kuendelea na safari yao, Mangi na Komando wakanza kuwafukuzia.

Baada ya kufika Arusha, wakachukua chumba hotel moja pale Sakina jirani na 'induce' . Baadae wakakubaliana, waka nunue badhi ya mahitaji, maana walitaka kuanza safari ya Ngoro ngoro kesho yake mapema.

Alishuka na barabara ya mianzini kwenda stand kubwa, mpaka mjini kati, wakafanya shopping yao, wakaamua kupumzika hapo mjini kuvuta muda warudi hotelini. Mida ya saa 3 usiku, wakaanza safari kurudi hotelini.

Muda wote huo, komandoakikuwa anawafatilia bila wao kujua, huku Mangi akiwa na mwenzake, mwenyeji wao Arusha. wakiwa wanasubiri kwenye corolla. Tumuite Bonny.

Walipofika maeneo ya anex hotel kuna, corolla nyeupe iliingia barabarani mbele yao. Waliopofika round about ya florida, ile corolla ili 'block' bara bara, wakajidai imezima.

Yule Mzungu kutokana na ugeni, hakuwa mzoefu wa ile mitaa, ilibidi asimame nyuma yao.

Kosa alilofanya ni kushusha kioo ili awaulize kuna tatizo gani. Ghafla komando aliekuwa nyuma ya gari, alijitokeza dirisha la dereva na kumuelekezea bastola zusoni.

Mzungu alitulia, haraka haraka Mangi akiwa kaficha uso, akaja kumshusha dereva na kushika usukani.

Yule Mzungu alipandishwa nyuma, akawa na Komando na wale wanawake wawili. Ilitangulia kuondoka gari ya Bonny, ikafatiwa na prado aliyoendeshwa na mangi.

Walipandisha mpaka kule migombani nilikowakuta , wali waambia hawana shia ya kuwadhuru endapo watakuwa watulivu na kutoa ushirikiano.

Kiongozi alikuwa Mangi.Walishushwa pale migombani , wakawasachi na kuchukua kila kitu walichokuwa nacho. Jamaa walichukua mali zao zote, wakaacha passport tu. Pesa, cameras, laptops, nguo, viatu na vitu vingine vyote wakabeba.

**********

Part Five D: In every life we have some trouble.

We have to find them.
Table.jpg
Abduction%20incident%20.jpg
Hidden.jpg
Mianzini.jpg
Florida%20round%20about.jpg
 
Part Five D: In every life we have some trouble.
We have to find them.

Polisi wali fanya kazi yao, baada ya siku 5 walifanikiwa kumkamata Komando,alitaka kuuza camera na Laptop kwa mfanyakazi mmoja wa pale NBC, kumbe yule jamaa alikuwa amesikia kuhusu lile tukio.

'nahisi alikuwa informer' ni hisia zangu tu jamani baada ya kusoma thread ya mshana akielezea kuhusu tabia za 'informer' sijui zaidi ya hapo [emoji114] '

Wakakubaliana kesho yake aende pale kazini kwake, ampe pesa yake maana wakati huo alimpa nusu aliyokuwa nayo.

Yule mfanyakazi aliwasiliana na polisi, kesho yake Komando anafata hela yake, akakuta jamaa wako kwenye gari la kiraia hapo nje hakuwatambua.

Akaenda mapokezi akamuulizia mtu wake, akaja na hela kwenye bahasha. Akamwambia watoke hapo nje, ampe bahasha yake, pale kazini wasisanukie dili lao.

Jamaa akakubali, wakaenda kusimama pembeni ya lile gari la askari, alipokabidhiwa pesa tu, jamaa wakashuka wakawakamata wote na kuondoka nao.

Baada ya Komando kubanwa, alieleza tukio zima lilivyotokea na kupelekea wenzake kukamatwa. Wote walikutwa na mali walizoiba, ila fedha ningi zilishatumiwa.

Wakabanwa waonyeshe siraha waliyotumia, wakaonyesha toy . Wakadai hawakuwa na silaha ila wanatumia hilo toy kufanyia matukio.

Taarifa ikatumwa Dar, ubalozi wakasema wale wazungu wameenda kwao, watawasiliana nao.

Mangi, Komando na Bonny walikaa kisongo mwaka mzima ndio yule mzungu alikuja kuvitambua vitu vyake.

Baada ya kesi kuisha jamaa walifungwa kwa kesi ya unyang'anyi (robbery case).

Mzungu akaomba polisi akutanishwe na mimi na yule mzee kanali, difenda ya polisi ikaja nyumbani, mzungu akiwemo.

Mama aliwakaribisha ndani, sikuwepo muda huo, ikabidi ufanyike utaratibu wa kufatwa nilipokuwa maana nilimuaga maza kuwa naenda wapi.

Nilipofika nyumbani kuona farasi mweupe nje nikaingiwa na hofu sana nikijua labda kuna tatizo kubwa.

Baada ya kuingia ndani nikamuona mzungu, nikapata amani baada ya kujua lengo la ugeni ule . Baada ya story chache, akasema ana maongezi na mimi, anaomba twende hotelini kwake ili tupate utulivu wa kuongea.

Kabla ya kuondoka waliomba niwapeleke kwa yule mzee kanali, ili tujumuike wote kwenye maongezi yetu.

Tulipofika kwake tuliambiwa Mzee anaumwa, amelazwa muhimbili mwezi wa pili sasa, likuwa na kansa ya damu.

Tukapelekwa na ile difenda mpaka Mount Meru Hotel, mzungu akatoa pesa, akawapa asante wale askari wawili, wakamwambia akiwahitaji apige simu kwa namba aliyopewa (Rpc alimpa namba ya ofisini kwake).

Pale hotelini, nilimkuta mzungu mwingine ambae alikuwa ametoka ubalozini, kwa ajili ya kufatilia ile kesi ya mwenzao.

Kwa mara ya kwanza nikakanyaga Mount Meru Hotel, kipindi hicho inavuma sana sana. Tukapata chakula kisha tukaendelea na vinywaji huku maongezi yakiendelea.

Mwenyeji wangu alijitambulisha anaitwa Collins, ni raia wa Finland, na mwenzake Mathew.

Aliniambia anashukuru sana kwa msaada niliowapa mwaka moja nyuma walipotekwa, kaniambia kuwa familia yake imetuma salamu na shukrani zao, kwangu na kwa mzee kanali.

Tuliongea mengi sana siku ile, alinieleza story nzima jinsi tukio lilivyotokea. Mwenzake alikuwa anatumia maneno magumu magumu, wakati mwingine namkubalia tu hata kama sijaelewa. Ila Mr. Collins alikuwa anatumia Kiingereza kinachoeleweka bila shida.

Siku hiyo niliachana nao saa 2 za usiku, baada ya kumwambia mama atakuwa ananisubiri . Mama alinipenda sana kuliko ndugu zangu wote.

Akaitwa mhudumu akaombwa atuitie taxi, ikaja nikaondoka. Mr. Collins aliniambia kesho yake atauja nyumbani tuonane kabla hajaondoka mchana kwenda Dar.

Kesho yake mida ya saa 3 asubuhi jamaa wakaja na taxi mpaka nyumbani. Walitumia taxi ile ile niliyotumia jana yake. Mama akaanda chai japo walikunywa kwa aibu tu. Baada ya chai wakaanza kutoa shukrani zao kwa mama, kisha Mr.Collins akampa mama kibegi cheusi kizuri sana.

Mimi nilipewa laptop moja aina ya IBM ThinkPad 700, camera camon Eos 5 moja na zawadi zingine nyingi. Maana alipitia madukani akanifanyia shoping ya maana sana. Very expensive clothes & Shoes, akanipatia saa aina ya rolex ya gold aliyokuwa amevaa.

Akanipa Fedha kiasi cha dollar 1500 kipindi hicho shilingi 1 ya Tanzania ni dola 0.85,ilikuwa pesa nyingi sana kwanngu. Mama baada ya kufungua lile begi alikuta kuna dola 500. Saa nzuri ya gold, na zawadi nyingine ndogo ndogo. Nilimpa mama zile pesa zote akaingiza kwenye biashara zake.

Baada ya Mr. Collins kuchukua taarifa zangu zangu, ikiwepo Email Adress yangu (hii niliifungua kwa ajili ya kuchati kipindi hicho yahoo messanger inatamba, unaende kulipia internet cafe.

Wakaniomba niwapeleka kwa yule mzee kanali, tuliiacha ile taksi pale nyumbaani maana hapakuwa mbali na unapita njia za migombani. Tulimkuta mke wa yule mzee, alitupokea tukapewa maziwa maana mzee alikuwa na ng'ombe hapo kwake. Baada ya maziwa, niliwatambulisha wageni wale na wao wakaeleza lengo la ujio wao huku nikiwa mkalimani.

Walimpatia mama zawadi na fedha dola 1000 kwa ajili ya matibabu ya mzee. Pia waliahidi wakifika Dar wataenda kumtembelea kule muhimbili. Kwa hiyo waliochukua taaria muhimu namna ya kumpata.

Baada ya kumaliza kilichotupeleka pale tuliaga wakarudi kwenye taksi wakaondoka. Walikuwa wamebeba mizigo yao kwenye taksi, kwa hiyo walienda moja kwa moja uwanja wa ndege KIA wakaondoka.

Mzee kanali alifariki wiki mbili baada ya ujio wa yule mzungu, nilishiriki mazishi yake huko kwao chumbageni Tanga.

***
Song: Bad things happen to good people
Album: Pain Paints Paintings
Artist: Dax
Released: 2021
Genre: Hip-Hop/Rap

Bad things happen to good people
It's not fair, but with good comes evil
Look to God as I climb these steeples
And He says all men were created equal
Equal, equal-al-al
We're all created equal
Bad things happen to good people
I know it's not fair, but with good comes evil
I look to God as I climb these steeples
And He says all men were created equal

Nobody's beatin' Father Time (Father Time)
Evil walks among the people, it's not hard to find (find)
We play the game of life and search for terms, when all the while
The only guarantee is that nobody makes it out alive
Faith in hand, we overlook (overlook)
'Cause human nature's bad is good (bad is good)
We tryna walk straight as we tightrope with the Holy Book
Readin' passages while judgin' others, givin' dirty looks
We teeter-totter on the line of sinner and misunderstood (misunderstood)

No one's perfect, we're exposed
We try to hide, but God knows
And water seeds we didn't plant
Then wonder why they don't grow (don't grow)
Fake friends, good foes
A world together, all alone
An oxymoron, seven billion people lost with one home

Bad things happen to good people (good people)
It's not fair, but with good comes evil (comes evil)
Look to God as I climb these steeples (these steeples)
And He says all men were created equal (equal)
Equal, uh (equal), equal-al-al (equal)
We're all created equal (we're all created equal)
Bad things happen to good people
I know it's not fair, but with good comes evil (with good comes evil)
I look to God as I climb these steeples
And He says all men were created equal (He says all men were created equal)

Young girls gettin' trafficked (yeah)
People like the way you innocent
While these little kids gettin' cancer (yeah)
God, tell me, what's the benefit?
He reminded me that He's still good
Got a perfect plan when it's all bad
Even if you never really understand
We can still hit our knees and ask Dad

Whole world full of evil (evil)
Should we take it out? Should we put it down?
But He's patient with His lil' people (yeah)
While the dark powers keep on runnin' 'round
Come a time when He bring peace
When He bring rest, when He bring love (bring love)
Gotta hope in the meantime
That He mean well and He need somethin'

When the good people die young (when the good people die young)
And the bad habits to the good folks
That the Kingdom is still comin'
In Christ, that's where I gotta put hope
You ain't gotta see it 'same as I see it
But you gotta see it for yourself (yeah)
If it ain't of God, can it be of good?
I don't know at all, tryna help, yeah (woo)

Bad things happen to good people (good people)
It's not fair, but with good comes evil (comes evil)
Look to God as I climb these steeples (these steeples)
And He says all men were created equal (equal)
Equal, uh (equal), equal-al-al (equal)
We're all created equal (we're all created equal)
Bad things happen to good people
I know it's not fair, but with good comes evil (with good comes evil)
I look to God as I climb these steeples
And He says all men were created equal (He says all men were created equal)

Next
Part Six A :Tasting honey with the tip of a knife[emoji182]

1994-1996


'******

svaagat hai apanon ka (Karibuni wapendwa )
Table.jpg

View attachment 2556654View attachment 2556656View attachment 2556657
 
Back
Top Bottom