Mke wa Kafulila abadili jina lake facebook

unafikiri atabaki huko.......subiri....... chadema waendelee kuficha malazi watajuta
 
Kuna wanawake wanaamini kuwa waume zao wanajigeuza kitandani sio kwenye kauli zao. Hivyo ukigeuza kauli unashudhiwa credibility yako na kudharauliwa naye pia anajisikia vibaya kukuamini usiyeaminika
Chakaza, Mkuu kama ni Usaliti kwanini hakuukemea toka alipotoka NCCR kwenda Chadema, ila ni anapotoka Chadema tu? Au Credibility huwa inashuka tu unapotoka Chadema?
 
Mke mwema ni yule anapoona umejiunga na shetani ambaye kila siku mlikuwa mnamkemea kwa maombi anakuonyesha hakuungi mkono ikiwa ni pamoja na kukunyima unyumba.
Nenda hukohuko shetani akakupe unyumba![emoji33] [emoji33]
Kama huyo mama kaamua kumsusa mume wake sababu ya political motives sina cha kusema ila maandiko (Mungu mwenyewe) ndio mhukumu lakini ukishaapa Kanisani umeapa mbele za Mungu ....huwezi kuvunja kiapo kwa motives za kisiasa! Kafulila angesaliti ndoa Kishoa angemsamehe? In short huyu mama ameshindwa kubeba pressure za akina Lema ....ila atakuja kujua makosa anayofanya ....ugomvi wa ndani unahamia hadi mitandaoni? Hapo Kafulila kamuoa Kishoa au Chadema? Acheni kuchukulia siasa too personal kiasi hiki .....mtachukiana wote kadri muda unavyoenda ...
 
Chakaza, Mkuu kama ni Usaliti kwanini hakuukemea toka alipotoka NCCR kwenda Chadema, ila ni anapotoka Chadema tu? Au Credibility huwa inashuka tu unapotoka Chadema?
Huoni tofauti hapo mkuu? Unadhani angetoka Chadema na kwenda ACT au hata UDP kungekuwa na maneno? Kwa sababu wote hao malengo yao ni mamoja, kupambana na udhalimu wa chama tawala.
Ni kama mtu kuhama dhehebu la dini tuu lakini malengo ni kumpiga vita shetani, sasa mtu huyo akihamia kwa shetani kabisa na kusema eti siku hizi shetani kawa mwema itashangaza! Lini ccm imebadilika?
 
Kwa kweli huyu dada ana haki kabisa ya kufuta hilo neno"kafulila"kwenye jina lake.
Umalaya hautaishia kwenye siasa tu.....ukishakuwa ccm wewe ni mwizi hata nyumbani kwako!!
Mmesahau katibu mkuu alivyokuwa anawalenga ndovu wetu??
Dada kaa pembeni akimaliza yake atakukuta tu kama ni riziki kwake
 
Nikweli Mkuu hilo ni tatizo, lakini kwa Siasa hizi tunazoshuhudia sasa naamini Wanasiasa wengi wao washafanya kuwa Siasa ni ajira hivyo kwao kwanza ni Masilahi then ndo inakuja political affairs., tuliowaamini wengi wamekengeuka kiasi hata sisi Walalahoi tunaosubiri kukombolewa imani yetu imepungua kutokana na Siasa uchwara hizi tunazoshuhudia ukizingatia safari bado ni ndefu!!!
 
Daudi Kafulila atabeba mzigo wake mwenyewe, kalianzisha atamaliza mwenyewe!
 
Tungetoa kibali cha wenyeviti wa vyama vyote nchini kufungisha ndoa ingependeza.
 
Kafulila ilitakiwa amtaarifu mke wake kwanza hata kama asingekubaliana ingeonyesha heshima kwake.
 
Mbunge wa viti maalum Chadema ambaye pia ni mke wa David Kafulila Mh Jesca Kishoa amebadilisha jina kwenye profile yake badala ya kuwa #Jesca_Kishoa_Kafulila na kuwa #Jesca_Kishoa mi sijaelewa maana yake!

hivi jina "Kafulila" maana yake nini?
 
Too much kufuatiliana. Huu uzi una dalili za kimbeambea kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…