Mkenya aliyeshikiliwa Tanzania na kuachiwa, akamatwa tena, pia aliyekwenda kumpokea naye akamatwa

Mkenya aliyeshikiliwa Tanzania na kuachiwa, akamatwa tena, pia aliyekwenda kumpokea naye akamatwa

Hahaha!, eti maombolezo bila pilau! 😀😀😀

Kunani tena Jirani!..
Alie enda kumtoa na yeye kawekwa ndani?
Kweli Tized ya Magufuli.
Yalianza alipochoma protein zetu pale Namanga hadi leo hii bado maombolezo hajaisha. Hata pilau baada ya maombolezo hatuoni, yakiisha msiba mwingine unabisha mlangoni. Hii ni zaidi ya moto wa Jehanam. [emoji1]
 
😀😀😀 Dah! Kwenye haya maombolezi hamna hata pilau buana? Yataisha lini tuende zetu home? Kila siku ni msiba mpya juu ya ule msiba mwingine wa jana. Nalendwa, njoo tuomboleze pamoja, usiwe hivyo.
😀😀😀hapa ni kuomboleza tu pilau kwenu..
na kwetu misiba haiishi kila day kuna msiba mupya kabisa
 
😀😀😀hapa ni kuomboleza tu pilau kwenu..
na kwetu misiba haiishi kila day kuna msiba mupya kabisa
Hahaa! [emoji1][emoji1][emoji1] Msiba mupya mupya kila leo hadi akiba ya machozi imefifia, kilichobaki sasa ni machozi ya unga jombaa. [emoji38]
 
Hahaa!
emoji1.png
emoji1.png
emoji1.png
Msiba mupya mupya kila leo hadi akiba ya machozi imefifia, kilichobaki sasa ni machozi ya unga jombaa.
emoji38.png
😀😀😀
na sijui ikiisha machozi ya unga tutatumia stock ya machozi gani😀😀
 
Yalianza alipochoma protein zetu pale Namanga hadi leo hii bado maombolezo hajaisha. Hata pilau baada ya maombolezo hatuoni, yakiisha msiba mwingine unabisha mlangoni. Hii ni zaidi ya moto wa Jehanam. [emoji1]


Hahah!, jamani.

Pengine we'll need the African Union to engagement in this..
 
Tatizo hakuna maelezo yanayotolewa kisa cha huyu Mkenya kupitia masaibu yote hayo ya kukamatwa, kuachiwa na kukamatwa tena, hamna taarifa za tuhuma zinazomkabili, halafu kiongozi wa asasi ya kiraia inayoshughulkia haki za jamii Kenya, inayoitwa Hakia Africa, alikwenda kumpokea huyo Mkenya ila naye akatiwa mbaroni papo hapo.

Japo huyu kiongozi hupenda sana kulaumu uongozi Kenya na kusema tunaendeshwa kidikteta, sasa kaenda Tanzania na kukuta nini maana ya neno 'dikteta', nafikiri siku akiachiwa na kurudi Kenya, atakua amepata darasa la kutosha
Hahahahhaaa MBUZI KAFIA kwa muuza SUPU.
 
Udikteta ni pale unamshikilia mtu bila kusema kisa nini, ifahamike ni haki ya kila nchi kumkamata yeyote wakati wowote siku yoyote, ila pia ni ustaarabu kusema kwanini unamkamata, unamtuhumu kwa lipi, hata kama kaua watu huko, iseme tu ili ifahamike Mkenya ananyea debe Tanzania kwa tuhuma za kuwaua watu.
Lakini hili la kumkamata kimya kimya, kumuachia kisha kumkamata tena na kukamata mtu aliyekwenda kumpokea wakati mlikua mumeachia, inadhihirisha kasoro kubwa sana kwenye mfumo wenu.
Uongozi wa Kenya unafaa kuanza kuwajibika, wanakaa kama mamburula wakati raia wetu wanapitia mahangaiko Tanzania, ni muhimu sana vyombo vya habari Kenya kuanza kuangaza haya mambo ili kieleweke kimoja.
Sindano ishaanza kuwaingia,kuweni wapole tu
 
Uongozi wa Kenya unafaa kuanza kuwajibika, wanakaa kama mamburula wakati raia wetu wanapitia mahangaiko Tanzania, ni muhimu sana vyombo vya habari Kenya kuanza kuangaza haya mambo ili kieleweke kimoja.
Tehe tehe tehe
Hata kama anashukiwa kua ni gaidi au shushu shu tumuachie?
Tulia tu kwanza,hata mie nikiingia kenya kihalifu nitashughulikiwa tu,kuita magazeti hukuwezi kuitisha serikali
 
Tehe tehe tehe
Hata kama anashukiwa kua ni gaidi au shushu shu tumuachie?
Tulia tu kwanza,hata mie nikiingia kenya kihalifu nitashughulikiwa tu,kuita magazeti hukuwezi kuitisha serikali

Hehehe! Huwa mna matatizo sana kiuelewa na ndio maana elimu yenu huwa chini, nimesema na narudia mara kumi labda ubongo wenu utafaulu kuelewa baada ya mara hizo kumi, kwamba ni shwari na mpo sahihi na ni haki yenu kumkamata mtu yeyote asiyeendana na sheria za nchi, hata huku tunao watu waliokamatwa akiwemo hata Matanzania aliyekamatwa akiua wanafunzi Garissa, kwa hivyo kumkamata Mkenya hiyo sio issue yangu, wakamateni wote mnaotaka kuwakamata, lakini mnafaa kutoa taarifa kisa na maana kwanini mumemkamata, inaitwa natural justice.
Mkenya yeyote atakayevuka mpaka na kuja huko kuhusika kwenye uhalifu wowote au ugaidi, ashughulkiwe tu tena bila huruma, lakini hili la kukamata mtu na hamsemi kisa nini, mnamuachia huru halafu mnamkamata tena, ni wazi tunakokwenda hakufai, ifahamike raia wa nchi zetu hizi wameingiana kibiashara na kijamii, hatufai kufanyiana mambo yasiyo.
 
Mnatumika na mabeberu.. Lazima tuwe makini. Mugabe alikuwa akiwaogopa Sana.. Hamfai.
 
Mkenya yeyote atakayevuka mpaka na kuja huko kuhusika kwenye uhalifu wowote au ugaidi, ashughulkiwe tu tena bila huruma, lakini hili la kukamata mtu na hamsemi kisa nini, mnamuachia huru halafu mnamkamata tena, ni wazi tunakokwenda hakufai,
Mkuu si ulisema FM wenu aliingilia kati au mpaka uambiwe wewe ndio utahisi imese
wa?
 
Jibu jepesi la kukamatwa ni maelekezo kutoka juu, juu sana!
 
Back
Top Bottom