Mkoa wa Chato na siasa za Kanda ya Ziwa nyuma ya pazia

Mkoa wa Chato na siasa za Kanda ya Ziwa nyuma ya pazia

MKOA WA CHATO NA SIASA ZA KANDA YA ZIWA NYUMA YA PAZIA

Nimesoma maandiko kadhaa kuhusiana na kuundwa kwa Mkoa wa Chato. Huwezi kuelewa vizuri kinachoendelea sasa bila kujua siasa za Kanda ya Ziwa zilizopo nyuma ya pazia.

Labda niwaeleze kidogo mambo ambayo yako nyuma ya Pazia na huwa hayaelezwi katika forum rasmi ili maamuzi ya busara yafanyike katika hili.

Kwanza kabisa nataka niwajulishe jambo moja. Chato ipo katikati ya Bukoba na Mwanza. Kutoka Chato hadi Bukoba ni takribani km 200 kama ilivyo kutoka Chato hadi Mwanza km 200.

Kusini mwa Chato kabla ya kulifikia Jiji la Mwanza kuna mji wa Geita yapata kama km 100. Na Kaskazini mwa Chato kabla ya kuifikia Bukoba kuna mji wa Muleba yapata km 132.

Mashariki mwa Chato mwanzo mwisho kuna Ziwa Victoria na Magharibi mwa Chato kuna Biharamulo yapata km 61, na Ngara yapata km 130.

Ukweli ni kwamba wilaya ya Ngara iko mbali sana na Bukoba. Ni km 300! Pia wilaya ya Kakonko iko mbali sana na Kigoma. Ni km 284! Haya ni maeneo ambayo zamani yalikuwa mapori lakini kwa sasa yana makazi mengi ya watu wanaohitaji huduma ya karibu.

Ukiangalia kwa makini hasa kwa masuala ya huduma, Runzewe ni kama imeunganika na Nyakanazi. Na Nyakanazi kihuduma imeunganika na Kakonko kuliko Kakonko na Kibondo. Nyakanazi pia imeunganika na Lusahunga. Lusahunga imeunganika na Biharamulo. Runzewe imeunganika na Bwanga. Bwanga imeunganika na Biharamulo. Maeneo yote hayo pamoja na Ngara yako mbali na mikoa yao yaani Kigoma, Kagera na Geita ukilinganisha na Chato ambayo iko katikati ya maeneo hayo.

Idadi ya watu Kanda ya Ziwa imekuwa inakua kwa kasi sana na kuzaliwa kwa Mkoa wa Chato kunatoa solution ya umbali wa huduma ya mkoani kati ya Kakonko kwenda Kigoma na Ngara kwenda Bukoba.

Sasa mzizi wa tatizo linaloibuka kuhusu ukinzani wa kuanzishwa Mkoa wa Chato nyuma ya Pazia umegubikwa na sababu za kikabila hasa ugomvi wa kiasili kati ya Biharamulo na Chato. Na pili watu waliojeruhiwa na Mwendazake Mwendazake wanahakikisha hakuna kizuri cha Mwendazake kinakatisha bila kukitia nyongo. Hawataki Mwendazake "apate furaha yoyote" huko aliko wakidhani ni fursa yao ya kulipiza kisasi.

Kwanza ieleweke kwamba Chato ilikuwa mojawapo ya tarafa za wilaya ya Biharamulo ambayo ni wilaya iliyoko Mkoa wa Kagera. Wakazi wa wilaya ya Biharamulo ni Wasubi ambao kutokana na kuwepo Mkoa wa Kagera kwa muda mrefu wamekuwa wakichukuliwa kama jamii ya Wahaya. Ukiwa nje ya Mkoa wa Kagera watu hujua Wahaya tu.

Migration ya Wasukuma kutoka Geita iliwafanya waijaze Chato kiasi kwamba baadaye Chato ikawa kama Sukumaland. Japo Chato kuna makabila mengi (Wasukuma, Wasubi, Wahaya, Wazinza na Wajita) lakini kabila ambalo limekuwa dominant ni Wasukuma.

Ukiwa pale Chato mjini lugha kuu ni Kisukuma. Ukiingia kwenye Kata za Chato Kisukuma ndio lugha kuu kasoro kata moja iliyoko karibu na Biharamulo inayoitwa Kasenga.

Sasa baada ya Wasukuma kuwa dominant Chato, wakawa wanaona shida kwenda mkoani Bukoba. Walitamani kuwa sehemu ya Mwanza lakini Mwanza ilikuwa kushoto kwao kwa sababu ili ufike Mwanza lazima uvuke maji.

Ulipoanza mkoa wa Geita, Chato ikapumua kwamba "tumetoka Uhayani". Lakini Hayaland wakaona eneo Lao limemegwa kwenda sukumaland.

Mtakumbuka kwamba mkoa wa Kagera awali ulikuwa na wilaya tano. Bukoba, Biharamulo, Muleba, Ngara na Karagwe. Wilaya zote hizo zilionekana kama ni Hayaland.

Mwendazake alipambana kuwa Mbunge wa Biharamulo kuanzia mwaka 1990 lakini alishindwa kwa sababu hizo za "anatoka usukumani".

Katika uchaguzi wa mwaka 1990 Mwendazake alishinda kata zilizoko Mashariki mwa Biharamulo (Chato) ambako kuna Wasukuma wengi waliohamia kutoka Geita.

Hata asili ya Mwendazake ni kwenye visiwa vya Nkome vilivyopo Kaskazini Magharibi mwa Geita ambavyo vinapakana na visiwa vya Rubondo kuliko na Hifadhi ya Taifa.

Biharamulo wanatoka Wasubi ambayo ni kama jamii ya Wahaya. Ni watu conservative sana. Ikaonekana ili Mwendazake apate jimbo lazima Biharamulo igawanywe. Ile Sukumaland ya Biharamulo iitwe Biharamulo Mashariki. Na baadaye ikaitwa Chato.

Kipindi cha utawala wa Mzee Mwinyi, Biharamulo ikagawanywa na kupatikana Biharamulo Mashariki ambayo ndio Chato. Ulipofanyika uchaguzi 1995 Mwenzazake akashinda kirahisi hilo Jimbo.

Hayaland wakaona eneo lao limetekwa usukumani na kubadilishwa jina kuitwa Chato. Kukawa na uhasama wa maneno ya kisiasa kati ya Chato na Biharamulo.

Mwendazake alivyoingia tu madarakani kama Mbunge 1995 akawa Naibu Waziri wa Ujenzi. Wakati huo vuguvugu la Chato Biharamulo lilikuwa limepamba moto.

Baada ya kukosa kura 1990 na kushinda 1995 na hasa alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi ukaibuka uvumi kuwa Mwendazake kawaapia watu wa Biharamulo kwamba lami wataisikia tu kwenye radio.

Ni uvumi ulioenea kwa kasi sana. Kwamba Mwendazake aliongea kwa Kisukuma. Eti alisema "Butabaaba du eebiharamulo mutaleebona elami" (Haki ya Mungu nyie watu wa Biharamulo lami mtaisikia tu).

Eti pia aliwaapia kwamba Chato itasonga mbele kwa kasi kubwa kuliko Biharamulo kwa sababu Wasukuma ni watu wa kazi. Wasubi na Wahaya ni wavivu walikuwa wanawachelewesha Wasukuma.

Uvumi huo ulitamalaki zaidi hasa baada ya Mwendazake kuanza kujenga barabara ya lami inayopitia Chato kutoka Bukoba badala ya kupitia Biharamulo.

Ili muweze kunielewa vzr labda kwanza niwaeleze jiografia ya barabara inayounganisha Tanzania na Kanda ya Ziwa Magharibi yaani barabara anayetoka Kahama hadi Kagera. Ni kwamba ili ufike Kagera kutokea Kahama unaweza kuamua upitie Chato au Biharamulo. Ukipita Chato unapita Ziwani kama Dar Chalinze kupitia Bagamoyo na Ukipita Biharamulo unapita "Bara" kama Dar Chalinze kupitia Kibaha&Mlandizi.

Junction ya kufanya maamuzi ya kupitia Chato au Biharamulo iko kwenye mji mmoja unaitwa Runzewe ambao uko karibu na Nyakanazi.

Sasa ukiamua kupitia Biharamulo maana yake ni kwamba kutoka hapo Runzewe utaenda mpaka Nyakanazi-Lusahunga-Biharamulo-Kyamyorwa-Muleba-Bukoba.

Na ukiamua kupitia Chato kuanzia hapo Runzewe route itakuwa Runzewe- Bwanga - Chato -Kyamilyorwa-Muleba-Bukoba.

Sasa, sehemu kubwa ya route ya Biharamulo barabara hiyo inapita porini katika pori la hifadhi la Biharamulo ambalo kwa sasa imekuwa Mbuga ya Burigi Chato, Lakini ukipitia Chato unapita ukanda wa Ziwani ambao ndio una miji mingi ya watu.

Kutokana na hilo, Mwendazake wakati akiwa Waziri wa Ujenzi na kutokana na ushawishi wake alianza kujenga barabara inayopitia Chato ambayo sio barabara ya Kitaifa. Barabara ya kitaifa ni ile inayopitia Biharamulo.

Hoja ya Mwendazake ni kwamba ni Bora kuanza kujenga lami kwenye makazi mengi ya watu kuliko kuanzia "porini" maana jukumu la serikali ni kuwasogezea huduma wananchi. Hiyo hoja watu wa Biharamulo hawakuielewa kwa kuwa kama Taifa kipaumbele kilitakiwa kuwekwa kwenye barabara ya kitaifa badala ya barabara ya Mkoa.

Baada ya barabara hiyo kujengwa gari nyingi sana za Mwanza - Bukoba zikawa zinapitia Chato. Mji wa Chato ukakua kwa kasi ukilinganisha na Biharamulo.

Kutokana na uwingi wa watu unaoongezeka kwa kasi kanda ya Ziwa upo umuhimu wa kuanzisha Mkoa wa Chato lakini changamoto zinazoibuliwa zina harufu ya ukabila kwamba kwanini Wahaya kutoka Ngara na Bukoba wahamishiwe usukumani.

Ni kweli Mwendazake alikuwa anapapenda sana nyumbani kwake. Na alitamani pawe na maendeleo makubwa. Nadhani haya pia ni matamanio ya mwanasiasa yoyote mwenye akili timu. Lakini uamuzi wa kupeleka maendeleo kwake kwa nia ya kuanzisha Mkoa wa Chato ameujengea hoja zinazoingia akilini.

Why Mkoa wa Chato ni muhimu. Utasababisha kuyaunganisha maeneo ya Kakonko, Nyakanazi, Lusahunga, Ngara, Biharamulo, Bwanga, Runzewe na kupata huduma ya mkoani karibu kwa umbali chini ya km 150 badala ya kulazimika kusafiri mpaka km takribani 300 unaenda mkoani.

Na Teacher Wa Professors Captain Enough (Negrosign).
Chato haina sifa ya kuwa mkoa!!!
 
Umefafanua vizuri. Tumejua kuanzishwa mkoa wa Chato ni ndoto ya zamani ya mwendazake iliyosukumwa na ukabila.
 
Siioni Chato kuwa katikati ya maeneo uliyotaja, labda Lusahunga itakuwa sahihi zaidi kwa maana ya kuingiza Kakonko, Ngara, Runzewe, Biharamulo, na Chato katika mkoa huo. Kama kuna maeneo yalimegwa Geita yakaingizwa Chato, hayo yarudishwe Geita.
Pili hoja za ukabila hazina mashiko; hatuundi mkoa wa wasukuma au wahaya. Hoja za ukabila zinafaa zaidi kwenye matambiko! Tanzania tushatoka huko, tunajenga Tanzania ya Watanzania na ndio maana wewe mwenyewe umeandika kuwa wasukuma wengi walihamia Chato.
Uko sahihi!
 
Walau, huenda kauli hizi zikatunusuru.


"Iwapo kuunda mkoa no kusogeza huduma jirani na wananchi, ni busara mkoa huu kuundwa kwa kuweka makao makuu Biharamulo au Nyakanazi.
Sioni maana/mantiki ya wakazi wa wilaya za Ngara na Kakonko kuvuka wilaya ya Biharamulo wakienda Chato.
Makao Makuu ya mkoa hui mpya yatakuwa pembeni mwa mkoa huu mpya.

Mkoa huu badala ya kuwanufaisha wakazi wake wengi, utawaumiza.

Pia sioni manufaa atakayoyapata mkazi wa Buseresere na Katoro kwa kuwa ataongeza umbali wa kwenda makao makuu ya mkoa.

Nashauri serikali badala ya kuwaza kuongeza mikoa na wilaya, ijikite kupunguza ukubwa wa vijiji na kata.
Hili liende sambamba na kuwarahisishia utendaji wa kazi zao viongozi wa vijiji na kata kwa kuwapa usafiri, vifaa vya kazi kama kompyuta mpakato, simu zinazoweza kupata matukio[picha] vema nk.

Hapa Ngara kwenye kata ya Muganza, umbali kutoka Kitongoji cha Nyakafandi hadi makao makuu ya Kijiji chao cha Mukubu ni km.15.
Kutoka kitongoji hicho hadi makao makuu ya kata ni zaidi ya km.30.

Mtendaji wa kata na wa kijiji hawana usafiri wowote.
Wanatumia usafiri wa kudandia au kukodi.
Huko hakuna umeme wa TANESCO.
Wangeweza kusaidiwa kupewa umeme wa jua kwenye ofisi zao ili wachaji simu zao ambazo kwa sehemu kubwa zinafanya kazi za ofisi.

Wananchi hatuna hitaji la mikoa na wilaya.
Tunahitaji zaidi huduma bora za vitongoji vijiji na kata.

Ikumbukwe miaka michache iliyopita ukubwa wa vitongoji uliongezwa badala ya kupunguzwa.
Kuna sehemu mitaa/vitongoji vitatu viliungwa kuwa kimoja.
Mzigo uliongezeka."

Wasomi nendeni mtafiti/mjiulize au muwaulize wananchi wa kawaida wanakwenda mkoani na hata wilayani kwa ajili ya nini?
Wengi wao, maisha yao yote hawatakuwa na shida yoyote mkoani.

Ikumbukwe kuwa kuanzisha mkoa Kuna gharama nyingi na kubwa mno.
Gharama za kuanzisha mkoa au wilaya zikielekezwa vijijini au katani zitaleta tija.

Kazi iendelee.
 
mhn! ni mguno sina ninachonusa!
ninachokiangalia kwangu ni rasilimali zilizowekezwa Chato jinsi gani zinaweza kuisaidia taifa na watu wake; vinginevyo tukubali kuwa tumepoteza kila kitu.
busara na maamuzi yenye tija yatumike ili yale yaliyojengwa yanufaishe nchi yote.
kazi kwenu watawala! ndo mjifunze na muache ubinafsi
 
Ni kwamba Chato haina sifa ya kuwa mkoa huo ndio ukweli acha kuzunguka muanzisha mada.Ni ukweli ulio wazi mwenda zake alikuwa mbinafsi kupitiliza ukitaka kujua zaidi ya hilo kwanini ajenge uwanja wa ndege Chato asijenge mkoani Geita ambapo ni makao makuu ya mkoa?.Kibaya zaidi alitoa maamuzi bila kupitia bungeni.

Mwenda zake alikuwa na chuki za wazi kwa baadhi ya mikoa hasa mkoa wa Kilimanjaro alikuwa na dhana kwamba ni wezi.Ni waambie ndugu zangu baadhi ya maendeleo ya Tanzania,Kenya,Uganda na sehemu zingine zilisababishwa na athari ya mkoloni.Mkoloni alivyokuja Kilimanjaro,Wakikuyu na Wabaganda kwa Uganda aliona hali ya hewa ya kule ilifanana na kwao ulaya na akapiga hesabu kupanda mazao ya cash crops kwa vyovyote vile sehemu hizo alianza kujenga makanisa na shule kwa vyovyote hawa watu lazima waonekane wako mbele kuliko sehemu zingine.

Hakuna kabila ambalo tunaweza sema wana akili kuliko wengine wote wako sawa na mtu akitangulia ametangulia tu.Nenda mkoani Mbeya na Bukoba mashule yalijengwa siku nyingi.

Pamoja na yote kila utawala una zama zake na kitabu chake huwezi kuwa raisi au kiongozi wa ngazi yeyote hata ya kata usiwe na mazuri yako na mapungufu yako hayo ni mapungufu yake kama binadamu wengine.Nyerere alikuja alileta mazuri yake na mapungufu yake.Hali kadhalika kwa Mwinyi,Mkapa na Kikwete nao ni binadamu wana nyama na damu.

Ila ni ukweli ulio wazi toka tupate uhuru hatujawahi pata kiongozi aina ya mwenda zake kipindi kifupi alileta mabadiliko makubwa mno na aliwazidi watangulizi wake tujiulize je mungu asingeamua kumchukua watanzania tungefikia wapi?Raisi wa zamani wa Bukina Faso marehemu capt Thomas Sankara alipata kusema wakati mwingine ukitaka kuleta mabadiliko lazima uwe na level flani ya wehu alimaanisha kuna mahali inabidi ukengeuke utumie nguvu.

Mhe wetu Mwenda zake aligundua tumechezewa mno mno na nidhamu ya kazi ilikuwa haipo na ubadhirifu wa mali ya uma ulikidhiri ndio maana akawa anatumia misimamo mikali kwa hapa kwa kweli hatutamtendea haki kumpa pongezi zake kipindi chake kulikuwa hakuna tofauti ya mnyonge na mtu aliye nacho aliyenacho akikosea anafungwa sawa na asiye nacho katika kipindi chake ndio haki zilizokuwa zinafinywa kwa wanyonge alizifungua.


Mungu ambarikia amlaze pema mhe wetu.Sio vyema kuhesabu mabaya yake ila tuyaenzi mazuri yake na pale alipokosea turekebishe.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Mzizi wa hii yote ni "Ubinafsi tu"
Uko sahihi kabisa. Kwanza nimebaini kwamba hao wahamiaji kutoka usukumani, wamevamia mkoa wa wenzao na kulazimisha uwe wa kwao na kutaka kufuta historia ya wenyeji na kuleta za kwao. Pili hapa Tanzania kuna mambo mengi ya ajabu sana, imagine mwendazake, ambaye amevamia mkoa wa watu akashawishi mpaka jimbo likagawanywa ili eti yeye ashinde uchaguzi. Yaani badala ya jimbo kugawanywa for public interest likagawanywa ili fulani ashinde uchaguzi!!!
 
Ni kwamba Chato haina sifa ya kuwa mkoa huo ndio ukweli acha kuzunguka muanzisha mada.Ni ukweli ulio wazi mwenda zake alikuwa mbinafsi kupitiliza ukitaka kujua zaidi ya hilo kwanini ajenge uwanja wa ndege Chato asijenge mkoani Geita ambapo ni makao makuu ya mkoa?.Kibaya zaidi alitoa maamuzi bila kupitia bungeni.

Mwenda zake alikuwa na chuki za wazi kwa baadhi ya mikoa hasa mkoa wa Kilimanjaro alikuwa na dhana kwamba ni wezi.Ni waambie ndugu zangu baadhi ya maendeleo ya Tanzania,Kenya,Uganda na sehemu zingine zilisababishwa na athari ya mkoloni.Mkoloni alivyokuja Kilimanjaro,Wakikuyu na Wabaganda kwa Uganda aliona hali ya hewa ya kule ilifanana na kwao ulaya na akapiga hesabu kupanda mazao ya cash crops kwa vyovyote vile sehemu hizo alianza kujenga makanisa na shule kwa vyovyote hawa watu lazima waonekane wako mbele kuliko sehemu zingine.

Hakuna kabila ambalo tunaweza sema wana akili kuliko wengine wote wako sawa na mtu akitangulia ametangulia tu.Nenda mkoani Mbeya na Bukoba mashule yalijengwa siku nyingi.

Pamoja na yote kila utawala una zama zake na kitabu chake huwezi kuwa raisi au kiongozi wa ngazi yeyote hata ya kata usiwe na mazuri yako na mapungufu yako hayo ni mapungufu yake kama binadamu wengine.Nyerere alikuja alileta mazuri yake na mapungufu yake.Hali kadhalika kwa Mwinyi,Mkapa na Kikwete nao ni binadamu wana nyama na damu.

Ila ni ukweli ulio wazi toka tupate uhuru hatujawahi pata kiongozi aina ya mwenda zake kipindi kifupi alileta mabadiliko makubwa mno na aliwazidi watangulizi wake tujiulize je mungu asingeamua kumchukua watanzania tungefikia wapi?Raisi wa zamani wa Bukina Faso marehemu capt Thomas Sankara alipata kusema wakati mwingine ukitaka kuleta mabadiliko lazima uwe na level flani ya wehu alimaanisha kuna mahali inabidi ukengeuke utumie nguvu.

Mhe wetu Mwenda zake aligundua tumechezewa mno mno na nidhamu ya kazi ilikuwa haipo na ubadhirifu wa mali ya uma ulikidhiri ndio maana akawa anatumia misimamo mikali kwa hapa kwa kweli hatutamtendea haki kumpa pongezi zake kipindi chake kulikuwa hakuna tofauti ya mnyonge na mtu aliye nacho aliyenacho akikosea anafungwa sawa na asiye nacho katika kipindi chake ndio haki zilizokuwa zinafinywa kwa wanyonge alizifungua.


Mungu ambarikia amlaze pema mhe wetu.Sio vyema kuhesabu mabaya yake ila tuyaenzi mazuri yake na pale alipokosea turekebishe.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Yaani umeanza vizuri lakini kwenye hitimisho umejichanganya... Jifunze kwamba unapojenga hoja yako hakikisha conclusion ina support your original arguments... Huwezi kuwa na paragraph tatu za mwanzo unaelezea mapungufu ya mwendazake ikiwemo ubinafsi, ukabila na upendeleo halafu umalizie tofauti...
 
Shida siyo ukubwa wa maeneo ya kiutawala bali tuna tatizo la utawala bora, Nchi ambayo tuna watendaji mpaka ngazi ya Kijiji,hatuhitaji kuongeza mikoa Zaidi tunahitaji utawala bora tu.
 
MKOA WA CHATO NA SIASA ZA KANDA YA ZIWA NYUMA YA PAZIA

Nimesoma maandiko kadhaa kuhusiana na kuundwa kwa Mkoa wa Chato. Huwezi kuelewa vizuri kinachoendelea sasa bila kujua siasa za Kanda ya Ziwa zilizopo nyuma ya pazia.

Labda niwaeleze kidogo mambo ambayo yako nyuma ya Pazia na huwa hayaelezwi katika forum rasmi ili maamuzi ya busara yafanyike katika hili.

Kwanza kabisa nataka niwajulishe jambo moja. Chato ipo katikati ya Bukoba na Mwanza. Kutoka Chato hadi Bukoba ni takribani km 200 kama ilivyo kutoka Chato hadi Mwanza km 200.

Kusini mwa Chato kabla ya kulifikia Jiji la Mwanza kuna mji wa Geita yapata kama km 100. Na Kaskazini mwa Chato kabla ya kuifikia Bukoba kuna mji wa Muleba yapata km 132.

Mashariki mwa Chato mwanzo mwisho kuna Ziwa Victoria na Magharibi mwa Chato kuna Biharamulo yapata km 61, na Ngara yapata km 130.

Ukweli ni kwamba wilaya ya Ngara iko mbali sana na Bukoba. Ni km 300! Pia wilaya ya Kakonko iko mbali sana na Kigoma. Ni km 284! Haya ni maeneo ambayo zamani yalikuwa mapori lakini kwa sasa yana makazi mengi ya watu wanaohitaji huduma ya karibu.

Ukiangalia kwa makini hasa kwa masuala ya huduma, Runzewe ni kama imeunganika na Nyakanazi. Na Nyakanazi kihuduma imeunganika na Kakonko kuliko Kakonko na Kibondo. Nyakanazi pia imeunganika na Lusahunga. Lusahunga imeunganika na Biharamulo. Runzewe imeunganika na Bwanga. Bwanga imeunganika na Biharamulo. Maeneo yote hayo pamoja na Ngara yako mbali na mikoa yao yaani Kigoma, Kagera na Geita ukilinganisha na Chato ambayo iko katikati ya maeneo hayo.

Idadi ya watu Kanda ya Ziwa imekuwa inakua kwa kasi sana na kuzaliwa kwa Mkoa wa Chato kunatoa solution ya umbali wa huduma ya mkoani kati ya Kakonko kwenda Kigoma na Ngara kwenda Bukoba.

Sasa mzizi wa tatizo linaloibuka kuhusu ukinzani wa kuanzishwa Mkoa wa Chato nyuma ya Pazia umegubikwa na sababu za kikabila hasa ugomvi wa kiasili kati ya Biharamulo na Chato. Na pili watu waliojeruhiwa na Mwendazake Mwendazake wanahakikisha hakuna kizuri cha Mwendazake kinakatisha bila kukitia nyongo. Hawataki Mwendazake "apate furaha yoyote" huko aliko wakidhani ni fursa yao ya kulipiza kisasi.

Kwanza ieleweke kwamba Chato ilikuwa mojawapo ya tarafa za wilaya ya Biharamulo ambayo ni wilaya iliyoko Mkoa wa Kagera. Wakazi wa wilaya ya Biharamulo ni Wasubi ambao kutokana na kuwepo Mkoa wa Kagera kwa muda mrefu wamekuwa wakichukuliwa kama jamii ya Wahaya. Ukiwa nje ya Mkoa wa Kagera watu hujua Wahaya tu.

Migration ya Wasukuma kutoka Geita iliwafanya waijaze Chato kiasi kwamba baadaye Chato ikawa kama Sukumaland. Japo Chato kuna makabila mengi (Wasukuma, Wasubi, Wahaya, Wazinza na Wajita) lakini kabila ambalo limekuwa dominant ni Wasukuma.

Ukiwa pale Chato mjini lugha kuu ni Kisukuma. Ukiingia kwenye Kata za Chato Kisukuma ndio lugha kuu kasoro kata moja iliyoko karibu na Biharamulo inayoitwa Kasenga.

Sasa baada ya Wasukuma kuwa dominant Chato, wakawa wanaona shida kwenda mkoani Bukoba. Walitamani kuwa sehemu ya Mwanza lakini Mwanza ilikuwa kushoto kwao kwa sababu ili ufike Mwanza lazima uvuke maji.

Ulipoanza mkoa wa Geita, Chato ikapumua kwamba "tumetoka Uhayani". Lakini Hayaland wakaona eneo Lao limemegwa kwenda sukumaland.

Mtakumbuka kwamba mkoa wa Kagera awali ulikuwa na wilaya tano. Bukoba, Biharamulo, Muleba, Ngara na Karagwe. Wilaya zote hizo zilionekana kama ni Hayaland.

Mwendazake alipambana kuwa Mbunge wa Biharamulo kuanzia mwaka 1990 lakini alishindwa kwa sababu hizo za "anatoka usukumani".

Katika uchaguzi wa mwaka 1990 Mwendazake alishinda kata zilizoko Mashariki mwa Biharamulo (Chato) ambako kuna Wasukuma wengi waliohamia kutoka Geita.

Hata asili ya Mwendazake ni kwenye visiwa vya Nkome vilivyopo Kaskazini Magharibi mwa Geita ambavyo vinapakana na visiwa vya Rubondo kuliko na Hifadhi ya Taifa.

Biharamulo wanatoka Wasubi ambayo ni kama jamii ya Wahaya. Ni watu conservative sana. Ikaonekana ili Mwendazake apate jimbo lazima Biharamulo igawanywe. Ile Sukumaland ya Biharamulo iitwe Biharamulo Mashariki. Na baadaye ikaitwa Chato.

Kipindi cha utawala wa Mzee Mwinyi, Biharamulo ikagawanywa na kupatikana Biharamulo Mashariki ambayo ndio Chato. Ulipofanyika uchaguzi 1995 Mwenzazake akashinda kirahisi hilo Jimbo.

Hayaland wakaona eneo lao limetekwa usukumani na kubadilishwa jina kuitwa Chato. Kukawa na uhasama wa maneno ya kisiasa kati ya Chato na Biharamulo.

Mwendazake alivyoingia tu madarakani kama Mbunge 1995 akawa Naibu Waziri wa Ujenzi. Wakati huo vuguvugu la Chato Biharamulo lilikuwa limepamba moto.

Baada ya kukosa kura 1990 na kushinda 1995 na hasa alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi ukaibuka uvumi kuwa Mwendazake kawaapia watu wa Biharamulo kwamba lami wataisikia tu kwenye radio.

Ni uvumi ulioenea kwa kasi sana. Kwamba Mwendazake aliongea kwa Kisukuma. Eti alisema "Butabaaba du eebiharamulo mutaleebona elami" (Haki ya Mungu nyie watu wa Biharamulo lami mtaisikia tu).

Eti pia aliwaapia kwamba Chato itasonga mbele kwa kasi kubwa kuliko Biharamulo kwa sababu Wasukuma ni watu wa kazi. Wasubi na Wahaya ni wavivu walikuwa wanawachelewesha Wasukuma.

Uvumi huo ulitamalaki zaidi hasa baada ya Mwendazake kuanza kujenga barabara ya lami inayopitia Chato kutoka Bukoba badala ya kupitia Biharamulo.

Ili muweze kunielewa vzr labda kwanza niwaeleze jiografia ya barabara inayounganisha Tanzania na Kanda ya Ziwa Magharibi yaani barabara anayetoka Kahama hadi Kagera. Ni kwamba ili ufike Kagera kutokea Kahama unaweza kuamua upitie Chato au Biharamulo. Ukipita Chato unapita Ziwani kama Dar Chalinze kupitia Bagamoyo na Ukipita Biharamulo unapita "Bara" kama Dar Chalinze kupitia Kibaha&Mlandizi.

Junction ya kufanya maamuzi ya kupitia Chato au Biharamulo iko kwenye mji mmoja unaitwa Runzewe ambao uko karibu na Nyakanazi.

Sasa ukiamua kupitia Biharamulo maana yake ni kwamba kutoka hapo Runzewe utaenda mpaka Nyakanazi-Lusahunga-Biharamulo-Kyamyorwa-Muleba-Bukoba.

Na ukiamua kupitia Chato kuanzia hapo Runzewe route itakuwa Runzewe- Bwanga - Chato -Kyamilyorwa-Muleba-Bukoba.

Sasa, sehemu kubwa ya route ya Biharamulo barabara hiyo inapita porini katika pori la hifadhi la Biharamulo ambalo kwa sasa imekuwa Mbuga ya Burigi Chato, Lakini ukipitia Chato unapita ukanda wa Ziwani ambao ndio una miji mingi ya watu.

Kutokana na hilo, Mwendazake wakati akiwa Waziri wa Ujenzi na kutokana na ushawishi wake alianza kujenga barabara inayopitia Chato ambayo sio barabara ya Kitaifa. Barabara ya kitaifa ni ile inayopitia Biharamulo.

Hoja ya Mwendazake ni kwamba ni Bora kuanza kujenga lami kwenye makazi mengi ya watu kuliko kuanzia "porini" maana jukumu la serikali ni kuwasogezea huduma wananchi. Hiyo hoja watu wa Biharamulo hawakuielewa kwa kuwa kama Taifa kipaumbele kilitakiwa kuwekwa kwenye barabara ya kitaifa badala ya barabara ya Mkoa.

Baada ya barabara hiyo kujengwa gari nyingi sana za Mwanza - Bukoba zikawa zinapitia Chato. Mji wa Chato ukakua kwa kasi ukilinganisha na Biharamulo.

Kutokana na uwingi wa watu unaoongezeka kwa kasi kanda ya Ziwa upo umuhimu wa kuanzisha Mkoa wa Chato lakini changamoto zinazoibuliwa zina harufu ya ukabila kwamba kwanini Wahaya kutoka Ngara na Bukoba wahamishiwe usukumani.

Ni kweli Mwendazake alikuwa anapapenda sana nyumbani kwake. Na alitamani pawe na maendeleo makubwa. Nadhani haya pia ni matamanio ya mwanasiasa yoyote mwenye akili timu. Lakini uamuzi wa kupeleka maendeleo kwake kwa nia ya kuanzisha Mkoa wa Chato ameujengea hoja zinazoingia akilini.

Why Mkoa wa Chato ni muhimu. Utasababisha kuyaunganisha maeneo ya Kakonko, Nyakanazi, Lusahunga, Ngara, Biharamulo, Bwanga, Runzewe na kupata huduma ya mkoani karibu kwa umbali chini ya km 150 badala ya kulazimika kusafiri mpaka km takribani 300 unaenda mkoani.

Na Teacher Wa Professors Captain Enough (Negrosign).
Huo mkoa uundwe lakini makao makuu ya mkoa yasiwe Chato yawe Runzewe
 
Yaani umeanza vizuri lakini kwenye hitimisho umejichanganya... Jifunze kwamba unapojenga hoja yako hakikisha conclusion ina support your original arguments... Huwezi kuwa na paragraph tatu za mwanzo unaelezea mapungufu ya mwendazake ikiwemo ubinafsi, ukabila na upendeleo halafu umalizie tofautbro lakini kumbuka kuna ubaya na uzuri huwezi kuwa na mabaya peke yake yapo mazuri pia unapofanya hvyo unanilazimisha nitoe mabaya tu sio haki kabisa
sawa bro ila kumbuka upande mmoja wa shillingi unakuwa na upande mwingine pia huwezi ukawa mzuri kwa yote sasa mimi nimeeleza mabaya yake na mazuri pia usije dhani hayapo yapo pia ukifanya hivyo unanilamisha kukandia kitu au unanilazimisha kuwa na mawazo yanayofanana.
Hata wewe uliyenkosoa una mazuri yako lakini pia una mapungufu yako kama binadamu mtu akikuambia usimlazimishe ataje mabaya yako tu na mazuri yako pia
 
Back
Top Bottom