Mke wangu kalipendea nini hili jitu?

Mke wangu kalipendea nini hili jitu?

Mwambie hapo nyumbani watu hawatakiwi kukaa zaidi ya siku kadha ulizia shughuli zake zitachukua muda gani. Amefikia kuondoka na familia yako kwenye bichi, chunga atachukua mkeo.
 
Ukiwa boya nani atajali kuwa wewe ndo mwenye nyumba. Hata mkeo atakupuuza tu na atatoka na hilo jitu.
Hapo ndo shida sasa. Hata maelezo yake yanaonyesha ni boya, mwanaume mwenzio anatembea ni kichupi mbele ya mkeo kisha unanyamaza kimya unakuja kulia huku JF.
 
Waheshimiwa nina mgeni ambae sasa anaelekea kumaliza wiki akiwa hapa kwangu, ni binamu yangu huwa anaishi mkoani amekuja kwa shughuli zake binafsi, ataondoka atapokamilisha yaliyomleta.

Nimewaandikia kwa sababu, huyu jamaa amenishangaza sana, imagine weekend hii iliyokwisha anashinda na boxer kutwa nzima tena kifua wazi, au kwasababu amevimba kifua anataka tumwone au?

Mke wangu na house girl wanafua nguo Jumamosi asubuhi eti anaenda pale awasaidie kufua, natoka ndani namuuliza wife mbona mgeni anafua nguo, najibiwa kuwa eti ameomba mwenyewe, hii ni sawa kweli?

Yote tisa, kumi ni Jana, inafikia hatua linamkuta wife jikoni anasonga ugali linaomba limsaidie kusonga ugali, mgeni gani wa namna hii?

Wadau nitumie njia gani kulitimua hili jitu hapo nyumbani? Kabla halijaleta madhara maana mdogo wa mke wangu naona kama yuko nalo karibu sana, pia wife kaniuliza kama mimi pia naweza kufanya mazoezi nikawa kama hilo jitu badala ya kitambi, ingawa alinieleza kwa utani huku tukifurahi na kutaniana ila najiuliza kwanini aseme sasa wakati hili jitu lipo?

Linakaa hapo sebuleni kwenye video hadi usiku mwingi likiwa na mdogo wa mke wangu bila kujali maadili.

Jumapili nilienda kwenye Bonanza la timu yetu ya veterans narudi nimekuta nyumba nzima hawapo wameenda beach wote pamoja na huyu jamaa.

Hivi unaendaje ugenini halafu unaanza kuleta ujuaji wa namna hii?

Wadau msaada wa mawazo unatakiwa haraka.
Mwanaume mashine.
 
images-1.jpeg
ww upo hivi
images.jpeg
hill jitu
 
Aliomba afikie hapo kwenu? Kwa miaka hii kuna kufikia kwa mtu?
Fasta amevunja masharti na vigezo, aondoke hapo. Kabana hela zake ndio hizo anatanua anapeleka watu beach, halafu anajifanya anajua kujali. Kama kampenda mdogo wa mkeo, aende kwao na mkeo ajitambulishe na apewe taratibu. Asilete ukware kwenye miji ya wengine, wakati analishwa bure. Halafu huyo mkeo, hana ustaraabu hata kidogo. Period huwezi kumtoa mke wa mwingine outing bila taarifa yake. Niite mimi nina uzoefu kwa kushughulikia wakware uchwara hao.
 
Back
Top Bottom