Mkenya awa Mwafrika wa kwanza kushinda tuzo ya mwalimu bora duniani

Mkenya awa Mwafrika wa kwanza kushinda tuzo ya mwalimu bora duniani

siku hizi naona umeanza kuwa kiboga...... unaharibika kadiri unavyokua.
Dah! 😀😀😀 Nilijua tu utasema kitu kama hicho mkuu, amini nikikuambia kwamba sina ubaya mjomba wangu. Jumatatu huwa haifanani na jumanne, tuko pamoja kama kawa.
 
SHULE YA SEKONDARI MAURICE inawatangazia wazazi na walezi wote kwamba tunapokea wanafunzi kidato cha kwanza mwaka 2019, nafasi za kuamia kidato cha kwanza na cha pili pia tuna kituo cha mitihani kwa watahiniwa wa kujitegemea na Q.T. Vile vile pia tunapokea wanafunzi wa kidato cha tano kwa michepuo ya ECA, HGE, HGK, HKL na HGL. ADA ni nafuu sana. Shule ni ya kutwa na bweni kwa wavulana na wasichana. Shule ipo Dar es salaam wilaya ya temeke, eneo LA mbande kisewe. Simu 0785907371. Wote munakaribishwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo la kutia moyo kwa Mwalimu Peter Tabichi kutoka Kenya aliyeshinda tuzo ya global teacher award a.k.a mwalimu mahiri wa dunia kwa mwaka huu 2019. Sifa kuu kati ya nyingi zilizompa heshima hii ni kutoa 80% ya mshahara wake kusaidia watoto/wanafunzi wanaotoka mazingira magumu. Pia ni Bruda wa kanisa Katoliki huko Kenya. Tumpongeze. Ameiwakilisha vyema Afrika. Je walimu wa Tanzania wana la kujifunza kwa Mwalimu Peter Tabichi?
 
Watanzania hatunaga neno shukrani? Au Asante? Au tuige mifano mizuri basi

Hivi asante kwa kimakonde inasemwaje? Au nashukuru?
 
Pongezi kwake....
Ila kama angeshinda mtanzania unafikiri angepewa coverage
Hku tunataka waskia wakina Daktari shika,Pierre liquid,sjui msabwanda mkubwa etc

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Licha ya global coverage aliyopewa Mwalimu huyu amepewa $1,000,000 ambayo ukiibadilisha kwa hela yetu ni zaidi ya 2 billion
 
Ni jambo la kutia moyo kwa Mwalimu Peter Tabichi kutoka Kenya aliyeshinda tuzo ya global teacher award a.k.a mwalimu mahiri wa dunia kwa mwaka huu 2019. Sifa kuu kati ya nyingi zilizompa heshima hii ni kutoa 80% ya mshahara wake kusaidia watoto/wanafunzi wanaotoka mazingira magumu. Pia ni Bruda wa kanisa Katoliki huko Kenya. Tumpongeze. Ameiwakilisha vyema Afrika. Je walimu wa Tanzania wana la kujifunza kwa Mwalimu Peter Tabichi?
Mabruda weka mbali na watoto!
 
Ni jambo la kutia moyo kwa Mwalimu Peter Tabichi kutoka Kenya aliyeshinda tuzo ya global teacher award a.k.a mwalimu mahiri wa dunia kwa mwaka huu 2019. Sifa kuu kati ya nyingi zilizompa heshima hii ni kutoa 80% ya mshahara wake kusaidia watoto/wanafunzi wanaotoka mazingira magumu. Pia ni Bruda wa kanisa Katoliki huko Kenya. Tumpongeze. Ameiwakilisha vyema Afrika. Je walimu wa Tanzania wana la kujifunza kwa Mwalimu Peter Tabichi?

Sasa mtoa mada unashawishi na walimu wa Tanzania waige mfano wa huyo Bruda kutoa hiyo 80% kwenye mshahara upi? Huu huu wa laki nne na nusu hapo ukiwa hujakopa ili upate hata kakibanda ka kujisitiri? Bado unalipishwa kodi "paye" iliyokwenda shule, achana na makato mengine yaliyojaa kwenye salary slip!

Je, pia unafahamu maana ya Bruda ni mtawa wa kiume wa kanisa la Katoliki? Huyo hana cha kupoteza maana haruhusiwi kuwa na familia yake, maisha yake ni utawani, anakula chakula kizuri na kulala mahali pazuri tena pasipo kulipia chochote! Isitoshe huyo bruda yupo kiimani zaidi(akiamini ktk utakatifu)!

Kwanini ushawishi walimu ambao hadi muda huu stahiki zao za kupandishwa madaraja, kuongezewa mishahara, kulipwa hela zao za likizo, nk. zimekiukwa wafe njaa kwa kumuiga tu mtawa wa Kenya ambaye anafanya pia kazi ya ualimu kwa ziada! Mtoa mada una huruma kweli dhidi ya hawa walimu wanyonge wa nchi hii?
 
Sasa mtoa mada unashawishi na walimu wa Tanzania waige mfano wa huyo Bruda kutoa hiyo 80% kwenye mshahara upi? Huu huu wa laki nne na nusu hapo ukiwa hujakopa ili upate hata kakibanda ka kujisitiri? Bado unalipishwa kodi "paye" iliyokwenda shule, achana na makato mengine yaliyojaa kwenye salary slip!

Je, pia unafahamu maana ya Bruda ni mtawa wa kiume wa kanisa la Katoliki? Huyo hana cha kupoteza maana haruhusiwi kuwa na familia yake, maisha yake ni utawani, anakula chakula kizuri na kulala mahali pazuri tena pasipo kulipia chochote! Isitoshe huyo bruda yupo kiimani zaidi(akiamini ktk utakatifu)!

Kwanini ushawishi walimu ambao hadi muda huu stahiki zao za kupandishwa madaraja, kuongezewa mishahara, kulipwa hela ao za likizo, nk. wafe njaa kwa kumuiga tu mtawa wa Kenya ambaye anafanya pia kazi ya ualimu kwa ziada! Mtoa mada una huruma kweli dhidi ya hawa walimu wanyonge wa nchi hii?
Sijashawishi walimu wa Tanzania watoe huo mshahara wao uliosema ni mdogo na mambo mengine uliyoeleza hapo. Nimewauliza kama kuna la kujifunza hapo. Haswa kujitoa. Yeyote mwenye moyo wa kujitoa hata kama anapokea mshahara mdogo kiasi gani atatoa tu
 
Sijashawishi walimu wa Tanzania watoe huo mshahara wao uliosema ni mdogo na mambo mengine uliyoeleza hapo. Nimewauliza kama kuna la kujifunza hapo. Haswa kujitoa. Yeyote mwenye moyo wa kujitoa hata kama anapokea mshahara mdogo kiasi gani atatoa tu

Sawa nimekupata. Ngoja walimu nao waje kuchangia. Ila jambo nililojifunza ni moja tu; huyo mwalimu ni "Mtawa wa kanisa Katoliki" na bahati nzuri nawafahamu hao watawa in and out. Ana utofauti mkubwa sana na mwalimu wa kawaida ambaye si mtawa.
 
Sijashawishi walimu wa Tanzania watoe huo mshahara wao uliosema ni mdogo na mambo mengine uliyoeleza hapo. Nimewauliza kama kuna la kujifunza hapo. Haswa kujitoa. Yeyote mwenye moyo wa kujitoa hata kama anapokea mshahara mdogo kiasi gani atatoa tu
Nakubaliana na wewe,Kutoa ni moyo,usambe..... Hata kama tungepata mamilioni,kama MTU huna moyo wa utoaji haitoshi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijashawishi walimu wa Tanzania watoe huo mshahara wao uliosema ni mdogo na mambo mengine uliyoeleza hapo. Nimewauliza kama kuna la kujifunza hapo. Haswa kujitoa. Yeyote mwenye moyo wa kujitoa hata kama anapokea mshahara mdogo kiasi gani atatoa tu
Wewe ushatoa nini ili uwaoneshe mfano walimu wa kujitolea kwa ajili ya "Taifa hili Changa?"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MKENYA ALIYESHINDA TUZO YA MWALIMU BORA DUNIANI AKUTANA NA TRUMP: walimu Peter Tabichi kutoka nchini Kenya aliyetunukiwa Tuzo ya Mwalimu Bora Duniani Machi mwaka huu, amekutana na Rais wa Marekani, Donald Trump katika Ikulu ya nchi hiyo huku akitarajiwa baadaye kuhutubia mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Mwalimu huyo ambaye ni mwalimu wa somo la Sayansi, akiwa ni mtawa wa Shirika la Kikatoliki la Mtakatifu Fransisco wa Kapuchini ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda washiriki 10,000 waliochaguliwa kutoka nchi 179.

Akizungumzia umuhimu wa tuzo hizo mwalimu Tabichi amesema, anatamani kila mtoto afikie ndoto yake na ndiyo maana inasemekana kuwa katika kipato chake (mshahara) mwalimu huyo hutoa takribani asilimia 80 ya fedha yake kusaidia familia masikini.

Akiwa mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Mseto ya Keriko iliyopo katika Kaunti ya Nakuru,Kaskazini magharibi mwa jijini la Nairobi, mwalimu Tabichi amesema, kazi hiyo inakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwemo za ukosefu wa vifaa kama vitabu na upungufu ya walimu shuleni kwake.

Aidha ameongeza kuwa, kazi ya ufundishaji pia huwawia ngumu kutokana na darasa moja linalopaswa kuwa la wanafunzi 35 – 40 hulazimika kuwa na wanafunzi 70 -80 huku wengi wa wanafunzi hao wakilazimika kutembea umbali mrefu katika barabara mbovu.

Akizungumzia sababu ya kushinda Tuzo hizo, Stephanie Grisham mmoja wa watendaji wa Ikulu ya Marekani amesema, "Uwajibikaji wake na kazi yake ngumu na imani kwa talanta ya wanafunzi, imeifanya shule anayofundisha kuibuka kidedea baada ya kushindana na shule zilizo bora nchini katika mashindano ya kitaifa ya sayansi.”
#AZAMTWO #AzamUTV #Azamtvtz #AzamTVApp
IMG-20190917-WA0009.jpeg
IMG-20190917-WA0010.jpeg
IMG-20190917-WA0008.jpeg
 
Back
Top Bottom