Mkong'oto wanaotembezewa wastaafu wanaotumia mafao kuanzisha biashara ni funzo kwamba uzoefu ni muhimu, Biashara zinabuma stress zinawamaliza wazee !

Mmh hapana nliona mambo ni mchanganyiko asee nikimpigia sijui alikua anahisi nataka hela zake, anapokea hasemi halooo akipokea "eeh unasemaje" nikaona hapana.....

Mi mbona sitoleagi mate mali ya mtu yoyote nkaamua kukaa kimya kwanza.
Mwaka 2014 nikiwa nimechapika vibaya nilimpigia my young blood brother aliyekua na ajira yenye maslahi manono akawa hapokei kabisa ili kumjulia tu hali. Nikampigia mtu wa karibu yake akapokea na kukiri kuwa yuko na ndugu yangu ila kasema hataki kuongea na nami. Hiyo siku dogo alinisababishia doa la maisha moyoni mwangu kuhusu yeye. Alidhani nataka nimwombe hela. Nikaacha kumpigia simu toka hiyo siku. Mkataba wa ile kazi ulipoisha kama mwaka mmoja baadae akarudi kwenye kibano kikali kiuchumi wakati huo mimi nimeshajipata kibiashara. Nikampa ajira kwenye biashara yangu akataka kuleta undugu na kuwadharau wafanyakazi wengine. Baada ya maonyo kadhaa nikaamua nimpige chini bila huruma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…