Mkataba wa IGA Ulitengenezwa Kuwa na Vipengele Hasi kwa Tanzania, na Viongozi Wetu Walijua na Kushiriki Uhujumu Huo

Hakuna anayepinga uwekezaji. Muhimu transparency.
 
Serikali ya Tanzania imeingiwa mkataba na Jimbo au kampuni ya DP World? Kulikuwa na umuhimu gani kufanya hii IGA? Kwanini, kuna umuhimu gani tujifunge kwenye vipengele fulani?

Nakubaliana na wewe kwenye paragraph yako ya mwisho
 
Hao viongozi wana kinga gani ya kutoshitakiwa kwa kuhujumu nchi? Muda ndio huu sio mpaka baadaye ndio waje washitakiwe wakiwa hawapo madarakani kama kina yona na mramba
 
Unaifahamu VIEITE wewe ?
Jibu sahihi hapa ni HAPANA, tena iliyokolezwa kabisa!

Nchi yetu hii imefika hapa, na sisi wananchi tukicheka tu na hawa nyani wanaovuruga shamba letu?
 
Hao viongozi wana kinga gani ya kutoshitakiwa kwa kuhujumu nchi? Muda ndio huu sio mpaka baadaye ndio waje washitakiwe wakiwa hawapo madarakani kama kina yona na mramba
Hapa 'stelingi' wa sinema ndiye mhusika wa mradi, na anayokinga kisheria asishitakiwe wakati wowote.
Hawa vidagaa ya aina ya akina Mramba na huyo Yona, hivi vinapewa maagizo tu na huyo stelingi.
 
Serikali ya Tanzania imeingiwa mkataba na Jimbo au kampuni ya DP World? Kulikuwa na umuhimu gani kufanya hii IGA? Kwanini, kuna umuhimu gani tujifunge kwenye vipengele fulani?

Nakubaliana na wewe kwenye paragraph yako ya mwisho
Kampuni ya DP World ipo katika jimbo la Dubai. IGA imekwenda bungeni ili kuipa kinga na uhalali biashara yenyewe.

Hii sio kampuni ya kitoto, inakuja kuwekeza kwenye masuala ya upakuaji na upakiaji wa makasha pale TPA, inakuja kukuza uelewa wa wanafunzi wa masuala ya bandari kwa ujumla pale DMI.
 
Issue ni kwamba IGA inatufunga kwenye migogoro, utatuzi wa migogoro. Tukienda mahakamani kwa hii IGA tutashindwa kesi zote.

Ni msingi mbaya sana wa mkataba wowote hata wako binafsi.

Kwanini tuingie IGA na Jimbo, kampuni binafsi? IGA ya hovyo? USA,UK walifanya hivyo?
 
Kwanini IGA ya jimbo itufunge?, una uhakika hii ni IGA ya kwanza kusainiwa na Tanzania?, mbona hazijatufunga hizo IGA nyingine?.

Punguzeni huu unabii wa majanga usiolisaidia taifa kwa namna yoyote ile.
 
Kwanini IGA ya jimbo itufunge?, una uhakika hii ni IGA ya kwanza kusainiwa na Tanzania?, mbona hazijatufunga hizo IGA nyingine?.

Punguzeni huu unabii wa majanga usiolisaidia taifa kwa namna yoyote ile.
1. Tuoneshe muda wa kuisha huo mkataba?
2. Kama taifa litanufaikaje na huo mkataba?
 
1. Tuoneshe muda wa kuisha huo mkataba?
2. Kama taifa litanufaikaje na huo mkataba?
Ukomo upo kwenye project contracts IGA haiwezi kuandikwa ukomo. Ni mradi wenye mawanda ya utekelezaji [scope] hivyo kila eneo lina mkataba wake wa utekelezaji.

Taifa litanufaika kupitia teknolojia ya ushushaji na upakiaji wa mizigo wa melini, foleni itaondoka kabisa pia upitishaji wa madawa ya kulevya utaondolewa, tukumbuke wanayo mitambo ya kubaini biashara hizo haramu.

Taifa litafaidika kwa kuongeza elimu ya wataalam wa masuala ya bandari tulionao, watafanya kazi kwa ushirikiano na chuo cha masuala ya bandari DMI, na kwenye mkataba wameandikiwa hivyo.
 
Kinachoendelea ni ufisadi wala hauonekani ni mkataba bali ni makubaliano tu.
1. Mkataba hauna ukomo, kama kila eneo lina mkataba mbona halioneshi muda wa kuisha kwa mkataba kwa kila eneo?
2. Hauoneshi watanzania watanufaikaje bali sijui teknolojia, sijui machines, sijui kupitisha madawa ni maelezo ya kitoto kabisa uliyoandika. Madawa ya kulevya yalishaundiwa tume na timu ya kutosha kushughulikia hili kipindi cha magufuli. Hakuna kitu kama hicho
3. Serikali inanufaikaje na huo mkataba feki?Ni upigaji tu unaoendelea
Nyie viongozi, wananchi wa watanzania siyo wale ya miaka 1970 hawa wanaelewa kwahiyo mnachozungumza au kuandika mkitazame sana.
Haya maelezo uliyoandika ni ufisadi unaoendelea Tanzania. Sijashawishika kukubali maelezo yako
 
Boss,
CCM unawajua au una wasikia tu? Likija suala la maslahi yao binafsi kushinda kesi ni ngumu, kumbuka wamevuta pesa kwa DP world , wengine watakuwa na share kwenye hiyo kampuni, so mahakama usitegemee sana utashangazwa vibaya sana.

CCM haiwezi kuleta maebdeleo hata wakiwekeza kila kitu, Havana hiyo akili, hivi wewe unaona Samia kuna lolote anaelewa kweli? Huyo ni Rais wa kufanya basic things kama kumualika kwenye makongamano huko ndo anaweza.
 
Jitahidi uelewe ili usitumiwe kama condom halafu ukatupwa na kusahaulika.

Mikataba yenye ukomo ni ile ya utekelezaji wa biashara, huwezi kuwepo ukomo kwenye mkataba unaopita bungeni.

Ukomo unawekwa kwenye mikataba ya kibiashara sio kwa ule mkataba mama unaopita bungeni.

Serikali inanufaika kwa ongezeko la mapato yanayokatwa kodi na TRA pamoja na kuwepo ufanisi unaokwenda kuondoa foleni za ushushaji na upakiaji wa makontena.

Utoto ni wa kwako ambaye hujui chochote kuhusu bandari na unairukia mada kwa sababu ya wepesi wa kuingia kwenye mijadala hapa JF.

Kutoridhika kwako na maelezo yangu hayo ni matatizo yako binafsi. Haupo uwezekano wa serikali kumridhisha kila mtu, upeo wetu wa akili unatofautiana.
 
Wacha kupotosha. Serikali kupitia Mradi wake na WB ishafanya maboresho hayo ya miundombinu. Anachokuja kukifanya DP W ni uendeehaji tu.
Taifa litafaidika kwa kuongeza elimu ya wataalam wa masuala ya bandari tulionao,
Serikali ishakuwa ikitoa elikunkwa Wataalamu waliopo. DP.W inakuja(hope not) kuendesha tu
Usipotoshe
watafanya kazi kwa ushirikiano na chuo cha masuala ya bandari DMI

, na kwenye mkataba wameandikiwa hivyo.
Mkataba gani huo, kama sio mkataba wa World bank? Sasa unaunganisha unganisha kuaminisha DP world ndio inayoenda kufanya hivyo.....huko ni kupotosha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…