Kuna muda naona sio kweli ni ndoto lakini ndio ukweli,tulifahamiana na marehemu kwa muda mchache akawa kama rafiki ambae nimemjua maisha yangu yote,tukipiga story za maisha hata utani utasikia embu nishauri jambo flani kama wewe utafanyaje namwambia mbona wewe ndo nategemea akili zako,ujumbe ambao siusahau kamwe nimelala nakutana na meseji nataka nikufanyie jambo ambalo utanikumbuka maisha yako yote sema kiasi cha pesa chochote ambacho utafanya biashara ikulipe zaidi nijibu kabla ya tarehe 28 kuanzia tarehe 2 nitakuwa hospital unaweza ukachelewa kupata majibu nitakujulisha namna ya kupata hizo pesa au unataka zikufikie kwa njia ipi nikashangaa sana habari za hospital akaniambia ana tatizo la tachycardia anaenda ku replacement battery ya pacemaker ikabidi ni google tachycardia chanzo Kuna chanzo kimoja nikamtania akasema kweli mie napenda sana na pia msiba wa Mama ulichangia nilikuwa na mawazo sana Nika google side effects za pacemaker ukiwekewa ambayo unapata blood clot kwenye mkono unao wekewa,kupata infection damage kwenye blood vessels au nerves na madhara mengine kwa kweli niliogopa akataniuliza wazo la biashara nikampa wazo langu nikiwa nasita akasema mbona unasita pesa za mwingine unazionea ubahili au huamini nitakupa nikamwambia no wewe mwanadamu mie mwanadamu lolote laweza tokea embu katibiwe kwanza ndo muhimu kuliko biashara zangu,mpaka anaenda hospital tunawasiliana aniambia nakuletea Iphone 14 pro max upigie picha biashara zako namwambia embu pona kwanza achana na simu nikamwambia una jua Triple G unafanana na baba yangu sana kuanzia mwili unavyo tabasamu na hio miwani akacheka nikamtumia picha za Baba akasema Mzee flani kweli tunafanana umbo nikamwambia Baba yangu alikuwa na matatizo ya moyo kama wewe nilimkosa naogopa kukukosa akanitumia baadhi ya vifungua kwenye biblia,nilichelewa kuwasha data siku ya Juma2 nikakuta meseji yake nikamjibu haikujibiwa nikashangaa nikawa na wasiwasi mpaka
Gily anakuja kunipa taarifa yupo ICU kwa kweli nilikosa amani moyoni nikawa namuombea Allah ampe shifaa nakuja kuambiwa na Gily amekufa aise niliona anatania akaniambia siwezi tania kuhusu kifo anakuja aniambia 🌹kapata presha nikakosa raha zaidi nasikia amefariki Aisee nguvu ziliniisha Yaani Alkhamis Rose 🌹 Kuna ujumbe alinitumia eti nae hayupo nilikuwa nasema wanae wamepoteza Baba ila Mama wanae kumbe usilolijua kwa kweli nawaonea huruma sana wanae wamepoteza Bibi Baba na Mama ndani ya muda mchache ila na Imani na 💜anawapenda kama wanae atakuwa nao kuwapenda kuwajali kuwaongoza hapo ndio namuelewa G kwanini hakumuacha 💜aende na kwanini 🌹alimkubali 💜awe kwenye maisha yake na akae na wanae.namuomba Mwenyeezi Mungu awarehemu wapendwa wetu hawa awape familia subra kwenye kipindi hiki kigumu kwao kufiwa kunauma sana haswa wazazi.