Mkopo kwa dhamana ya nyumba, Msaada wenye Nyumba

Mkopo kwa dhamana ya nyumba, Msaada wenye Nyumba

Milioni 10 ni pesa ndogo sana ukiwa nayo!! Lakini kama hauna utaiona ni pesa nyingi sana!! Zinaweza kuisha kama upepo halafu ukafikiri umeibiwa kumbe umezitumia mwenyewe! Inatakiwa zikitoka benko ziende moja kwa moja kwenye kazi iliyokusudiwa, vinginevyo ni maumivu!!
 
Habari zenu wana jamiii, ni matumaini yangu mu wazima wa afya tele.

Nina Shida ya Pesa ya dharura nimejaribu kukopa kwa watu binafsi hawana, katika taasisi nao wanahitaji dhamana (hasa nyumba).

Nimefika Bank CRDB nimewambia hitaji langu,wakaniambia mahitaji kwa mfanyabiashara kama mimi, Vyote walivyo taja ninavyo na vinapatikana 100%

Kitu ambacho mpaka sasa kinanikosesha huu Mkopo ni DHAMANA ya nyumba.

Kiwanja ninacho lakini hawataki kiwanja ambacho hakijaendelezwa na mimi sijajenga.

Hivyo wameniambia nitafute mdhamini atakaeweza nidhamini mwenye Nyumba.

Nimekileta HAPA JamiiForums nikiamini kuja watu wengi ambao mpo mtaweza nisaidia katika hili.

Nina uhitaji wa Mil.10 lakini CRDB wameangalia Account na kusema wanaweza nipa up to 20Mil.

Kwa atakae nidhamini nilikua nimepanga Kumpa 3m (kama asante) hiii nitampa yeye na hatoirudsha.

Kurudisha mkopo Aniachie Mimi nitaurudsha wote.

Au

Nichukue 20m tugawane 50/50 lakini kurejesha turejeshe wote "tusaidiane"

Naomba kwa yeyote anaeweza nisaidia nitashukuru hata kama Si kwa nyumba basi mtu atakae weza nisaidia mahali naweza jidhamini kwa biashara yangu na mali zangu zingine nikapata huo mkopo nitashukuru pia.

Hitaji Langu kubwa ni 10m TU. Asante kwa yeyote atakaeweza nisaidia fanikisha hili jambo.

MREJESHO :

Si kila mtu ana mashaka kuna watu wana nia ya kusaidia wenye uhitaji. Nimefanikiwa kupata mtu wa kunipa Nyumba yenye HATI lakini kikwazo kikawa BANK tena.

Bank hawataki dhamana ya nyumba ya mtu asie familia yako kwahiyo wameikataa nyumba na kusema ni lazima nyumba iwe ya Baba,mama,mtoto,mke,mume. na si nnje ya hapo.

Asante kwa Aliejitoa na Asante kwa waliotilia shaka.
Mkuu
Sharti la benki ni la kipuuzi
Idea ya kukopa benki ni sahihi.

Hapo ulixhoshindwa kuelewa ni kuwa huyo afisa wa bank anataka umkatie hela aidhinishe mkopo
 
Mimi aje tuyajenge,nampa Hati ORIGINAL hata leo hii,lakini akileta janjajanja nimeshampa ONYO kabisa!!maana kwa uzoefu wangu nimeshashuhudia sana hayo mambo,kwamba mtu anamdhamini mtu Hati anapata Mkopo kisha anaingia mitini kufanya marejesho,mwisho wa siku Bank wanakuja kuuza nyumba
Tapeli kwa tapeli

Niko paleee!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lete hilo deal I will finance endapo kama ni perfect project, then nitakuwa mbia.
 
Yaani mtu akupe hati yake ya nyumba ukapeleke benki ili upatiwe mkopo? Duh huo ni muhali mkubwa sana kwani ukishindwa au ukiamua kutokulipa nyumba ndiyo imekwenda hiyo.
Yule Mbunge mwenye PhD huku akiwa na elimu ya darasa la 7 aliwahi kumfanyia ndezi mmoja kule Mbezi DSM kitu cha aina hii hii. Kilichompata yule ndezi, hatokuja kukisahau kamwe.

Jamaa alivuta mkopo benki kwa kutumia hati ya nyumba ya ghorofa moja Ndezi kule Mbezi! Halafu baada ya kuvuta mkopo akawa harejeshi marejesho. Benki ikaja kupiga mnada nyumba, Ndezi akajikuta ameduwaa tu na kushindwa cha kufanya.
 
Mkuu
Sharti la benki ni la kipuuzi
Idea ya kukopa benki ni sahihi.

Hapo ulixhoshindwa kuelewa ni kuwa huyo afisa wa bank anataka umkatie hela aidhinishe mkopo
Daaah,ina mana mkuu endapo nitamwambia naweza mkatia chochote kitu mkopo ukitoka ataidhinisha?

inakuaje yeye akiidhinisha halafu wale wakaguzi wakienda ikagua nyumba,nao sio itabidi niwagaie tena chochote kitu?

Hapo anaetakiwa kupoozwa ni nani mkuu?
 
Unaomba mkopo , Na huo mkopo unaukatia insurance /bima. Hiyo insurance ndio collateral yao...waulize NMB, Exim au CRDB.
Yani bila colateral yoyote ile naweza pata huo mkopo nikiukatia bima mkuu?

Kwa Mkopo wa 20m nikiukatia BIMA gharama yake ipoje?

Hii kitu inawezekana kweliii mkuu? mbona sijawahi isikia?
 
Daaah,ina mana mkuu endapo nitamwambia naweza mkatia chochote kitu mkopo ukitoka ataidhinisha?

inakuaje yeye akiidhinisha halafu wale wakaguzi wakienda ikagua nyumba,nao sio itabidi niwagaie tena chochote kitu?

Hapo anaetakiwa kupoozwa ni nani mkuu?
Kwani waliokupa masharti ni wakaguzi au muidhinishaji mikopo?
 
Yani bila colateral yoyote ile naweza pata huo mkopo nikiukatia bima mkuu?

Kwa Mkopo wa 20m nikiukatia BIMA gharama yake ipoje?

Hii kitu inawezekana kweliii mkuu? mbona sijawahi isikia?
Mkuu, ongea na bank tajwa- watakupa maelekezo. Hakuna kitu kisichowezekana duniani humu labda kifo tu. Penye nia Pana Njia
 
Mkuu
Sharti la benki ni la kipuuzi
Idea ya kukopa benki ni sahihi.

Hapo ulixhoshindwa kuelewa ni kuwa huyo afisa wa bank anataka umkatie hela aidhinishe mkopo
Benki hukopesha nyumba iliyokamilika hasa hupenda nyumba ya biashara na sio.gofu hata kama gofu liwe prime area wanajua usipolipa linauzika chap chap

Lengo la benki kukopesha sio kuchukua maki iliyowekwa dhamana ni marejesho

Nyumba iko porini huko kuna hadi majoka kibao nani achukue dhamana? Jaribu hata kuiuza upate basi hiyo pesa uza mwenyewe usisukumie benki kama unaona hiyo nyumba ina thamani
 
Back
Top Bottom