Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa


Bora kaombe kanisani, mbona nappe na makamba wameomba msaaha tena mwanaume mwenzao, kwa magoti toka IFM mpaka ikulu
 
Kisha danganywa na mchungaji huyo. Hapo hakuna msamaha kinachotafutwa ni promo ya kanisa.
 
hii thread ilinifanya nipigwe ban, leo sitii neno , naunga mkono upuuz wa huyu mwanamke 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kama ni swala la kweli yani inaonyesha ndoa za vijana wa leo hazina misingi mizuri ya kimakuzi na heshima ya ndoa. Wazee wetu walioana vijana sana ila maadili na uadilifu wa nafasi zao ulikuwa wa kiwango cha juu sana. Tuwe na maandalizi mazuri kwa watoto wetu aisee maana sisi tumeshakuwa maututi tayari, wanaopona ni wachache sana.

Kwa sasa ni kheri kuchelewa kuoana ili kujitafakari na kufanya maamuzi yaliyotukuka ukiwa umeiva na sekta hii ya ndoa na sio maandalizi ya harusi nzuri/kifahari. Issue ni mda tu, haina kufeli.
 
Asipochukua huu ushauri basi, ndoa sio ubabe !
 
Wanandoa wengi hawana ufahamu wa kuishi na ndoa wanachojua ni kimoja tu
 
Hii dhambi itakuwa alichepuka na mchepuko 😂😂😂
 
Kuna siku nilienda kubariki pete ya ndoa kanisani, wife akaona ndio fursa ya kuchomekea kwa mchungaji mambo (madhambi) yangu mengine mchungaji anishauri, nilimkata jicho moja akajua leo huko home hakukaliki akabadili hapo hapo na kumwambia mchungaji ananiombea na anaona mabadiliko, baada ya kutoka hapo church aliomba msamaha meenyewe kwa kuwa nilishamuambia mambo yetu ya ndani ni ya ndani nisikie tena kwa mtu mwingine
 
Kama madhambi yako mwenyewe unayaonea aibu si uache jamani...heee
 
Kama madhambi yako mwenyewe unayaonea aibu si uache jamani...heee

Ishu siyo madhambi yangu, ni namna ya kutatua changamoto zetu za maisha ya ndoa, sasa yeye kutaka kumwambia mchungaji ninarudi usiku ama ninakunywa pombe inasaidoa nini?na kuacha siwezi

Pili kupeleka mambo kanisani maana yake yameshindikana kabisa katika ngazi zote kuanzia kwetu wanandoa, wasimamizi wa ndoa, na wazazi...hatujapitia kote huko na tatu hayakuwa mambo ambayo tulienda kufanya hapo siku hiyo
 
Hahaha
 
Hahaha
 
Ukute kosa lenyewe hata halieleweki!
Sana sana hapo ukute jamaa kafanya ubaharia nje ya ndoa.
Walokole mimi nawajua, tena kama ni mwanamke, unakuta hata akili hazimo.
Hahaha jf bwana. ... vicheko na asubuhi hii mtanitoa mbavu aise
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…