Mkataba wa Dubai na Tanzania kuhalalisha Kambi 88 za Masetla wa Kiarabu nchini Tanzania?

Mkataba wa Dubai na Tanzania kuhalalisha Kambi 88 za Masetla wa Kiarabu nchini Tanzania?

Mleta uzi ana hoja usiibeze, sualalakuifanya Kigali kuwa Dubai in africa ina miaka kadha takribani 15 hivi,lengo si kumpenda Paulo au kuwapenda Wanyarwanda lengo DRC nautajiri wake, Tanzania tunakuwa obstacle kwa sababu sisi ni lango, kama hutaki kupisha njia mwenye nguvu atapita na mlango, utababkia kupiga kelele,JPM alipinga kitu hiki sana na alisema nanukuuu " ni mwendawazimu pekee anayeweza kukubalianana mashalti haya" sina hakika kama wenye nguvu walipita na mlango au vipi lakini mleta hoja ana hoja.
 
Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??
Inashangaza sana, unajiita The Boss huku una upeo mdogo kama watoto wa chekechea!.

Mleta mada ametumia neno masetla baada ya kuonesha maeneo ya kimkataba yaliyowapa waarabu mamlaka ya kujitawala ndani ya ardhi ya Tanganyika, ameonesha bandari za maziwa, na bahari.

Ajabu wewe unapinga hoja yake kwa kusema waarabu pia wamewekeza Germany na kwingineko, kwani huko Germany wamepewa mkataba wa hovyo unaowaruhusu waarabu kujitawala ndani ya nchi za wazungu, kama walivyopewa hapa kwetu na serikali yetu?

Halafu kwa huu ujinga wako ndio unawaomba mods waufute uzi!, wewe endelea kuwekeza kwenye udini tu.
 
Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??

Hebu weka bandari za maji wanazo operate UK , zuzu kama wewe tukupe Elimu DP Rwanda na UK wanaendesha bandari kavu sawa na
Mamlaka ya bandari ingewapa waendeshe Kwala ile bandari kavu kwa mkataba wa miaka mitano mitano na kutakua na review kila baada ya muda, sasa wewe na mapoyoyo wenzio kugawa bandari za maji ya bahari na ziwa mnajiona wajanja kumbe hamna kitu
 
"Kambi 88 za masetla" wa kiarabu..
Na mods mnaacha hizi hate speech na uwongo ?
Maxence Melo Paw Cookie

Soma hoja vizuri. Hakuna kauli za chuki hapo, Ni ukweli mtupu. kwa kifupi nimeandika hoja ifuatayo:

1. Kuna wakoloni wa aina mbili, yaani mkoloni wa kimapokeo (traditional colonialism) na mkoloni wa kilowezi (setller colonialism), ambapo, mkoloni wa kimapokeo anafika kwenye koloni ili kuteka rasilimali watu na kuitumia kuvuna maliasili na kuhamisha faida kwa ajili ya kuipeleka katika nchi mkoloni, wakati mkoloni mlowezi anafika kwenye koloni kuteka ardhi, watu na rasilimali zao ili kujenga makazi mapya ya kudumu, ama kwa kuwahamisha wazawa au kuwateketeza.

2. Mkataba wa Tanzania-Dubai umetoa haki ya umiliki wa milele wa haki za matumizi (eternal use ownership rights) ya bandari 88 za Tanzania Bara, na pia umetoa haki ya umiliki wa milele wa haki za kuvuna faida (eternal fruits ownership rights) kutokana na bandari 88 za Tanzania Bara, jambo ambalo linaipa Dubai haki ya kuanzisha makazi ya kudumu katika ardhi ya Tanzania, na hivyo kuwa na sifa ya kuitwa mkoloni mlowezi.

3. Kwa hiyo, nikahitimisha kwamba, Mkataba wa Tanzania-Dubai unafungua milango ya kuanzishwa kwa kambi 88 za walowezi wa Kiarabu nchini Tanzania, ambapo kambi hizo zitakuwa kwenye mwambao wa Pwani na kwenye mmaeneo ya mmaziwa ya Tanganyika, Viktoria na Tanganyika.

Hate speech iko wapi?
Naona unaendelea kujitoa ufahamu.
Na bado naboresha hoja hii.
NItaiandika kwa Kiswahili na Kiingereza ili tuelewane vizuri.
Tulia sindano ikuingie...
 
Dah sasa itakuwaje
JF ondoeni uzushi huu wa kipuuzi, au nanyi mnafaidika na upuuzi huu? Kumbukeni tuna nchi moja na mauaji ya kimbari ya Rwanda yalianza na chuki km hizi na uwongo mwingi uliopaliliwa na vyombo vya habari. Tambueni wajibu wenu km mhimili wa nne wa dola
 
View attachment 2675281

Hofu tuliyo nayo dhidi ya Mkataba wa Tanzania-Dubai inao msingi thabiti katika ubaya unaoambatana na historia ya "makoloni ya walowezi wa kigeni" katika Afrika.

Kwa mujibu wa "TPA Handbook, 2019-20," kwenye ukurasa wa tisa, TPA inasimamia bandari 88 zifuatazo:
  1. Bandari 18 zilizo katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi, zikiwemo bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Kilwa, Lindi, Mafia, Pangani, na Bagamoyo.
  2. Bandari 30 za Ziwa Victoria, zikiwemo Mwanza, Bukoba, Kemondo Bay, Nansio, na Musoma.
  3. Bandari 25 za Ziwa Tanganyika, zikiwemo Kigoma, na Kasanga.
  4. Bandari 15 za Ziwa Nyasa, zikiwemo Itungi, na Mbamba Bay.
Mkataba wa wali uliopitishwa na Bunge unaziweka bandari hizi chini ya Kampuni ya DP World, iliyo mali ya Mfalme wa Dubai. Hatimaye makoloni ya walowezi wa kiarabu yatakuwa kama ramani hapa chini inavyoonyesha.

View attachment 2675295
Ramani ya makoloni ya walowezi wa Kiarabi nchini Tanzania miaka 30 ijayo

Mkataba huo hautaji ukomo wa mahusiano kati ya Tanzania na Dubai. Mikataba ya nyongeza haikuwasilishwa Bungeni ili Wabunge wajue haya ni mapatano ya miaka mingapi.

Sina amani na mkataba huu, hata kama Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, anaendesha elimu ya "kufuta hofu".

Kwa ufupi, hakuna uatata kwamba huu ni mkataba wa kutengeneza "makoloni 88 ya walowezi wa kiarabu" ("88 Arabic settler colonies") nchini Tanzania, kama ilivyokuwa huko Afrika Kusini, kulikokuwa na "European settler colonies"

Kitaalam, "makoloni ya walowezi" (settler colonies) ni makoloni kama makoloni mengine, lakini yanakuwa kama kiraka ndani ya nchi iliyo huru kisiasa katika maeneo baki.

Isipokuwa Ukoloni wa Cape Town, ulioanzishwa mwaka wa 1652, makoloni ya walowezi barani Afrika hayakuanzishwa hadi karne ya 19 na kusababisha utawala wa Wazungu wachache dhidi ya wakazi wengi wa kiasili.

Migogoro kati ya walowezi na wakazi wa eneo hilo ililipuka juu ya rasilimali zinazodaiwa na pande zote mbili, hasa juu ya ardhi.

Mara nyingi, kuondolewa kwa ukoloni kwa makoloni ya walowezi barani Afrika kuliambatana zaidi na migogoro ya kivita. Tuangalie tulikotoka, ili tujua tuko wapi na tunapaswa kwenda wapi.

Makoloni ya walowezi wa Kiarabu ni jambo la kuogopwa kama ukoma. Makoloni ya walowezi wa Kiarabu nchini Tanzania hapana.

Na kama kuna mtu bado hajaelewa mantiki ya hii "hapana" haelewi maana na aina za ukoloni. Basi, namwalika asome ufafanuzi ufuatayo kuhusu swali lifuatalo: Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani? Nalijibu kikamilifu hapa chini.

Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani?

Ukoloni ni hali ambapo nchi moja, ama kwa kutumia nguvu za kijeshi au nguvu za ushawishi wa hoja za kilaghai, hudhubiti nchi nyingine kisiasa, kiutamaduni, kijamii na kiakili, ama kwa asilimia ndogo au kwa asilimia zote, hii ikiwa ni mbinu ya kufanikisha unyonyaji wa kiuchumi.

Wanahistoria wanatofautisha aina kuu mbili za ukoloni.

Kuna, ukoloni unaofanyika kwa mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism).

Na kuna ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache wanaoweka makazi ya muda maalum kwenye ardhi ya koloni (metropolitan colonialism).

Kwa upande mmoja, katika ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache (metropolitan colonialism), nchi moja hutumia nguvu kuidhibiti nchi nyingine kwa kuwatumia wenyeji kufanya kazi za kitumwa katika kuvuna rasilimali zao wenyewe kwa faida ya wakoloni.

Hapa, Taifa linalofanya ukoloni huongeza mali yake kwa kuwatumia wenyeji kama watendakazi wanaolipwa ujira kidogo sana.

Katika utaratibu huu, tofauti na ukoloni wa walowezi, Taifa linalofanya ukoloni hutuma watu wachache kwenye koloni, kama watawala wanaowawakilisha, kama mameneja wa miradi ya kikoloni pekee, bila kuwahamisha wenyeji katika makazi yao.

Ukoloni huu hufanikishwa zaidi kwa njia ya mashamba makubwa, ambapo wakoloni hujikita kwenye madini au zao moja la kibiashara kama vile pamba, kahawa, tumbaku, mpira, au miwa.

Mfano mzuri wa ukoloni wa aina hii umetokea DRC tangu enzi za Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alipoamuru DRC ifanywe koloni lake miaka 1870.

Lakini, ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, kupitia kwa wawakilishi wake wachache (metropolitan colonialism), huweza kutekelezwa kwa njia tofauti.

Mosi, mkoloni huweza kuwakilishwa na magavana kutoka makao makuu ya serikali ya nchi ya mkoloni.

Pili, Serikali ya nchi mkoloni huweza kuunda kampuni ambayo itafika kwenye koloni na kusimamia maslahi ya mkoloni.

Tatu, serikali ya nchi mkoloni inaweza kuteua kampuni ya kimataifa iliyosajiliwa katika nchi nyingine ili kufanya kazi kama wakala wake katika koloni.

Na nne, serikali ya nchi mkoloni huweza kuteua serikali ya nchi nyingine kufanya kazi kama wakala wake katika koloni, lakini serikali wakala ikawa nafanya kazi hizo kupitia kampuni yake ya kibiashara.

Na kwa upande wa pili, katika ukoloni unaofanyika kwa njia ya mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism), kundi kubwa la watu huondoka nchini kwao na kuhamia kwenye nchi nyingine.

Wakiwa katika nchi mpya huweka makazi ya kudumu huko, kujiimarisha kiuchumi kwa kutwaa na kuvuna maliasili walizozikuta, kujijenga kisiasa na kijamii, na hatimaye kuwahamisha, au kuwajumuisha wenyeji katika ustaarabu mpya wa kigeni, au kuwateketeza. Lakini, walowezi hawa hubaki watiifu kwa nchi za kibeberu walikotoka.

Mifano mizuri ya mchi ambazo ni makoloni ya walowezi ni Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini. Katika nchi hizi, wageni waligeuka wakazi wa kudumu, na katika baadhi ya nchi hizi wazawa wakateketezwa kabisa.

Kwa kuangalia maudhui ya kifungu cha 4(1) na kifungu cha 20 kama vikisomwa pamoja na kifungu cha 23(4) ni wazi kwamba, mkataba wa awali wa Tanzania-Dubai unatoa “eternal use ownership rights,” “eternal fruits ownership rights.

Katika utaratibu wa kawaida wa miammala ya kiuchumi, hakuna kitu kama “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights.” Kilichopo, na kinachopaswa kuwepo ni “temporay use ownership rights” au “temporary fruits ownership rights” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Hivyo, kutaja “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights” katika mkataba ni sawa na kutoa “substantive ownership rights,” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Chini ya mkataba huu naiona Tanzania ikianza safari ya kugeuka koloni la walowezi wa Kiarabu kama ilivyotokea huko Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini, japo walowezi wa huko hawaku wa waarabu.

Tunapinga jambo hili kwa nguvu zote.

Nimeambatanisha Handbook (2019/20) hapa chini.
we hata siku yako ya kuzaliwa inatakiwa ilaaniwe kwa upuuzi wako huu. Una pepo wewe siyo bure. Watanzania mpuuzeni mpuuzi km huyu
 
Boss huoni kuwa mleta mada ana hoja? Kumilikisha waarabu bandari zote hizo kwa mkataba usiojulikana ukomo wake unaelewa maana yake?
na we ni zuzu km yeye, yaani mtu mpumbavu akueleze jambo la kipumbavu na we unamkubalia? Mwishowe anakudharau anakuona zuzu tu. Sahivi anasoma comment kupima mazuzu yaliyoingia ktk upuuzi wake.
 
Watu wanagombania mfumo dah inatisha sana kampuni ambayo ipo nchi nyingi ulaya ije ilete ukoloni Tanzania sema tu ukweli mleta Uzi kuwa una hofu na uislam kupewa nguvu na waarabu na mfumo wenu uliotengenezwa kwa miaka mingi kukosa nguvu hapa kila mtu anatetea maslah yake akitawala raisi mkristu inakuwa Tanzania akitawala mwislam inageuka kuwa Tanganyika duh
mkuu umechanganyikiwa? wewe mambo ya uislamu/ukristo/utanganyika umeyasoma wapi kwenye hilo bandiko?
 
JF ondoeni uzushi huu wa kipuuzi, au nanyi mnafaidika na upuuzi huu? Kumbukeni tuna nchi moja na mauaji ya kimbari ya Rwanda yalianza na chuki km hizi na uwongo mwingi uliopaliliwa na vyombo vya habari. Tambueni wajibu wenu km mhimili wa nne wa dola

Hakiondoki kitu. Nanyumbulisha hoja hapa chini ili akili ikuingie:

Kwa kifupi nimeandika hoja ifuatayo:

1. Kuna wakoloni wa aina mbili, yaani mkoloni wa kimapokeo (traditional colonialism) na mkoloni wa kilowezi (setller colonialism), ambapo, mkoloni wa kimapokeo anafika kwenye koloni ili kuteka rasilimali watu na kuitumia kuvuna maliasili na kuhamisha faida kwa ajili ya kuipeleka katika nchi mkoloni, wakati mkoloni mlowezi anafika kwenye koloni kuteka ardhi, watu na rasilimali zao ili kujenga makazi mapya ya kudumu, ama kwa kuwahamisha wazawa au kuwateketeza.

2. Mkataba wa Tanzania-Dubai umetoa haki ya umiliki wa milele wa haki za matumizi (eternal use ownership rights) ya bandari 88 za Tanzania Bara, na pia umetoa haki ya umiliki wa milele wa haki za kuvuna faida (eternal fruits ownership rights) kutokana na bandari 88 za Tanzania Bara, jambo ambalo linaipa Dubai haki ya kuanzisha makazi ya kudumu katika ardhi ya Tanzania, na hivyo kuwa na sifa ya kuitwa mkoloni mlowezi.

3. Kwa hiyo, nikahitimisha kwamba, Mkataba wa Tanzania-Dubai unafungua milango ya kuanzishwa kwa kambi 88 za walowezi wa Kiarabu nchini Tanzania, ambapo kambi hizo zitakuwa kwenye mwambao wa Pwani na kwenye mmaeneo ya mmaziwa ya Tanganyika, Viktoria na Tanganyika.
 
Back
Top Bottom