Naiusia nafsi yangu pamoja na kuwausia ndugu zangu katika kujitahidi juu ya hili. Duniani tunapita na makazi yetu ni akhera hivyo tujitahidi katika njia ambazo zitatufikisha.
Hakika utukufu ni kutafuta radhi za Allaah kwa kujikurubisha katika ibada zake hasa hizi ambazo si wengi wanazifanya. Kwani m bora wa watu ni Yule mwenye kumcha Mwenyezimungu na si vinginevyo.
MWENYEZIMUNGU ndiye mjuzi zaidi