Mkataba wa IGA Ulitengenezwa Kuwa na Vipengele Hasi kwa Tanzania, na Viongozi Wetu Walijua na Kushiriki Uhujumu Huo

Mkataba wa IGA Ulitengenezwa Kuwa na Vipengele Hasi kwa Tanzania, na Viongozi Wetu Walijua na Kushiriki Uhujumu Huo

Jitahidi uelewe ili usitumiwe kama condom halafu ukatupwa na kusahaulika.

Mikataba yenye ukomo ni ile ya utekelezaji wa biashara, huwezi kuwepo ukomo kwenye mkataba unaopita bungeni.

Ukomo unawekwa kwenye mikataba ya kibiashara sio kwa ule mkataba mama unaopita bungeni.

Serikali inanufaika kwa ongezeko la mapato yanayokatwa kodi na TRA pamoja na kuwepo ufanisi unaokwenda kuondoa foleni za ushushaji na upakiaji wa makontena.

Utoto ni wa kwako ambaye hujui chochote kuhusu bandari na unairukia mada kwa sababu ya wepesi wa kuingia kwenye mijadala hapa JF.

Kutoridhika kwako na maelezo yangu hayo ni matatizo yako binafsi. Haupo uwezekano wa serikali kumridhisha kila mtu, upeo wetu wa akili unatofautiana.
Ni kweli mnatutumia km condom kwa uongozi wa CCM. Bado haujanishawishi kuukubali huu mkataba.
Mkataba wenyewe wa milele hauna ukomo. Km hauna ukomo kwa maana hiyo bandari ishauzwa hivyo.
1. Hizo gharama za kuendesha bandari, kununua vifaa winchi, camera, kuajiri watu n.k inaweza kuzidi gharama ya kununua ndege 5 za ATCL?
2. Hakuna njia au ubunifu wa kufanya ili kuziendeleza rasilimali zetu tofauti na uwekezaji?
Ubinafsishaji, sioni faida yoyote zaidi ya kuwafanya wananchi waishi maisha magumu. Mfano Gesi ya Mtwara kwa tamaa zenu za ubinafshaji leo mtungi wa kati unajazwa kwa elfu 57. Hakuna unafuu wowote
Leo hii vifurushi vya data vipo juu kulinganisha na vipato vya wananchi. Hata TTCL tulitegemea iwe mkombozi nalo linatunyonya, huduma mbovu, laini hazipatikani, vocha hakuna, vifurushi vipo juu.
Unatetea huo mkataba wa milele kwasababu tayari meshachukua asilimia zenu.
Hii DP world ikipita, kodi zitapanda kwasababu hamna sehemu za kupata kipato cha kuongoza hii nchi, mtarudi kubuni mbinu ya kuwakamua wananchi ili serikali ipate hela.
Dhahabu, almasi, Tanzanite na gesi zote mebinafsisha na matokeo yake hamna sehemu za kupata hela, mkakimbilia kuweka tozo kwenye miamala ya simu.
Mkimaliza kuuza bandari, mtakuja na tozo au kodi mpya kwa ajili kuwakamua wananchi kwasababu hakuna mapato tena.
Viongozi wa Tanzania wanawaza wanufaishe matumbo yao, kubinafsisha na kubuni mbinu za kodi na tozo ili kuchukua visenti vya wananchi hawawazi watumie njia gani ili waendeleze rasilimali za Tanzania. Hamuwezi kuanzisha mradi wowote mkafanikiwa kwasababu ya rushwa na ufisadi wenu.
Ndiyo maana miradi yote iliyoanzishwa na serikali yote inapumulia mashine. ATCL, TTCL n.k hasara tu
Utasema nchi inaongozwa kwa kodi, sikatai hata Nyerere alisema "anatamani kila mwananchi alipe kodi ila utawatoza nini?" Mtu anauza mchicha unataka alipe 20,000 ili apate kibali cha kuuza.
Nyie viongozi, mjitafakari mnavyoongea au kuandika, watu sasa wameelimika.
 
Jitahidi uelewe ili usitumiwe kama condom halafu ukatupwa na kusahaulika.

Mikataba yenye ukomo ni ile ya utekelezaji wa biashara, huwezi kuwepo ukomo kwenye mkataba unaopita bungeni.

Ukomo unawekwa kwenye mikataba ya kibiashara sio kwa ule mkataba mama unaopita bungeni.

Serikali inanufaika kwa ongezeko la mapato yanayokatwa kodi na TRA pamoja na kuwepo ufanisi unaokwenda kuondoa foleni za ushushaji na upakiaji wa makontena.

Utoto ni wa kwako ambaye hujui chochote kuhusu bandari na unairukia mada kwa sababu ya wepesi wa kuingia kwenye mijadala hapa JF.

Kutoridhika kwako na maelezo yangu hayo ni matatizo yako binafsi. Haupo uwezekano wa serikali kumridhisha kila mtu, upeo wetu wa akili unatofautiana.
Ujinga ni mzigo mzito sana, mtu anapokuwa nao anadhani kila mtu kabeba mzigo kama alivyoubeba yeye.

Kutokana na jinsi ulivyohangaika na swala hili la Bandari tokea mwanzo, ni wazi kabisa kwamba umewekeza sana kwenye jambo hili.
Matokeo yake sasa, hata unayoendelea kutetea humu kuhusu jambo lenyewe unashindwa kutambua kwamba unazidi kujionyesha ujinga ulionao juu ya swala lenyewe, wakati ukidhani kurudia mara kwa mara ujinga huo huo utawafanya na watu wengine wawe wajinga kama wewe.

Sasa sijui mwishoni utafikia wapi na jambo hili ambalo sasa ni wazi kwamba ni hujuma mahsusi iliyofanyiwa taifa letu.
 
Ujinga ni mzigo mzito sana, mtu anapokuwa nao anadhani kila mtu kabeba mzigo kama alivyoubeba yeye.

Kutokana na jinsi ulivyohangaika na swala hili la Bandari tokea mwanzo, ni wazi kabisa kwamba umewekeza sana kwenye jambo hili.
Matokeo yake sasa, hata unayoendelea kutetea humu kuhusu jambo lenyewe unashindwa kutambua kwamba unazidi kujionyesha ujinga ulionao juu ya swala lenyewe, wakati ukidhani kurudia mara kwa mara ujinga huo huo utawafanya na watu wengine wawe wajinga kama wewe.

Sasa sijui mwishoni utafikia wapi na jambo hili ambalo sasa ni wazi kwamba ni hujuma mahsusi iliyofanyiwa taifa letu.
Nikiwa mzalendo niliyeishi nchi hii tangu awamu ya kwanza mpaka ya sita ninayo haki ya kuipigania ili ifaidike na uwekezaji wenye lengo la kuondoa wapigaji wote wa pale TPA.

Huu ni wajibu wa msingi kabisa, nikiwa mtanzania niliyemuona Mwalimu Nyerere live akihutubia katika viwanja vya ikulu miaka ile ya themanini mwanzoni ninao wajibu wa kimaadili wa kuipigania nchi hii iweze kuondoka katika mikono ya mafisadi na madalali wao kina Kalamu.
 
Ni kweli mnatutumia km condom kwa uongozi wa CCM. Bado haujanishawishi kuukubali huu mkataba.
Mkataba wenyewe wa milele hauna ukomo. Km hauna ukomo kwa maana hiyo bandari ishauzwa hivyo.
1. Hizo gharama za kuendesha bandari, kununua vifaa winchi, camera, kuajiri watu n.k inaweza kuzidi gharama ya kununua ndege 5 za ATCL?
2. Hakuna njia au ubunifu wa kufanya ili kuziendeleza rasilimali zetu tofauti na uwekezaji?
Ubinafsishaji, sioni faida yoyote zaidi ya kuwafanya wananchi waishi maisha magumu. Mfano Gesi ya Mtwara kwa tamaa zenu za ubinafshaji leo mtungi wa kati unajazwa kwa elfu 57. Hakuna unafuu wowote
Leo hii vifurushi vya data vipo juu kulinganisha na vipato vya wananchi. Hata TTCL tulitegemea iwe mkombozi nalo linatunyonya, huduma mbovu, laini hazipatikani, vocha hakuna, vifurushi vipo juu.
Unatetea huo mkataba wa milele kwasababu tayari meshachukua asilimia zenu.
Hii DP world ikipita, kodi zitapanda kwasababu hamna sehemu za kupata kipato cha kuongoza hii nchi, mtarudi kubuni mbinu ya kuwakamua wananchi ili serikali ipate hela.
Dhahabu, almasi, Tanzanite na gesi zote mebinafsisha na matokeo yake hamna sehemu za kupata hela, mkakimbilia kuweka tozo kwenye miamala ya simu.
Mkimaliza kuuza bandari, mtakuja na tozo au kodi mpya kwa ajili kuwakamua wananchi kwasababu hakuna mapato tena.
Viongozi wa Tanzania wanawaza wanufaishe matumbo yao, kubinafsisha na kubuni mbinu za kodi na tozo ili kuchukua visenti vya wananchi hawawazi watumie njia gani ili waendeleze rasilimali za Tanzania. Hamuwezi kuanzisha mradi wowote mkafanikiwa kwasababu ya rushwa na ufisadi wenu.
Ndiyo maana miradi yote iliyoanzishwa na serikali yote inapumulia mashine. ATCL, TTCL n.k hasara tu
Utasema nchi inaongozwa kwa kodi, sikatai hata Nyerere alisema "anatamani kila mwananchi alipe kodi ila utawatoza nini?" Mtu anauza mchicha unataka alipe 20,000 ili apate kibali cha kuuza.
Nyie viongozi, mjitafakari mnavyoongea au kuandika, watu sasa wameelimika.
Kuuita mkataba ni wa milele tayari ni kielelezo cha kutoelewa nini kimepitishwa bungeni.

Yote uliyoandika baada ya hapo ni sawa na bure yaani ni sawa na kuupaka rangi upepo.
 
Wacha kupotosha. Serikali kupitia Mradi wake na WB ishafanya maboresho hayo ya miundombinu. Anachokuja kukifanya DP W ni uendeehaji tu.

Serikali ishakuwa ikitoa elikunkwa Wataalamu waliopo. DP.W inakuja(hope not) kuendesha tu
Usipotoshe



Mkataba gani huo, kama sio mkataba wa World bank? Sasa unaunganisha unganisha kuaminisha DP world ndio inayoenda kufanya hivyo.....huko ni kupotosha
Ukiwa umefuata kilichoandikwa na website ya World Bank tayati umepotoshwa na wewe. Benki ya dunia haikumtaka DP World achukue uendeshaji wa bandari yetu.

Wakaja na taarifa ya kutengeneza ya kwamba pesa imetoka Marekani wakati ni upotoshaji tu kama mwingine wowote ule.
 
Sote tuanelewa kwamba nchi yetu Rais ni kila kitu kwetu, hahojiwi na mbaya zaidi huwezi kumshtaki mahakama yoyote nchini, akiwa madarakani au baada ya kuachia madaraka.

Wananchi wa nchi hii wamezoea, kwamba hawawezi kumwajibisha kiongozi huyo kwa njia yoyote ile; na Bunge ambalo sheria inaruhusu kumwajibisha jinsi wawakilishi wa Bunge hilo wanavyopatikana kwa fadhira za mtu huyo huyo mmoja (Rais), halina uwezo wa kumwajibisha mtu huyu.

Bila shaka yoyote, Rais wetu Samia yote haya aliyajua, na hasa baada ya kuona ni namna gani mtangulizi wake alivyokanyaga kila kitu kutimiza matakwa yake.
Kwa hiyo Samia hakuwa na hana hofu yoyote juu ya kufanya aliyonuia kuyafanya siku nyingi, kama angepata fursa hiyo ya kuyafanya

Kwa bahati nzuri kwake, na mbaya kwetu wengine fursa hiyo ikamwangukia bila ya mategemeo yoyote

Sasa anatimiza alichonuia toka siku nyingi.
Hapa nataka kuonyesha mambo yaliyofanyika, kwa maksudi, tokea mwanzo alipochukua uongozi wa nchi ili kufanikisha lengo lake la kuiumiza nchi yetu. Nitaorodhesha mambo aliyoyafanya au kutoyafanya ili kufanikisha IGA hii iliyoletwa kwetu ifanikiwe. Kumbuka wakati wote, yeye anajua hakuna lolote wananchi wanaloweza kufanya kumzuia au kumuwajibisha sasa au baadae.

1. Uteuzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali katika eneo husika, na kuwaondoa viongozi ambao hawakukidhi mahitaji yake. Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara, Wakurugenzi TPA na kwingineko. Sitataja majina, kwani wanafahamika.
Hawa ni watu maalum walioteuliwa kuhakikisha lengo la IGA (mbovu) linafanikiwa.

2. Kufanya viini macho ili kupoteza lengo.
Paliwahi kuwepo mjadala wa kufufua mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, na yeye Rais aliwahi kueleza kuwa kuna timu ya majadiliano na waChina. Hili halikufika mbali, kabla ya kugeukia kwenye ujenzi wa hatua za mwanzo sisi wenyewe.

Wakati haya yakiendelea, imebainika sasa kwamba DPWorld tayari walikuwa kwenye kibarua cha kutengeneza IGA na wataalam wetu hapa ambao haijulikani walipatikana kwa mpango upi kushughulikia kazi hiyo. Bila shaka ni sahihi pia kusema kuwa ni watu walioaminiwa kutengeneza kitu alichokitaka mteuzi wao kwenye nafasi hiyo.

3. TICTS - abaki/asibaki? moja ya viini macho kuzuga watu, bila shaka hata wao TICTS hawakujua hatma yao itakuwa vipi. Wakati wote huu wa sintofahamu, DP World na wataalam wetu wapo kazini wakisuka IGA ya kutukomesha sisi.
4. Mara BUUUUU! DP World anaingia kwa kishindo kikubwa. Sasa ndipo watu wanaanza kuunganisha doti
Bendera yetu na picha ya Rais wetu juu ya jengo refu kabisa duniani; mara fununu za viongozi kwenda kwenye EXPO Dubai kimya kimya na Rais kukaa huko kwa siri kubwa, kumbe anatia saini mkataba wa kutuuza!

5. Mkataba unavujishwa? Juhudi kubwa zinaanza kufukia mahandaki. Hapana, huo siyo Mkataba, hayo ni "Makubaliano tu, ikiambatana na upotoshaji mwingi mwingine, toka kwa waziri na mtu mwingine aliyeaminiwa sana kusimamia kujua kilichomo ndani ya Mkataba/Makubaliano" hayo. Mtaalam wa sheria mbobezi (tunaambiwa), Hamza Johari ndiye mkuu wa timu. Watu wanajiuliza, na Mwanasheria mkuu wa Serikali alishiriki vipi hadi kufika kwenye hatua hii?
Mwanasheria Mkuu wa Serikali hasemi kitu, bali kukanusha tu kwamba "Bandari haijauzwa". Hakuna anayejua kiwango cha ushiriki wake kwenye mkataba huo, na kama yeye, kwa nafasi yake anakubaliana na yaliyomo kwenye mkataba. Sijasikia akisema lolote juu ya hayo.

6. Taratibu na Hatua sahihi za kuingia mikataba kama huu (IGA) - Je, sisi kama taifa tunao utaratibu wowote tuliojiwekea wa kuingia kwenye mikataba kama hii? Huu siyo mkataba wa kwanza Tanzania iliouingia, je hiyo mingine kulifanyika mambo gani ambayo yamezoeleka kufanywa, lakini safari hii ikawa ni tofauti?

Hili ni swali lililo wazi, kama kuna utaratibu maalum, je ulifuatwa, hata kwa kiasi fulani tu?
jambo la kwanza linaloniingia akilini ni "Vikao vya Baraza la Mawaziri". Kwa mtizamo wangu, jambo kubwa kama hili haliwezi kufanyika bila ya uwepo wa angalao kikao cha Mawaziri kulijadili..
Vikao hivi vya Baraza la Mawaziri siku hizi vimekuwa kama ni siri kubwa sana, hata kule kutaja tu kulikuwepo na kikao siku hizi ni nadra sana, hata bila ya kutaja yaliyojadiliwa kwenye kikao hicho.
Kwa hiyo hili ni swali tu kuuliza kama kulikuwa na kikao cha kujadili, au kujulishwa tu kwamba kuna mpango wa ujio wa DP World na hatua zilizokuwa zikifanyika kuwakaribisha hapa.
Kama Mawaziri nao hawakuwa na habari, hilo litakuwa jambo la kushangaza sana linaloongeza uzito katika hoja za andiko hili.
7. Ushirikishwaji wa Bunge katika "kuridhia Mkataba" Bila shaka yoyote palikuwepo na mpango kabambe wa kulishirikisha Bunge katika kufanya hujuma hizi, siyo kwa nia njema bali kwa nia ovu..
a) Kundi la wabunge lililopelekwa Dubai, ni utaratibu upi uliotumika kuwachagua hao waliokwenda? Wanazo sifa maalum ambazo zingewawezesha kutambua mambo ambayo hayana manufaa kwetu?
b) Waliandaliwa na kupewa semina wajiandae kuhusu maswala nyeti katika kazi wanayokwenda kuifanya huko walikokwenda? Walipewa Mkataba wausome wajue yaliyomo kabla hawajaondoka hapa?
Hawa wabunge ni akina nani hasa?

Kama maswali yote haya hayana majibu, maana yake ni kwamba hii ilikuwa ni mbinu tu, iliyotegeshwa kuhalalisha maovu juu ya nchi yetu, maovu waliyoyajua walioandaa mkataba huo na washirika wao wote.
c) Bungeni wakati wa kikao cha Bunge, ni wabunge wapi waliopewa nafasi ya kujadili yaliyomo kwenye mkataba, na ni nani aliyetoa nafasi hiyo kwa wabunge hao maalum? Hawa wabunge walijua kilichokuwemo kwenye huo Mkataba? Mbona hta mmoja wao hakujitokeza na anagalao kutaja tu hata kifungu kimoja alichokuwa nacho mashaka? Hawa wote waliandaliwa kwa maksudi kwa ushirikiano na uongozi wa Bunge?
d) Ushirikiwa wananchi, wanapewa masaa 24 kuleta maoni yao. Maana ya hili ni kwamba hapakutakiwa kuwepo na mchango wa wananchi ili lengo la kuhujumu nchi litekelezwe.

DPWorld wanao uzoefu mkubwa sana katika maswala haya ya Mikataba, kwa sababu kila sehemu walikokwenda wamekutana na chngamoto chungu nzima zilizowakabili.
Wamekuja hapa kwetu, wakamkuta mkuu wetu aliye tayari kabisa kuwapokea kwa masharti waliyoyapenda wao. Mkuu wetu hana uzoefu wowote, na isitoshe hana uchungu mkubwa kuhusu nchi anayoiongoza yeye, ila anayo madaraka ya kufanya lolote analotaka bila kuwajibishwa na yeyote.

Hapa ndipo tulipofikia sasa hivi.

Ingekuwa ni nchi nyingine, Mkataba huu usingemwacha huyu mkuu abaki salama, tena akiendelea kwenye madaraka yake kana kwamba hakuna lolote lililofanyika.
Lakini hii ni Tanzania. Yeye kishasema "Ameziba masikio", wenye kupiga kelele wapige kelele hadi wachoke wenyewe; lakini DP World hakuna wa kumzuia kuja hapa.

SAWA.
Sasa tumebaki na moja tu tunaloweza kulitegemea kuondokana na hujuma hii juu ya nchi yetu.
Je, tunaweza kumpata kichaa mwingine (bila ya baadhi ya mambo ya aliyetangulia mbele ya safari) atuondolee uchafu huu ndani ya nchi yetu? (Bila kujali hasara tutakayoingia kwa kuvunja mkataba (kwani kuendelea na mkataba wa aina hii ni hasara kubwa zaidi ya kulipa hiyo fidia tutakayodaiwa).
Na kwa kuwa ni 'kichaa', bila shaka baadhi ya hawa wahujumu watachukuliwa hatua bila ya kuwaonea aibu.

IGA baina ya Tanzania na Dubai ni hujuma iliyo andaliwa maksudi kuihujumu Tanzania.

N.B. Sikutegemea na wala siyo kawaida yangu kuandika gazeti, lakini leo acha iwe hivyo, kwani hakuna namna.

Samahani kwa makosa ya kiuandishi kama yamo kwenye andiko hili..
Walikuwa wanawaza wanamtengenezea Magufuli huo mkataba
 
Nikiwa mzalendo niliyeishi nchi hii tangu awamu ya kwanza mpaka ya sita ninayo haki ya kuipigania ili ifaidike na uwekezaji wenye lengo la kuondoa wapigaji wote wa pale TPA.
Kwa kukusoma tangia umeingia humu JF kwa jina hili, utakuwa ni tapeli wa hali ya juu sana kujitangazia sifa hiyo uliyojitangazia mwenyewe katika mistari hiyo miwili.
Of course, kila mtu anayo haki ya kujitangazia lolote apendalo mwenyewe, hiyo ni haki yako.

Kuhusu "...swala la wapigaji wote wa pale TPA", sidhani kuwa wewe na hao mnaoshriki katika mkataba huu wa DP World; kuwa hilo ndilo lengo lenu kuu, ila ni kisababu tu kizuri mojawapo cha kukitumia kuhalalisha lengo kubwa nyuma ya mkataba wenyewe.

Na kama huelewi ngoja nikufanyie mhtasari: ukilinganisha hasara inayosababishwa na hao wapigaji wa pale TPA na hujuma hii mnayolifanyia taifa letu, ni mara mia nchi ibaki na visamaki hivyo vya TPA kuliko nyie mapapa wa hujuma.
Hivyo vidagaa vya TPA tunao uwezo sisi wenyewe, hapa hapa kuvishughulikia na kuviondoshea mbali, kuliko huu mkataba wa kitumwa mnaotafuta kutuingiza kwa hujuma zenu tu kwa taifa letu.

Imenilazimu nikujibu, kwa sababu unarudiarudia ujinga huu wa upotoshaji, kana kwamba sisi wengine wote tunafurahia hali hiyo ya hapo TPA.
 
Hoja kwa sasa iwe ni kuchunguza hawa watu wamepewa nini na sio tena ubovu wa mkataba kwani ni wazi huu mkataba ni mbovu kupindukia.
Una akili kubwa sana mkuu, Lissu aliwataja baadhi kama mbunge msukuma kuwa waliipewa rushwa na wengine ambao hawajakanusha tuhuma hizo mahakamani kuwa wamechafuliwa jina, hii ni dharihi kuwa hawa watu wamepokea hongo na sasa ni wakati wa kujua ni kiasi gani walihongwa na kwangu mimi wananchi tunatakiwa tuwaadhibu kama vibaka kwa kuwachoma moto
 
Kwa kukusoma tangia umeingia humu JF kwa jina hili, utakuwa ni tapeli wa hali ya juu sana kujitangazia sifa hiyo uliyojitangazia mwenyewe katika mistari hiyo miwili.
Of course, kila mtu anayo haki ya kujitangazia lolote apendalo mwenyewe, hiyo ni haki yako.

Kuhusu "...swala la wapigaji wote wa pale TPA", sidhani kuwa wewe na hao mnaoshriki katika mkataba huu wa DP World; kuwa hilo ndilo lengo lenu kuu, ila ni kisababu tu kizuri mojawapo cha kukitumia kuhalalisha lengo kubwa nyuma ya mkataba wenyewe.

Na kama huelewi ngoja nikufanyie mhtasari: ukilinganisha hasara inayosababishwa na hao wapigaji wa pale TPA na hujuma hii mnayolifanyia taifa letu, ni mara mia nchi ibaki na visamaki hivyo vya TPA kuliko nyie mapapa wa hujuma.
Hivyo vidagaa vya TPA tunao uwezo sisi wenyewe, hapa hapa kuvishughulikia na kuviondoshea mbali, kuliko huu mkataba wa kitumwa mnaotafuta kutuingiza kwa hujuma zenu tu kwa taifa letu.

Imenilazimu nikujibu, kwa sababu unarudiarudia ujinga huu wa upotoshaji, kana kwamba sisi wengine wote tunafurahia hali hiyo ya hapo TPA.
Nchi haiwezi kubaki na visamaki wakati teknolojia za kisasa kabisa zipo. Samia kakataa hujuma za wachache wanaowafanya wengi wajinga, Mtalia na kusaga meno lakini upigaji hapo TPA ndio umefika mwisho.

Mkataba hauna utumwa wowote kama unaielewa vyema mantiki nzima ya IGA na HGA zinazokwenda kujadiliwa na wadau wa bandari.

Tunawadhulumu sana wadau halisi wa bandari kwa kuendekeza siasa zetu za mijadala mingi isiyobadilisha chochote katika mienendo ya biashara zao.
 
Nikiwa mzalendo niliyeishi nchi hii tangu awamu ya kwanza mpaka ya sita ninayo haki ya kuipigania ili ifaidike na uwekezaji wenye lengo la kuondoa wapigaji wote wa pale TPA.

Huu ni wajibu wa msingi kabisa, nikiwa mtanzania niliyemuona Mwalimu Nyerere live akihutubia katika viwanja vya ikulu miaka ile ya themanini mwanzoni ninao wajibu wa kimaadili wa kuipigania nchi hii iweze kuondoka katika mikono ya mafisadi na madalali wao kina Kalamu.
Hii fani ya "kuigiza" haifai kabisa kwako. Nakushauri uachane nayo moja kwa moja.
 
Nchi haiwezi kubaki na visamaki wakati teknolojia za kisasa kabisa zipo. Samia kakataa hujuma za wachache wanaowafanya wengi wajinga, Mtalia na kusaga meno lakini upigaji hapo TPA ndio umefika mwisho.

Mkataba hauna utumwa wowote kama unaielewa vyema mantiki nzima ya IGA na HGA zinazokwenda kujadiliwa na wadau wa bandari.

Tunawadhulumu sana wadau halisi wa bandari kwa kuendekeza siasa zetu za mijadala mingi isiyobadilisha chochote katika mienendo ya biashara zao.
Kama ilivyo kawaida yako unajifanya kujisahaulisha kinachozungumziwa kwenye mkataba ni nini.
Peleka hadaa hiyo kwingine siyo kwangu
 
Hao viongozi wana kinga gani ya kutoshitakiwa kwa kuhujumu nchi? Muda ndio huu sio mpaka baadaye ndio waje washitakiwe wakiwa hawapo madarakani kama kina yona na mramba
Hawastahili kushitakiwa mbona wezi wa kuku tunawachoma moto hawa wanatakiwa tuwapige moto mchana kweupe
 
Nchi haiwezi kubaki na visamaki wakati teknolojia za kisasa kabisa zipo. Samia kakataa hujuma za wachache wanaowafanya wengi wajinga, Mtalia na kusaga meno lakini upigaji hapo TPA ndio umefika mwisho.

Mkataba hauna utumwa wowote kama unaielewa vyema mantiki nzima ya IGA na HGA zinazokwenda kujadiliwa na wadau wa bandari.

Tunawadhulumu sana wadau halisi wa bandari kwa kuendekeza siasa zetu za mijadala mingi isiyobadilisha chochote katika mienendo ya biashara zao.
Acha ujinga wewe rubbish
 
Hii fani ya "kuigiza" haifai kabisa kwako. Nakushauri uachane nayo moja kwa moja.
Nimekulia maeneo ya gymkhana, karimjee na ikulu nikiwaona wanasiasa kina Samuel Sitta, Nalaila Kiula na wengi wakubwa serikalini.

Sio muigizaji kama unavyodhani ni mzalendo halisi.
 
Kama ilivyo kawaida yako unajifanya kujisahaulisha kinachozungumziwa kwenye mkataba ni nini.
Peleka hadaa hiyo kwingine siyo kwangu
Kila kilichomo kwenye mkataba uliopita bungeni mnakipotosha halafu mkiambiwa ukweli mnasema eti ni hadaa. Hovyo kabisa.
 
Nimekulia maeneo ya gymkhana, karimjee na ikulu nikiwaona wanasiasa kina Samuel Sitta, Nalaila Kiula na wengi wakubwa serikalini.

Sio muigizaji kama unavyodhani ni mzalendo halisi.
Mkuu, mimi sina uwezo wa kuhoji ulizaliwa na kukulia wapi. Uwezo huo sina.

Ninachojua na kutokuwa na wasiwasi nacho ni maandishi yako mengi humu JF tangia ulipoingia ukitumia jina hili la 'Steve Joel Ntamusana'.
Maandishi yako yanajieleza vizuri kabisa kuweza kutambua wewe ni mtu wa aina gani hata bila ya kujitangazia sifa hiyo unayotaka watu wakutambue nayo.
 
Kila kilichomo kwenye mkataba uliopita bungeni mnakipotosha halafu mkiambiwa ukweli mnasema eti ni hadaa. Hovyo kabisa.
Hapa unatufanya sisi tusiwe na akili timamu na uelewa wa tunachokisoma ndani ya mkataba huo, huoni kwamba utakuwa na upungufu mkubwa akilini mwako?

Halafu hata unadiriki kusema "mkataba uliopita bungeni..."!

Huyu ndiye "mzalendo" tunayepaswa kumtambua ndani ya nchi hii!
 
Back
Top Bottom