Mke wangu ananitesa na kuninyanyasa sina raha na ndoa sijui nifanyaje

Mke wangu ananitesa na kuninyanyasa sina raha na ndoa sijui nifanyaje

Jamani jamani.
Kwahiyo miaka mitatu yote umekubali kuteswa tu?Pamoja na mateso bado ukamjengea?Pamoja na mateso bado unawahi nyumbani?Pamoja na mateso bado unamwomba unyumba mpaka unaambulia kipigo?Pamoja na mateso bado umeendelea kukaa nae na kukubali kukaanyumbani na watoto wakati yeye akienda kufanya 'who knows what' ?

Embu amka baba. Wewe ni mwanaume, act like one.Kama kweli umechoka hizo tabia zake mweke chini umweleze kwamba hiyo ndoa yenu haitofika popote iwapo hatojirekebisha. (Ningeweza ningekwambia siku nyingine akileta ujeuri umchape vibao kama mtoto) but anyway cha muhimu ni kumjulisha kwamba huwezi na wala hutaki kuendelea kuishi nae katika hali mnayoishi sasa hivi. Ila sasa kwa kumweleza haya uwe tayari kwa lolote (including kuachana) maana anaweza akakuambia kwamba alikua anafanya hayo yote ili uondoke uache kumganda akae na mtu wake anaempenda.

Sasa hivi jifikirie wewe na wanao, sidhani kama kitendo cha mama yao kukupiga (kama nao wanaona) ni mfano mzuri kwao. Fanya mpango uwalee katika mazingira mazuri.

akifata ushauri wako atafanikiwa.big up gal
 
You are too weak to be her husband or she is too strong to be your wife

Advice; Switch codes to get your equivalent
 
Wana JF...

Naandika huku nafsi yangu ikiwa na majonzi makubwa.

Mke wangu wa ndoa tuna miaka 8 toka tufunge ndoa, tumejaliwa kupata watoto 2 mapacha wa kiume na kike.

Lakini taingia mwaka juzi kabadilika kaanza vituko nyumbani, sio kawaida yake ananipiga na vitu bila sababu.

Kaenda mbali zaidi ananiambia lazima nikitoka kazini niwahi kufika nyumbani nikae na watoto yeye yupo bize..

Kanilizimisha nimjengee nyumba kwao Same nimemjengea nyumba kubwa tu lakini hana shukurani..

Tendo la ndoa napewa mara moja kwa mwezi nikihoji napigwa na mwiko..

Kila baada ya wiki anasema anasafiri anakwenda kwenye semina nibaki na watoto.

Ndugu zangu nisaidieni nifanyeje??

Hii sredi nina mashaka na ukweli wake! Hapo kwenye RED mwiko kwa kawaida hukaa jikoni iweje ukiomba tendo la ndoa upigwe mwiko? unataka kulifanyia jikoni? au mwiko unakaa chumba cha kulala?

Hapo kwenye bluu, Haiwezekani kila baada ya wiki 2 aende semina, Hakuna semina za jinsi hiyo kwa hapa BONGO.

Hapo kwenye kijani, Kwa kuwa una uwezo wa kujenga nyumba kwao, basi kipato chako si haba. Haiingii akilini kwa mwanaume mwenye kipato cha kujenga nyumba hadi ukweni usiheshimiwe, Haiwezekani.

La msingi Komaa, kwa hizo amri zake uone atakachokifanya.
 
duh pole kaka mie nilidhani wanawake wananyanyasika kumbe na wanaume pia dah
 
Mchuzi wa bata wewe nahisi una mtindio wa ubongo. Hivi huyo mwanamke ulikutana nae bar? kama una ndoa nae mrudishe kanisani wampe somo. La sivyo mpe talaka aenda nyumbani. hivi nye mnaishije maisha ya kujibana kiasi hicho?

Sometimes naona kama ni ujinga unaonyesha hapa.
 
Kama wewe ni Mkristo, basi soma Mathayo 7:24-27.
Then, chukua hatua na kila kitu kitakuwa sawa.
 
Nimeona hii Post nikakumbuka wimbo wa Bushoke ,Lakini wewe si ndo kichwa cha nyumba inakuwaje hapa?tafuta msaada wa wazazi wenu
 
f***......haiingi kichwani...unapigwaje na wife??we pimbi kwa kweli.hizo semina anasuguliwa na wajanja nje...
 
mmmh...lakini kwa mwenendo wa maisha ya sasa (mambo ya utandawazi) uhalisia wa kisa hiki unaanza kunipa mashaka..!!! Ni kwelindoa nyingi zinakuwa na matatizo lakini kwa siku hizi eti mwanaume kufanyiwa haya unayofanyiwa wewe..(tena inaonekana wazi ni mtu wa mjini huyu!)..ni kitu kigumu sana..wanawake wenyewe tu huwezi kuwanyanyasa hivi..leo hii wewe mwanaume mzima eti unaomba ushauri kwa mambo haya (tena bora yangekuwa ndo yameanza juzi...miaka 3 iliyopita..kweli!!??)..unapigwa mwiko..tendo la ndoa kwa bajeti..na nyumba umejenga...mmmh!!? labda kama ameshakuweka kwenye chupa...na hata ingekuwa mambo ya kishirikina si ulishajua mambo hayo tangu mwaka juzi..!? :noidea:
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Wewe umeoa au umeolewa? Fanya maamuzi magumu.
Iko siku atakwambia umfulie na nguo za ndani ....
 
ina maana huo uvumilivu ulikuwa unahitaji ili iweje ?? keshachukua chake same wewe unajiuliza nini na kwa nini uendeshwe kwa stail hiyo???
 
Nimejickia kucheka na kumuonea huruma hapo hapo jamani. Wanaume huwa wanakutana na mambo kweli sometimes na hv jamii inawachukulia km strong bs wakipata vipigo na manyanyaso mengne hawana pa kusemea as wanayamezea, watamwambia nani? Bora ya wanawake...! Nadhani mpaka sasa nimeshajua ki2 cha kufanya...nafungua chama cha wanaume walio ktk unyanyasaji wa ndoa niwasaidie....sasa kakangu nikuulize, je hujawai hata kumrudishia japo konde? Na unakubalije kutumikishwa ktk mapenz to that abusive extent? Ila wadada wa kipare ndo zao...nackia lazma wakufanye Asha, Mwajuma huku wakijigeuza John, juma...pole thana meen!
 
pole mkuu
mketetishe mkeo mzungumze ikishindikana kuna wazee
kama unafurahia kipigo endelea kunyamaza
 
pole mkuu mketetishe mkeo mzungumze ikishindikana kuna wazee kama unafurahia kipigo endelea kunyamaza

hivi kweli hata akimketisha ni kitu gani atamweleza akaelewa iwapo ameshakuwa mnyonge kwake muda mrefu???
 
Aisee.. Inaweza kuwa kweli. Tangu jamaa aliposema mkewe amerudi hatujamuona tena humu! Huenda alimstukia akampa tena kichapo.
 
Hata kama ndoa tunaambiwa ni kuvuliliana, not this much... tafakari..... chukua hatua....
 
  • Thanks
Reactions: BPM
Back
Top Bottom