Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Toka wajue kupima mkojo imekua tabhhhuuuu thuphuuuuu
Kisa tuu wanaendeshwa kimihemko so stupidKweli tumepoteza mwelekeo.
Gharama zote ; muda na pesa tumepoteza na tunaendelea kupoteza kubaini kuwa MSANII mmoja ni mvuta bangi?
Halafu inafanywa ni JAMBO LA KITAIFA?
Sent using Jamii Forums mobile app
Sio mkojo ? 😀Akatoe ya moyoni sasa!
We ni punguani mkemia ni kitengo cha serikali na Polisi walomuwekea wema bangi ni kitengo cha serikali huku serikali ikiwa ni bashite aliyeshikilia kichwa cha sisonje, bashite ie serikali ndye aliyeamuru wema akamatwe na apimwe mkojo, naamini siku moja mahakama ya dunia itatoa kibali sisonje, NASEMA TENA SISONJE apimwe mkojo ndo watanzania mtashangaa kiasi cha ubongo wake kilivyoharibiwa na unga cha sisonje kama tu maneno ya lema 2018 hayatatimiaHata na yule jamaa alie kataa kuchukuliwa aliogopa kugundulikaaaa.
Xafi xaaana serikali ya awamu ya tano kwa umakini muliotuonesheaaaa
Hahahahahaha, kweli mkuuWe ni punguani mkemia ni kitengo cha serikali na Polisi walomuwekea wema bangi ni kitengo cha serikali huku serikali ikiwa ni bashite aliyeshikilia kichwa cha sisonje, bashite ie serikali ndye aliyeamuru wema akamatwe na apimwe mkojo, naamini siku moja mahakama ya dunia itatoa kibali sisonje, NASEMA TENA SISONJE apimwe mkojo ndo watanzania mtashangaa kiasi kilichoharibiwa na unga cha sisonje kama tu maneno ya lema 2018 hayatatimia
anawajua upumbavu wao uchochezi na bangi haviusianindio maana lisu aligomea ili aibu isimpate
ni ya kwao Mkuu, ila ujinga waliufanya wenyewe kwanini walikubali kuutoa, kama unajijua hauko vizuri ni bora ugome.Hii mikojo ni kweli ya watu hawa? Au ni zengwe? 😱
DuuhOfisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, baada ya kupima mkojo wa Wema Sepetu walibaini una bangi.
SHAHIDI wa kwanza, Mkemia Elias Mulima (40), katika kesi inayomkabili Wema Sepetu na wenzake, amedai mahakamani kuwa mshtakiwa huyo alifikishwa ofisini kwake akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi na baada ya kutoa sampuli ya mkojo wake, vipimo vilionyesha ni mtumiaji wa bangi.
Hatua hiyo ilizua mabishano ya kisheria baadaye.
Aidha, shahidi huyo alidai alipokea sampuli ya majani na baada ya kufanya vipimo alibaini kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.
Shahidi huyo alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.
Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kalula.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano ya wakili Kalula na shahidi:
Wakili: Shahidi unakumbuka Februari 6, mwaka huu ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa ofisini.
Wakili: Je, siku hiyo nini kilitokea?
Shahidi: Siku hiyo nilipokea kielelezo kutoka jeshi la polisi kama sehemu ya majukumu yangu ya kazi.
Wakili: Ulipokea kutoka kwa nani?
Shahidi: Nilipokea kutoka kwa Koplo Robart.
Wakili: Je, kielelezo hicho kilikuwa kinahusu nini?
Shahidi: Kielelezo hicho kilikua sampuli ya misokoto idhaniwayo kuwa dawa za kulevya aina ya bangi ambacho kililetwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili kuthibitisha kuwa ni dawa za kulevya au la.
Wakili: Nini kilifuata?
Shahidi: Nilipima uzito wa yale majani nikapata gramu 1.08, nilianza kufanyia uchunguzi wa awali kwa kuchanganya na dawa maalumu na majibu yalikuwa ni bangi. Nilifanya kipimo cha pili kupitia mitambo maalumu majibu yakaonyesha kuwa ni bangi.
Wakili: Shahidi, wewe kama mkemia bangi ina madhara gani kwa binadamu?
Shahidi: Bangi inasababisha mtumiaji kupata ulevi ambao hauwezi kutibika na husababisha mtumiaji kuharibikiwa akili.
Wakili: Shahidi iambie mahakama Februari 8, mwaka huu unakumbuka nini?
Shahidi: Nakumbuka niliandaa taarifa kuhusiana na uchunguzi wa sampuli ya dawa zidhaniwazo kuwa za kulevya aina ya bangi na majibu yalitoa kuwa majani yale ni bangi.
Wakili: Je, unakumbuka tukio gani jingine kutokea siku hiyo?
Shahidi: Nilipokea sampuli nyingine ya mkojo wa Wema Sepetu, ambaye aliletwa ofisini kwangu akiwa chini ya ulinzi wa Inspekta Willy na askari mwanamke, Marry.
“Nilimpa kontena maalumu na akiwa chini ya ulinzi wa Marry alikwenda kutoa mkojo na nilipoufanyia vipimo majibu yalionyesha kuwa na dawa za kulevya aina ya bangi” alidai shahidi huyo.
Shahidi alidai kuwa baada ya kumaliza kufanya vipimo aliandaa taarifa, kuiweka sahihi na ilihakikiwa na Kaimu Mkemia Mkuu.
Akifafanua zaidi alidai kuwa bangi inaonekana kwenye mkojo ikikaa muda wa siku 28.
Shahidi huyo aliomba mahakama kupokea taarifa zake mbili za uchunguzi wa bangi na mkojo.
Hata hivyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala alipinga mahakama kupokea taarifa hiyo kama kielelezo katika kesi hiyo kwa sababu ilikuwa na mapungufu ya kisheria.
Kibatala alidai kuwa taarifa hiyo haijakidhi matakwa ya kisheria kwa uchunguzi wa mtu aliyeko chini ya ulinzi kwamba ni lazima akaape mbele ya hakimu.
Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulidai kuwa taarifa hiyo iko sahihi kisheria na kwamba mahakama itupilie mbali pingamizi la utetezi.
Hakimu Simba alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zoe mbili mahakama yake itatoa uamuzi keshokutwa.
Mbali na Wema, washtakiwa wengine ni wafanyakazi wake Angelina Msigwa na Matrida Abas.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Februari 4, mwaka huu eneo la Kunduchi Ununio, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.
Katika Shitaka la pili, katika tarehe tofauti kati ya Februari Mosi na 3, mwaka huu, mahali pasipojulikana, jijini Dar es Salaam, Wema alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.
Washtakiwa walikana mashitaka na waliposomewa maelezo ya awali walikiri anuani zao na majina tu.
Chanzo: Nipashe
=======
Wema Sepetu kukamatwa na kuhukumiwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya
Yaliyojiri katikati ya mchakato wa upelelezi wa kesi ya wema
- Wema Sepetu, Mr. Blue, TID, Recho wahusishwa na Dawa za Kulevya. Watakiwa kuripoti kituo cha Polisi
- Kamanda Siro: Wema Sepetu, TID na Nyandu Tozi bado wanashikiliwa na jeshi la polisi
- Sakata la Madawa ya Kulevya: Wema Sepetu afikishwa Mahakamani, apata dhamana
- Wema Sepetu kapatikana na bangi
Wema kukutwa na kesi ya kujibu
- Tundu Lissu kumtetea Wema Sepetu
- Maajabu: Serikali haiwajui Vigogo wa Dawa za Kulevya hadi inataka Wema awatajie?
- Makonda kumfuata Wema mahabusu nyakati za usiku, hii imekaaje?
- Sauti ya Wema Sepetu iliyosambaa akiwatoa hofu Mashabiki
- Kesi ya Wema Sepetu hadi mwakani
- Wema Sepetu amefiwa, kesi yake yapigwa kalenda
- Dawa za Kulevya: Wema adai Makonda anatembea na Agnes Masogange ndio maana hakamatwi
- Wema Sepetu Apandishwa Tena Kizimbani Kisutu leo
- Vita ya Dawa za Kulevya: Steve Nyerere alivyopiga kambi Bungeni Kumuokoa Wema Sepetu
- Kesi ya Wema Sepetu yaahirishwa, uchunguzi haujakamilika
- Kutoka mahakamani: Wema Sepetu hakufanyiwa upekuzi kwenye maungo ya mwili wake, asema Hakimu
- Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi
- Kibatala aandika barua ya kujitoa kesi ya Wema Sepetu, Alberto Msando aandika barua ya kuwa wakili mpya
- KISUTU: Wema Sepetu afika na Wakili wake Msando kwenye kesi. Diamond na Hamisa nao wafika Mahakama ya watoto
- Shahidi kesi ya Wema asema bangi ilikutwa jikoni
- Kisutu: Korti yakataa vielelezo vya ushahidi kesi ya Wema Sepetu. Masogange akutwa na kesi ya kujibu
Kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini