Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

Majibu unayo alafu bado unasema upo njia panda !!!

Kaka zetu mnatufundisha nini yani uende kanisani ukaombe msamaha huyo mwanamke anatoa wapi jeuri na kibri cha kukupa condition hizo..

Amekuzidi umri japo unasema wa ujanani
Amekuzidi kipato japo unasema wa ujanani
Amekuzidi nini haswa ??
Je wewe ni mlemavu mke wako anakuhudumia ??
Una matatizo ya kiafya ??

Umuite mama yeye ndio alikunyonyesha ??mke wako ni mkristo mwambie biblia gani inasema tuwaite wake zetu Mama..


Nyoko we
Asiejua maana haambiwi maana
 
Kosa umeshalifanya tayari.
Unamuomba msamaha ili iwe nini.
Mwambie huna haja na msamaha wake. Hata ulivyomuomba msamaha mwambie ulikuwa unamtania tuu.
Mwambie afanye analoona litafaa. Pia mwambie kuwa ukienda kanisani kusema ulitoka nje ya ndoa mwambie utajihukumu kumuacha hapo hapo kanisani.
Na utatangaza kuwa unatafuta mke mwingine.
Mkumbushe wewe ni mwanaume hupangiwi la kufanya bali unafanya utakavyo.
Mwambie wewe ndiye mume wake ndiye mtawala wa hiyo nyumba. Kama hataki asepe apishe watakaoweza kutawaliwa na wewe.
Mwambie bi kweli umekosea lakini sio kigezo cha kufanya upuuzi kama aliosema.
Pia mwambie umemheshimu kusikili maoni yake ya kipumbavu ambayo kimsingi ungepaswa umchape makofi mawili makali sana.
Mke wako inaonekana amekupanda kichwani sana. Mpaka inafikia anafikiria kusema hivyo achilia mbali kutamka upupu huo.
Binafsi mwanamke niliyemuoa hawezi fikiria huo upuuzi achilia mbali kuutamka. Kwani anajua joka si mtu wa mchezo.
Joka katika ubora wake
 
M
Msimamo wako na uwe huo huo mkuu,

umeshamuomba msamaha yeye kama yeye, na bila shaka ulimkosea yeye kama yeye!
Sasa inakuaje tena ukaombe msamaha mbele ya kanisa?
Tena eti na mkanda wa video uchukuliwe.

Aise mliooa walokole kazi mnayo.
Mimi akinitamkia huo upuzi eti nikapige magoti mbele ya kanisa na huku narekodiwa, nitamnasa kibao huyo.
Kumuomba msamaha tu umempatia heshima, yake inatosha.
Mkewe atakuwa akina Atuganile Mwakifulefule,,,unamkosea dada msamaha unaomba ukoo mzima 😂😂😂 pambana na hali yako.
 
Wewe kama ulitembea na mwimba kwaya, au church elders mkafumaniwa kabisa na kanisa likajua basi ni haki kumuomba msamaha mbele ya kanisa na kurudi kundini[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].
Na bado.
 
Nenda nae kanisani,
Muombe msamaha na yote anayotaka uyafanye,
Hii itafanya upime ujinga wa mkeo,ujinga wa viongozi wa kanisa,
Halafu ukisha Fanya anayotaka tangaza hapo hapo kuachana nae mbele ya hao hao anaotaka waone unavyomuomba msamaha
Vipi kama lengo la huyo mwanamke ni waachane? Atakuwa karahisisha kazi.
Maana kuambiwa aombe msamaha mbele ya kanisa mwanamke anajua ni jambo ambalo mwanaume hataweza.
 
Huyu mke Lengo lake Siyo jema, usijekuta kuna baharia kamwambia akufanyie hivyo ili amseti kama anampenda haswa,
Kuna madhara haya ukikubali masharti yake;
1.Kudhalilika fika
2.Kumpoteza mke
3.Kugeuzwa mke humo ndani
4.Kupoteza ubaharia wako
5.Kupoteza utu wako kwa ajili ya mapenzi
6.Kuwa kichaa
 
Majibu unayo alafu bado unasema upo njia panda !!!

Kaka zetu mnatufundisha nini yani uende kanisani ukaombe msamaha huyo mwanamke anatoa wapi jeuri na kibri cha kukupa condition hizo..

Amekuzidi umri japo unasema wa ujanani
Amekuzidi kipato japo unasema wa ujanani
Amekuzidi nini haswa ??
Je wewe ni mlemavu mke wako anakuhudumia ??
Una matatizo ya kiafya ??

Umuite mama yeye ndio alikunyonyesha ??mke wako ni mkristo mwambie biblia gani inasema tuwaite wake zetu Mama..
Kamwene Kamwene kamwene
 
Majibu unayo alafu bado unasema upo njia panda !!!

Kaka zetu mnatufundisha nini yani uende kanisani ukaombe msamaha huyo mwanamke anatoa wapi jeuri na kibri cha kukupa condition hizo..

Amekuzidi umri japo unasema wa ujanani
Amekuzidi kipato japo unasema wa ujanani
Amekuzidi nini haswa ??
Je wewe ni mlemavu mke wako anakuhudumia ??
Una matatizo ya kiafya ??

Umuite mama yeye ndio alikunyonyesha ??mke wako ni mkristo mwambie biblia gani inasema tuwaite wake zetu Mama..
umedungua
 
Kanisani ya Magogoni.

Wakuu nawasalimu,

Niko katika hali hii kwa sasa.

Ni kweli nilimkosea mke wangu. Nilifanya dhambi kama binadamu wengine wafanyavyo dhambi. Nimejutia kosa langu na nikaamua kumuomba msamaha mke wangu ili maisha yaendelee.

Jambo la kushangaza ni kuwa mke wangu huyu wa ujanani amekataa kunisamehe. ametoa mashariti kadhaa ili niweze kupata msamaha wake. Mashariti hayo ni haya.

1. Jumapili hii twende kanisani nikaombe msamaha mbele ya kanisa.

2. Turekodi mkanda wa video ili hata watu wengine ambao hawatakuwepo kanisani waweze kuona tukio hilo hapo badae.

3. Amesema pia nikiwa namuomba msahama mbele ya kanisa nimuite mama na wala siyo mke huku nikiwa nimepiga magoti.

Wakuu, nimefikiri sana swala hili. Nia hasa ya mke wangu ni nini. Hivi ndivyo msamaha unavyoobwa?

Nimejiuliza tena kwani atapungukiwa nini kama atanisamehe tukiwa wawili tu bila kamera?

Nilichopanga ni hiki , nataka kugoma kufanya kitendo hiki. Ninagoma kwa sababu nataka kulinda utu wangu. Kufanya dhambi au kumkosea mke wangu hakuondoi utu wangu hata kidogo.

Siko tayari kuuza utu wangu kwa gharama ya kulinda ndoa. Utu huwekwa na Mungu ndani ya mtu. Kuuza utu wako kwa mtu ni kumfanya mtu huyo kuchukua nafasi ya Mungu katika maisha yako. Siko tayari.

Msamaha una misingi yake. Moja ya misingi hiyo ni kulindiana heshima.Msahama ni upendo .Upendo haudhalilishi wengine.

Kama ndoa ni ndoano , basi ndoano hii haitaninasa.
 
Anataka utoe boko ili apate bonge la ushuhuda amsingizie Mungu katenda wakat amekushurutisha kwa mtutu wa talaka , kataa hiyo roho
 
Back
Top Bottom