Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Na mimi sikwenda hata darasa moja la Uandishi, kwa nini nyinyi wahariri hamuoni hivyo vitu?
mwandishi naye ameshangaa kuoana hawa wawili wakiwa wanapigania mambo yanayofanana lakini wakiwa na itikadi tofauti.
Nilikubaliana na Kithuku kwamba Mama alipoanza kumpigia debe Baba unaweza kusema plausibly kwamba ilikuwa ni aina ya usanii.
Mh. Dr. Slaa, niajuavyo ni kweli aliwahi kugombea ubunge kupitia CCM, kamati kuu kwenye kuchuja majina wajumbe wengi walitaka Dr. Slaa apewe hiyo nafasi kwa sababu CCM wana kamati ya kutathmini hali ya jimbo ambapo hufanya utafiti wa hali ya juu sana kwamba nani anayekubalika katika lile jimbo, na hii huwa ni kazi ya makamu wa mwenyekiti wa CCM.
Mapendekezo yao kwa kamati kuu ya CCM, ilikuwa ni DR. Slaa ndiye anayekubalika katika lile jimbo, la Karatu. Kati ya majina ya wagombea kulikuwa na jina la rafiki wa karibu wa mwenyekiti wa CCM then, Mkapa, kama sikosei alikuwa ni Quaresi, kikao kilimalizika na hayo makubaliano kuwa DR. Slaa ndiye apewe ile nafasi kwa tiketi ya CCM, lakini Mkapa akaamua kutumia ubabe wake na kumpitisha rafiki yake over chaguo la wananchi wa Karatu na kamati kuu ya CCM, DR. Slaa,
Ndipo DR. Slaa akaamua kugombea ubunge kwa kupitia Chadema na akashinda ushindi wa kishindo, tena sio mara moja so far na hajawahi since then kurudi CCM, na amekuwa nyota njema kwa taifa kwa sababu ya kuweza kuwafichua mafisadi wengi kutoka chama chake cha zamani CCM, ni majuzi tu hapa niliona baadhi mambers wakimtaka Nape kuhamia Upinzani, baada ya kuamini kuwa ameonewa kule CCM,
Sasa naomba kuuliza what is this topic all about, maana so far sijaelewa vizuri?Kwamba mke wa Dr. slaa ni lazima naye awe na siasa za upinzani au? Hiyo inapswa kuwa ni sheria au maneno ya mtaaani tu ambayo hapa JF tunayakataa sana!
Mh. Dr. Slaa, niajuavyo ni kweli aliwahi kugombea ubunge kupitia CCM, kamati kuu kwenye kuchuja majina wajumbe wengi walitaka Dr. Slaa apewe hiyo nafasi kwa sababu CCM wana kamati ya kutathmini hali ya jimbo ambapo hufanya utafiti wa hali ya juu sana kwamba nani anayekubalika katika lile jimbo, na hii huwa ni kazi ya makamu wa mwenyekiti wa CCM.
Mapendekezo yao kwa kamati kuu ya CCM, ilikuwa ni DR. Slaa ndiye anayekubalika katika lile jimbo, la Karatu. Kati ya majina ya wagombea kulikuwa na jina la rafiki wa karibu wa mwenyekiti wa CCM then, Mkapa, kama sikosei alikuwa ni Quaresi, kikao kilimalizika na hayo makubaliano kuwa DR. Slaa ndiye apewe ile nafasi kwa tiketi ya CCM, lakini Mkapa akaamua kutumia ubabe wake na kumpitisha rafiki yake over chaguo la wananchi wa Karatu na kamati kuu ya CCM, DR. Slaa,
Ndipo DR. Slaa akaamua kugombea ubunge kwa kupitia Chadema na akashinda ushindi wa kishindo, tena sio mara moja so far na hajawahi since then kurudi CCM, na amekuwa nyota njema kwa taifa kwa sababu ya kuweza kuwafichua mafisadi wengi kutoka chama chake cha zamani CCM, ni majuzi tu hapa niliona baadhi mambers wakimtaka Nape kuhamia Upinzani, baada ya kuamini kuwa ameonewa kule CCM,
Sasa naomba kuuliza what is this topic all about, maana so far sijaelewa vizuri?Kwamba mke wa Dr. slaa ni lazima naye awe na siasa za upinzani au? Hiyo inapswa kuwa ni sheria au maneno ya mtaaani tu ambayo hapa JF tunayakataa sana!
Kwa ujumla hawa jamaa (Rose na Wilbroad) ni wasanii, wanawachezea akili wairaqw huko Karatu, na hakika wamefanikiwa! Huyu mama anatudanganya "anachukia" CHADEMA, chama ambacho mumewe ni Katibu Mkuu. Hapohapo tunafahamu kuwa huyo Dr Slaa aligombea ubunge kupitia CCM mwaka 1995 wakamwondoa "kimizengwe" licha ya kuwa alishinda kwenye kura za maoni, na ndiyo sababu pekee iliyomfanya akimbilie CHADEMA. Nadhani hata ile kadi ya CCM bado Wilbroad anayo. Nawasifu hawa jamaa kwa maigizo, hakika wamebobea!
Kithuku , you are not being reasonable at all .Comments kama hizi sikutegemea zitoke kwako mkuu .Duh!!! am kweli
Tukirudi kwenye topiki ninachosema ni kwamba Dr Slaa na mkewe wanafuata utashi wao zaidi kuliko chama, na wanafuata sauti na imani ambazo katika hali halisi si lazima zikawa za vyama vyao, wako more committed to themselves kuliko kwenye vyama (hata hayo mambo ya "public interest" wanayofanya, nakiri ni mema sana, lakini faida bado zinarudi kwao binafsi). Wako wajanja sana katika kulinda himaya zao. Hiyo kuwa kwenye vyama tofauti ililetwa tu na mazingira, haikuwa mpango wao toka awali maana wote walikuwa CCM. Bila shaka Dr Slaa alijadili na mama baada ya ile mizengwe aliyofanyiwa kwenye CCM, wakakubaliana basi baba aende CHADEMA. Ile hali ya kuwa baba CHADEMA na mama CCM inawasaidia kama "buffer system" ya kuwahakikishia kama familia kuwa maslahi yao yako salama, na kikubwa ni kuwa wamefanikiwa kuufanya umma wa Karatu kuwa upande wao, ndio usanii ninaozungumzia.
Mh. Dr. Slaa, niajuavyo ni kweli aliwahi kugombea ubunge kupitia CCM, kamati kuu kwenye kuchuja majina wajumbe wengi walitaka Dr. Slaa apewe hiyo nafasi kwa sababu CCM wana kamati ya kutathmini hali ya jimbo ambapo hufanya utafiti wa hali ya juu sana kwamba nani anayekubalika katika lile jimbo, na hii huwa ni kazi ya makamu wa mwenyekiti wa CCM.
Mapendekezo yao kwa kamati kuu ya CCM, ilikuwa ni DR. Slaa ndiye anayekubalika katika lile jimbo, la Karatu. Kati ya majina ya wagombea kulikuwa na jina la rafiki wa karibu wa mwenyekiti wa CCM then, Mkapa, kama sikosei alikuwa ni Quaresi, kikao kilimalizika na hayo makubaliano kuwa DR. Slaa ndiye apewe ile nafasi kwa tiketi ya CCM, lakini Mkapa akaamua kutumia ubabe wake na kumpitisha rafiki yake over chaguo la wananchi wa Karatu na kamati kuu ya CCM, DR. Slaa,
Ndipo DR. Slaa akaamua kugombea ubunge kwa kupitia Chadema na akashinda ushindi wa kishindo, tena sio mara moja so far na hajawahi since then kurudi CCM, na amekuwa nyota njema kwa taifa kwa sababu ya kuweza kuwafichua mafisadi wengi kutoka chama chake cha zamani CCM, ni majuzi tu hapa niliona baadhi mambers wakimtaka Nape kuhamia Upinzani, baada ya kuamini kuwa ameonewa kule CCM,
Sasa naomba kuuliza what is this topic all about, maana so far sijaelewa vizuri?Kwamba mke wa Dr. slaa ni lazima naye awe na siasa za upinzani au? Hiyo inapswa kuwa ni sheria au maneno ya mtaaani tu ambayo hapa JF tunayakataa sana!
Mke wa Dk. Slaa awa kivutio mkutanoni
Na Burhani Yakub
MBUNGE wa Jimbo la Karatu kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbrod Slaa na mkewe Rose Kamili, ambaye ni diwani wa Kata ya Basotu wilayani Hanang kwa tiketi ya CCM, ni wapinzani wa kisiasa, lakini wanashirikiana katika kufichua ufisadi kama ilivyodhihirika mwishoni mwa wiki.
Akiiwakilisha asasi isiyo ya kiserikali ya Pingo inayofanya kazi zake chini ya programu ya PETS katika mkutano wa wadau wa maendeleo wa Pact, mke huyo wa katibu wa Chadema alisisimua wengi alipoeleza jinsi alivyofichua kiasi cha Sh119.8 milioni ambacho hakikutumika kukarabati vituo saba vya afya wilayani Hanang.
Alisema wakati wakitekeleza jukumu walilopewa wajumbe wa asasi ya Pingo kuchunguza matumizi ya ruzuku ya serikali zinazopelekwa katika halmshauri ya Wilaya ya Hanang, uongozi uliwapa nyaraka zenye taarifa za kughushi.
Diwani huyo alisema mbali ya kutoa taarifa ya kughushi, uongozi huo wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ulimtuma afisa maendeleo ya jamii kupeleleza kinachofanyika wakati wa kuchunguza matumizi ya fedha za serikali ili kutafuta njia za kuficha ukweli.
Baada ya kugundua hilo, nilitumia nafasi yangu ya udiwani kwenda halmashauri kuomba taarifa za matumizi ya fedha, lakini hata mimi nilinyimwa ndipo nikaenda nyumbani kupekua mafaili ya vikao vya Full Council tukagundua kumbe walitupa taarifa feki, alisema Rose.
Alisema baada ya kufanya uchunguzi ikabainika kuwa katika mwaka wa fedha wa 2005/2006 Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ilipokea kiasi cha Sh119,880,000 kwa ajili ya ukarabati wa vituo saba vya afya ambavyo hadi walipokuwa wakichunguza mwanzoni Mei 2008 zilikuwa hazijatumika.
Alivitaja vituo ambavyo havikukarabatiwa licha ya halmashauri kuchukua fedha zake kuwa ni Masakta, Bassodesh, Endasak, Gidahababieq, Sirop, Dawr na kituo cha afya cha Katesh.
Baada ya kuchachamaa, mwaka huu halmashauri ilitoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa vituo hivyo. Haijulikani sababu za kuziweka fedha hizo kwa kipindi cha miaka miwili bila kuzitumia.
Diwani huyo machachari alisema licha ya halmashauri kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo vya afya, Pingo imebaini kuwa kiasi cha Sh55,128,000 bado hazijaingizwa kwenye akaunti husika na haifahamiki zimepelekwa wapi na kwa sababu zipi.
"Hili ni jambo ambalo naahidi kulifanyia kazi kwani hatuwezi kukubali kuona wananchi wanacheleweshewa maendeleo kwa makusudi," alisema.
Baada ya kutoa taarifa hiyo ukumbi ulilipuka kelele za shangwe huku wale wanaofahamu uhusiano wake na Dk. Slaa wakijiuliza ni vipi wakaweza kuwa kitu kimoja wakati wanatofautiana kiitikadi.
"Mimi siipendi kabisa Chadema na kwenye eneo langu la udiwani nahakikisha wafuasi wa CCM hawarubuniwi kuhama. Lakini nipo pamoja na Dk. Slaa katika suala zima analofanya la kufichua mafisadi," alisema Kamili.
"Mume wangu ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake."
Mkutano huo ulioandaliwa na Pets kwa kushirikiana na Pact Tanzania na Shirika la Misaada la Marekani (Usaid) na mfuko wa rais wa Marekani wa Millenium Challenge ulifayika kwa siku mbili na kushiriki wajumbe wa asasi mbalimbali kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani
source: mwananchi
Big up FM. Nionavyo mimi Dr. Silaa si kwamba anatafuta umaarufu. alichokuwa anatafuta whether through CCM or any other Chama cha siasa ni kutaka kuwa heard katika harakati za kupinga ufisadi na maovu mengine Tanzania. Fahamu kuwa Bungeni ni sehemu pekee yenye ulinzi ambayo mtu anaweza kutoa dukuduku lake na Slaa amekuwa akifanya hivyo. Ninaamini hata kama angekuwa CCM babo angetoa dukuduku lake ila sasa hapa ingekuwa hatari maana ungekuta ameshavuliwa uanachama na Ubunge. Kidog tu angalia jinsi ambavyo Anne Kilango anatizamwa kwa jicho la chuki na CCM!!!
Pia Siasa kila mtu ana itikadi yake. Si lazima mke na mume wawe na itikadi moja ya kisiasa. Ila yanapokuja masuala ya familia and other issues mambo ya itikadi za siasa yanawekwa pembeni kabisa. So nakataa kuwa Mr and Mrs. Slaa ati ni wasanii.
Tukae chini tuchambue masuala critically kabla ya kuandika. Ninachofahamu Fisadizs wanatumia kila mbinu kuhakikisha kuwa Dr. Slaa hafurukuti. Kwa Mtanzania mwenye akili timamu ni lazima amheshimu sana Dr. Slaa na michango yake, tena tuwe tayari kumtetea popote pale unaposikia mafisadi au watoto wa mafisadi au ndugu wa mafisadi wakimsema vibaya. Big up and long live dedicated FJ members including Dr. Slaa.
Nakubaliana na aliyesema kwamba hawa ni wasanii, kwa kuwa tu siasa ni sanaa na ukiitumia vyema hii sanaa kwa nia njema na kwa maslahi ya Taifa, sanaa ya siasa haina ubaya.
Mfano, Dk. Slaa alifanya sanaa ya siasa kutoa ile hoja yake bungeni na kuiwasilisha kwa wanananchi katika mkutano wa hadhara baada ya kuona inacheleweshwa na mambo yanazidi kuharibika na matokeo yake, Jk naye akafanya sanaa yake wakawapa wakaguzi wa nje kwa akaunti moja tu ya EPA wakague tena kwa mwaka 2005/2006 tu, bila kujali EPA ilianza zamani na wengi walichota karibu chaguzi zote tokea 1995. Halafu wakafanya sanaa nyingine kwa kuunda Timu ya kina Mwanyika, ambayo nayo baadaye wakaifanyia sanaa nyingine kuiongezea muda, sasa CCM wanafanya sanaa nyingine kumpongeza JK kwa sanaa aliyoifanya katika hotuba yake bungeni kwamba fedha za EPA zitapelekwa kwenye kilimo na watakaoshindwa kurudisha hadi Oktoba 31 watafikishwa mahakamani, ikiwa na maana watakaolipa wamepona!!! Tunasubiri sanaa nyingine.
Kama Dk. Slaa alifanya sanaa baada ya kutoswa na CCM akaingia Chadema, matunda yake tumeyaona na wengine waige kufanya hiyo sanaa, wahame CCM waingie upinzani na huko wafanya kazi ya kutetea wananchi na si matumbo yao, hapo tutaipongeza hiyo sanaa.
So far wakuu I am lost, what is the argument hapa? Eti kweli hapa kuna a serious debate inayoweza kulisaidia taifa letu, na matatizo ya sisi wananchi au?
Dr. Slaa amefanya kazi nzuri sana ya kuwaibua mafisadi na hakuna cha kudebate kuhusiana na hilo. Ila kwa Dr. & Mrs. Slaa as a couple, kupigiana debe licha ya tofauti za vyama vyao inashangaza kidogo na kudadisiwa ni vema kabisa. Hii misimamo yao imetuwezesha kuchunguza na kutafakari kwa undani evolution ya Dr. Slaa toka CCM hadi CHADEMA ambapo inaonyesha sura tofauti kidogo;
1. Dr. Slaa & Mrs.; siasa ndani ya familia ni ajira,
2. Dr. Slaa upinzani wake kwa CCM umetokana na hasira ya kunyimwa nafasi ya uongozi ndani ya CCM na si wa kiitikadi.
Dr. Slaa kiongozi ndani ya CHADEMA ambaye anakubaliana na m'kiti wake 100% bila kuangalia maslahi ya chama na hivyo kutokusaidia chama kuepuka migogoro. Tusimpunje anapostahili sifa lakini tusiache pia kuangalia kwa undani anayofanya maamuzi yake ili tumsadie awe kiongozi bora zaidi
Kwa ujumla hawa jamaa (Rose na Wilbroad) ni wasanii, wanawachezea akili wairaqw huko Karatu, na hakika wamefanikiwa! Huyu mama anatudanganya "anachukia" CHADEMA, chama ambacho mumewe ni Katibu Mkuu. Hapohapo tunafahamu kuwa huyo Dr Slaa aligombea ubunge kupitia CCM mwaka 1995 wakamwondoa "kimizengwe" licha ya kuwa alishinda kwenye kura za maoni, na ndiyo sababu pekee iliyomfanya akimbilie CHADEMA. Nadhani hata ile kadi ya CCM bado Wilbroad anayo. Nawasifu hawa jamaa kwa maigizo, hakika wamebobea!
1.
Mkuu haya maneno yanaweza kuwa na ukweli, iwapo utathibitisha hapa kuwa kabla ya kuwa mbunge, Dr. Slaa alikuwa hana kazi yoyote, lakini kama alikuwa nayo basi hii kauli unahitaji kuifuta, maana ni kumpaka matope Dr. Slaa bila sababu ya msingi politically au iwe personally!
Dr. Slaa ni mzaliwa wa Karatu, sio mgeni wa kutoka jimbo lingine, sasa kama ameona ana uwezo wa kuwasidia wananchi wake, na nafasi ipo kupitia Chadema, what is wrong with that? Yaani unasema sisi wananchi tuache kutafuta njia za kuyasaidia majimbo yetu kwa kuwazikiliza baadhi ya viongozi mafisadi wa CCM?
Kwa hiyo unasema kwua viongozi wote wa upinzani waliowahi kuwa wanachama wa CCM waliondoka kwa hasira kwa sababu walijua kuwa hawana chance ya uongozi kule? Kwa hiyo una maana hawa viongozi ni wasalaiti kama anavyosema Makamba? Alichofanya DR. slaa ndiyo hasa demokrasia yenyewe at work!
Labda uifafanue zaidi hii point!
4.
Migogoro ya siasa ipo katika kila chama cha siasa dunaini haikwepeki, na ndio demokrasia yenyewe, sio kwamba viongozi wa chama cha siasa lazima wakubali tu kila wanachoambiwa na wengine, hapa kwa kweli hatumsaidi Dr. Slaa na anything kama hii ishu, ila ninaamini tumefikia mahali tuna-abuse tu kuwepo kwake hapa JF.
Infact recently tumenza kushindwa kuitumia nafasi ya DR. slaa kisiasa na kuwepo kwake hapa na tumeanza kuitumia nafasi yake na kuwepo kwake hapa kama adhabu kwake, nafikiri tunahitaji kufikiria tena umuhimu wa kuwepo kwake hapa JF na tuweze kuitumia nafasi hiyo kwa faida ya taifa badala ya never ending attacks tena personally, that is low!
Samahani mzee kama nimekukwaza, ni mtazamo wangu tu. Namaanisha tu kwamba katika ngazi ya familia, Rose & Wilbroad Slaa wanayo malengo yao ambayo wanaendelea kuyatimiza kupitia hivyo vyama vyao ambavyo vinatofautiana kiitikadi, na ili wayafanikishe inabidi wafanye hayo ambayo kwa mtazamo wangu ni usanii.