Mke wangu wa ndoa kapewa Mimba na mtu mwingine

Mke wangu wa ndoa kapewa Mimba na mtu mwingine

Duh.....ndoa zina kazi sana!
 
Aisee pole sana kaka yangu, ila jiulize kama wewe je bado wampenda, na uko tayari kumsamehe na una uhakika gani kama hatorudia na ukizingatia bado waishi mbali na yeye?
 
Kapime DNA ya mtoto majibu nenda nayo kanisani kama ushahidi ili ndoa itenguliwe. Sio mwanamke huyo
 
Huyu mtoa mada kaniuzi hadi nataka kutapika hivi we kidume kweli?! Visa vyote upo tu!? Au ndio wale mnasomaa weee hamuonji kokote mkimaliza chuo baada ya kupata kazi mnaoa sasa unamuona mwanamke Kama maini yako yakotoka unakufa!! Ushauri wangu endelea nae na mtoto kambatize!!
 
Wana jamvi naomba msaada wenu katika jambo hili;Mimi mwaka 2009 nilifunga ndoa na binti mmoja ambae nilikutana nae kazin na baada ya kama miez kadhaa tuliamua kufunga ndoa kanisani lakin wakati nafunga nae ndoa yeye alikuwa tayar kaacha kaz katika shirika tulilokutana so baada ya kufunga ndoa maisha yaliendelea lakin mie nikikaa mkoan yeye akikaa Dar kutokana na majukumu ya kikazi mie nafanya mkoan yeye Dar kwan alipata kaz nae baada ya kukaa mtaan muda flan.
Mahusiano yaliendelea vizur tu lakin nikaja gundua ya kwamba anachat na mtu ambae tuliwah ishi nae mkoan na nilipoamua kumtafuata akasema binti alimwambia hajaolewa,akakubali kuacha kuchat nae.Vitimbi vikawa vingi sana hatak kuja tena mkoan kuniona mpaka mie niende Dar na kwa bahat mbaya mie nilikosa likizo kwa miaka 3 mfululizo na nikawa kama kuja Dar ni training ya cku mbil mpaka tatu nikawa nakutana na vituko sana mara ninuniwe mara kahama nyumba wakati yy yupo pale pale,stand kuja kunipokea hatak na wakat tuna gar la kutumia nyumban.
Mahusiano yakawa yanaenda kwa mazoea tu mwaka jana kuna mtu akanipigia cm kunipongeza kwa ujauzito wa mke na nilipata shock ukitegemea nina mwaka cjaonana nae kimwili kwan nikienda training fup mara nyingi anasema yupo period,nikazima so kwa kukubali ile hongera nikaanza upelelezi na wakati huo alikuwa anaweza akakaa hata wiki asipokee simu yangu na akipokea da sio dharau hizo kwamba anitak.Kupitia dada ake mmoja akakubali kuniambia ukwel wa jambo hilo kwamba ana mimba na wao wamejua co yangu kumuuliza hawaezi nikawa na uhakika na jambo hilo nikaamua kumwambia tuweke sawa kwan naamin kateleza na tuendelee na maisha kama kawaida akasema hatak na niendelee na maisha yangu kama kawaida japo nilimbembeleza sana
Mwez wa kwanza nikaamua kwenda Dar kwan nilipata ruhusa kama ya siku 9,ndugu zangu wakasema niende nikahakikishe kwa macho yangu na kwa msaaada wa yule dada alinicholea mchoro muda ambao yupo nikaenda nilimkuta na yy ndio alinifungulia mlango kwanza aliponiona kidogo asifungue mlango ila akaamua baada ya dk kama tano akafungua nikawa na aman sana kumwona na ile hali japo yeye alikosa raha kabisa nikajaribu kumsocialise asijione mkosaji nikapiga stori baada ya dk kumi nikaaga kuondoka kwan cku iliyofuata nilikuwa narud mkoan japo nilimwambia ntaenda kesho yake na ndio nikathibitisha ya kwamba ana mimba
Baada ya kurud mkoan akawa amerudisha sana mapenz kama mwanzo simu za mara kwa mara na msg sasa mie nami kuogopa acjepata matatizo wakat wa uzaz nikawa namjal kama mie ndio mwenye mimba na akawa na aman kila ktu akawa ananiambia kuhusu mimba hyo,Juz Mungu kasaidia kajifungua mtoto wa kike nikaambiwa na mpaka sasa kila ktu maambiwa mtoto anasumbua hik mara kile kwa kifup kaona kama mtoto wangu
Picha ya cku ya harus aliitoa sebulen muda sana lakin sasa nimeambiwa kaiweka sebulen tena na anaonesha kukumbuka kuna mtu alimpenda,sasa wana jamvi mie naomba ushauri wenu nafanyaje ktk suala hilo,mimba sio yangu na je kama nikiamua kuwa na mtu mwingine je ntafunga nae ndoa kwan mie ni mkristo?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

ndugu yangu kimbia, ikiwezekana mpaka upoteze mguu hafai huyo!!!!!!!!!!!!!!! utajajuta.
 
kuoa ni kujiongezea matatizo. pole sana mkuu. mia

Mkuu sio kihivyo ... huyu Bwana ana behave very childish au Inocent? ... anafaa kuishi mbinguni na si hapa duniani ...seems to be very naive maybe?
 
Nafikiri hana watu wa kumshahuri vizuri, inavyoelekea huyo mkewe kakataliwa na jamaa aliyempa mimba sasa anajidai anarudisha majeshi. kama alishindwa kujizuia kwa mara ya kwanza ndiyo ataweza sasa ambapo huyu bwana bado yuko mbali nae? Trigger funguka macho yako kaka yangu hata biblia inaruhusu kumwacha mke mzinzi.
 
Achana naye huyo co mwanamke mwema.vilevile hyo ni skendo mme mwenzako kuja kukuzalia mtoto ndan ya familia yako as if we hauwez.kuhusu suala la ukristo na ndoa hyo tayari iko kinyume na maagano ya din,ndoa ni kiapo cha wawili sasa kama mwenzako kazin nje tayari hyo imeharbika kwa wote.piga chin tafuta dem mwngn

kaka fanyia kazi ushauri huu
 
Nathubutu kusema ulichagua kazi over ndoa yako. Ndoa sasa imekufa, eleza kama kazi nayo imekufa, wapi! Kazi iko palepale! Ulitakiwa kubalansi vitu hivi. Mlikuwa hamshauriani? Something was not right from the beggining! Kwa sala la ndoa kuvunjwa ili uoe tena linawezekana endapo ushahidi etc vitakuwepo. Nimeshuhudia ndoa mbili zimevunjwa tena mimba zimehusishwa. Mlolöngo ni mrefu pia. Uamuzi wako tu. Ila ukijaoa tena wajibika kiume, alaa!
 
Kama nafsi yako ilikutuma kumsamehe basi msamehe moja kwa moja. Nina jamaa yangu ilimtokea hiyo kitu alimsamehem mke wake mpaka leo wanaishi.
 
Jamaa lililotia mimba limesepa, demu akaona ajirudishe kwa bushoke wake, wewe bushoke hebu jitambue bana, piga chini dakika sifuri.
 
Anaomba ushauri kama anaweza kumuacha na kuoa mwingine kwa sababu alifunga ndoa ya kikristo
sasa kama alitakaushauri huo si aende kule alikofungia ndoa wamshauri?...kweli wanaume wengine mna roho ngumu...binafsi nikisikia ana cheat tu napiga chini sembuse kuzaa mtoto kabisa! halafu unakuja kutuomba ushauri nini cha kufanya.....mi nakushauri uendelee nae maana huna guts za kumuacha!
 
Duh Wewe kweli ni mshamba wa mapenzi....Kuna kuomba ushauri hapo? Upi tena?...Basi endelea naye kaka.
 
hivi ww unakaa mwaka mzima hujaonana na mke wako unategemea nin? Acha wakutombee ili ujue maana ya ndoa alah, kama n kaz ulishindwa kumhamishia huko uliko au na ww una mke huko?
 
Achana naye huyo co mwanamke mwema.vilevile hyo ni skendo mme mwenzako kuja kukuzalia mtoto ndan ya familia yako as if we hauwez.kuhusu suala la ukristo na ndoa hyo tayari iko kinyume na maagano ya din,ndoa ni kiapo cha wawili sasa kama mwenzako kazin nje tayari hyo imeharbika kwa wote.piga chin tafuta dem mwngn
Halafu ni mtoto wa kwanza. Aaah, mimi siwezi kabisa, yaani bora hata angekuwa wa pili au wa tatu, yaani tumbo la mkeo limefunguliwa na kunguru mwitu ilihali wewe ndiyo uliyeoa kwa harusi kanisani? Hata ingekuwaje siwezi kuishi naye.

Lakini wewe sikiliza moyo wako, kama uliweza kwenda kwake ukashuhudia hali aliyonayo na bado ukaendelea kupiga naye story, basi una moyo wa ajabu sijawahi kuona. Kuna akina siye hapa ungekuwa ndiyo mwisho wa mawasiliano.

Habari ya kufunga ndoa nyingine kwangu haina msingi sana, ndoa tunafunga ili kulifurahisha kanisa tu, biblia haijasema popote kwamba ufunge ndoa. Na zaidi ya yote, mbinguni hakuna kuoana, hata ungeoa wake kumi, siku ya hukumu hutaulizwa ni yupi alikuwa mke wako.

Piga chini, tafuta anayekufaa, endelea na maisha bila kujali kanisa linasema nini. Maisha ni yako binafsi, siyo ya kanisa wala ya wachungaji au majirani. Na siku ya hukumu hutasimama na yeyote kati ya hao. Wakati mwingine usiwasikilize sana wachungaji, jisomee biblia mwenyewe, halafu ujipe amani ya moyo, bila kujali wengine wanakutazamaje.
 
Back
Top Bottom