Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

Mkeo atakuwa 'ameokoka', anataka wapendwa waone jinsi gani 'mlivyookoka' hadi kanisani wajue ya familia yenu.

Hakika amekupanda kichwani
 
Huyu mke Lengo lake Siyo jema, usijekuta kuna baharia kamwambia akufanyie hivyo ili amseti kama anampenda haswa,
Kuna madhara haya ukikubali masharti yake;
1.Kudhalilika fika
2.Kumpoteza mke
3.Kugeuzwa mke humo ndani
4.Kupoteza ubaharia wako
5.Kupoteza utu wako kwa ajili ya mapenzi
6.Kuwa kichaa
Huyu siyo baharia, baharia kama baharia hakai namna hii
 
Ungemuuliza tu swali dogo.
Je umelikosea kanisa au yeye?
Umewakosea waumini au yeye?
Ulipomkosea mlikuwa kanisani?
Fanya jambo moja la kijasiri, mkubalie nenda kanisani ukifika muda wa kwenda kuomba msamaha pokea maiki na useme maneno haya.
Mimi fulani nipo mbele ya kanisa kuwatangazia wachungaji na waumini wenzangu wote kuwa kuanzia leo tarehe fulani bila kulazimishwa na mtu yoyote, mimi na mke wangu tukiwa na akili timamu tumeamua kuachana rasmi na mke wangu na kila mtu afuate maisha yake. Tumeamua kuachania kanisani kwakuwa ndipo tulipofungishwa ndoa, asanteni.
Baada ya hapo ondoka kbs kanisani nenda home katoe vijinguo vyake muwekee sehemu salama, kama kwao karibu vipeleke home kwao.
Najua pande zote kanisa, wazazi wa pande zote hawatakubali, mkikutanishwa meza ya duara ndio ueleze pande zote haya mkeo anayotaka kama ni sahihi. Baada ya hapo atakujua wewe kirambasi hatokuletea tena mapigo ya kingeda.
 
Wakuu nawasalimu,

Niko katika hali hii kwa sasa.

Ni kweli nilimkosea mke wangu. Nilifanya dhambi kama binadamu wengine wafanyavyo dhambi. Nimejutia kosa langu na nikaamua kumuomba msamaha mke wangu ili maisha yaendelee.

Jambo la kushangaza ni kuwa mke wangu huyu wa ujanani amekataa kunisamehe. ametoa mashariti kadhaa ili niweze kupata msamaha wake. Mashariti hayo ni haya.

1. Jumapili hii twende kanisani nikaombe msamaha mbele ya kanisa.

2. Turekodi mkanda wa video ili hata watu wengine ambao hawatakuwepo kanisani waweze kuona tukio hilo hapo badae.

3. Amesema pia nikiwa namuomba msahama mbele ya kanisa nimuite mama na wala siyo mke huku nikiwa nimepiga magoti.

Wakuu, nimefikiri sana swala hili. Nia hasa ya mke wangu ni nini. Hivi ndivyo msamaha unavyoobwa?

Nimejiuliza tena kwani atapungukiwa nini kama atanisamehe tukiwa wawili tu bila kamera?

Nilichopanga ni hiki , nataka kugoma kufanya kitendo hiki. Ninagoma kwa sababu nataka kulinda utu wangu. Kufanya dhambi au kumkosea mke wangu hakuondoi utu wangu hata kidogo.

Siko tayari kuuza utu wangu kwa gharama ya kulinda ndoa. Utu huwekwa na Mungu ndani ya mtu. Kuuza utu wako kwa mtu ni kumfanya mtu huyo kuchukua nafasi ya Mungu katika maisha yako. Siko tayari.

Msamaha una misingi yake. Moja ya misingi hiyo ni kulindiana heshima.Msahama ni upendo .Upendo haudhalilishi wengine.

Kama ndoa ni ndoano , basi ndoano hii haitaninasa.


Tafuta tu hela...ukiwa nazo zaidi yake lazima akusamehe
 
Kama uliweza kuonyesha nia ya kumpenda kwa kufunga ndoa kanisani.. unashindwaje kuonyesha unampenda kwa mara nyingine kwa kuungama kanisani??

Trust is the most scarce commodity nowdays, ukishavunja uaminifu kwa mtu kuupata tena lazima ufanye kazi ya ziada.

Acha ujeuri! wewe ni mkosaji, jishushe na umpe mwenzio sababu ya kukuamini tena.
 
Gud idea ikiwezekana aandae kabisa na watu ambao watakua tayari. Yaani pindi amalizapo tu ku omba msamaha wamkabidhi na begi lake kabisa
Nenda nae kanisani,
Muombe msamaha na yote anayotaka uyafanye,
Hii itafanya upime ujinga wa mkeo,ujinga wa viongozi wa kanisa,
Halafu ukisha Fanya anayotaka tangaza hapo hapo kuachana nae mbele ya hao hao anaotaka waone unavyomuomba msamaha
 
Njoo uwe mke wangu uone moto wangu.

Na umbo lako namba nane hilo. Umbo tamu. Walahi utanilaumi kama ukileta upuuzi
Niwe mke wa pili? Daah eti umbo namba nane[emoji3][emoji3] hujaacha tu matusi
 
Heheheeee....Hivi naanzaje kumwambia mume wangu hayo mambo ya kuniomba msamaha mbele ya kanisa? Khaaa...Nikishamsamehe mie inatosha saaana.
Inawezekana kafanya makosa makubwa sana alafu humu watu wanampa kichwa[emoji3][emoji3][emoji3] inawezekana mtaa mzima unajua uovu wake,, mke lazima ampeleke mbele ya kadamnasi ili apate amani ya moyo na amwamini tena.. mbona siku ya harusi walienda humohumo kanisani.

Kwani kumwomba msamaha umpendaye mbele ya watu kunashida gani? Ninachojua kutakua kuna shida kama maombi hayamaanishwi.
 
Back
Top Bottom