Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

mchane ukweli halafu mwambie alichofanya ni ujinga na uzembe hayo mambo aliyoficha yapo toka zamani alivyokufikilia sivyo kwahiyo mwambie umemsamehe na umsamehe kweli mapungufu kama haya ndio huwa ya kujengea ndoa na sio kubomolea ndoa

Simama kama mwanaume mpe mwelekeo asilete mbwembwe na ujuaji halafu na umkanye haswa zen maisha yaendelee.
 
Sasa kusema ugonjwa wa mama yke hataki wakat mmeshakuwa pamoja Bora angekuwa bado mpo kwenye uchumba bado mjazoeana tungesema anaogopa huta muacha huyo hakupendi au yeye ameone alikwambia huta mpa ushirikiano kulingana na tabia zako ambazo yeye ana zijua maana mpaka mmezaa ina maana anakujua jins ulivyo
Suala la ushirikiano sio kweli nampa ushirikiano nimesomesha mdogo wake nimemfungulia biashara japo alishindwa kuindesha ikafungwa Baba ake akiniomba msaada na mtumia japo yeye alinikataza kwa sababu ya migogoro ya familia na mama, mimi nimtu peace sana katika ushirikiano wa maendeleo nda udhaifu wangu huo.
 
Boss,

Kwanza kabisa hakikisha unamtumia nauli anakuja home.

Akifika home wewe mkaushie usimsemeshe kitu chochote kile zaidi ya kumpa hela ya matumizi tu, najua atataka suluhu tu, sasa wewe mwambie akueleze kuanzia mwanzo hadi mwisho hapo unampima atakudanganya au LA

Kisha mrudishe kwao mwezi 1 akajifunze
 
Ilikuwa ni mwaka gani hilo tukio. Ukimwi sio ugonjwa kwa maana kamili ya kitabibu ila ni upungufu wa kinga mwilini. Mama mkwe alijisahau nini kuchukua tahadhari asife kwa fedheha maana naona kifo huwezi kukikwepa ila unaweza jieupusha na kufa kifo cha aibu kama icho. Maana MARADHI aliyokufa nao mama ni ule ukimwi wa miaka ya 80 sasa ivi ukishajitambua umeathirika ukafata masharti huwezi kufa kifo kama icho cha fedheha madonda kudhohofu naona hilo ndo walikuwa wanalificha. Samehe ishi na mkeo. Alichokuwa kuwa anafanya wyf wako na ndugu ni kuficha aibu ya mama yao
 
Mtumie nauli arudi mkae kitako muyamalize kama wana_ndoa, Mweleze kwa kina kuwa hukupendezwa na tabia yake ya kukuficha mambo kama hayo

Mwisho kabisa,... Legeza moyo msamehe mkeo, yeye pia ni mwanadamu kukosea kupo.
 
  • Thanks
Reactions: HLM
Babyseater or baby walker mkuu..... Unajua lakini maana ya haya majina?!

Babyseater ni mtu anaekaa na mtoto kukuangalizia ukiwa haupo.

Baby walker ni vile vigari vya kusukumia watoto vile vinakuwa na matairi manne halafu mtoto anakalishwa kwa ndani analala huku ananyonya chuchu ya maziwa halafu mtu mzima anakisukuma kumuendesha......

Sent using Jamii Forums mobile app
Ulitaka kulenga nini hapa mkuu.?
Manake umeniacha na mimi njia panda.
 
Ilikuwa ni mwaka gani hilo tukio. Ukimwi sio ugonjwa kwa maana kamili ya kitabibu ila ni upungufu wa kinga mwilini. Mama mkwe alijisahau nini kuchukua tahadhari asife kwa fedheha maana naona kifo huwezi kukikwepa ila unaweza jieupusha na kufa kifo cha aibu kama icho. Maana MARADHI aliyokufa nao mama ni ule ukimwi wa miaka ya 80 sasa ivi ukishajitambua umeathirika ukafata masharti huwezi kufa kifo kama icho cha fedheha madonda kudhohofu naona hilo ndo walikuwa wanalificha. Samehe ishi na mkeo. Alichokuwa kuwa anafanya wyf wako na ndugu ni kuficha aibu ya mama yao
Mkuu ni sawa hilo unalo sema, kilicho sababisha ungonjwa umdhohofishe haraka nikuuficha sanaa, mimi sikatae kuficha aibu ya mama yao, lakini mimi nilikua sehemu ya familia yao, pili kama wasingetaka mimi nijue wasinge mleta kwangu, kwasababu alikua na watoto wengine wakubwa kuzidi mke wangu, kwanini mimi nitoe hera ya usafiri ya chakula Malazi arafu nifichwe?
 
Hilo nikweli kabisa ni msiri sana na hofia huku mbeleni itakuaje?, nikiacha hili lipitehivi hivi, sasa hivi ananihitaji kwasababu ya msada wangu kwake, je kesho nikiwa sina uwezo huo wakumsaidia kweli atanivumilia?
Sidhani Kama ina tatizo saana, mtu kuwa msiri kwa mambo ya nyumbani kwao, na Mara nyingi hi husababishwa na upande wa pili, maana kwa kawaida binadamu tuna tabia ya kufunguka kwa watu ambao tumesoma attitude zao na kijihakikishia usalama.
Sasa kwa mfano Kama mtu amekusoma kukuona una dharau, majivuno, nk, anafunguka vipi kwako mambo mazito ya nyumbani kwao..
Hata hivo pamoja na kukuficha mwisho wa siku umefahamu Kila kitu, hi Ina muanika yeye kwamba hata Kama amekuficha, Kuna mambo hayafichiki na ukiyaficha mwisho wake Ni kuumbuka tu kama mtu anayejaribu kuficha Moto.
Hivyo ushauri, cha kwanza jitathmini hasa approach zako unazotoa dhidi yake au familia yake uone Kama Zina ukakasi wowote katika hisia za binadamu na uziboreshe,
Pili. Kama alivyosema mchangiaji mmoja, muweke wazi kwamba umejua Kila kitu ili ajue kwamba Ni ujinga tu kuficha mambo ambayo yanaweza kujitokeza yenyewe,
Tatu, mueleze faida za uwazi na hasara za usiri..
 
Ni mkeo na mna watoto wawili. Muulize sababu ya kukuficha kuugua kwa mkweo na pia kuficha kuhusu kifo chake, labda anaweza kuwa na maelezo ya kukuridhisha vinginevyo ni wa kuwa naye makini sana huyo kwani ana tabia ya uongo ya kuficha mambo yenye umuhimu mkubwa. Pia anatakiwa kujutia alichokifanya hivyo akuombe samahani.
 
Mkuu hiyo ni changamoto ndogo sana!imagine siku ukijua hao unaowaita wanao sio wanao wa damu si utajiua sasa!tuishi nao kwa akili mke sio kiumbe wa kushirikiana siri zako maana hizo ndio zitageuka kuwa silaha siku za baadae
 
Ndugu zanguni habari zenu, nimekuja kwa ushauri wenu pamoja nakuweza kupanua mawozo yangu nakupunguza stress za kifamilia.

Mimi nina mke na tumejaliwa watoto wawili (2) wakike na wakiume, Mwaka jana mnamo mwezi wa saba (7) mke wangu alinipa taarifa kwamba Mama wake mzazi (mama mkwe) anakuja mjini nijiadae kwenda kumpokea hiyo siku ikifika na ni sisafiri paka nimpokee, kwasababu shughuri zangu nasafiri za nje ya mkoa, nikamuliza amekuja kufanya nini? Eti kufuatilia mafao yake ya pensheni, mmh wakati alisha pokea tangu mwezi wa pili, niliguna tu nikamjibu sawa ntampokea, baada ya kama siku tatu aliniambia amepanda basi, siku hiyo nikaendesha ki 'babywalker' (gari) changu nikaenda standi ya ma basi ya mikoa kumpokea, alingia kama saa sita usiku nikampokea nikaweka mizigo yake ndani ya gari tukaelekea nyumbani vizuri bila kunotisi kitu chocolate.

Baada kama ya siku mbili mie nikasafiri kuenda kwenye kazi zangu, nilirudi baada ya siku tatu (3) nikamukuta bado yupo si ku mind walaa, sisi kiutamaduni na kimila mama mkwe ni mwiko kwangu kuingia chumbani mwake au kumshika mkononi au kutumia choo kimoja kwahiyo nilikuwa namsalimia nikiwa sembuleni kila asubuhi na jioni hiyo wiki nilio kaa sikumtizama sanaa isipokuwa usiku wakati namleta aliendelea kukaa nyumbani kwa takrbani miezi mitatu, mie naenda safari zangu na rudi kila wiki kwa kufichwa na mke wangu.

Kumbe Mama alikuja kufanikisha masuala mawili: hayo yote nilikuja kugundua badaye sana.

Yule mama alikuja kuugulia kwangu auguzwe na mtoto wake (mke wangu) na kuaga watoto wake wengine walioko jijini. Kwangu ndo pakawa kitovu cha mikutano na kuendesha vikao vyao wakati mimi sijui lolote.

Wife kanificha sijawahi ku-imagine kitendo kama hicho. Kumbe mama alikuwa ameshaathirika siku nyingi na virusi vya huu ugonjwa wa kisasa (VVU). Mwili wote ulikuwa umejaa vidonda na ulishabadilika kuwa mweusi na vipele kote.

Kuna siku nilichelewa kutoka nikakuta watoto wake wote watano wako nje, nikashangaa lakini sikumind sana kwasababu wife kaniambia wamekuja kusalimia mama yao. Nikasema poa kumbe kilikuwa kikao cha familia.

Huyu suala la pili baada ya kupokea pensheni yake alikuja kununulia watoto wake nyumba kama kitega uchumi kwasababu siku zake zilianza kuhesabika, kifo kinasongea na hali yake iliendelea kuzorota.

Lakini kumbuka mtoto wake wa mwisho ana miaka 27. Alifanikiwa kupata nyumba hapa mjini, alivyofanikisha hayo akawa anataka kuaga kurudi mkoani baada ya kukaa kwangu miezi mitatu bila mimi kujua. Hata hakuniaga, natoka safari zangu nakuta mama kasharudi mkoani wife ndo kanipa taarifa eti amenipa salamu tu.

Kama mtafutaji na asiye na makuu wala kinyongo niliyapuuzia wala wife sikumuuliza tena kuhusu Mama. Nilikaa nyumbani kama siku tano hivi, tena nikawa nataka kusafiri kuenda kwenye biashara.

Kama kawaida nilimuachia mahitaji ya nyumbani nikaondoka. Baada ya siku kama mbili wife kanipigia simu huku analia tena kilio chenyewe cha kwikwi. Nikamuuliza kulikoni, kanijibu mama anaumwa kalazwa hospitali ya rufaa na kawekewa oksijeni.

Niliduwaa kwasababu sikuwa na taarifa yoyote nyuma kwamba alikuwa anaumwa. Nikamuuliza alipata ajali? Akajibu hapana nitakuambia we tuma pesa niende nimuone.

Sikuchelewa nilijipigapiga nikamrushia laki mbili za nauli na kujikimu. Alivyofika nikaanza kumuuliza mama anaumwa nini hanijibu. Nilikazana kweli kweli kumuuliza kweli ila anaishia kuniambia yuko kwenye oksijeni.

Nikagoma kumtumia pesa mpaka aniambie Mama anaumwa nini? Baada ya siku mbili kaniambia ila baadhi ya wake zetu ni waongo tena uongo wa kitoto. Aliniambia eti anasumbuliwa na (ulcers) vidonda vya tumbo, ndo kawekwa kwenye mtungi wa oksijeni!!!!!!!

Ilikua Alhamisi mwezi jana mtu tunayefamiana naye ambaye ni jirani na ukweni pale kanipigia simu kunipa pole ya kufiwa.

Sikutaka kumuuliza nani amekufa angejua kama kuna usiri mkubwa kati yangu na wife na angenishangaa kutojua huo msiba. Niliitikia vizuri na nilihisi atakuwa mama ndo amefariki.

Kusema ukweli wife hakunipa taarifa mpaka saa 11 jioni wakati mtu alifariki saa mbili asubuhi. Nilijiongeza haraka nikapata usafiri mpaka mkoani. Nilifika mapema tu kwasababu nilikuwa na hela ya ziada nikapanda ATCL ya mchana nikidhani mazishi yatakuwa siku hiyo hiyo. Wife anakuja kunipa taarifa tayari nimeshafika kwao, hana taarifa, lengo lake lilikua nishindwe kuhudhuria mazishi.

Mazishi yalipangwa kesho yake saa saba. Wife alidhani kuniambia saa 11 sitaweza kupata usafiri wa haraka ili nikae na wafiwa pamoja na nzengo.

Kusema ukweli nilishindwa kukutana na wife hiyo siku kwasababu hasira na jaziba nikakimbia makaburini kule kushiriki na wachimbaji. Kule ndo nilipata mkanda mzima wa kuugua na kufa kwake mama mkwe wangu.

Watu wana maneno wanadai “alikufa kwa ngoma” eti alienda kujificha kwa watoto wake jijini. Anyway nilipata kila kitu pale vyote wife alivyonificha.

Sasa naomba msaada wa ushauri kwenu. Siku 40 (arobaini) zimetimia na dua ya arobaini tayari. Wife tangu wiki jana ananipigia simu nimtumie pesa za kurudi nyumbani. Nilisita kidogo sijamjibu chochote kwa sababu bado nina hasira nae, kunitumia kama boya-jinga-fala kwa kunificha hayo yote.
Mi ningeomba kukuuliza swali. Je huu ni mke wako wa ndoa? Au ni mwanamke uliemzalisha kisha mmeamua kuenshi pamoja
 
Mambo mengine kuyawka rohoni utakuja it's kabla ya siku zako
Msamehe tu be a man!
 
Sidhani Kama ina tatizo saana, mtu kuwa msiri kwa mambo ya nyumbani kwao, na Mara nyingi hi husababishwa na upande wa pili, maana kwa kawaida binadamu tuna tabia ya kufunguka kwa watu ambao tumesoma attitude zao na kijihakikishia usalama.
Sasa kwa mfano Kama mtu amekusoma kukuona una dharau, majivuno, nk, anafunguka vipi kwako mambo mazito ya nyumbani kwao..
Hata hivo pamoja na kukuficha mwisho wa siku umefahamu Kila kitu, hi Ina muanika yeye kwamba hata Kama amekuficha, Kuna mambo hayafichiki na ukiyaficha mwisho wake Ni kuumbuka tu kama mtu anayejaribu kuficha Moto.
Hivyo ushauri, cha kwanza jitathmini hasa approach zako unazotoa dhidi yake au familia yake uone Kama Zina ukakasi wowote katika hisia za binadamu na uziboreshe,
Pili. Kama alivyosema mchangiaji mmoja, muweke wazi kwamba umejua Kila kitu ili ajue kwamba Ni ujinga tu kuficha mambo ambayo yanaweza kujitokeza yenyewe,
Tatu, mueleze faida za uwazi na hasara za usiri..
Ahsante kwa ushauri mzuri, mimi sikutaka kujua ya kwao na sijawahi kumuuliza, ila suala la mama kuumwa paka kufa bila kuniambia ili niuma sana, kwasabb yule mama alikua nguzo kubwa kwenye familia yangu na yakwao huenda kunamambo ningemuuliza kabla ya kukata roho.
 
Samehe saba mara sabini alificha aibu ya mama yake na familia yake! Mimi nadhani alikuheshimu! Potezea mzee baba! Kwenye ndoa mambo
Mengi yanatokea hilo
Mbona dogo! Mie mke wangu kununua nyumba bila Mie kujua na tuna nyumba tatu! Na nimesamehe aliniambia kitendo kimeshatokea! Kuuliza why akasema “surprise”
 
Back
Top Bottom