Mkataba wa Dubai na Tanzania kuhalalisha Kambi 88 za Masetla wa Kiarabu nchini Tanzania?

Mkataba wa Dubai na Tanzania kuhalalisha Kambi 88 za Masetla wa Kiarabu nchini Tanzania?

Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??
Ishu si kusema tu "mbona hata kule......... DP World wako?"

Unajua terms and conditions (mikataba) waliyoingia na nchi hizi unazozitaja? Je, ni sawa na terms & conditions zinaowaingiza hapa Tanganyika...?

Ungesema "...mbona hata UK, USA au Rwanda au Kenya na kwingineko DP World wako na mikataba ni kama huu huu wa kwetu".. ungeleeweka...

Please leteni hoja na sio viroja vyenu hapa....
 
Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??
Rwanda na German kuna CCM na Bunge la Tulia!!??
 
View attachment 2675281

Hofu tuliyo nayo dhidi ya Mkataba wa Tanzania-Dubai inao msingi thabiti katika ubaya unaoambatana na historia ya "makoloni ya walowezi wa kigeni" katika Afrika.

Kwa mujibu wa "TPA Handbook, 2019-20," kwenye ukurasa wa tisa, TPA inasimamia bandari 88 zifuatazo:
  1. Bandari 18 zilizo katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi, zikiwemo bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Kilwa, Lindi, Mafia, Pangani, na Bagamoyo.
  2. Bandari 30 za Ziwa Victoria, zikiwemo Mwanza, Bukoba, Kemondo Bay, Nansio, na Musoma.
  3. Bandari 25 za Ziwa Tanganyika, zikiwemo Kigoma, na Kasanga.
  4. Bandari 15 za Ziwa Nyasa, zikiwemo Itungi, na Mbamba Bay.
Mkataba wa wali uliopitishwa na Bunge unaziweka bandari hizi chini ya Kampuni ya DP World, iliyo mali ya Mfalme wa Dubai. Hatimaye makoloni ya walowezi wa kiarabu yatakuwa kama ramani hapa chini inavyoonyesha.

View attachment 2675295
Ramani ya makoloni ya walowezi wa Kiarabi nchini Tanzania miaka 30 ijayo

Mkataba huo hautaji ukomo wa mahusiano kati ya Tanzania na Dubai. Mikataba ya nyongeza haikuwasilishwa Bungeni ili Wabunge wajue haya ni mapatano ya miaka mingapi.

Sina amani na mkataba huu, hata kama Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, anaendesha elimu ya "kufuta hofu".

Kwa ufupi, hakuna uatata kwamba huu ni mkataba wa kutengeneza "makoloni 88 ya walowezi wa kiarabu" ("88 Arabic settler colonies") nchini Tanzania, kama ilivyokuwa huko Afrika Kusini, kulikokuwa na "European settler colonies"

Kitaalam, "makoloni ya walowezi" (settler colonies) ni makoloni kama makoloni mengine, lakini yanakuwa kama kiraka ndani ya nchi iliyo huru kisiasa katika maeneo baki.

Isipokuwa Ukoloni wa Cape Town, ulioanzishwa mwaka wa 1652, makoloni ya walowezi barani Afrika hayakuanzishwa hadi karne ya 19 na kusababisha utawala wa Wazungu wachache dhidi ya wakazi wengi wa kiasili.

Migogoro kati ya walowezi na wakazi wa eneo hilo ililipuka juu ya rasilimali zinazodaiwa na pande zote mbili, hasa juu ya ardhi.

Mara nyingi, kuondolewa kwa ukoloni kwa makoloni ya walowezi barani Afrika kuliambatana zaidi na migogoro ya kivita. Tuangalie tulikotoka, ili tujua tuko wapi na tunapaswa kwenda wapi.

Makoloni ya walowezi wa Kiarabu ni jambo la kuogopwa kama ukoma. Makoloni ya walowezi wa Kiarabu nchini Tanzania hapana.

Na kama kuna mtu bado hajaelewa mantiki ya hii "hapana" haelewi maana na aina za ukoloni. Basi, namwalika asome ufafanuzi ufuatayo kuhusu swali lifuatalo: Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani? Nalijibu kikamilifu hapa chini.

Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani?

Ukoloni ni hali ambapo nchi moja, ama kwa kutumia nguvu za kijeshi au nguvu za ushawishi wa hoja za kilaghai, hudhubiti nchi nyingine kisiasa, kiutamaduni, kijamii na kiakili, ama kwa asilimia ndogo au kwa asilimia zote, hii ikiwa ni mbinu ya kufanikisha unyonyaji wa kiuchumi.

Wanahistoria wanatofautisha aina kuu mbili za ukoloni.

Kuna, ukoloni unaofanyika kwa mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism).

Na kuna ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache wanaoweka makazi ya muda maalum kwenye ardhi ya koloni (traditional colonialism).

Kwa upande mmoja, katika ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache (traditional colonialism), nchi moja hutumia nguvu kuidhibiti nchi nyingine kwa kuwatumia wenyeji kufanya kazi za kitumwa katika kuvuna rasilimali zao wenyewe kwa faida ya wakoloni.

Hapa, Taifa linalofanya ukoloni huongeza mali yake kwa kuwatumia wenyeji kama watendakazi wanaolipwa ujira kidogo sana.

Katika utaratibu huu, tofauti na ukoloni wa walowezi, Taifa linalofanya ukoloni hutuma watu wachache kwenye koloni, kama watawala wanaowawakilisha, kama mameneja wa miradi ya kikoloni pekee, bila kuwahamisha wenyeji katika makazi yao.

Ukoloni huu hufanikishwa zaidi kwa njia ya mashamba makubwa, ambapo wakoloni hujikita kwenye madini au zao moja la kibiashara kama vile pamba, kahawa, tumbaku, mpira, au miwa.

Mfano mzuri wa ukoloni wa aina hii umetokea DRC tangu enzi za Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alipoamuru DRC ifanywe koloni lake miaka 1870.

Lakini, ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, kupitia kwa wawakilishi wake wachache (traditional colonialism), huweza kutekelezwa kwa njia tofauti.

Mosi, mkoloni huweza kuwakilishwa na magavana kutoka makao makuu ya serikali ya nchi ya mkoloni.

Pili, Serikali ya nchi mkoloni huweza kuunda kampuni ambayo itafika kwenye koloni na kusimamia maslahi ya mkoloni.

Tatu, serikali ya nchi mkoloni inaweza kuteua kampuni ya kimataifa iliyosajiliwa katika nchi nyingine ili kufanya kazi kama wakala wake katika koloni.

Na nne, serikali ya nchi mkoloni huweza kuteua serikali ya nchi nyingine kufanya kazi kama wakala wake katika koloni, lakini serikali wakala ikawa nafanya kazi hizo kupitia kampuni yake ya kibiashara.

Na kwa upande wa pili, katika ukoloni unaofanyika kwa njia ya mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism), kundi kubwa la watu huondoka nchini kwao na kuhamia kwenye nchi nyingine.

Wakiwa katika nchi mpya huweka makazi ya kudumu huko, kujiimarisha kiuchumi kwa kutwaa na kuvuna maliasili walizozikuta, kujijenga kisiasa na kijamii, na hatimaye kuwahamisha, au kuwajumuisha wenyeji katika ustaarabu mpya wa kigeni, au kuwateketeza. Lakini, walowezi hawa hubaki watiifu kwa nchi za kibeberu walikotoka.

Mifano mizuri ya mchi ambazo ni makoloni ya walowezi ni Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini. Katika nchi hizi, wageni waligeuka wakazi wa kudumu, na katika baadhi ya nchi hizi wazawa wakateketezwa kabisa.

Kwa kuangalia maudhui ya kifungu cha 4(1) na kifungu cha 20 kama vikisomwa pamoja na kifungu cha 23(4) ni wazi kwamba, mkataba wa awali wa Tanzania-Dubai unatoa “eternal use ownership rights,” “eternal fruits ownership rights.

Katika utaratibu wa kawaida wa miammala ya kiuchumi, hakuna kitu kama “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights.” Kilichopo, na kinachopaswa kuwepo ni “temporay use ownership rights” au “temporary fruits ownership rights” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Hivyo, kutaja “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights” katika mkataba ni sawa na kutoa “substantive ownership rights,” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Chini ya mkataba huu naiona Tanzania ikianza safari ya kugeuka koloni la walowezi wa Kiarabu kama ilivyotokea huko Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini, japo walowezi wa huko hawaku wa waarabu.

Tunapinga jambo hili kwa nguvu zote.

Nimeambatanisha Handbook (2019/20) hapa chini.
Hadi Mama Amon unapinga?

Sijui huko ccm wamepewa nini hadi wakakubali hayo mambo.

Nimeamini Waarabu ni wachawi sana.

Majini is real
 
Watu wanagombania mfumo dah inatisha sana kampuni ambayo ipo nchi nyingi ulaya ije ilete ukoloni Tanzania sema tu ukweli mleta Uzi kuwa una hofu na uislam kupewa nguvu na waarabu na mfumo wenu uliotengenezwa kwa miaka mingi kukosa nguvu hapa kila mtu anatetea maslah yake akitawala raisi mkristu inakuwa Tanzania akitawala mwislam inageuka kuwa Tanganyika duh
Kwa nini mnaingiza dini? Magufuli alipingwa yeye pamoja na usukuma wake, Hadi leo bado wasukuma wanapingwa

Nyie hiyo dini yenu imewafanya muwe inferior, kila jambo mnahisi dini yenu inashambuliwa
 
na we ni zuzu km yeye, yaani mtu mpumbavu akueleze jambo la kipumbavu na we unamkubalia? Mwishowe anakudharau anakuona zuzu tu. Sahivi anasoma comment kupima mazuzu yaliyoingia ktk upuuzi wake.
Hoja hujibiwa kwa hoja na si viroja. Ukishajiona katika mjadala wa kikubwa unachoweza kuchangia ni matusi tu basi ujijue wewe hamna kila kitu. Huwezi kupewa nafasi mbele ya wanaojielewa.
 
Watu wanagombania mfumo dah inatisha sana kampuni ambayo ipo nchi nyingi ulaya ije ilete ukoloni Tanzania sema tu ukweli mleta Uzi kuwa una hofu na uislam kupewa nguvu na waarabu na mfumo wenu uliotengenezwa kwa miaka mingi kukosa nguvu hapa kila mtu anatetea maslah yake akitawala raisi mkristu inakuwa Tanzania akitawala mwislam inageuka kuwa Tanganyika duh
Unafikiri huko Ulaya wameingia mkataba wakijinga kama wetu
 
Kuna watu humu wanachuki mbaya sana na waarabu, ndio maana hawaendelei.
Nenda sehemu alizokaa Mwarabu kipindi kile hakuna maendeleo yoyote. Aje akuletee maendeleo sasa hivi?
Shinyanga mjini, Nzega, Pwani, Singida nenda Mtwara, Morogoro, Lindi hadi Zanzibar. Kama utakuta maendeleo.
Mwarabu akikusaidia sana atakujengea msikiti na kukuchimbia kisima cha kujitawazia
 

Hofu tuliyo nayo dhidi ya Mkataba wa Tanzania-Dubai inao msingi thabiti katika ubaya unaoambatana na historia ya "makoloni ya walowezi wa kigeni" katika Afrika.

Kwa mujibu wa "TPA Handbook, 2019-20," kwenye ukurasa wa tisa, TPA inasimamia bandari 88 zifuatazo:
  1. Bandari 18 zilizo katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi, zikiwemo bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Kilwa, Lindi, Mafia, Pangani, na Bagamoyo.
  2. Bandari 30 za Ziwa Victoria, zikiwemo Mwanza, Bukoba, Kemondo Bay, Nansio, na Musoma.
  3. Bandari 25 za Ziwa Tanganyika, zikiwemo Kigoma, na Kasanga.
  4. Bandari 15 za Ziwa Nyasa, zikiwemo Itungi, na Mbamba Bay.
Mkataba wa wali uliopitishwa na Bunge unaziweka bandari hizi chini ya Kampuni ya DP World, iliyo mali ya Mfalme wa Dubai. Hatimaye makoloni ya walowezi wa kiarabu yatakuwa kama ramani hapa chini inavyoonyesha.

Ramani ya makoloni ya walowezi wa Kiarabi nchini Tanzania miaka 30 ijayo

Mkataba huo hautaji ukomo wa mahusiano kati ya Tanzania na Dubai. Mikataba ya nyongeza haikuwasilishwa Bungeni ili Wabunge wajue haya ni mapatano ya miaka mingapi.

Sina amani na mkataba huu, hata kama Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, anaendesha elimu ya "kufuta hofu".

Kwa ufupi, hakuna uatata kwamba huu ni mkataba wa kutengeneza "makoloni 88 ya walowezi wa kiarabu" ("88 Arabic settler colonies") nchini Tanzania, kama ilivyokuwa huko Afrika Kusini, kulikokuwa na "European settler colonies"

Kitaalam, "makoloni ya walowezi" (settler colonies) ni makoloni kama makoloni mengine, lakini yanakuwa kama kiraka ndani ya nchi iliyo huru kisiasa katika maeneo baki.

Isipokuwa Ukoloni wa Cape Town, ulioanzishwa mwaka wa 1652, makoloni ya walowezi barani Afrika hayakuanzishwa hadi karne ya 19 na kusababisha utawala wa Wazungu wachache dhidi ya wakazi wengi wa kiasili.

Migogoro kati ya walowezi na wakazi wa eneo hilo ililipuka juu ya rasilimali zinazodaiwa na pande zote mbili, hasa juu ya ardhi.

Mara nyingi, kuondolewa kwa ukoloni kwa makoloni ya walowezi barani Afrika kuliambatana zaidi na migogoro ya kivita. Tuangalie tulikotoka, ili tujua tuko wapi na tunapaswa kwenda wapi.

Makoloni ya walowezi wa Kiarabu ni jambo la kuogopwa kama ukoma. Makoloni ya walowezi wa Kiarabu nchini Tanzania hapana.

Na kama kuna mtu bado hajaelewa mantiki ya hii "hapana" haelewi maana na aina za ukoloni. Basi, namwalika asome ufafanuzi ufuatayo kuhusu swali lifuatalo: Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani? Nalijibu kikamilifu hapa chini.

Ukoloni ni kitu gani na sio kitu gani?

Ukoloni ni hali ambapo nchi moja, ama kwa kutumia nguvu za kijeshi au nguvu za ushawishi wa hoja za kilaghai, hudhubiti nchi nyingine kisiasa, kiutamaduni, kijamii na kiakili, ama kwa asilimia ndogo au kwa asilimia zote, hii ikiwa ni mbinu ya kufanikisha unyonyaji wa kiuchumi.

Wanahistoria wanatofautisha aina kuu mbili za ukoloni.

Kuna, ukoloni unaofanyika kwa mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism).

Na kuna ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache wanaoweka makazi ya muda maalum kwenye ardhi ya koloni (traditional colonialism).

Kwa upande mmoja, katika ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, lakini kupitia kwa wawakilishi wake wachache (traditional colonialism), nchi moja hutumia nguvu kuidhibiti nchi nyingine kwa kuwatumia wenyeji kufanya kazi za kitumwa katika kuvuna rasilimali zao wenyewe kwa faida ya wakoloni.

Hapa, Taifa linalofanya ukoloni huongeza mali yake kwa kuwatumia wenyeji kama watendakazi wanaolipwa ujira kidogo sana.

Katika utaratibu huu, tofauti na ukoloni wa walowezi, Taifa linalofanya ukoloni hutuma watu wachache kwenye koloni, kama watawala wanaowawakilisha, kama mameneja wa miradi ya kikoloni pekee, bila kuwahamisha wenyeji katika makazi yao.

Ukoloni huu hufanikishwa zaidi kwa njia ya mashamba makubwa, ambapo wakoloni hujikita kwenye madini au zao moja la kibiashara kama vile pamba, kahawa, tumbaku, mpira, au miwa.

Mfano mzuri wa ukoloni wa aina hii umetokea DRC tangu enzi za Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alipoamuru DRC ifanywe koloni lake miaka 1870.

Lakini, ukoloni unaofanyika bila mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye koloni, kupitia kwa wawakilishi wake wachache (traditional colonialism), huweza kutekelezwa kwa njia tofauti.

Mosi, mkoloni huweza kuwakilishwa na magavana kutoka makao makuu ya serikali ya nchi ya mkoloni.

Pili, Serikali ya nchi mkoloni huweza kuunda kampuni ambayo itafika kwenye koloni na kusimamia maslahi ya mkoloni.

Tatu, serikali ya nchi mkoloni inaweza kuteua kampuni ya kimataifa iliyosajiliwa katika nchi nyingine ili kufanya kazi kama wakala wake katika koloni.

Na nne, serikali ya nchi mkoloni huweza kuteua serikali ya nchi nyingine kufanya kazi kama wakala wake katika koloni, lakini serikali wakala ikawa nafanya kazi hizo kupitia kampuni yake ya kibiashara.

Na kwa upande wa pili, katika ukoloni unaofanyika kwa njia ya mkoloni kuweka makazi ya kudumu kwenye ardhi ya koloni, yaani ukoloni wa walowezi (settler colonialism), kundi kubwa la watu huondoka nchini kwao na kuhamia kwenye nchi nyingine.

Wakiwa katika nchi mpya huweka makazi ya kudumu huko, kujiimarisha kiuchumi kwa kutwaa na kuvuna maliasili walizozikuta, kujijenga kisiasa na kijamii, na hatimaye kuwahamisha, au kuwajumuisha wenyeji katika ustaarabu mpya wa kigeni, au kuwateketeza. Lakini, walowezi hawa hubaki watiifu kwa nchi za kibeberu walikotoka.

Mifano mizuri ya mchi ambazo ni makoloni ya walowezi ni Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini. Katika nchi hizi, wageni waligeuka wakazi wa kudumu, na katika baadhi ya nchi hizi wazawa wakateketezwa kabisa.

Kwa kuangalia maudhui ya kifungu cha 4(1) na kifungu cha 20 kama vikisomwa pamoja na kifungu cha 23(4) ni wazi kwamba, mkataba wa awali wa Tanzania-Dubai unatoa “eternal use ownership rights,” “eternal fruits ownership rights.

Katika utaratibu wa kawaida wa miammala ya kiuchumi, hakuna kitu kama “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights.” Kilichopo, na kinachopaswa kuwepo ni “temporay use ownership rights” au “temporary fruits ownership rights” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Hivyo, kutaja “eternal use ownership rights” au “eternal fruits ownership rights” katika mkataba ni sawa na kutoa “substantive ownership rights,” zinazohusu bandari zetu 88, kwa Mfamle wa Dubai, kupitia kampuni yake ya DP World.

Chini ya mkataba huu naiona Tanzania ikianza safari ya kugeuka koloni la walowezi wa Kiarabu kama ilivyotokea huko Kanada, Amerika, Australia, Kenya, Argentina, New Zealand na Afrika Kusini, japo walowezi wa huko hawaku wa waarabu.

Tunapinga jambo hili kwa nguvu zote.

Nimeambatanisha Handbook (2019/20) hapa chini.
Kilichoandikwa hapo ni ushuzi mtupu.
 
Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??
Mkataba wetu una tofauti kubwa na wa hizo nchi ulizozitaja hapo juu mkuu
 
Back
Top Bottom