Kuna faida gani ya kuugawa wakati kodi yoote inayokusanywa inaenda dodoma?Ukiuangalia mkoa wa Tabora utagundua ni mkubwa mno kieneo hata kiwilaya kuna Urambo, Kaliuwa, Nzega, Igunga, Manonga, Sikonge, Uliankuru na kadhalika, itafaa ukigawanywa.
Na mimi labda nitabahatisha ukuu wa mkoa.
Mindset is everythingHizi bangi hizi za mtu mweusi,hakuna tija ya kiuchumi ya kugawa mkoa,Kwanza haiingezi kipato kwa nchi, zaidi inaongeza matumizi tu, RC, DED.
Cha muhimu mungewaza kwamba viwanda vya kutengeneza matairi ya gari, au viwanda vya nondo au saruji, au sukari havitoshi, tuongeze viwe vingi, ili tutengeneza mapato, nyie mnawaza kuteuliwa. Bora kuongeza hospitari, vyuo vya Elimu ya juu, au kufungua campus ya UD mkoani Tabora, au Bora mseme, hatuwezi kutegemea mvua kwa kilimo, sasa tuje na mpango wa kutumia maji ya ziwa victoria kufanya umwagiriaji.
Mkoa wa Tabora, unatumia maji ya victoria, lakini na yenyewe ni mgao,maana mkoa hauna mapato ya kuwezesha kutembwza pump 24/7.
Hakuna faida ya kuongeza mkoa, ukisema unasogeza huduma kwa jamii, kwani eneo linaongezeka? Geographical area ipo vile vile, kuongeza mkuu wa mkoa. Kuna msaidia vipi mwananchi wa kawaida, sie hatutski kuona sura, tunataka huduma, vituo vya polisi, barabara, Elimu, afya.
Jiografia darasa la ngapi kufundisha kuwa mkoa wa Tabora kuna wilaya zinazoitwa Manonga ama Ulyankulu?Ukiuangalia mkoa wa Tabora utagundua ni mkubwa mno kieneo hata kiwilaya kuna Urambo, Kaliuwa, Nzega, Igunga, Manonga, Sikonge, Uliankuru na kadhalika, itafaa ukigawanywa.
Na mimi labda nitabahatisha ukuu wa mkoa.
Hamna lolote.... Majimbo mengine na mikoa inagawanywa kwa sababu tu za kisiasaLengo ni usimamizi na ukaribu wa huduma
Bora ingakuwa Tabora na Sikonge badala ya Nzegamikoa ya Tabora ukiwa na wilaya saba na mkoa wa Nzega ukiwa na wilaya nne.
Hivi kuna improvement kwenye maisha ya wananchi sehemu ambazo wamegawa mikoa na wilaya? mwenye mfano atusaidie hapa.
Kitu cha uhakika wakigawa mikoa na wilaya japo si la mara zote, ni watu fulani kunufaika kwa tenda za ujenzi wa makao makuu ya wilya au mkoa husika. Guest House au Lodge za waheshimiwa kupata biashara ya uhakika wakati wilaya au mkoa unaanzishwa sehemu fulani ambako tayari wametegesha vitu vyao.
Hizo hela za wilaya au mkoa mpya wakipeleka kwenye huduma za afya au mashule katika maeneo hayo itakuwa bora zaidi.
Lindi pia. Ingawa kuna wanaosema Tobora Moro Lindi ni makubwa kieneo ila misitu na hifadhi ni kubwa na watu wachachePwani pia
Dodoma Ile Kondoa iwe mkoa
Wanataka chato iwe mkoa.Mkoa wa Tabora 76,150 km² hakuna mpango wa kuugawa, Geita 20,054 km² tunagawa
Huenda kuna mahali tumefungwa kamba.
Sekretarieti ya Mkoa wa Tabora imependekeza kuugawa Mkoa wa Tabora ugawanywe na kuwa mikoa miwili ,kutokana na ukubwa kuliko yote nchini,kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi kwa urahisi na ufanisi zaidi.
Akisoma mapendekezo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora , Bibi Kudra Mwinimvua amesema, Mkoa wa Tabora una eneo la Kilomita za mraba Elfu-75 na 865, ukiwa na wakazi milioni- 2, laki 2 Elfu-91 na 623.
Unapendekezwa kugawanywa katika mikoa ya Tabora ukiwa na wilaya saba na mkoa wa Nzega ukiwa na wilaya nne.
Naufahamu mkoa wa Tabora...
Ni kweli ni Mkubwa, lakini sehemu kubwa ni mapori yasiyokuwa na wakazi...
Ni ukweli kwa ujumla ni mkoa wenye wakazi milioni 2.5 (labda)..
Hata hivyo watu hawa wengi wako mijini. Sehemu kubwa ya eneo la mkoa wa Tabora ni wazi likiwa na misitu na mapori tu..
Hakuna haja ya kuugawa mkoa. Haukidhi vigezo...
Kuna mikoa midogo kieneo lakin huduma za wananchi HAKUNA.. Kwahiyo nayenyewe waigawe? Mi nadhan wilaya zote ziitwe mikoa na tarafa ziwe wilaya... Na kata ziwe tarafa, na vijiji viwe kata, na vitongoji viwe vijiji Ili mfurahi... Maana ni upumbavu mnatuletea kila wakati... Eti kuwasogezea wananchi maendeleo..MAENDELEO YANAKUJA KWA KUFANYA KAZI KUWA WABUNIFU NA KUWATUMIKIA WANANCHI..Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu