Mahondaw
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 67,252
- 168,563
Fanya wepesi umfurahishe huyo mwamba banaa kwa udhamini wako sie tunasubiria kwa hamuu sana XXX rated ๐๐!Hahaha mkimfurahisha atawapa kitu roho inapenda
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Fanya wepesi umfurahishe huyo mwamba banaa kwa udhamini wako sie tunasubiria kwa hamuu sana XXX rated ๐๐!Hahaha mkimfurahisha atawapa kitu roho inapenda
๐๐๐๐Fanya wepesi umfurahishe huyo mwamba banaa kwa udhamini wako sie tunasubiria kwa hamuu sana XXX rated ๐๐!
Tena wakaliii...hatari kabisa ๐ ๐ ๐Kweli Kabisa sis kweli siku hazigandi hatimae nasie leo tunawapiga biti mabinti olee wao niwakute na wanaume mtanitambua yanii nitawapasua ivo vichwa๐๐๐!!
Asante sana ccy
K. Rogers!! What a lesson[emoji848]Part Four B: Maisha ya ujana
1990 - 1993
Tukiacha ubabe wa shule za boarding, tulikuwa wababe kwa wanafunzi wa chuo cha ualimu matogolo , maana shule yenye form 1 - 6 mchanganyiko toka mikoa tofauti, haikuwa rahisi kui handle.
Matogolo ni jirani, kuna wasichana na sisi tunawataka , na ma boy wao hapo chuo wanawataka.
Ni mwendo wa bifu za mapenzi na mambo mengine, kuna wale wanywa ulanzi wakiwashiwa moto, wanaleta taarifa jeshi la box 2 linaenda kumaliza kazi. Nilikuwa doja wa hatari kwenye matukio kama hayo.
Siku moja mbawala aliniambia nimsindikize rizaboni , ilikuwa siku ya jumapili, (kila jumapili tunaruhusiwa kutoka kwenda kanisani mwisho saa 10 jioni)
Tumefika rizaboni , kumbe mwamba amemfata mtoto wa mwanajeshi, wamesimama wanaongea pembeni ya njia, akaibuka mtu migombani mara jamaa ameshikwa. Binti akachanganyikiwa, nikaunganishwa na mimi.
Kumbe ni baba yake na binti, akatupeleka kambi ya jeshi pale Ruhuwiko, wakatupatia machangu matatu ya adhabu.
Ya kwanza, tufanye kama tunaendesha gari, tunashikana mashati, tuzunguke jengo flani pale mara 100 kisha tupotee
(Hapa kuna konda na dereva, unatakiwa usimame uite abiria, uchukie nauli, mpige story, hope unajua watoto wakicheza lazima kila kitendo wakielezee)
Ya Pili wawashe moto, tukae kuota hapo juani kama saa 7 /8 hivi, moto ukizima tupotee.
(moto wenyewe kuni kubwa sio wa mabua na ni kiangazi mko juani).
Ya tatu tuletewe wali ndoo ndogo umejaa, tuhakikishe umeisha kisha tupotee.
(watu wawili wali ndoo ya lita 10, hakuna kudondosha, akishindwa kumaliza mnapiga push up kuita njaa, mnarudi kumalizia.)
Siku hiyo ndio nilichukia kazi ya jeshi, tuliona option ya kwanza ni nafuu, nikawa dereva mwenzangu konda.
Kazi yangu mungurumo wa gari na honi visikike, mwenzangu ahakikishe anapiga debe kuita abiria, adai nauli, awakemee abiria wakorofi nk
(matukio yote common yanayotokea kwenye daladala yasikike loud and clear. )
Baada ya rounds 50 wakatufukuza, na kupewa onyo tusionekane na yule binti tena. Tumetoka yule boya anacheka eti.
Baada ya wiki tatu anasema yule binti amemtumia ujumbe, wakutane mfaranyaki, nikatoka nduki maana nisije ponzwa tena. [emoji125][emoji125]
โฆโฆ.
Mara nyingi kipindi cha likizo nilikuwa nakaa wiki 1 Songea na 3 Arusha kwa mama.
Kuna kipindi niliachiwa chumba na rafiki yake kaka (askari), alienda kusoma, ilikuwa likizo ya pasaka.
Likizo Ilipoisha niliacha funguo kwa kaka, ila ikawa kila nikienda nalala kwenye kile chumba.
Siku moja kulikuwa na michezo ya kishule, tukaenda uwanja wa zimani moto. Michezo ikiwa inaendele pale zimani moto. Nilimpanga mdigo wangu tukatoe 'singo' akakubali nikam 'pack' kwenye kile chumba.
Kilikuwa chumba cha 4 kutoka geti kuu la kuingia uwanja wa maji maji mkono wa.......[emoji119]
Lengo langu lilikuwa akae kwa muda pale ili mchezo ninao shiriki, ukiisha tupongezane kwa mara ya kwanza, nilikuwa nacheza 'volleyball' na nilikuwa kwenye Playlist vinginevyo ninge doji.
Yeye alikuja kama mshangiliaji tu hakuwa na mchezo anaoshiriki, ni wale 'usiniumizie'.
Lengo langu halikutimia, niliponzwaa kijinga, waswahili walisema usilolijua ni usiku wa giza.
Jasmin alinishawishi tunywe pombe kidogo, mwenzangu alikuwa mzoefu, nikajidanganya nikanywa ili mtoto asinione wa kuja hata bia sinywi.
' hivi vile vijumba vya nyasi kwenye ile chupa ya safari vina maana gani?'
Ndio mara ya kwanza na ya mwisho kuonja pombe, nilikunywa chupa 2 za 'safari lager' nikiwa nimekaa, nilipo simama ndio nikajua pombe sio chai.
Jasmin nae alikunywa chupa 2, ila cha kushangaza alikuwa sawa tu, tena aibu ziliondoka kabisa akachangamka hatari.
Kilichotokea nilitapika sana siku hiyo na kichwa kiliuma sana.
Namuona kabisa Jasmini amevua nguo, mapaja yananiita, chuchu zimesimama ila nguvu ya kusimama sina.[emoji3064]
(alipoingia alivua shati na sketi ili visijikunje, akavaa t-shirt ilikuwepo hapo mdami na taulo).
'kwanza bia chungu sijui wanazipendea nini'
Nililala toka saa 6 mchana mpaka saa 9 jioni mda wa kurudi shule, Jasmin muda wote amenilaza mapajani mwake mimi sijielewi, ilipofika jioni ikabidi aniamshe ili turudi shule na wenzetu.
Waliosema pombe sio chai hawakukosea, sikupata tunda la Jasmin wangu siku hiyo.Nikawa nimefanya harakati za dr. Pimbi wa jarida la sani , nilishindwa hata kumsindikiza nikamfungulia mlango akaondoka.
Nikaoga maji baridi nikalala hapo hata chakula hakipandi, nilimwambia sitaweza kwenda shule nikiwa vile, ilikuwa jumamosi nikapanga niende jumapili.
Nilimpanga kaka kuwa siko vizuri, kesho yake nikazuga kwenda kupima malaria ili nipate cheti cha hospitali nikaende shule.
โฆโฆโฆ.
Baada ya siku hiyo hatukupata tena nafasi kama ile, tuliendelea na mapenzi ya nadharia tu.
Kumbe Jasmin alikuwa anatembea na mwanajeshi flani wa ruhuwiko kj, ndie alimfundisha kunywa pombe, sijui walikutanaje[emoji35]. Ila akiwa na mimi ananipanga kuwa hakuna zaidi yangu, sijawahi ufanya, kumbe ni kungwi.
Ndio yale yale ya Kelly Rowland kwenye wimbo dilemma anasema
'Boy, you know I'm crazy over you,
No matter what I do.
All I think about is you
Even when I'm with my boo
You know I'm crazy over you'
Just imagine, Wanawake wa hivi watafika mbinguni wamechoka sana, au huenda pia wasifike.
(ila na mimi nilizingua, sasa kama siwezi kuogelea baharini, nilifata nini ufukweni.)
**********
Kilicho sababisha nisimle Jasmin, sikuwa serious na mapenzi kipindi hicho, nilikuwa na 'enjoy' tu 'love story',akili yangu iko kwenye kitabu pekee. Mizagamuano haikuwa fun yangu tofauti na Mbawala.
Ile kitu ingekuwa inaisha, mbawala angebaki na kishungi tu cha sigara, songea girls wanamjua, matogolo wanamjua, bado mitaani.
Hatimaye Jasmin alimaliza kidato cha nne akaondoka kurudi Tanga. Likawa penzi lilio potea 'lost love' niliotea romance pekee .
โฆโฆ.
Adui yangu mkuu pale shule alikuwa mwalimu moja kijana hivi, alizinguana na kaka huko mtaani kisa msichana wa pale matogolo, kumbe kaka anatoka nae tangu 'binti yuko sekondari' kufika chuo akatamani pesa ya mwalimu.
Siku wamekutana mjini 'binti' yuko na mwalimu, binti akakimbia. Kaka na jezi zake akamkamata mwalimu.
Ikabidi akatoa pesa akaachiwa , baadae alikuja kujua ni kaka yangu akawa anamalizia hasira zake kwangu.
[emoji35]Nilikuja kukutana nae ukubwani pale akiba 'DIT'nikiwa na drive nilitamani kufungia break miguu mwake. Nikakumbuka K. Rogers alisema kwenye coward of the country,
"Promise me, son, not to do the things I've done
Walk away from trouble if you can
Now it won't mean you're weak if you turn the other cheek
I hope you're old enough to understand
Son, you don't have to fight to be a man"
Kwanza hakuwa ananikumbuka, nikampa lift mpaka pale utumishi, alikuwa anafatikia mafao yake.
Nikamkumbusha tukio makusudi, akanikumbuka akaishiwa pozi, nikampa elfu 30 ya nauli nikaondoka. [emoji124][emoji124][emoji124]
*******'**
Disco la majimaji hall, Songea club.
Nakumbuka majina maarufu kama maatiko (matiko) mmiliki wa buhemba hotel na Anex
Mfyule , Matunda, Mkwepo, Saadi , Matomondo alikuwa na guest house nyingi, n. K
Baada ya miaka minne kupita, tukafanya mtihani. Nilitoka Songea boys bila Kumjua mwanamke(Clean sheet). Nikaenda kunyonya kwa mama Arusha.
Usengwile sana Songea
**********
Next Jioni
View attachment 2555327View attachment 2555328
View attachment 2555337
Leo nukta hapaaaaa.Part Five A: In every life we have some trouble.
1993-1994
Baada ya mtihani wa kidato cha nne, nilirudi kwa mama Arusha. Nilikuta biashara zake zimechanganya hivyo basi akawa bize sana. Pia alikuwa ameshafanya maendeleo pale nyumbani pameboreka sana.
Siku zote nikiwa na mama alikuwa anapenda kunipa usia sana kuhusu maisha, kuheshimu watu wote, kusamehe, kutoa msaada pale ninapoweza , kushiriki vitu na wengine na kikubwa zaidi kumuomba Mungu.
Nilimpenda sana maana na yeye alinipenda sana kuliko watoto wake wote.
Pamoja na upendo alinifundisha kupika nikiwa mdogo sana, tena tunafanyiana zamu ya kupika na kuosha vyombo bila kujali huyu ni mama.
โฆโฆ..
Nikawa niko mtaani tu nikisikilizia matokeo. Mzee alikuwa anamiliki nyumba za wapangaji mimi nikawa ndio bosi wao wa kufatilia kodi. Maisha nyumbani yalikuwa safi kiaina sio ile saana, ila pesa ya kutesea mtaani ilikuwa haikauki.
Nilikuwa na tabia ya kufanya jogging asubuhi saa 11 kila siku, natoka hapo nyumbani sakina mpaka pale chuo cha habari maalum.
Kama kawaida yangu sikuwa na marafiki wengi walikuwa wa nne tu na kati ya hao mmoja ndie nilikuwa nae karibu sana anaitwa Frank.
Jogging nilikuwa nafanya na huyu Frank wengine walikuwa wavivu nilikuwa nakutana na Frank pale sakina super market tunaliunga mdogo mdogo mpaka ngara mashamba ya serikali karibu na Habari maalum.
Siku moja nimetoka zangu home saa 11:00 nashuka mdogo mdogo, kuna semehu kulikua na shamba kubwa la migomba, huwa kuna giza sana hapo.
Nilipokaribia hilo eneo nikaona gari nyeusi imesimamishwa kwenye shamba la migomba.
Kipindi hicho Arusha ujambazi uko juu sana, sikuwa na hofu maana mida hiyo kuna watu wanaokwenda kufata nyama pale Arusha meat wanakuwa njiani.
Nika punguza mwendo ili nijue lile gari ni la nani na kwa nini liko migombani kama limefichwa, (ni shamba letu) lile shamba la migomba linapakana na nyumba za wapangaji wetu.
Sikufanikiwa kulikaribia gari maana nilihisi kama limeibiwa naweza pata matatizo na vyombo vya dola, au labda kuna mpuuzi kajificha pale ili kufanya ngono kwenye gari.
Ilikuwa kawaida sana kukuta mtu amepaki gari anafanya ngono maana njia yenyewe haikuwa busy sana na migomba ilikuwa mingi kwenye hilo eneo. Ikanibidi niendelee na safari zangu.
Nilikutana na Frank sakina supermarket, ilikuwa meeting point yetu. Tukaunga mpaka kwa idd akasema hajisikii vizuri ikabidi turudie hapo. Ikabidi nimwambie twende nyumbani maana ni karibu sana kuliko kwao.
Frank alikuwa anaishi jirani na 'Arusha Technical college' kama unaelekea mianzini. Wakati napandisha nikiwa na Frank tukalikuta lile gari pale pale, nikamwambia kuwa imekuwa pale toka nashuka.
Tukashauliana tusisogee maana tulihisi tu limeibiwa hatukutaka kujitafutia matatizo. Tukaenda nyumbani.
Ilikuwa 12:30 wakati tunarudi, kulikuwa kume pambazuka, Frank alioga akanywa paracetamol akalala.
Mimi nikatoka ili nikaangalie kama lile gari bado lipo, nikalikuta liko pale pale.kutokana na utundu niliotoka nao Songea boys ukiongeza mazoezi nikawa najiamini sana.
'kama pawa mabula au pawa suzuki vile,' .
Kutokana na tabia ya kufanya mazoezi nikapata ujasiri nikalisogelea maana tayari kulikuwa kume pambazuka na watu wako njiani wengi tu.
Nilipokaribia nikachungulia mbele nikaona mtu amekaa ananiangalia ila amefungwa kitambaa mdomoni. Alipo niona akawa anatikisa kichwa tu mwili umekaza nilitulia pale huku najiuliza nifanyeje.
Nikapata ujasiri wa kusogea karibu, nikamuona vizuri alikuwa ni mzungu ila amekuwa mwekundu kutokana na kamba alizofungwa. Akanipa ishara nikafungua mlango wa mbele, nilimkuta amefungwa kwenye siti ya dereva, miguu imefungwa kamba, amekalishwa kwenye siti na mikono imefungwa nyuma ya siti. Kamba zilipita karibu na mabega hivyo alishindwa hata kujitikisa kwa jinsi manila zilovyokuwa zimebana.
Usoni alifungwa kitambaa ili asipige kelele. Mpaka wakati huo akili ilisimama nisijue la kufanya, ghafla nikapata ujasiri wa kumfungua kitambaa cha mdomoni ndio akaanza kuongea ila kinyonge sana.
Baada ya kumfungua kamba zote, na yeye akajaribu kushuka kwenye gari ila akashindwa kusimama akajimwaga chini. Nilimsaidia kumkalisha akaegemea gari, akawa ananiambia
"Help my wife and my daughter pls. "
"Frankly, I was curious about what was happening there."
Today is Friday, Next later todayView attachment 2555443View attachment 2555445View attachment 2555446
Niko shamba napalilia migombaNakadori Antonnia Amehlo baby zu Dr Restart Depal Shunie Analyse Half american raraa reree Numbisa IamBrianLeeSnr Angel Nylon KatKit Johnnie Walker
Hiki kitu kimetoka tangu usiku aisee mmelala sana mnapitwa.
Hiyo kiitos umenikumbusha miez yangu 3 Finland jyvasklaPart Five B: In every life we have some trouble.
Mwanzo nikajua ni wenge tu ila nilipomwangalia kwa makini nikagundua kuna kitu anamanisha, nikachungulia tena nyuma ya gari, siti za kati hakukuwa na watu.
Nilipochungulia kwenye buti nikakuta viumbe wawili mwamefungwa kitaalam na wamekunjwa na kulala chini.
Hapo ikanibidi niwashtue jamaa flani walikuwa wanapita, wakaja ila wakaniambia dogo umeshanunua kesi, tena watu wenyewe wazungu.
Basi bahati nzuri kuna mzee mmoja alikuja, akashauri kwa kuwa wahusika wako hai, tuwasaidie tu hata wao wataeleza polisi kuwa tumewapa msaada tu.
Tukawafungua na kuwashusha . Alikuwa mama wa miaka kama 35 hivi na binti alikuwa na kati ya mika 16( kwa makisio yangu) . Ukafanyika utaratibu wa kumtafuta balozi, akaenda kutoa taarifa polisi ikaja difenda akawapeleka hospitali ya mount meru.
Kimbembe kikaja tulipotakiwa kwenda kutoa maelezo polisi, watu wote wakasema mimi ndie mtu wa kwanza kuwaona kwa hiyo naweza kutoa maelezo mazuri zaidi, ila yule mzee alietoa ushauri akajitolea kuungana na mimi tukapelekwa central pale.
Tumechukuliwa maelezo yetu pale, tukazuiliwa hakuna kutoka mpaka wale wagonjwa watoe maelezo yao. Tukawekwa chumba flani hapo na ulinzi ukawepo, chai na chakula mchana tuliletewa bila shida kabisa.
Tatizo tu hakuna uhuru wa kutoka hapo, baada ya kama dakika 20, yule mzee akaitwa nikabaki mwenyewe.
Alitumia kama nusu saa kule akarudishwa akiwa na mkuu wa kituo akawa amekaa pembeni yangu wakati mkuu wa kituo ananihoji.
Baada ya maswali mengi, nikaambiwa nisiwe na wasiwasi, wakishapata maelezo ya wale wageni watajua nini cha kufanya hivyo tuvute subira.
Kipindi hicho chote yule mzee hakuwa na hofu kabisa, alikuwa ananihoji vimaswali vya kunipima anacheka, nikajua tu ananitoa uoga ili nione ni jambo la kawaida.
Ilipofika saa 8 tukaitwa ofisi ya RPC, yule mzee akapewa kiti kwa heshima tu, akapewa pole na RPC mwenyewe.
(Nilikuja kufahamu kuwa yule mzee alikuwa ni Kanali wa JW alikuwa amestafu mwaka mmoja nyuma. Kumbe hata wakati ule ameitwa na mkuu wa kituo, alijitambulisha wakaridhia yeye aende ila nibaki mimi, mzee alikataa na kuwaambia akiniacha watanisumbua hivyo hata yeye atasubiri.)
Tukiwa tunaongea yule mzungu akaletwa na askari mle ofisini, tukawa watu watano. (RPC, Mzee Kanali, Edson , mzungu na mkuu wa upelelezi wa mkoa)
Yule mzungu alikuwa ametoa maelezo yake tayar, amewaeleza kuwa mimi ndie niliwasaidia, aliwaambia sihusika na tukio, wahusika akiwaona atawakumbuka.
Ripoti ya Dr. Ilisema wako salama, hakuna alieumia sana ila ni maumivu tu ya kamba na vibao walivyopigwa basi.
Simu ikapigwa makao makuu, wakaambiwa wawapeleke hotelini wakati wanafanya utaratibu wa kuwataarifu ubalozi husika. Ikabidi wapelekwe hotel ya mount meru kusubiri taratibu zingine.
Baada ya maongezi mengi tulirudishwa na difenda nikakabidhiwa kwa mama, nilikuta mama ametulia tu hana furaha kabisa, hofu imetanda moyoni.
Baada ya polisi kumweleza kilichotokea, wakaondoka kumpeleka Mzee kanali. Lengo la kunirudisha mpaka nyumbani, wapajue endapo kutakuwa na taarifa tofauti waweze kunipata kirahisi.
Ile gari iliyotumika kwenye tukio iliikodiwa na wale watalii toka Dar, walikuwa na safari ya kwenda serengeti.
Mwanaume alikuwa amekuja mara kadhaa Tanzania, hakuwa mgeni sana.
Kesho yake wale wazungu walipelekwa na polisi KiA, wakarudi Dar, Gari likapelekwa polisi kama kielelezo.
****
_We have a lesson here.[emoji116]
Artist: Tim McGraw
Album: Damn Country Music
Awards: Grammy Award for Best Country Song, American Music Award for Favorite Song Country.
Nominations: Grammy Award for Best Country Song, American Music Award for Favorite Song Country, more
Genre: Country
"Humble And Kind"
Tim McGraw Lyrics
Follow Tim McGraw
on Bandsintown
"Humble And Kind"
You know there's a light that glows by the front door
Don't forget the keys under the mat
When childhood stars shine
Always stay humble and kind
Go to church 'cause your mamma says to
Visit grandpa every chance that you can
It won't be wasted time
Always stay humble and kind
Hold the door, say "please", say "thank you"
Don't steal, don't cheat, and don't lie
I know you got mountains to climb
But always stay humble and kind
When the dreams you're dreamin' come to you
When the work you put in is realized
Let yourself feel the pride
But always stay humble and kind
Don't expect a free ride from no one
Don't hold a grudge or a chip and here's why
Bitterness keeps you from flyin'
Always stay humble and kind
Know the difference between sleeping with someone
And sleeping with someone you love
"I love you" ain't no pick-up line
So always stay humble and kind
Hold the door, say "please", say "thank you"
Don't steal, don't cheat, and don't lie
I know you got mountains to climb
But always stay humble and kind
When those dreams you're dreamin' come to you
When the work you put in is realized
Let yourself feel the pride
But always stay humble and kind
When it's hot, eat a root beer popsicle
Shut off the AC and roll the windows down
Let that summer sun shine
Always stay humble and kind
Don't take for granted the love this life gives you
When you get where you're going don't forget turn back around
And help the next one in line
Always stay humble and kind_
**********
Kiitos.
Next [emoji116]
Part Five C: In every life we have some trouble.
How this abduction happened.
View attachment 2555876View attachment 2555878View attachment 2555879View attachment 2555880
Nataka niwe shamba boy wako ๐ฌ๐๐๐Niko shamba napalilia migomba
Nikimaliza nakuja kusoma kwa utulivu.
Thank u Gilii
Aisee hujakutana na waandishi wazuri namna anavyopanga matukio unajikuta ushamaliza na bado unataka kuendelea.Hapana huyo bado sijasoma story zake!
Mi nikiona ndefu huwa naishia njiani hata nusu episode simalizi
[emoji23][emoji23][emoji23]Ile ilijengwa na mchina 1975. Hii ya mturuki ni kizazi kipya
Bado sijafikia uhenga, bado ni kijana mdogo kabisa[emoji16]
Ngoja nisome sasaNakadori Antonnia Amehlo baby zu Dr Restart Depal Shunie Analyse Half american raraa reree Numbisa IamBrianLeeSnr Angel Nylon KatKit Johnnie Walker Lovelovie Watching
Hiki kitu kimetoka tangu usiku aisee mmelala sana mnapitwa.
Hapana mkuu yani mimi hata story iwe nzuri vipi mfano nikikuta episodes zimekua nyingi tu hata kama episodes ni fupi fupi kusoma naona uvivu Huwa napenda kwenda nayo sambamba!Aisee hujakutana na waandishi wazuri namna anavyopanga matukio unajikuta ushamaliza na bado unataka kuendelea.
Kuna udambwi udambwi unawekwa acha kabisa unashuka na story tu [emoji23]