Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi

Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi

Mbona hata mimi natumia bang au kwakuwa wema ni msanii na mimi ni mwananchi wa kawaida to
 
Huko ni kukomoana ila ipo siku mwisho wa ubaya utafika na huwa ni aibuuuu
 
Toka wajue kupima mkojo imekua tabhhhuuuu thuphuuuuu
 
Wakili: Shahidi, wewe kama mkemia bangi ina madhara gani kwa binadamu?

Shahidi: Bangi inasababisha mtumiaji kupata ulevi ambao hauwezi kutibika na husababisha mtumiaji kuharibikiwa akili
 
Hata na yule jamaa alie kataa kuchukuliwa aliogopa kugundulikaaaa.

Xafi xaaana serikali ya awamu ya tano kwa umakini muliotuonesheaaaa
We ni punguani mkemia ni kitengo cha serikali na Polisi walomuwekea wema bangi ni kitengo cha serikali huku serikali ikiwa ni bashite aliyeshikilia kichwa cha sisonje, bashite ie serikali ndye aliyeamuru wema akamatwe na apimwe mkojo, naamini siku moja mahakama ya dunia itatoa kibali sisonje, NASEMA TENA SISONJE apimwe mkojo ndo watanzania mtashangaa kiasi cha ubongo wake kilivyoharibiwa na unga cha sisonje kama tu maneno ya lema 2018 hayatatimia
 
We ni punguani mkemia ni kitengo cha serikali na Polisi walomuwekea wema bangi ni kitengo cha serikali huku serikali ikiwa ni bashite aliyeshikilia kichwa cha sisonje, bashite ie serikali ndye aliyeamuru wema akamatwe na apimwe mkojo, naamini siku moja mahakama ya dunia itatoa kibali sisonje, NASEMA TENA SISONJE apimwe mkojo ndo watanzania mtashangaa kiasi kilichoharibiwa na unga cha sisonje kama tu maneno ya lema 2018 hayatatimia
Hahahahahaha, kweli mkuu
 
Mkemia ilibidi nae apimwe kinyesi maana anaonekana ubongo wake hauko sawa
 
Sasa huo mkojo umekutwa na bangi ya msokoto au puli zima?
 
Hii mikojo ni kweli ya watu hawa? Au ni zengwe? 😱
ni ya kwao Mkuu, ila ujinga waliufanya wenyewe kwanini walikubali kuutoa, kama unajijua hauko vizuri ni bora ugome.
 
Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, baada ya kupima mkojo wa Wema Sepetu walibaini una bangi.

SHAHIDI wa kwanza, Mkemia Elias Mulima (40), katika kesi inayomkabili Wema Sepetu na wenzake, amedai mahakamani kuwa mshtakiwa huyo alifikishwa ofisini kwake akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi na baada ya kutoa sampuli ya mkojo wake, vipimo vilionyesha ni mtumiaji wa bangi.

Hatua hiyo ilizua mabishano ya kisheria baadaye.

Aidha, shahidi huyo alidai alipokea sampuli ya majani na baada ya kufanya vipimo alibaini kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.
Shahidi huyo alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kalula.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano ya wakili Kalula na shahidi:

Wakili: Shahidi unakumbuka Februari 6, mwaka huu ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa ofisini.

Wakili: Je, siku hiyo nini kilitokea?

Shahidi: Siku hiyo nilipokea kielelezo kutoka jeshi la polisi kama sehemu ya majukumu yangu ya kazi.
Wakili: Ulipokea kutoka kwa nani?

Shahidi: Nilipokea kutoka kwa Koplo Robart.

Wakili: Je, kielelezo hicho kilikuwa kinahusu nini?

Shahidi: Kielelezo hicho kilikua sampuli ya misokoto idhaniwayo kuwa dawa za kulevya aina ya bangi ambacho kililetwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili kuthibitisha kuwa ni dawa za kulevya au la.

Wakili: Nini kilifuata?

Shahidi: Nilipima uzito wa yale majani nikapata gramu 1.08, nilianza kufanyia uchunguzi wa awali kwa kuchanganya na dawa maalumu na majibu yalikuwa ni bangi. Nilifanya kipimo cha pili kupitia mitambo maalumu majibu yakaonyesha kuwa ni bangi.

Wakili: Shahidi, wewe kama mkemia bangi ina madhara gani kwa binadamu?

Shahidi: Bangi inasababisha mtumiaji kupata ulevi ambao hauwezi kutibika na husababisha mtumiaji kuharibikiwa akili.
Wakili: Shahidi iambie mahakama Februari 8, mwaka huu unakumbuka nini?

Shahidi: Nakumbuka niliandaa taarifa kuhusiana na uchunguzi wa sampuli ya dawa zidhaniwazo kuwa za kulevya aina ya bangi na majibu yalitoa kuwa majani yale ni bangi.

Wakili: Je, unakumbuka tukio gani jingine kutokea siku hiyo?

Shahidi: Nilipokea sampuli nyingine ya mkojo wa Wema Sepetu, ambaye aliletwa ofisini kwangu akiwa chini ya ulinzi wa Inspekta Willy na askari mwanamke, Marry.

“Nilimpa kontena maalumu na akiwa chini ya ulinzi wa Marry alikwenda kutoa mkojo na nilipoufanyia vipimo majibu yalionyesha kuwa na dawa za kulevya aina ya bangi” alidai shahidi huyo.

Shahidi alidai kuwa baada ya kumaliza kufanya vipimo aliandaa taarifa, kuiweka sahihi na ilihakikiwa na Kaimu Mkemia Mkuu.
Akifafanua zaidi alidai kuwa bangi inaonekana kwenye mkojo ikikaa muda wa siku 28.

Shahidi huyo aliomba mahakama kupokea taarifa zake mbili za uchunguzi wa bangi na mkojo.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala alipinga mahakama kupokea taarifa hiyo kama kielelezo katika kesi hiyo kwa sababu ilikuwa na mapungufu ya kisheria.

Kibatala alidai kuwa taarifa hiyo haijakidhi matakwa ya kisheria kwa uchunguzi wa mtu aliyeko chini ya ulinzi kwamba ni lazima akaape mbele ya hakimu.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulidai kuwa taarifa hiyo iko sahihi kisheria na kwamba mahakama itupilie mbali pingamizi la utetezi.

Hakimu Simba alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zoe mbili mahakama yake itatoa uamuzi keshokutwa.

Mbali na Wema, washtakiwa wengine ni wafanyakazi wake Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Februari 4, mwaka huu eneo la Kunduchi Ununio, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Katika Shitaka la pili, katika tarehe tofauti kati ya Februari Mosi na 3, mwaka huu, mahali pasipojulikana, jijini Dar es Salaam, Wema alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.

Washtakiwa walikana mashitaka na waliposomewa maelezo ya awali walikiri anuani zao na majina tu.

Chanzo: Nipashe

=======
Wema Sepetu kukamatwa na kuhukumiwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya
Yaliyojiri katikati ya mchakato wa upelelezi wa kesi ya wema
Wema kukutwa na kesi ya kujibu
Kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini
Duuh
 
Back
Top Bottom