Mke wangu mtarajiwa hataki mtoto wake aliyempata kabla hatujakutana atumie ubini wangu

Mke wangu mtarajiwa hataki mtoto wake aliyempata kabla hatujakutana atumie ubini wangu

Natarajia kuoa hivi karibuni na mke mtarajiwa ana mtoto wa miaka 5. Huyu mtoto namhudumia kwa kila kitu na namuonesha upendo wote kama baba yake mzazi.

Kuna shida imejitokeza baada ya kumpeleka mtoto aanze shule (nursery school ). Katika kujiandikisha nikampa jina langu la ukoo (Eg. Ngwengwe) madaftari full mkoba jina nimeandika Kelvin Ngwengwe.

Bhana eeh, mama yake alivyoona madaftari amechana chana, kumuuliza kisa nini mbona umechana madaftari ya mtoto?? Jibu alilonipa limeniacha hoi.

Namnukuu "Huyu mtoto baba yake yupo hai kwanini usitumie jina la ubini wa baba yake mzazi badala yake umetumia jina la ubini wa kwenu! Zaa mtoto wako umuite jina la kwenu"

Maamuzi niliyochukua ni kumpiga chini tu

MREJESHO
Jana ugomvi ulikuwa mkubwa ila nilitumia busara nilikaa kimya sikusema chochote alienda mbali zaidi akasema tuachane kimoyo moyo nikasema umeisha.

Leo asubuhi amekuja na mama yake mzazi kusuluhisha ugomvi binti amekiri kuwa amekosa zilikuwa ni hasira tu.

Maamuzi niliyochukua sikupepesa macho nilimwambia mama kuwa siwezi kuendelea na binti yako pia mahari niliyoitoa nimesahmee.
Mpaka sasa simu yangu ina missed call 80, sms 30
Unalazimisha undugu Baby Daddy wa single mother... Muache akalelewe na aliplyapanda mbegu atakusumbua huyo kenge....
 
Kwa kweli inakera sana kulea mtoto ambaye si wako, mbaya zaidi utakuta aliyemzalisha anakula bata tu kuhudumia mtoto hataki na majukumu yote umeachiwa wewe.

Ukisema basi sawa acha nimlee kama wakwangu na atumie ubini wangu tatizo litaanzia hapo.

Suluhisho mtoto apelekwe kwa baba yake ,kinyume na hapo usihusishwe na chochote kuhusu yeye wakitaka hivyo basi wakubali kumbadilisha ubini .
Mkuu mtoto ana badilishwa ubini akiwa haliyeokotwa au yupo kwenye kituo cha kulelea yatima na wazazi wake hawajulikani, Siyo mtoto wazaz wake wote wapo hai na Mama mtoto anamjua Baba mtoto halafu wewe Baba mlezi utake kubadili jina la Baba mtoto iko kitu hakipo.
 
Na yeye huyo aliyezalisha kwa nini asihudumie mtoto wake?
Jambo la kuhudumia mtoto wewe Baba mlezi halikuhusu, Baba mzazi atoe huduma hasitoe wewe Baba mlezi haya kuhusu na wala hutakiwi kuyajua.
 
Jina la ubini wa baba ni Cheo cha heshima anachobeba mtoto kwa heshima ya baba!
Baba aliyepambana usiku na mchana kuhakikisha mtoto unaendelea kuwa hai, mwenye afya, mwenye kukua na kupata mahitaji yote ya kijamii

Kutelekeza mtoto ni kupoteza haki zako zote mbele ya mtoto

Mtoto aliyetelekezwa anaingizwa kwenye jamii mpya inayomtunza, na kumkuza

Niwakumbushe tu, watoto wengi wanazaliwa na wababa wa nje ya ndoa lakini wanatumia ubini wa baba mwenye ndoa,

Niwakumbushe tu watoto wengi walibadilishiwa ubini ili kurisiti mitihani ya darasa la Saba enzi zile

Niwakumbushe tu, wanawake hapo zamani ndani ya ajira zao ( mama yangu kwa mfano) walibadili ubini na kuchukuwa ubini wa mume

Masingle mother wawe na shukrani kwa waume wanaojitoa kulea watoto waliotelekezwa, wawaruhusu kujenga muunganiko na watoto Hawa kwa kutumia ubini wa baba
Kwa ninavyowajua Wanawake wa Ki Bongo unaweza kukuta Baba wote wawili wanamhudumia huyo mtoto.

Yaani baba halisi anadaiwa hela ya ada sababu ni damu yake na baba mlezi/mpya nae anadaiwa hela ya ada akidanganywa kua Baba halisi amemsusa mtoto.

Anaeujua huu mchezo ni Mama ndio ndio maana anagoma Mtoto kubadilishwa ubini sababu atamueleza nini baba halisi ambae amekua akitimiza majukumu yake ipasavyo.
 
Wengi wenu msioelewa hoja ya huyu ndugu mtakuwa hamjui nini maana ya kulea mtoto, mtoto ni gharama mtoto ni dhamana mtoto ni changamoto, haiwezekani ubebe majukumu ya kumfanya mtoto awe mtu duniani bila hata ka complementary ka kuacknowledge mchango huo eti kisa mbegu si zako! Kama ana mbegu zake kwanini nipewe majukumu mimi ilhali mwenye mbegu zake yupo?! Funzo kubwa hapa ni kwamba never engage any woman having kid already! Ni kuwakimbia kama ukoma yaani.
 
Wengi wenu msioelewa hoja ya huyu ndugu mtakuwa hamjui nini maana ya kulea mtoto, mtoto ni gharama mtoto ni dhamana mtoto ni changamoto, haiwezekani ubebe majukumu ya kumfanya mtoto awe mtu duniani bila hata ka complementary ka kuacknowledge mchango huo eti kisa mbegu si zako! Kama ana mbegu zake kwanini nipewe majukumu mimi ilhali mwenye mbegu zake yupo?! Funzo kubwa hapa ni kwamba never engage any woman having kid already! Ni kuwakimbia kama ukoma yaani.
Unapewaa majukumu sababu ya Ujingaa wakooo.. Si umeongozwaa na nyegee bhasii acha unyookee ilaa sio Kutaka mtoto wa mwenzio ummiliki kwa ubin wako kisa unatoa matumiziii wew leaaa akikua akamtafute baba yake maisha yaendeleee..!!
 
Natarajia kuoa hivi karibuni na mke mtarajiwa ana mtoto wa miaka 5. Huyu mtoto namhudumia kwa kila kitu na namuonesha upendo wote kama baba yake mzazi.

Kuna shida imejitokeza baada ya kumpeleka mtoto aanze shule (nursery school ). Katika kujiandikisha nikampa jina langu la ukoo (Eg. Ngwengwe) madaftari full mkoba jina nimeandika Kelvin Ngwengwe.

Bhana eeh, mama yake alivyoona madaftari amechana chana, kumuuliza kisa nini mbona umechana madaftari ya mtoto?? Jibu alilonipa limeniacha hoi.

Namnukuu "Huyu mtoto baba yake yupo hai kwanini usitumie jina la ubini wa baba yake mzazi badala yake umetumia jina la ubini wa kwenu! Zaa mtoto wako umuite jina la kwenu"

Maamuzi niliyochukua ni kumpiga chini tu

MREJESHO
Jana ugomvi ulikuwa mkubwa ila nilitumia busara nilikaa kimya sikusema chochote alienda mbali zaidi akasema tuachane kimoyo moyo nikasema umeisha.

Leo asubuhi amekuja na mama yake mzazi kusuluhisha ugomvi binti amekiri kuwa amekosa zilikuwa ni hasira tu.

Maamuzi niliyochukua sikupepesa macho nilimwambia mama kuwa siwezi kuendelea na binti yako pia mahari niliyoitoa nimesahmee.
Mpaka sasa simu yangu ina missed call 80, sms 30
Hilo Changa la macho .umepigwa na kitu kizito jibaba jipange upya huyo cyo mwanao jibaba .mama ndiyo unajua mtoto ni wa nan
 
Natarajia kuoa hivi karibuni na mke mtarajiwa ana mtoto wa miaka 5. Huyu mtoto namhudumia kwa kila kitu na namuonesha upendo wote kama baba yake mzazi.

Kuna shida imejitokeza baada ya kumpeleka mtoto aanze shule (nursery school ). Katika kujiandikisha nikampa jina langu la ukoo (Eg. Ngwengwe) madaftari full mkoba jina nimeandika Kelvin Ngwengwe.

Bhana eeh, mama yake alivyoona madaftari amechana chana, kumuuliza kisa nini mbona umechana madaftari ya mtoto?? Jibu alilonipa limeniacha hoi.

Namnukuu "Huyu mtoto baba yake yupo hai kwanini usitumie jina la ubini wa baba yake mzazi badala yake umetumia jina la ubini wa kwenu! Zaa mtoto wako umuite jina la kwenu"

Maamuzi niliyochukua ni kumpiga chini tu

MREJESHO
Jana ugomvi ulikuwa mkubwa ila nilitumia busara nilikaa kimya sikusema chochote alienda mbali zaidi akasema tuachane kimoyo moyo nikasema umeisha.

Leo asubuhi amekuja na mama yake mzazi kusuluhisha ugomvi binti amekiri kuwa amekosa zilikuwa ni hasira tu.

Maamuzi niliyochukua sikupepesa macho nilimwambia mama kuwa siwezi kuendelea na binti yako pia mahari niliyoitoa nimesahmee.
Mpaka sasa simu yangu ina missed call 80, sms 30
Utampaje mtoto ambae sio wako ubini wako bila ya kushauriana na wazazi wake? Hata kama umemlea toka anazaliwa uamuzi wa kumpa ubini wako sio wa kwako kabisa!
 
Wengi wenu msioelewa hoja ya huyu ndugu mtakuwa hamjui nini maana ya kulea mtoto, mtoto ni gharama mtoto ni dhamana mtoto ni changamoto, haiwezekani ubebe majukumu ya kumfanya mtoto awe mtu duniani bila hata ka complementary ka kuacknowledge mchango huo eti kisa mbegu si zako! Kama ana mbegu zake kwanini nipewe majukumu mimi ilhali mwenye mbegu zake yupo?! Funzo kubwa hapa ni kwamba never engage any woman having kid already! Ni kuwakimbia kama ukoma yaani.
point hapa ni kuwa huwezi tu ukarupuka na kumpa mtoto ubuni wako bila kujadiliana na mama yake mzazi. To be honest hata kisheria haikubaliki hata siku moja! Sasa yeye anampa ubini mwengine shuleni wakati cheti cha kuzaliwa ana ubini mwengine huoni kuwa anamzalishia matatizo mtoto huko mbeleni?. Alichokosea ni kufanya maamuzi makubwa bila ya kumshauri mama mzazi wa mtoto na anabidi alijue hilo,
 
Kuna kitu Naona hakiko Sawa kwako na kwa mwenzio.

Wewe

Ulipaswa kumuuliza wanamalibaliano gan ya kulea huyo mtoto wao,inawezekana wewe unatoa pesa na kuhudumia shule nk kumbe mwenzio nae anapokea hela toka kwa mzazi mwenza zamatunzo ya mtoto.

So wew kuandika Jina lako itakuwa shida kwake.

Anatamani kurudi kwa bwana ake huyo kwako anataka ndoa tu atoe mkosi kama wanavuosemaga. Hawezi kukutishia anakuacha wakati Uko katika hatua muhimu za kumuoa na mahari umetoa.
 
Akili yako nna mashaka nayo


Yaani aweke mimba mwingine mtoto azaliwe ubin atumie wa kwako?
We utajisikiaje ukubwani unaambiwa huyo sio bab’ako huyo kakulea tu?

Et na mahali ukalipa hivi nikuulize zimo kweli?
 
Natarajia kuoa hivi karibuni na mke mtarajiwa ana mtoto wa miaka 5. Huyu mtoto namhudumia kwa kila kitu na namuonesha upendo wote kama baba yake mzazi.

Kuna shida imejitokeza baada ya kumpeleka mtoto aanze shule (nursery school ). Katika kujiandikisha nikampa jina langu la ukoo (Eg. Ngwengwe) madaftari full mkoba jina nimeandika Kelvin Ngwengwe.

Bhana eeh, mama yake alivyoona madaftari amechana chana, kumuuliza kisa nini mbona umechana madaftari ya mtoto?? Jibu alilonipa limeniacha hoi.

Namnukuu "Huyu mtoto baba yake yupo hai kwanini usitumie jina la ubini wa baba yake mzazi badala yake umetumia jina la ubini wa kwenu! Zaa mtoto wako umuite jina la kwenu"

Maamuzi niliyochukua ni kumpiga chini tu

MREJESHO
Jana ugomvi ulikuwa mkubwa ila nilitumia busara nilikaa kimya sikusema chochote alienda mbali zaidi akasema tuachane kimoyo moyo nikasema umeisha.

Leo asubuhi amekuja na mama yake mzazi kusuluhisha ugomvi binti amekiri kuwa amekosa zilikuwa ni hasira tu.

Maamuzi niliyochukua sikupepesa macho nilimwambia mama kuwa siwezi kuendelea na binti yako pia mahari niliyoitoa nimesahmee.
Mpaka sasa simu yangu ina missed call 80, sms 30
[emoji23]Mkuu pole sana labda jina lako la ukoo limemshtua hilo Ngwengwe
 
Back
Top Bottom