Mkopo wa dharura unahitajika. Dhamana ni nyumba iliyopo Dar es Salaam

Mkopo wa dharura unahitajika. Dhamana ni nyumba iliyopo Dar es Salaam

Criterion

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2008
Posts
11,797
Reaction score
11,891
Ndugu zangu, nimefikiwa na watu wanahitaji shilingi milioni tano (5,000,000) kwa shughuli za kibiashara. Wanasema wako tayari kulilpa mkopo huo kwa riba ya miezi miwili. Nilipowahoji, ili kuwasaidia, wakasema

1) Wanamazao yao ya biashara wanatakiwa kuyaweka sawa na kuyafikisha sokoni kabla mvua haijakolea.

2) Wanahitaji shilingi milioni tano kwa mpigo na kwa haraka.

3) Wana mtu mmoja anayewaelewa na hivyo ametoa nyumba yake iwadhamini katika mkopo huo.

4) Wamejaribu kutafuta kwa wakopeshaji binafsi wanaambiwa wanatakiwa kuwa na dhamana ya gari ambapo ili wapate huo mkopo, hitaji ni kwamba wapeleke gari la dhamana lika paki kwa mkoopeshaji na hati ya gari, na waandikishiane kwamba gari hilo wamemuuzia mkopeshaji, eti ili kama wasipolipa auze chapu chapu. Bahati mbaya hawana mtu mwenye gari miongoni mwao. Mazao hayo wanategemea yawasimamishe.

Kwa kuwa mimi sina uwezo wa kuwakopesha, nimeona nilete hapa jamvini. Kama kuna mtu mwenye nia ya kutoa mkopo huo bila hila, kwa utaratibu wa wazi kwamba miezi 2 alipwe na riba yake, la sivyo nyumba ya dhamana iwe halali yake, naomba ani inbox, ili nimuunganishe na hao wateja.

Natanguliza Shukrani.
 
Mods peleka biashara na uchumi

Twende kwenye mada hakuna mkopo wa dharura Tanzania hiyi labda kama hao wakopeshaji ndugu jamaa nk
Unaweza ukakopa na ikibuma usirudishe ndio mana mmewekewa hayo mashart
kama kweli nyumba ipo ina hati kila kitu fuaten utaratibu mliowekewa mbona simpo tu
huku kwingine ni kutafuta kutapeliana labda kama mnaajenda nyingine

Mana binadamu wa sikuiz amna mambo mengi nyuma ya macho na midomo yenu
 
Nina access na JF, na pia kuwasaidia kama ndugu zangu. Naijua shida yao nadhani hapa si uharifu.

Pili kwa wataalamu wa mikopo wanaelewa maana ya third party quarantee. Hope tuko pamoja kiongozi.

Kila kitu kiko sawa. Wataalamu wanaeelwa.
Muanzisha uzi sio muhitaji mkopo

Muweka dhamana ya nyumba sio mchukua mkopo.

Kuna jambo halipo sawa hapa.
 
Zipo taasisi nyingi za kukopesha, waende huko wafuate utaratibu waache janja janja.

Wamekuambia wanahitaji emergency loan. Bank gani wanatoa mikopo ya dharura na ya miezi 2 ili niwashauri waende?
 
Sasa hapo akishindwa kulipa unaenda kuuza nyumba ya dhamana kwa vigezo vipi? Aliyekopa sio mwenye nyumba. Hati haina jina la mkopaji.

Nimesema, wataalamu wa mikopo wanajua kile ninasema. Mtu asiyejua nidye anakuwa na maswali kama haya.

Hakuna sheria ya dhamana inayosema dhamana lazima iwe na jina la mkopaji. Huo ni upungufu wa maarifa ya kitaaluma. Kuna kitu kinaitwa thrid party quarantee na kwa mwelewa anatengeneza tool ya dhamana yenye urahisi huo. Ni kitu cha kawaida sana kudhaminiana.

Naomba kama kuna mtaalamu mwenye hizo fedha ndiye nijadili naye kwa kuwa yeye ni rahisi kuelewa.
 
Nimesema, wataalamu wa mikopo wanajua kile ninasema. Mtu asiyejua nidye anakuwa na maswali kama haya.

Hakuna sheria ya dhamana inayosema dhamana lazima iwe na jina la mkopaji. Huo ni upungufu wa maarifa ya kitaaluma. Kuna kitu kinaitwa thrid party quarantee na kwa mwelewa anatengeneza tool ya dhamana yenye urahisi huo. Ni kitu cha kawaida sana kudhaminiana.

Naomba kama kuna mtaalamu mwenye hizo fedha ndiye nijadili naye kwa kuwa yeye ni rahisi kuelewa.
Sawa. Kwahiyo mwenye hiyo nyumba ndio anawadhamini? Yaani inakuwa kama yeye ndio anachukua mkopo?
 
Sawa. Kwahiyo mwenye hiyo nyumba ndio anawadhamini? Yaani inakuwa kama yeye ndio anachukua mkopo?
Kwa faida ya wengi. Mkopo wowote halali lazima kwanza ufanyike kwa uwazi na ukweli. Ukipindisha lolote katika uhalisia, umetengeneza mkopo chechefu au non-performing loan ambayo mwisho wa siku ni kuharibu vitabu, taswira na kupoteza mtaji.
Kwa mantiki hiyo:-

1.Anayekopa, anatakiwa atambuliwe kama mkopaji kwa majina yake na vigezo vingine ambavyo mkopeshaji atakuwa kaviweka.

2. Dhamana inayowekwa kwenye mkopo huo inatakiwa itathminiwe peke yake kama dhamana ya mkopo. Pamoja na mambo mengine, umiliki wa dhamana hiyo hata uwe wa serikali ya kijiji, ujulikane kwa maana ya nani mmiliki kisheria. Hapo utakwenda kuangalia jina la nyaraka zozote zilizopo mnazoafikiana kutumia. Halafu mwenye majina yanayoonekana kwenye hizo nyaraka, ndiye aseme kama anaweka nyumba ama mali hiyo kuwa rehani ya mkopo wa mkopaji fulani anayekopa sh. kadhaa kutoka kwa fulani kwa mashart a b c,.

Pamoja na governing procedures zingine, hii inamweka mkoopeshaji sehemu salama kabisa ya kushughulika na dhamana bila chenga. Halafu wao waelewane kivyao kwa walivyodhaminiana.

Bahati mbaya sina fedha hiyo, mimi ningefanya biashara nzuri nikapata na fedha za riba mwaka mpya..

Kwa nyongeza, kama anaamua mdhamini kuwa kama mkopaji, "basi atakuwa mkopaji halisi na fedha atachukua yeye, kila kitu yeye kitu ambacho, pia hakimtendei haki mdhamini.
 
Ninacho cha kukusidia ndugu yangu katika Tanzania
Hiyo biashara inaonekana ni nzuri sana na inalipa ndio maana yuko tayari kutoa nyumbayake kama dhamana
Kiuhalisia hapo yupo kwenye level muhimu kabla ya kutapeliwa rasmi,utapeli huo una pande mbili pande ya kwanza ni anaeoneshwa mchongo wa pili anaepokea Hati kama dhamana
Mwisho.
 
Umetumia tathmini gani kufikia hiyo conclusion?

Anayetapeliwa ni nani kwa utafiti wako?

Wewe huna hata chembe ya moyo wa kumsaidia ndugu yako wa karibu akihitaji msaada wako? Au kwenu nyote ni manunda wala watu?

Unaelimu gani katika masuala ya mikopo?
Unajua lakini kwamba mikopo ni taaluma?

Ulishawahi kusikia mtu kakopo na kurejesha hata bila dhamana?

Unaposema anayepokea hati anatapeliwa, wewe ulitaka apokee nini kama dhamana kwa elimu yako?

Naomba nisiwe na poteza muda wangu na kundi la "Others".

Ulishawahi kuchukua mkopo sehemu yoyote?
Ninacho cha kukusidia ndugu yangu katika Tanzania
Hiyo biashara inaonekana ni nzuri sana na inalipa ndio maana yuko tayari kutoa nyumbayake kama dhamana
Kiuhalisia hapo yupo kwenye level muhimu kabla ya kutapeliwa rasmi,utapeli huo una pande mbili pande ya kwanza ni anaeoneshwa mchongo wa pili anaepokea Hati kama dhamana
Mwisho.
 
Back
Top Bottom