Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

Mke wangu kanificha mengi, naomba ushauri

Samehe saba mara sabini alificha aibu ya mama yake na familia yake! Mimi nadhani alikuheshimu! Potezea mzee baba! Kwenye ndoa mambo
Mengi yanatokea hilo
Mbona dogo! Mie mke wangu kununua nyumba bila Mie kujua na tuna nyumba tatu! Na nimesamehe aliniambia kitendo kimeshatokea! Kuuliza why akasema “surprise”
Aisee!
 
Mkuu ni sawa hilo unalo sema, kilicho sababisha ungonjwa umdhohofishe haraka nikuuficha sanaa, mimi sikatae kuficha aibu ya mama yao, lakini mimi nilikua sehemu ya familia yao, pili kama wasingetaka mimi nijue wasinge mleta kwangu, kwasababu alikua na watoto wengine wakubwa kuzidi mke wangu, kwanini mimi nitoe hera ya usafiri ya chakula Malazi arafu nifichwe?

Hili swali kaa ujiulize kwa nini ufichwe? Lazima kuna sababu na hiyo sababj mkeo anaijua. Ameshakusoma anakujua vizuri. Ndio maana kaamua ku mute. Inawezekana kuna neno moja tu ulimtaka kuhusu familia yake likamuumiza basi ni hilo ndio limenfanya awe msiri, kwa mwanamke hata kama utatoa mamilioni hata kama utamlisha mpk avimbiwe lakini kauli moja tu itamfanya asahau mema yote.
Kama unatoa hela na hata huchukui muda hata siku moja kumsindikiza kuona mama hospital tayari anajua huyu hmm.
Uko na binti atakua utaona atakavyokuwa anajali sana familia yake.
Kuishi na mwanamke inahitaji akili nyingi kutuelewa.
 
Ni mke wa ndoa kamili mkuu
Kama ni mke wa ndoa. Baci nakusihi usiendelee kumlaumu mke wako. Kwa mila na tamaduni za mswahili hilo tatizo ulitakiwa kuchirikichwa na wakwezako . Mke wako amedhibitiwa na ndugu zake au mama ake amewalazimisha watoto wafanye siri
 
Mkuu unmuuliza wa kazi gani na mtumie nauli aende mpe pole mambo yaendelee mkuu
 
Mke anaona aibu kwa yaliyomsibu mama yao.
 
Pole, mwambie kabla hujamtumia nauli aseme ukweli wote asikufiche na umwambie umejua mengi kupitia majirani zao

Akishaweka ukweli wote

Mwambie nakupa rikizo ya kujifunza kuwa muwazi.
Sidhani kama utaitaji ushauri mwingine tofauti na huu sidhani kwakweli
 
Mkuu hili jambo hata mimi liliwahi kunikuta lkn ni tofauti kidogo na la kwako....zaidi ni uwongo kwa mkewangu nilivumilia kwa muda mrefu na mwisho hivi karibuni niliitisha kikao cha dharula na washenga pamoja na baadhi ya ndugu zake na ktk hicho kikao msimamo wangu ulikuwa ni kuhitisha mahusiano yetu ndani ya ndoa kwakuwa sikuona haja tena ya kuendelea kuwa na huyu mwanamke hali ya kuwa ni muongo muongo sana na nikaeleza mambo yote niliyokuwa nikiyajua

Basi ndipo nikapata wasaa mzuri wa kuujua ukweli baada ya rafiki yake wa karibu kutuelezea baadhi ya mambo aliyokuwa anayajua na mengine aliyokuwa hayajui kikao kiliendeshwa kwa muda mrefu na mwisho wa siku yeye mwenyewe alikili makosa na alijutia sana na kuomba msamaha sana,nilikuja kuukibali msamaha wake baada ya wamama watuwazima kunipigia magoti tena mpk machozi kuumuombea msamaha ndipo nikakubali sasa hivi heshima ipo mpk inamwagika[emoji38]
 
Covax Kwa umri wake Mkeo kubadilika si rahisi labda AOKOKE..

Ushauri Wangu Kwako ni huu muite yeye na Nduguze wote walokuwa wakifanyia vikao hapo Kwako na umuulize mbele yao Kwanini alifanya alivyofanya ili kuweka defensive mechanism kwa Siku zijazo!

Hofu yangu kama ameweza kukuficha kifo cha Mamake mzazi je, unadhani atakuwa na hofu gani nyingine hapa duniani?

TAFAKARI NA CHUKUA HATUA !!
 
Mkuu ni sawa hilo unalo sema, kilicho sababisha ungonjwa umdhohofishe haraka nikuuficha sanaa, mimi sikatae kuficha aibu ya mama yao, lakini mimi nilikua sehemu ya familia yao, pili kama wasingetaka mimi nijue wasinge mleta kwangu, kwasababu alikua na watoto wengine wakubwa kuzidi mke wangu, kwanini mimi nitoe hera ya usafiri ya chakula Malazi arafu nifichwe?
Kimsingi alikudharau na kukuona boya (samahani kwa kutumia neno hili) akadhani huwezi kujua Nini kinaendelea...
 
Kuna wanawake vichwa maji kweli, kuna vitu vya kuficha ila sio kwa situation yenu hii, anyways huwa siikubali dini ya kiislam ila pona ya mwanaume Ni kuoa/kuzaa na mke zaidi ya mmoja mmoja akikosa akili na kukufariji mwingine atakuwa na akili na utapata faraja ya maisha,,

Mkeo ni mjinga tu, anajichetua kukuficha lakini mama yake alimfikishia hapo kwako na huduma inakutegemea wewe, kufikia kuugua bado anaficha Hadi msiba,, akili za wanawke wengine bhana dah sijui mnawaokoteaga wapi
 
Kuna wanawake vichwa maji kweli, kuna vitu vya kuficha ila sio kwa situation yenu hii, anyways huwa siikubali dini ya kiislam ila pona ya mwanaume Ni kuoa/kuzaa na mke zaidi ya mmoja mmoja akikosa akili na kukufariji mwingine atakuwa na akili na utapata faraja ya maisha,,

Mkeo ni mjinga tu, anajichetua kukuficha lakini mama yake alimfikishia hapo kwako na huduma inakutegemea wewe, kufikia kuugua bado anaficha Hadi msiba,, akili za wanawke wengine bhana dah sijui mnawaokoteaga wapi
Hadi leo hajaona kama kuna kosa kafanya, anaomba kwa haki zote nimtumie nauli tena ya ndege eti kwasababu anasafiri na mwanangu mdogo wa mwaka moja na nusu.
 
Mkuu hilo sio kosa msamehe na mtumie nauli sio ya ndege bali ya basi
kuna wengine wanaleta magonjwa ndani km UKIMWI kwa kutembea na vidume huko nje, sasa huyo kamleta mama yake , na ni makosa ya mama alikoupata atajijua mwenyewe baada ya kupokea pensheni
 
Fanya hivi hukuoa mama mkwe tuma nauli arudi watoto wamuone mama yao
 
Huyo ni mkeo hamna namna zambi tunayochukia wanaume ni ya usaliti hayo mengine mnakaa na kuambiana ukweli kwamba hujapenda na siku zote ajifunze kuwa muwazi.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hakutaka ujue ugonjwa wa mama yake ndio maana alikuficha msiba.

Nadhani huo ugonjwa wa mama yake aliuchukulia vibaya akahisi nawe pia utamjudge mzazi wake.Muache aje muyazungumze punguza hasira.
Ushauri bora kabisa huu, mleta uzi chukua huu ushauri.
 
Nahisi mke wako alihisi kwamba akikwambia mama ana hako ka-ugonjwa labda ungemzuia afikie kwako na mengine mengi.. ila cha kukushauri hapo Mkuu we mtumie tu nauli aje nyumban kisha ukae nae vizuri kumuuliza kwanini hakukuweka wazi na pia muonye wakati mwingine asirudie hiyo tabia ya usiri sio nzuri...Hakuna kosa lisilosameheka mkuu...sisi wote sio wakamilifu mkae chini myamalize..
well said....busara itumike japo kuna kosa la kusudia,na kosa la kimantiki,na kosa la bahati mbaya....yote yanawezwa fanya na binadamu walio tumamu
 
Ndugu zanguni habari zenu, nimekuja kwa ushauri wenu pamoja nakuweza kupanua mawozo yangu nakupunguza stress za kifamilia.

Mimi nina mke na tumejaliwa watoto wawili (2) wakike na wakiume, Mwaka jana mnamo mwezi wa saba (7) mke wangu alinipa taarifa kwamba Mama wake mzazi (mama mkwe) anakuja mjini nijiadae kwenda kumpokea hiyo siku ikifika na ni sisafiri paka nimpokee, kwasababu shughuri zangu nasafiri za nje ya mkoa, nikamuliza amekuja kufanya nini? Eti kufuatilia mafao yake ya pensheni, mmh wakati alisha pokea tangu mwezi wa pili, niliguna tu nikamjibu sawa ntampokea, baada ya kama siku tatu aliniambia amepanda basi, siku hiyo nikaendesha ki 'babywalker' (gari) changu nikaenda standi ya ma basi ya mikoa kumpokea, alingia kama saa sita usiku nikampokea nikaweka mizigo yake ndani ya gari tukaelekea nyumbani vizuri bila kunotisi kitu chocolate.

Baada kama ya siku mbili mie nikasafiri kuenda kwenye kazi zangu, nilirudi baada ya siku tatu (3) nikamukuta bado yupo si ku mind walaa, sisi kiutamaduni na kimila mama mkwe ni mwiko kwangu kuingia chumbani mwake au kumshika mkononi au kutumia choo kimoja kwahiyo nilikuwa namsalimia nikiwa sembuleni kila asubuhi na jioni hiyo wiki nilio kaa sikumtizama sanaa isipokuwa usiku wakati namleta aliendelea kukaa nyumbani kwa takrbani miezi mitatu, mie naenda safari zangu na rudi kila wiki kwa kufichwa na mke wangu.

Kumbe Mama alikuja kufanikisha masuala mawili: hayo yote nilikuja kugundua badaye sana.

Yule mama alikuja kuugulia kwangu auguzwe na mtoto wake (mke wangu) na kuaga watoto wake wengine walioko jijini. Kwangu ndo pakawa kitovu cha mikutano na kuendesha vikao vyao wakati mimi sijui lolote.

Wife kanificha sijawahi ku-imagine kitendo kama hicho. Kumbe mama alikuwa ameshaathirika siku nyingi na virusi vya huu ugonjwa wa kisasa (VVU). Mwili wote ulikuwa umejaa vidonda na ulishabadilika kuwa mweusi na vipele kote.

Kuna siku nilichelewa kutoka nikakuta watoto wake wote watano wako nje, nikashangaa lakini sikumind sana kwasababu wife kaniambia wamekuja kusalimia mama yao. Nikasema poa kumbe kilikuwa kikao cha familia.

Huyu suala la pili baada ya kupokea pensheni yake alikuja kununulia watoto wake nyumba kama kitega uchumi kwasababu siku zake zilianza kuhesabika, kifo kinasongea na hali yake iliendelea kuzorota.

Lakini kumbuka mtoto wake wa mwisho ana miaka 27. Alifanikiwa kupata nyumba hapa mjini, alivyofanikisha hayo akawa anataka kuaga kurudi mkoani baada ya kukaa kwangu miezi mitatu bila mimi kujua. Hata hakuniaga, natoka safari zangu nakuta mama kasharudi mkoani wife ndo kanipa taarifa eti amenipa salamu tu.

Kama mtafutaji na asiye na makuu wala kinyongo niliyapuuzia wala wife sikumuuliza tena kuhusu Mama. Nilikaa nyumbani kama siku tano hivi, tena nikawa nataka kusafiri kuenda kwenye biashara.

Kama kawaida nilimuachia mahitaji ya nyumbani nikaondoka. Baada ya siku kama mbili wife kanipigia simu huku analia tena kilio chenyewe cha kwikwi. Nikamuuliza kulikoni, kanijibu mama anaumwa kalazwa hospitali ya rufaa na kawekewa oksijeni.

Niliduwaa kwasababu sikuwa na taarifa yoyote nyuma kwamba alikuwa anaumwa. Nikamuuliza alipata ajali? Akajibu hapana nitakuambia we tuma pesa niende nimuone.

Sikuchelewa nilijipigapiga nikamrushia laki mbili za nauli na kujikimu. Alivyofika nikaanza kumuuliza mama anaumwa nini hanijibu. Nilikazana kweli kweli kumuuliza kweli ila anaishia kuniambia yuko kwenye oksijeni.

Nikagoma kumtumia pesa mpaka aniambie Mama anaumwa nini? Baada ya siku mbili kaniambia ila baadhi ya wake zetu ni waongo tena uongo wa kitoto. Aliniambia eti anasumbuliwa na (ulcers) vidonda vya tumbo, ndo kawekwa kwenye mtungi wa oksijeni!!!!!!!

Ilikua Alhamisi mwezi jana mtu tunayefamiana naye ambaye ni jirani na ukweni pale kanipigia simu kunipa pole ya kufiwa.

Sikutaka kumuuliza nani amekufa angejua kama kuna usiri mkubwa kati yangu na wife na angenishangaa kutojua huo msiba. Niliitikia vizuri na nilihisi atakuwa mama ndo amefariki.

Kusema ukweli wife hakunipa taarifa mpaka saa 11 jioni wakati mtu alifariki saa mbili asubuhi. Nilijiongeza haraka nikapata usafiri mpaka mkoani. Nilifika mapema tu kwasababu nilikuwa na hela ya ziada nikapanda ATCL ya mchana nikidhani mazishi yatakuwa siku hiyo hiyo. Wife anakuja kunipa taarifa tayari nimeshafika kwao, hana taarifa, lengo lake lilikua nishindwe kuhudhuria mazishi.

Mazishi yalipangwa kesho yake saa saba. Wife alidhani kuniambia saa 11 sitaweza kupata usafiri wa haraka ili nikae na wafiwa pamoja na nzengo.

Kusema ukweli nilishindwa kukutana na wife hiyo siku kwasababu hasira na jaziba nikakimbia makaburini kule kushiriki na wachimbaji. Kule ndo nilipata mkanda mzima wa kuugua na kufa kwake mama mkwe wangu.

Watu wana maneno wanadai “alikufa kwa ngoma” eti alienda kujificha kwa watoto wake jijini. Anyway nilipata kila kitu pale vyote wife alivyonificha.

Sasa naomba msaada wa ushauri kwenu. Siku 40 (arobaini) zimetimia na dua ya arobaini tayari. Wife tangu wiki jana ananipigia simu nimtumie pesa za kurudi nyumbani. Nilisita kidogo sijamjibu chochote kwa sababu bado nina hasira nae, kunitumia kama boya-jinga-fala kwa kunificha hayo yote.
Yaani wife wako kakaa msibani mpaka siku 40 zimeisha?
Hana kazi!?
Hana biashara za kusaidia kusukuma maisha?
Hajali familia yake!?

By the way, msamehe tu mkuu.
Kuna wakati akili huwa inachanganyikiwa.
Na Mambo yanakuwa magumu.
Kuuguliwa sio mchezo hasa pale unapojua mgonjwa Ana ugonjwa mgumu usiokuwa na matumaini ya kupona.
Alichokosea ni kutosema tu mwanzoni kuwa mama anaumwa amekuja kujiuguza!!
Lakini hata Kama walikuwa wanajadili Mambo yao wewe yasingekuhusu mpaka yawe yanaingilia na familia yako.
 
Back
Top Bottom