Mke wangu anapitia wakati mgumu sana hadi nimemuonea huruma

Mke wangu anapitia wakati mgumu sana hadi nimemuonea huruma

Joined
Jun 2, 2022
Posts
96
Reaction score
294
Tatizo kubwa lilianza pale nilipogundua anachepuka na ex wake. Baada ya kuligundua hilo sikutaka kuchukua hatua za shari sana papo kwa papo, bali nilichukua hatua ambazo mpaka leo anashindwa kuelewa afanyeje, sasa imefikia hatua muda wote ni analia tu, saikolojia hayupo sawa na kama anataka kuchanganyikiwa hivi.

Baada ya kugundua kwamba anachepuka nilichukua maamuzi yafuatayo

1. Siku hiyo hiyo niliyogundua sikutaka kumuuliza kama ni kweli au siyo kweli kwa sababu nilishajihakikishia kwa asilimia 100.

2. Sikula Chakula chake, nilifika naingia jikoni na kuandaa Chakula mwenyewe (hii imeendelea hadi leo)

3. Najitahidi sana niwahi kurudi nyumbani tofauti na siku za nyuma.

4. Tukilala kitandani mimi nageukia mzungu wa nne.

5. Tangia siku hiyo sijawahi kumuomba unyumba(japo anaweka mazingira ya jambo hili kila siku)

6. Akiniuliza namjibu kidogo halafu naendelea na utaratibu wangu.

7. Kila kitu najifanyia hadi nguo chafu zote za kwangu nakusanya na kufua mwenyewe nikipata nafasi(Ninapokuta amezifua narudia kufua)

8. Simtukani wala kumuongelesha vibaya bali nafanya mambo yangu ndani ya nyumba kivyangu.

9. Baada ya kuona hivyo, akasema anataka akaonane na Mama yake(ilikuwa Ijumaa usiku, nikampatia nauli muda huo huo na kumwambia asubuhi na mapema aende, ghafla akasema ameahirisha hadi sasa yupo)

10. Nimeacha kuchangia naye kitu chochote ndani ya nyumba isipokuwa sehemu ya kulala tu(kitandani na penyewe mzungu wa nne au nalala sebuleni wakati mwingine).

Sasa leo ni siku ya 6 tangia nimeanza kuishi hivyo na mke, mke wangu amenyongonyea ghafla, amekonda, amekuwa mtu wa mawazo na wasiwasi muda wote.

Katika kipindi hiki chote alijua sababu ya mimi kuishi hivyo ni yeye kuchepuka, hii ni baada ya jana jioni kuniita Chumbani na kusema anajutia sana kufanya vile na hatarudia, jambo baya zaidi akasema ameshafikiria mara mbili kunywa Sumu, anaona hana thamani tena kwangu, Dah [emoji24][emoji24] nilimwonea huruma sana na nikaamua kumsamehe tuendelee na maisha lakini naona hali haijabadilika kwake yaani ni mtu wa mawazo na wasiwasi muda wote, kiufupi anapitia wakati mgumu sana.

Wito kwa wanaume na wanawake hasa wanaoishi pamoja kama mke na mume kwa namna yoyote ile, kupigana siyo adhabu tosha ya kusuruhisha migogoro, mimi huyu mwanamke nimempa adhabu hiyo lakini naona imemnyoosha kweli kweli japo naona kabisa imemuharibu kisaikolojia kabisa.
 
Yote ya nini?? Kama amediriki kuchepuka basi ni dhahiri hathamini penzi lako wala utu wako.

Maradhi mengi siku hizi ya nini kuleteana vifo mapema. Mwenye asili yake haachi. Leo ka cheat na X kesho ata cheat na Y yote akijua adhabu itakuwa kununiwa na yeye atajinyong'onyesha na wewe utasamehe.

Pale ulipogundua kacheat ndipo palipaswa pawe ukomo wa ndoa yenyewe. Mpaka wewe kujua inamaanisha aidha aliamini sana 'ujanja' wake ama alitambua kuwa wewe ni mpumbavu kwake.

Niamini, hata mkisameheana hutomuangalia kwa mtazamo ule ule tena kabla ya kumkamata, daima atakuwa msaliti kwako hivyo adhabu ni yenu wote.
 
Kununa hajujawahi kua suluhisho la kudumu kwenye migogoro Kama hiyo.

Ulichokifanya Ni kana kwamba uyo mwanamke ni unaiba tu (Mchepuko au hawala yako).
Hujaonesha Yale makucha na mAmlaka ya kiume kuonesha umekasirishwa na alichokifanya.

Na kwasababu umemsamehe kirahisi Sana, nna imani atachepuka Tena maana keshakusoma una moyo mwepesi Sana wa kusamehe haraka.

Ulitakiwa uoneshe advertise Moja matata Sana kama unamwacha Moja kwa moja.
(Hata Kama huna.mpango wa kumuacha)

Pia uyo ex wake nae umchimbe mkwara mzito Sana kwamba umejua na akiendelea dawa yake inachemka. Ajutie kabisa Ujinga aliufanya. Yaan ikiwezekana uyo kijana ndio amkimbie mkeo.

Unapojificha eti unanuna na hufunguki kwa pande zote mbili kilichokukasirisha. Eti unajifulia nguo n.k
Huo unakua Ni ufala.

Wote wanakuona Ni mwanaume mwenye wivu sana na kisirani tu. Na ulivosamehe kirahis wameshakuchora Ni mwanaume kisirani na laini asiye na msimamo kabisa.

BE A MAN and be a HUSBAND[emoji120]
Simamia ndoa yako, ilinde familia yako
 
Mwanamke anaeamua kuchepuka akiwa na wewe ni hatari kuliko bomu la nyuklia.

Wanawake wako makini sana inapokuja swala la kuchepuka ama kugawa penzi, mwanamke akiamua kugawa penzi huyu amedhamiria kwa 100% na yuko tayari kwa lolote.

Kanuni ni moja tu, mwanamke akikupiga risasi ama akakupiga panga ya shingo lakini bahati nzuri ukapona, huyo msamehe na mpe mapenzi zaidi ya mwanzo ila mwanamke akichepuka kwa sababu yoyote ile huyo hakuna msamaha. Huyo ni hatari kuliko bomu la nyuklia.

Ni wewe uchague, uishi na bomu ndani ya nyumba au lah.
 
Tatizo kubwa lilianza pale nilipogundua anachepuka na ex wake. Baada ya kuligundua hilo sikutaka kuchukua hatua za shari sana papo kwa papo...
Umeenda vizuri ukaharibu mwishoni.

Kama uliamua kumsamehe baada ya kukiri ilitakiwa umlambe makofi kadhaa kwa hasira ndio umpe onyo. Ulivyo samehe kilaini hivyo ndio maana bado haamini kama kweli umemsamehe.
 
Nikusifu kwa kuwa mtulivu wa nafsi ila don't dare ku-discus ishu za uzinzi na mwanamke mzinifu yaani ulipoamua tu kukaa nae kujadili hilo jambo wewe umekwisha,huyo hakufai option ya kusema sijui namuonea huruma kuna siku itakuponza huyo atafanya tena tena na tena na hutokaa ujue tena!

Kwa matokeo haya yapo mambo mawili hatari kwa ustawi wako kama mwanaume,kukuletea magonjwa mabaya na watoto wasiokuwa wa kwako!

Watch yo steps!
 
Tatizo kubwa lilianza pale nilipogundua anachepuka na ex wake. Baada ya kuligundua hilo sikutaka kuchukua hatua za shari sana papo kwa papo, bali nilichukua hatua ambazo mpaka leo anashindwa kuelewa afanyeje, sasa imefikia hatua muda wote ni analia tu, saiklojia hayupo sawa na kama anataka kuchanganyikiwa hivi.
Huu mwaka hutoboi, huwajui wanawake huyo hanywi sumu bali atakuua wewe
 
Back
Top Bottom