Mke wangu ni mchawi ama mama ndio mchawi?

Sasa mkuu kama hakuna uchawi kwanini kila mmoja ajinadi kwa kusema atanipa dawa ili nimuone mwenzake
 
Hapo wote wachawi wameshindwana hivyo wamekimbilia kwako kuitafuta amani. Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu wote wametoa dawa ili ushuhudie, kwa kawaida aliye na uwezo wa kuona visivyoonekana kwa jicho la kawaida kwa madai kuwa anawatu kichwani huwa Hana dawa zaidi ya kutegemea wale Majini/Mashetani waliopo kichwani. Kuja kwako Mungu amekuchagua wewe ili uwasaidie tumia hekima jambo linaisha hilo kiongozi.
 
Hizi Mambo zinaweza zikakupotezea Hadi taste ya maisha!
Kwa experience yangu mm na hayo Mambo na kwa yaliyonikuta hapo inaelekea Mama ako sio mtu mzuri! Mkeo anajua hilo...atakachokifanya ni kumchukua mkeo na kufanya kila mbinu muachane! Pole ndio ukubwa
 
Mkuu unayasikiliza na kuamini majini?
Shetani ni baba wa uongo cha kufanya hapo wachukue wote wapeleke kwenye maombi au mlete mchungaji aje afanye maombi hapo nyumbani kwako
 
Mama ako hana madhara kwako? Biblia iliposema "usimwache mwanamke mchawi aishi" haikudanganya. Subiri ifikre zamu ya mama yako kutoa sadaka kama hajawatoa nyie watoto wake au wajukuu zake. Au subiri hadi amrithishe mtoto wako mmoja mikoba, ndiyo utajua hana madhara.

Wachukue hao wote mkeo na mama yako, wapeleke kwenye maombi
Ndio mama hana madhara kwangu ila mke ananiambia kuwa anataka kuchukua uhai wake hivi karibuni!..
 
Huo muda unaokoment koment watu ungekuwa umeshaendeleza hadith yako
 
KAMA NI MUISLAM NJOO PM HARAKA NIKUPE MAELEKEZO YA KUFANYA BILA GHARAMA YOYOTE. HARAKA IWEZEKANAVYO.

INSHAA ALLAAH, BI IDHNI LLAAH ITAKUSAIDIA NA UTAFANIKIWA.

KAMA SI MUISLAAM, NACHELEA NAMNA YA KUKUSAIDIA...
 
Inaonekana mama yako alianzisha ligi, ndipo akakutana na mwamba;ila ndio ukubwa hutakiwi kukimbia ndoa, kusuluhisha wachukue wote wawili wapeleke kwenye maombi; atakayekataa ndio chanzo cha ugomvi.
 
UCHAWI UNADHURU HATA KAMA HUUAMINI...UTAKUDHURU TU ALLAAH AKIRUHUSU UKUDHURU...NA VILE VILE MWENYE UWEZO WA KUZUIA MADHARA YA UCHAWI NI ALLAAH...

CHUKUA KILA AINA YA TAHADHARI YA UHAKIKA NA SALAMA JUU YA MADHARA YA UCHAWI WA MAMA YAKO NA MKEO.
 
Pole sana kwakweli ni mtihani. Nimejikuta nacheka sana kama ni mazuri vile
 
Okey mkuu nimekuelewa,je hawa wanao nifuata inbox ni waganga au watu wa maombi?..ningependa zaidi wangejipambanua maana hata mie nina hofu nikienda kiuganga nitaweza kupotea zaidi

Hao wa inbox achana nao, achana na wafuatao:

  • Manabii wanaofuatwa na famous.
  • Kwenda kichwa kichwa kanisan

Cha kufanya:

Create muscle - Omba Mungu peke yako serious, hata Kama Hujui kuomba wewe funga na mwombe Mungu tu alone.

Nina uhakika atakuongoza Kwenda Kanisa Fulani ambalo litakuwa la Msaada kwako, sincerely: Kuna Makanisa Mazuri Sana Dar and are not famous!

Hapa pagumu, ukiyumba hapa unaharibu kila kitu, don't take this light, you real need God at a personal level kwanza, then maombi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…