Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi

Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi

waliitwa kujisalimisha na kukiri.
Walioitikia ni wachache...waliokataa ni wengi.

Usijidai msahaulifu!
Kwahiyo sheria zetu zinasema uki kiri kosa una achiwa na ukikana kosa una stahili kufungwa?
Yaani kukuiri kutumia cocaine kusiwe big issue, ila kukana matumizi ya bangi kupelekee matumizi mabovu ya pesa ya umma?
 
Hata kama Wema anavuta na mkojo ulikuwa na bangi sijaona bado kesi ya kujibu sababu ya mihemko ya Jeshi la Polisi.

Nilishasema Jeshi la Polisi ni wahuni na hawana weledi wa kufanya kazi zao,

Utampimaje mtu mkojo bila ya kibali cha mahakama halafu upeleke mkojo huo ukawe ushahidi mahakani?

Kama bangi inakaa kwenye mkojo siku 28 walikuwa na haraka gani ya kupima bila kibali cha mahakama?

Japokuwa ana vyeti vyake vya chuo kikuu lakini Sirro ni Zero brain, ameweka tamaa ya madaraka mbele mpaka kasahau wajibu wake kama POLISI.
Hahahaaa...hao mawakili wenu wanawajaza pumba kichwani afu mnakuja kuonesha upumbavu wenu humu, vitu usivyovijua usikurupuke kuvieleza, nani kakudanganya kibali cha mahakama ni cha lazima? kibali kinaombwa pale tu mtuhumiwa hayuko tayari kupima kwa hiari kama vile alivyofanya Lissu, hapo Wema wala hachomoki na hata hao mawakili wake wanalielewa hilo.
 
Hahahaaa...hao mawakili wenu wanawajaza pumba kichwani afu mnakuja kuonesha upumbavu wenu humu, vitu usivyovijua usikurupuke kuvieleza, nani kakudanganya kibali cha mahakama ni cha lazima? kibali kinaombwa pale tu mtuhumiwa hayuko tayari kupima kwa hiari kama vile alivyofanya Lissu, hapo Wema wala hachomoki na hata hao mawakili wake wanalielewa hilo.



Kutoka Bush Lawyer! na sasa unataka kuwa Sheikh Yahaya (Mnajimu) wewe una ushahidi gani kuwa Wema alikubali? Una ushahidi gani kuwa Wema aliweka sahihi ya kuridhia mkojo wake utumike kwenye vipimo? Una ushahidi gani kuwa Wema hakulazimishwa kutoa mkojo? Usiongee vitu usivyovijua kama punguwani. Umeona maelezo ya upande mmoja tu, mwandani kashakubana, na matokeo umeshayajua wewe na unaanza kutoa maneno ya khanga.

Kama hujui mambo ya mahakama utulie kama unanyolewa. Ushahidi lazima ufate vifungu vya sheria na pasipo shaka ndiyo unatumika kama kielelezo mahakamani. Ndiyo maana mahakani kuna maridhiano. Ujinga umekujaa ndiyo maana unashindwa hata kufikiri critically unaacha wakina Polepole wawashikie akili. Mafunzo ya chipukizi yamewafanya mmekuwa kama mazezeta.
 
Watanzania watu wa ajabu sana, kwahiyo majadiliano ya makinikia tumeachana nayo tunajadili mkojo wa wema!!
 
Sidhani kama ni jambo jema kuwataja kwa majina wataalamu wetu. Mkemia aajiri wanasheria watakao kuwa wanasimama mahakamani na kama kuna haja ya kuwahoji wahojiwe kwa siri, watalamu wetu wanakuwa katika risk ya kulipiziwa visasi,
Upo sahihi kabisa, hasa hawa wakemia wa kitengo cha madawa ya kulevya.
 
Napata mashaka na vijana humu mnaotetea uovu, cjui ni cdm au nyinyiemu. Nahisi mkipimwa mikojo yenu karibu wote mtakutwa na hiyo kitu ya Arusha, hahahaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, baada ya kupima mkojo wa Wema Sepetu walibaini una bangi.

SHAHIDI wa kwanza, Mkemia Elias Mulima (40), katika kesi inayomkabili Wema Sepetu na wenzake, amedai mahakamani kuwa mshtakiwa huyo alifikishwa ofisini kwake akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi na baada ya kutoa sampuli ya mkojo wake, vipimo vilionyesha ni mtumiaji wa bangi.

Hatua hiyo ilizua mabishano ya kisheria baadaye.

Aidha, shahidi huyo alidai alipokea sampuli ya majani na baada ya kufanya vipimo alibaini kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.
Shahidi huyo alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kalula.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano ya wakili Kalula na shahidi:

Wakili: Shahidi unakumbuka Februari 6, mwaka huu ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa ofisini.

Wakili: Je, siku hiyo nini kilitokea?

Shahidi: Siku hiyo nilipokea kielelezo kutoka jeshi la polisi kama sehemu ya majukumu yangu ya kazi.
Wakili: Ulipokea kutoka kwa nani?

Shahidi: Nilipokea kutoka kwa Koplo Robart.

Wakili: Je, kielelezo hicho kilikuwa kinahusu nini?

Shahidi: Kielelezo hicho kilikua sampuli ya misokoto idhaniwayo kuwa dawa za kulevya aina ya bangi ambacho kililetwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili kuthibitisha kuwa ni dawa za kulevya au la.

Wakili: Nini kilifuata?

Shahidi: Nilipima uzito wa yale majani nikapata gramu 1.08, nilianza kufanyia uchunguzi wa awali kwa kuchanganya na dawa maalumu na majibu yalikuwa ni bangi. Nilifanya kipimo cha pili kupitia mitambo maalumu majibu yakaonyesha kuwa ni bangi.

Wakili: Shahidi, wewe kama mkemia bangi ina madhara gani kwa binadamu?

Shahidi: Bangi inasababisha mtumiaji kupata ulevi ambao hauwezi kutibika na husababisha mtumiaji kuharibikiwa akili.
Wakili: Shahidi iambie mahakama Februari 8, mwaka huu unakumbuka nini?

Shahidi: Nakumbuka niliandaa taarifa kuhusiana na uchunguzi wa sampuli ya dawa zidhaniwazo kuwa za kulevya aina ya bangi na majibu yalitoa kuwa majani yale ni bangi.

Wakili: Je, unakumbuka tukio gani jingine kutokea siku hiyo?

Shahidi: Nilipokea sampuli nyingine ya mkojo wa Wema Sepetu, ambaye aliletwa ofisini kwangu akiwa chini ya ulinzi wa Inspekta Willy na askari mwanamke, Marry.

“Nilimpa kontena maalumu na akiwa chini ya ulinzi wa Marry alikwenda kutoa mkojo na nilipoufanyia vipimo majibu yalionyesha kuwa na dawa za kulevya aina ya bangi” alidai shahidi huyo.

Shahidi alidai kuwa baada ya kumaliza kufanya vipimo aliandaa taarifa, kuiweka sahihi na ilihakikiwa na Kaimu Mkemia Mkuu.
Akifafanua zaidi alidai kuwa bangi inaonekana kwenye mkojo ikikaa muda wa siku 28.

Shahidi huyo aliomba mahakama kupokea taarifa zake mbili za uchunguzi wa bangi na mkojo.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala alipinga mahakama kupokea taarifa hiyo kama kielelezo katika kesi hiyo kwa sababu ilikuwa na mapungufu ya kisheria.

Kibatala alidai kuwa taarifa hiyo haijakidhi matakwa ya kisheria kwa uchunguzi wa mtu aliyeko chini ya ulinzi kwamba ni lazima akaape mbele ya hakimu.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulidai kuwa taarifa hiyo iko sahihi kisheria na kwamba mahakama itupilie mbali pingamizi la utetezi.

Hakimu Simba alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zoe mbili mahakama yake itatoa uamuzi keshokutwa.

Mbali na Wema, washtakiwa wengine ni wafanyakazi wake Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Februari 4, mwaka huu eneo la Kunduchi Ununio, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Katika Shitaka la pili, katika tarehe tofauti kati ya Februari Mosi na 3, mwaka huu, mahali pasipojulikana, jijini Dar es Salaam, Wema alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.

Washtakiwa walikana mashitaka na waliposomewa maelezo ya awali walikiri anuani zao na majina tu.

Chanzo: Nipashe

Huyu shaidi Mkemia anapaswa kwenda shule tena maana hajui upande mwingine wa matumizi ya bhangi kama dawa ya uponyaji kwa mwili wa binadamu. Yafuatayo ni mafao
While you might have heard many people say that weed can cause diseases, scientific researches and studies show that it can actually cure many diseases and physical problems. From helping fight Glaucoma to controlling epileptic seizures to helping prevent cancer from spreading to slowing Alzheimer’s to easing multiple sclerosis pain to reducing Hepatitis C side-effects to treating inflammatory bowels to relieving arthritis pain to helping you get through chemo to a lot more, scientific researches confirm the effectiveness of marijuana.

You might be wondering if medical marijuana has so many benefits, why isn’t it legal already? Well, the big pharmaceutical companies can crumble down if a naturally growing, dirt-cheap plant gets legal and starts curing diseases which can otherwise only be cured with their expensive medicines at this point. Despite all that, medical cannabis is becoming legal in most of the states very quick
Smoking weed isn’t actually that bad for your lungs, and smokers actually have improved lung function when compared to both cigarette smokers – and people who have never smoked either.

The researchers, writing in the Journal of the American Medical Association, say that the big drags taken by weed smokers may actually ‘train’ lungs to be more efficient.

We investigated the effects of cannabis smoked naturalistically on schizotypy and divergent thinking, a measure of creativity.

Smoking weed helps patients give up opiates such as heroin, a new study has found.

A study in the journal Obesity found that regular weed smokers are less likely to be obese than non-smokers.
 
Wema anatafutwa kama anatumia je waliokiri kuwa wanatumia kila TID mbona wameachiwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani ni shida sana, mateja wa madawa ya kulevya wanahamasishwa waende kwenye vituo vinavyotoa tiba hizo tena bure kabisa. Basi na hao mateja wafunguliwe mashtaka pia. Kusiwena double standard sababu kafanya kosa mtu fulani.
 
Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, baada ya kupima mkojo wa Wema Sepetu walibaini una bangi.

SHAHIDI wa kwanza, Mkemia Elias Mulima (40), katika kesi inayomkabili Wema Sepetu na wenzake, amedai mahakamani kuwa mshtakiwa huyo alifikishwa ofisini kwake akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi na baada ya kutoa sampuli ya mkojo wake, vipimo vilionyesha ni mtumiaji wa bangi.

Hatua hiyo ilizua mabishano ya kisheria baadaye.

Aidha, shahidi huyo alidai alipokea sampuli ya majani na baada ya kufanya vipimo alibaini kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.
Shahidi huyo alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kalula.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano ya wakili Kalula na shahidi:

Wakili: Shahidi unakumbuka Februari 6, mwaka huu ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa ofisini.

Wakili: Je, siku hiyo nini kilitokea?

Shahidi: Siku hiyo nilipokea kielelezo kutoka jeshi la polisi kama sehemu ya majukumu yangu ya kazi.
Wakili: Ulipokea kutoka kwa nani?

Shahidi: Nilipokea kutoka kwa Koplo Robart.

Wakili: Je, kielelezo hicho kilikuwa kinahusu nini?

Shahidi: Kielelezo hicho kilikua sampuli ya misokoto idhaniwayo kuwa dawa za kulevya aina ya bangi ambacho kililetwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili kuthibitisha kuwa ni dawa za kulevya au la.

Wakili: Nini kilifuata?

Shahidi: Nilipima uzito wa yale majani nikapata gramu 1.08, nilianza kufanyia uchunguzi wa awali kwa kuchanganya na dawa maalumu na majibu yalikuwa ni bangi. Nilifanya kipimo cha pili kupitia mitambo maalumu majibu yakaonyesha kuwa ni bangi.

Wakili: Shahidi, wewe kama mkemia bangi ina madhara gani kwa binadamu?

Shahidi: Bangi inasababisha mtumiaji kupata ulevi ambao hauwezi kutibika na husababisha mtumiaji kuharibikiwa akili.
Wakili: Shahidi iambie mahakama Februari 8, mwaka huu unakumbuka nini?

Shahidi: Nakumbuka niliandaa taarifa kuhusiana na uchunguzi wa sampuli ya dawa zidhaniwazo kuwa za kulevya aina ya bangi na majibu yalitoa kuwa majani yale ni bangi.

Wakili: Je, unakumbuka tukio gani jingine kutokea siku hiyo?

Shahidi: Nilipokea sampuli nyingine ya mkojo wa Wema Sepetu, ambaye aliletwa ofisini kwangu akiwa chini ya ulinzi wa Inspekta Willy na askari mwanamke, Marry.

“Nilimpa kontena maalumu na akiwa chini ya ulinzi wa Marry alikwenda kutoa mkojo na nilipoufanyia vipimo majibu yalionyesha kuwa na dawa za kulevya aina ya bangi” alidai shahidi huyo.

Shahidi alidai kuwa baada ya kumaliza kufanya vipimo aliandaa taarifa, kuiweka sahihi na ilihakikiwa na Kaimu Mkemia Mkuu.
Akifafanua zaidi alidai kuwa bangi inaonekana kwenye mkojo ikikaa muda wa siku 28.

Shahidi huyo aliomba mahakama kupokea taarifa zake mbili za uchunguzi wa bangi na mkojo.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala alipinga mahakama kupokea taarifa hiyo kama kielelezo katika kesi hiyo kwa sababu ilikuwa na mapungufu ya kisheria.

Kibatala alidai kuwa taarifa hiyo haijakidhi matakwa ya kisheria kwa uchunguzi wa mtu aliyeko chini ya ulinzi kwamba ni lazima akaape mbele ya hakimu.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulidai kuwa taarifa hiyo iko sahihi kisheria na kwamba mahakama itupilie mbali pingamizi la utetezi.

Hakimu Simba alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zoe mbili mahakama yake itatoa uamuzi keshokutwa.

Mbali na Wema, washtakiwa wengine ni wafanyakazi wake Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Februari 4, mwaka huu eneo la Kunduchi Ununio, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Katika Shitaka la pili, katika tarehe tofauti kati ya Februari Mosi na 3, mwaka huu, mahali pasipojulikana, jijini Dar es Salaam, Wema alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.

Washtakiwa walikana mashitaka na waliposomewa maelezo ya awali walikiri anuani zao na majina tu.

Chanzo: Nipashe
Haya basi kamfungeni si memkuta ndio mtanzania nayekula ngada peke yake
 
hivi zile nchi zilizo ruhusu matumizi ya bangi kuna chochote tunawazidi japo huku bangi imekatazwa?
Huyu Mtumiaji mbona hana madhara yaliyotajwa na Shahidi? Pombe ni Dawa ya kulevya, Sigara ni dawa ya kulevya. U hakika hiyo sample ilionyesha Bangi na si sigara au viroba ni upi? Chemical composition ya Bangi kwenye Mkojo ni kiasi gani tofauti na Valium?
 
Back
Top Bottom