Katika yote kuna Mambo Kadhaa dhahiri
1.Mtu ambaye amekuwa kwenye Ajira,akiingia biashara tofauti na Ajira yake,anatakiwa awe na Ujuzi,Maarifa na Taarifa za Kutosha Juu ya Biashara.Mtaji ni kitu kipqna Sana,mbali na fedha.Ikiwezekana awe ameanza Biashara Miaka 5 Hadi 10 Wakati akiwa kazini.Kusudi akistafu tayari anajua Moto wa Biashara
2.Watu wengi hata waliochangia mada Hawana Ufahamu wa Fedha.Yaani Elimu ya Fedha (Tofauti na uhasibu au finance).Elimu hii unatakiwa uwe nayo toka utotoni,uizoee Fedha,ujue kuweka akiba na yote yanayohusu Fedha.Ndiyo maana hata ungepewa 10b kama huna Elimu hii zitaisha.
3.Unapostafu mwili na akili huwa imechoka.Mikikimikiki ya biashara inahitaji akili fresh,Biashara zina dynamics nyingi Tofauti na Ajira.
4.Kuna Maeneo Salama ya Kuweka Fedha baada ya kustaafu Mfano UTT au Dhamana za Serikali.Lakini pia Nyumba za a Kupangisha zimekuwa Maeneo ya Msaada Kwa wastafu.
5.Ni Vema Mtu anapostafu kufanya biashara Katika Eneo analolimudu na aanze mapema,Mfano kama taaluma yako ni Kada ya Afya,usicheze mbali na hapo.Binafsi ni Mfamasia na nishaendesha Biashara ya Pharmacy Miaka 7 Miaka ya Nyuma na Nina Leseni,hivyo hiyo ndiyo Biashara Hadi Kufa.Kama ni Mwalimu asione haya kuanzisha hata nursery au Kindergarten.Mhasibu afanye uhasibu hata kama ni consultant.Mwanasheria asione aibu Kubeba begi afanye uwakili.Mbona Msajiri wa Zamani wa Vyama vya Siasa alichukua begi na koti lake akaingia Kortini tena.Watu hawajui hii hata Nyerere alianzisha Mwalimu Nyerere Foundation ili awe anaitumia uzoefu wake kwenye Sasa Kuendelea Kupiga Kazi.Nikiwa JKT nilikuwa Kambi ambayo tulikuwa na hukumu la kumjengea Nyumba pale Butiama.Kuna siku alikuwa akienda Shamba Kulima na Wasaidizi wale,kisha Mkutano ikija anapotea kama wiki Kadhaa.Chezea ndani ya Eneo Lako la competency.
6.Kuna ajali ya Makazi,wale ambao hawajakuwa na Makazi Pesa zinakwenda huko.Ingekuwa Vema Miaka 10 kabla ya kustaafu Nyumba iwe ishaisha.Usihangaike na Nyumba tena.
Mwisho hii ni yangu:Waisraeli Hawana msamiati wa kustaafu,ila unabadili Kazi au Shughuli.Ndiyo maana ukisoma Biblia hujawahi Kuona nabii au Kuhani au wafalme wanastafu.Usione aibu kufanya kitu kurahisisha maisha yako.Kama kuna Shamba au Mifugo itunze.Mbona babu zetu hawakuwa na pesheni na wameishi Hadi kuwa wakongwe.
NB:Kama Wewe ni kijana tumia Changamoto hii unayoiona Kuepuka hayo makosa ya watangulizi wako.Wala usikae kusimulia madhira Yao.Usije kukaa kihasara unasubiri mzazi wako akupe portion ya pensheni wala usianze kumpangia,achilia mbali kumshauri maana Wewe Siyo financial advisor wake.