Lugoba Investment
Senior Member
- Dec 5, 2013
- 180
- 188
Kilichotokea ni madhara ya bosi kuwa na mahusiano na mfanyakazi wake na hatimaye kuoa mfanyakazi huyo na kumuacha akiendelea kufanya kazi ofisi hiyo hiyo na wafanyakazi wenzake wale wale.....
Chanzo cha Ugomvi kimeanzia mbali sana hata kabla hawajatua Kenya na aliyesababisha sekeseke lile litokee ni mrembo Cindy ambae Alikuwa ni mcheza shoo wa Koffi akaja akawa mpenzi wake na hatimaye mkewe.....Baada ya Cindy kuwa mke wa Koffi hali kwenye band ilibadilika....
Cindy alipandishwa cheo na kuwa kiongozi wa choreography ambaye Alikuwa na jukumu la kuongoza mazoezi ya kudance kubuni staili mbalimbali na mitindo kadha wa kadha ya kudance...Hilo halikuwapendeza waliokuwa wacheza shoo wenzake waliokuwa wanaamini nafasi aliyopewa hakustahili hata kama ni mke wa bosi kwani kulikuwa na wacheza shoo kibao wenye uwezo kumzidi na wazoefu na wako kwenye kundi kwa muda mrefu kuliko yeye,hao ndo wangepaswa kupewa nafasi hiyo...
Hali hiyo ikazua bifu kati ya Cindy na madensa hao wengine hususani wa kike...Sasaaaa Cindy hutumia madaraka yake kuwaadhibu hao mahasimu wake na huwaadhibu kwa kutowajumuisha kwenye tripu za kusafiri nje ya nchi.....Kwenye safari ya kuja Kenya kuna madada hatari sana na wakali wa kudance waliachwa kitendo kilichowakera dancers wengine akiwemo Pamela yule aliyepigwa teke.....
Pamela yeye bwana ni mropokaji hasa na hakusita kuzinguana na Cindy .......Pale airport sasaaaaa Cindy si akamfuata Pamela na kumuambia amsaidie kubeba begi, Pamela akachomoa kisha akamuongelea shombo Cindy na si unajua wale wanawake tena,basi walirushiana maneno kiasi cha kuchapana makofi,hali iliyofanya Koffi afikishiwe taarifa......Uamuzi wa Koffi ulikuwa mmoja tu,kumfuata Pamela kumsema na inasemekana Pamela aliambiwa baada ya kumalizika kwa tamasha lile yeye kazi basi.....Kama kawaida Pamela hakai na neno kifuani akaongea mbovu kwa Koffi....Unajua kilichofuata...NDO LILE TEKE.....
KWAHIYO UKIANGALIA NA KUFUATILIA KWA MAKINI SANA TATIZO NI HILO KUJIHUSISHA NA MAPENZI NA MFANYAKAZI WAKO,UNAMPA CHEO ILI AWAONGOZE WALE WALE ALIOKUWA ANAFANYA NAO KAZI LINE MOJA,WENGINE WAKO JUU YAKE NA WENGINE WAKO CHINI YAKE....
NI JAMBO LA KAWAIDA KUWA KUNA WAFANYAKAZI WENZIE WALIKUWA WAKIMZIDI SANA KIUTENDAJI JE UNADHANI WATARIDHIKA????NI KAWAIDA KUWA WATAKUWA NA KINYONGO NA MAMBO KAMA TAFRANI LAZIMA ZITATOKEA....
Chanzo cha Ugomvi kimeanzia mbali sana hata kabla hawajatua Kenya na aliyesababisha sekeseke lile litokee ni mrembo Cindy ambae Alikuwa ni mcheza shoo wa Koffi akaja akawa mpenzi wake na hatimaye mkewe.....Baada ya Cindy kuwa mke wa Koffi hali kwenye band ilibadilika....
Cindy alipandishwa cheo na kuwa kiongozi wa choreography ambaye Alikuwa na jukumu la kuongoza mazoezi ya kudance kubuni staili mbalimbali na mitindo kadha wa kadha ya kudance...Hilo halikuwapendeza waliokuwa wacheza shoo wenzake waliokuwa wanaamini nafasi aliyopewa hakustahili hata kama ni mke wa bosi kwani kulikuwa na wacheza shoo kibao wenye uwezo kumzidi na wazoefu na wako kwenye kundi kwa muda mrefu kuliko yeye,hao ndo wangepaswa kupewa nafasi hiyo...
Hali hiyo ikazua bifu kati ya Cindy na madensa hao wengine hususani wa kike...Sasaaaa Cindy hutumia madaraka yake kuwaadhibu hao mahasimu wake na huwaadhibu kwa kutowajumuisha kwenye tripu za kusafiri nje ya nchi.....Kwenye safari ya kuja Kenya kuna madada hatari sana na wakali wa kudance waliachwa kitendo kilichowakera dancers wengine akiwemo Pamela yule aliyepigwa teke.....
Pamela yeye bwana ni mropokaji hasa na hakusita kuzinguana na Cindy .......Pale airport sasaaaaa Cindy si akamfuata Pamela na kumuambia amsaidie kubeba begi, Pamela akachomoa kisha akamuongelea shombo Cindy na si unajua wale wanawake tena,basi walirushiana maneno kiasi cha kuchapana makofi,hali iliyofanya Koffi afikishiwe taarifa......Uamuzi wa Koffi ulikuwa mmoja tu,kumfuata Pamela kumsema na inasemekana Pamela aliambiwa baada ya kumalizika kwa tamasha lile yeye kazi basi.....Kama kawaida Pamela hakai na neno kifuani akaongea mbovu kwa Koffi....Unajua kilichofuata...NDO LILE TEKE.....
KWAHIYO UKIANGALIA NA KUFUATILIA KWA MAKINI SANA TATIZO NI HILO KUJIHUSISHA NA MAPENZI NA MFANYAKAZI WAKO,UNAMPA CHEO ILI AWAONGOZE WALE WALE ALIOKUWA ANAFANYA NAO KAZI LINE MOJA,WENGINE WAKO JUU YAKE NA WENGINE WAKO CHINI YAKE....
NI JAMBO LA KAWAIDA KUWA KUNA WAFANYAKAZI WENZIE WALIKUWA WAKIMZIDI SANA KIUTENDAJI JE UNADHANI WATARIDHIKA????NI KAWAIDA KUWA WATAKUWA NA KINYONGO NA MAMBO KAMA TAFRANI LAZIMA ZITATOKEA....