Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

Wanawake wengine ni pasua kichwa...

Kuna mwana mkewe wa ndoa kabisa hakumwambia kuwa ana mtoto aliyezaa kabla ya ndoa.


Mtoto huyu alizaliwa miaka mitatu nyuma kabla ya kuona na huyu mjewe.


Na mume kagundua miaka sita mbele. Wakati mtoto wa mke ana miaka 9.

Alijuaje?
Aliona mawasiliano ya simu yasiyoeleweka. Akaamua kutap mawasiliano. Ndio kwa umafia mkubwa akakutana na hayo.


All in all....kama hakuna usaliti, na bado una amani kuishi naye katika maeneo mengine yote, mvumilie tu.
La kua na mtoto kabla ya ndoa na kutomsema, angalau kdgo angalau, nasisi wanaumme tunaficha watoto wetu wa nje ya ndoa, ila kuficha msiba wa mama mzazi kwa mme wako inauma sana
 
Tatizo la mkewangu ni kutokua muwazi angeniambia mama anaumwa umekija kuugulia hapa kwa mda, hata angesema ana kisukali au pressure nisingekazana kuthibitisha hilo, kinacho niuma ni kua na mgonjwa maututi kwa mwezi mitatu ndani mwangu bila kunishirikisha kwani haniamini kwanini?
Hivi wewe huyo mama hukuona kama anaumwaa...?? Miezi mitatu unaishi naee ulitaka mkeo aanze kukwambia nini akati ameshachanganyikiwa mtoto wa watu mama yake anaumwa na anajua ana hali mbaya.

Sema unataka kumtafutia sababu tu mzee ila huyu mwanamke hana kosa kabisa. Labda kuchelewa kukupa taarifa kuhusiana na kifo cha mama yake hapo kidogo alikosea.

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
Hivi wewe huyo mama hukuona kama anaumwaa...?? Miezi mitatu unaishi naee ulitaka mkeo aanze kukwambia nini akati ameshachanganyikiwa mtoto wa watu mama yake anaumwa na anajua ana hali mbaya. Sema unataka kumtafutia sababu tu mzee ila huyu mwanamke hana kosa kabisa. Labda kuchelewa kukupa taarifa kuhusiana na kifo cha mama yake hapo kidogo alikosea.

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
Paka sasa hivi hajamueleza chochote wala kukiri kosa....huyu sio mke wakujenga nae maisha
 
Mkuu hata usihofu huyu mke wako ni wale wanawake baadhi ambao hawana elimu ya VVU thus hata yeye alikuwa anamnyanyapaa mama ake na ndo maana hajakwambia ,msamehe kisha mwelimishe songa mbele ila chukua tahafhari.
 
Hivi wewe huyo mama hukuona kama anaumwaa...?? Miezi mitatu unaishi naee ulitaka mkeo aanze kukwambia nini akati ameshachanganyikiwa mtoto wa watu mama yake anaumwa na anajua ana hali mbaya. Sema unataka kumtafutia sababu tu mzee ila huyu mwanamke hana kosa kabisa. Labda kuchelewa kukupa taarifa kuhusiana na kifo cha mama yake hapo kidogo alikosea.

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
fact
 
We jamaa unaonekana ni sample flani za watu ambao wanapenda kutukuzwa n kunyenyekewa sana,kwa kutoa vijihela vyako ulitaka ww ndo uwe mfalme sasa wa kuambiwa kila kitu cha familia nyingine?acha utoto ngoma sio kitu cha mchezo we bora ushajua chanzo cha kifo piga kimy maisha yaendelee,afu unaonekan huna utu kabisa maana unasema unaona kinyaa kulala na mtu muongo je ungeambiwa mama mkwe anangoma na yupo kwako si ungemyanyapaa sana? Jiangalie tabia zako kwanza kabl y kumjudg mke
 
Mke wangu asiniambie mama yake kafa halafu niende? Kufanya nini?

Halafu ninune nisimtumie nauli? Nigundue nini?

Mimi namtumia na bila kinyongo kwani mama yangu yule mpaka iniume?
 
Mkuu mchukue wife muende kituo cha afya mkaangalie status zenu, utakuwa umefichwa mengi
 
msamehe tu ila muonye asirudie kukuficha ficha chochote kile kinachokuhusu directly ama indirectly
 
Fukuza huyo duuuuh huyo hakupendi anakutumia tu
Ndugu zanguni habari zenu, nimekuja kwa ushauri wenu pamoja nakuweza kupanua mawozo yangu nakupunguza stress za kifamilia.

Mimi nina mke na tumejaliwa watoto wawili (2) wakike na wakiume, Mwaka jana mnamo mwezi wa saba (7) mke wangu alinipa taarifa kwamba Mama wake mzazi (mama mkwe) anakuja mjini nijiadae kwenda kumpokea hiyo siku ikifika na ni sisafiri paka nimpokee, kwasababu shughuri zangu nasafiri za nje ya mkoa, nikamuliza amekuja kufanya nini? Eti kufuatilia mafao yake ya pensheni, mmh wakati alisha pokea tangu mwezi wa pili, niliguna tu nikamjibu sawa ntampokea, baada ya kama siku tatu aliniambia amepanda basi, siku hiyo nikaendesha ki 'babywalker' (gari) changu nikaenda standi ya ma basi ya mikoa kumpokea, alingia kama saa sita usiku nikampokea nikaweka mizigo yake ndani ya gari tukaelekea nyumbani vizuri bila kunotisi kitu chocolate.

Baada kama ya siku mbili mie nikasafiri kuenda kwenye kazi zangu, nilirudi baada ya siku tatu (3) nikamukuta bado yupo si ku mind walaa, sisi kiutamaduni na kimila mama mkwe ni mwiko kwangu kuingia chumbani mwake au kumshika mkononi au kutumia choo kimoja kwahiyo nilikuwa namsalimia nikiwa sembuleni kila asubuhi na jioni hiyo wiki nilio kaa sikumtizama sanaa isipokuwa usiku wakati namleta aliendelea kukaa nyumbani kwa takrbani miezi mitatu, mie naenda safari zangu na rudi kila wiki kwa kufichwa na mke wangu.

Kumbe Mama alikuja kufanikisha masuala mawili: hayo yote nilikuja kugundua badaye sana.

Yule mama alikuja kuugulia kwangu auguzwe na mtoto wake (mke wangu) na kuaga watoto wake wengine walioko jijini. Kwangu ndo pakawa kitovu cha mikutano na kuendesha vikao vyao wakati mimi sijui lolote.

Wife kanificha sijawahi ku-imagine kitendo kama hicho. Kumbe mama alikuwa ameshaathirika siku nyingi na virusi vya huu ugonjwa wa kisasa (VVU). Mwili wote ulikuwa umejaa vidonda na ulishabadilika kuwa mweusi na vipele kote.

Kuna siku nilichelewa kutoka nikakuta watoto wake wote watano wako nje, nikashangaa lakini sikumind sana kwasababu wife kaniambia wamekuja kusalimia mama yao. Nikasema poa kumbe kilikuwa kikao cha familia.

Huyu suala la pili baada ya kupokea pensheni yake alikuja kununulia watoto wake nyumba kama kitega uchumi kwasababu siku zake zilianza kuhesabika, kifo kinasongea na hali yake iliendelea kuzorota.

Lakini kumbuka mtoto wake wa mwisho ana miaka 27. Alifanikiwa kupata nyumba hapa mjini, alivyofanikisha hayo akawa anataka kuaga kurudi mkoani baada ya kukaa kwangu miezi mitatu bila mimi kujua. Hata hakuniaga, natoka safari zangu nakuta mama kasharudi mkoani wife ndo kanipa taarifa eti amenipa salamu tu.

Kama mtafutaji na asiye na makuu wala kinyongo niliyapuuzia wala wife sikumuuliza tena kuhusu Mama. Nilikaa nyumbani kama siku tano hivi, tena nikawa nataka kusafiri kuenda kwenye biashara.

Kama kawaida nilimuachia mahitaji ya nyumbani nikaondoka. Baada ya siku kama mbili wife kanipigia simu huku analia tena kilio chenyewe cha kwikwi. Nikamuuliza kulikoni, kanijibu mama anaumwa kalazwa hospitali ya rufaa na kawekewa oksijeni.

Niliduwaa kwasababu sikuwa na taarifa yoyote nyuma kwamba alikuwa anaumwa. Nikamuuliza alipata ajali? Akajibu hapana nitakuambia we tuma pesa niende nimuone.

Sikuchelewa nilijipigapiga nikamrushia laki mbili za nauli na kujikimu. Alivyofika nikaanza kumuuliza mama anaumwa nini hanijibu. Nilikazana kweli kweli kumuuliza kweli ila anaishia kuniambia yuko kwenye oksijeni.

Nikagoma kumtumia pesa mpaka aniambie Mama anaumwa nini? Baada ya siku mbili kaniambia ila baadhi ya wake zetu ni waongo tena uongo wa kitoto. Aliniambia eti anasumbuliwa na (ulcers) vidonda vya tumbo, ndo kawekwa kwenye mtungi wa oksijeni!!!!!!!

Ilikua Alhamisi mwezi jana mtu tunayefamiana naye ambaye ni jirani na ukweni pale kanipigia simu kunipa pole ya kufiwa.

Sikutaka kumuuliza nani amekufa angejua kama kuna usiri mkubwa kati yangu na wife na angenishangaa kutojua huo msiba. Niliitikia vizuri na nilihisi atakuwa mama ndo amefariki.

Kusema ukweli wife hakunipa taarifa mpaka saa 11 jioni wakati mtu alifariki saa mbili asubuhi. Nilijiongeza haraka nikapata usafiri mpaka mkoani. Nilifika mapema tu kwasababu nilikuwa na hela ya ziada nikapanda ATCL ya mchana nikidhani mazishi yatakuwa siku hiyo hiyo. Wife anakuja kunipa taarifa tayari nimeshafika kwao, hana taarifa, lengo lake lilikua nishindwe kuhudhuria mazishi.

Mazishi yalipangwa kesho yake saa saba. Wife alidhani kuniambia saa 11 sitaweza kupata usafiri wa haraka ili nikae na wafiwa pamoja na nzengo.

Kusema ukweli nilishindwa kukutana na wife hiyo siku kwasababu hasira na jaziba nikakimbia makaburini kule kushiriki na wachimbaji. Kule ndo nilipata mkanda mzima wa kuugua na kufa kwake mama mkwe wangu.

Watu wana maneno wanadai “alikufa kwa ngoma” eti alienda kujificha kwa watoto wake jijini. Anyway nilipata kila kitu pale vyote wife alivyonificha.

Sasa naomba msaada wa ushauri kwenu. Siku 40 (arobaini) zimetimia na dua ya arobaini tayari. Wife tangu wiki jana ananipigia simu nimtumie pesa za kurudi nyumbani. Nilisita kidogo sijamjibu chochote kwa sababu bado nina hasira nae, kunitumia kama boya-jinga-fala kwa kunificha hayo yote.
 
Tena sio hilo tu huyu mke wangu ni muongo kiwango cha sgr..

kuna siku nilisafiri kuenda mkoani kwenye kazi zangu, nilivo toka tu nayeye kaondoka kwenda kwa Kaka yeke hapa jijini, majirani ndo walinishitua kwamba sasa wiki mbili taa za nje haziwashwi shemeji inaonekana hayupo ila hajatuaga,...mmh

nikampigia simu mbona haupo nyumbani? Kanijibu eti kaondoka jana kwa Kaka ake eti kuna mgonjwa!!!

Nikawapigia jirani kwakikisha wakaniambia nilivyo ondoka kesho yake nae katoka karibu wiki mbili na nusu.......kweli huyu ndo mke wa kuishi nae nakujenga maisha ya badaye?
Nb
Ila sijawahi kupata vyashiria vyovyote kama huenda inachochora na wanaumme simu yake naikagua mwanzo mwisho hamna kitu hicho, ila uongo wake
Kwahili hana sifa za kuwa Mke...
Japo wengi humu wanashauri umrudishe kisa tu watoto lakini binafsi naona Mkeo hana sifa za Mke.

Yaonekana majirani Wana mengi Sana wayajuayo kwa Mkeo na wameshachoka na tabia zake hadi wameanza "kufunguka".....iko Siku utakachosikia kinaweza kukuua kwa presha. Be careful !

Waweza kagua simu Siku zote na kamwe usione chochote cha kukutia hofu kumbuka wako wazinzi wabobevu hawakamatiki kamwe toka ujanani hadi uzeeni.
 
Nimekuelewa saba ambapo hukuuliza "nani kafariki" ili huyo mtu asijue kuna siri kati yako na mkeo..akili ya fasta hivi wengine hatuna.
 
Kwahili hana sifa za kuwa Mke...
Japo wengi humu wanashauri umrudishe kisa tu watoto lakini binafsi naona Mkeo hana sifa za Mke.

Yaonekana majirani Wana mengi Sana wayajuayo kwa Mkeo na wameshachoka na tabia zake hadi wameanza "kufunguka".....iko Siku utakachosikia kinaweza kukuua kwa presha. Be careful !

Waweza kagua simu Siku zote na kamwe usione chochote cha kukutia hofu kumbuka wako wazinzi wabobevu hawakamatiki kamwe toka ujanani hadi uzeeni.
Uchambuzi mzuri sana mkuu, unajua watu wengi humu wanaona uongo sio issue, nijambo la kawaida wakati uongo huzaa madhambi yote kwenye mahusiano.
 
Mwanamke muongo hanogi hata kwa mbali aisee.Yaani mimi kunidanganya ni tiketi ya kuachana kabisa
Ukipuuza uongo huu kuna kubwa zaidi atakudanganya utalia maisha yako yote.
Zungumza nae kwa uwaz kabisa ujue why alificha taarifa za msingi kama hizo then akili kumkichwa
 
Nitumie namba yake ya simu nimwulize halafu ntakwambia ukweli wote
 
Mtumie nauli mkeo aje nyumbani,akifika nyumbani kaa naye chini zungumza naye kwa upole akueleze nini sababu ya kukuficha habari ambazo tayari unazijua,kisha mpe pole na umsihi ajaribu kuwa muwazi,
Kumbuka mkeo amepoteza mama na wewe ndiyo faraja yake.
 
Kwa sisi ambao tushadanganywa mauongo makubwa makubwa sioni kama mkeo anatatizo hapo. Mtumie nauli arudi bana
 
Back
Top Bottom