Tetesi: MKT wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Kuanza Ziara ya Ulaya na US Kupitia Dubai 28/08/2016? !.

Tetesi: MKT wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Kuanza Ziara ya Ulaya na US Kupitia Dubai 28/08/2016? !.

Nilikuwa nadhani yule mwanamke niliyemwacha kutokana na tabia zake za kimbea ni kubuhu kwenye hizo tabia.
Ila Leo nimegundua huyu Pasco ni Kubuhu wa wambea. Sijui kama kuna mwanaume atakayemchumbia
 
Hicho kijiwe ulichokaa ni bora hata ungetumia muda huo kwenda hadi Bagamoyo na kurudi kwa miguu pengine hata ungekuwa umefanya jambo la maana sana

"Ziara hiyo inajumuisha matibabu..... " Anyaway angalia usije ukaota tende bure... Kwa hii post umezidiwa akili hadi na malumbano ya Mbutananga na LeMutuz ambao wanabishana kuwa ni nani kati yao anavaaga chupi kubwa..!
 
hata kwenye vita ya kagera mwalim hakushika mtutu front line lakini tunasema yeye ndie kiongozi kama watu wameandamana na kiongozi wao ndio aliesema waandamane kama swala hili ni kosa mbona hawaendi kuwakamata viongozi na kuwafunga badala yake wanatia virungu waandamanaji na kuwapiga mabomu ya machozi kwa kuwa hawajui sheria mimi nauliza hapa nchini yamefanyika maandamano mengi ambayo yalipingwa na polisi naweza kuambiwa idadi ya viongozi walioitisha maandamano hayo ambapo wamefungwa
 
Nilikuwa nadhani yule mwanamke niliyemwacha kutokana na tabia zake za kimbea ni kubuhu kwenye hizo tabia.
Ila Leo nimegundua huyu Pasco ni Kubuhu wa wambea. Sijui kama kuna mwanaume atakayemchumbia
Hahahahah makamanda poleni sana..
Hicho kijiwe ulichokaa ni bora hata ungetumia muda huo kwenda hadi Bagamoyo na kurudi kwa miguu pengine hata ungekuwa umefanya jambo la maana sana

"Ziara hiyo inajumuisha matibabu..... " Anyaway angalia usije ukaota tende bure... Kwa hii post umezidiwa akili hadi na malumbano ya Mbutananga na LeMutuz ambao wanabishana kuwa ni nani kati yao anavaaga chupi kubwa..!
 
Pasco wa sasa si wa zamani,sishangai maana majungu,unafiki unalipa sana awamu hii
 
Kuna jamaa aliwahi kupost humu jinsi mwanaume mmoja wa Dar anayejiita AT alivyomsuta Peter Msechu.. Ila Dar kuna wanaume wasutaji na wazushi sana..! Utamwambiaje mwanaume mwenzako eti ana tumbo kama kameza Vitz??
 
Wanabodi,

Naomba kuanza uzi huu kwa ku declare my interest kuwa Mimi Pasco wa JF, naunga mkono maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima na siku ya siku, nitajitokeza kushiriki na nitatoa wito wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, tujitokeze kwa wingi! .

Niko kwenye kijiwe fulani hapa mjini kati, jijini Dar es Salaam, nikainasa ndogondogo kuwa wakati chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema, kiko kwenye maandalizi ya maandamano na mikutano nchi nzima kuhamasisha UKUTA, siku ya Tarehe 1 September 2016, habari ambazo hazijathibitishwa, zimeeleza kuwa, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe, yuko kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuanza ziara binafsi ya Ulaya na Marekani kupitia Dubai. Ziara hiyo umeelezwa kuwa pia itahusisha matibabu, uchunguzi wa afya na mapumziko mafupi mjini Dubai. Mtoaji wa taarifa hiyo isiyothibitishwa, imesema ziara hiyo ni binafsi, ya kifamilia na ya kibiashara.

Mtoa habari huyu alijitambulisha rasmi kama mkereketwa wa Chadema, na kutaja majina yake, lakini kufuatia habari hizi bado hazijathibitishwa rasmi na uongozi wa Chadema, naomba nisilitaje jina la mtoa habari wangu chini ya kinga ya kihabari iitwayo "the confidentiality of the source " mpaka habari hizi zitakapothibitishwa au kukanushwa.

Kufuatia source wa habari hii sio a trusted source ndio maana habari hii ina lebo ya tetesi, ikiishatibitishwa, neno tetesi litaondolewa! . Sii mara moja wala mbili kwa tetesi mbali mbali kushuka jf na baadae zikathibitishwa au kukanushwa! .

Hii sii mara ya kwanza kwa kiongozi Mkuu wa Chadema kuanzisha maandamano lakini siku ya siku haongozi harakati hizo na badala yake huwa safarini kikazi au kibinafsi hivyo kuwaachia wengine waliopo.

Lengo la kuileta habari hii humu jf hata kabla haijathibitishwa ili ile jf spirit ya "be the first to know! ".

Ikitokea ikathibitika habari hii sii ya kweli bali ni uzushi tuu, nitamuomba mode, asiufute uzi huu bali aufunge tuu kusubiria hiyo tarehe 1 September tuthibitishe this time around, Mwenyekiti atakuwepo kuongoza maandamano.

Lengo la kuomba uzi usifutwe bali ufungwe tuu, ni kufuatia posibility ya Chadema kuikanusha taarifa hii kuwa sii kweli lakini siku ya siku ikaelezwa Mwenyekiti amepata safari ya dharura.

Pasco.
Wajinga ndiyo waliwao
 
Wewe Pasco hua ni mnafki sana, hujui kuusema ukweli halafu ndumi la kuwili. Hivi hela za sabasaba umeshamaliza?
 
Nilikuwa namuheshimu sana huyu Pasco, ila kwanzia Leo nimekudharau kuliko neno dharau. Heshima yote uliyojijengea apa Jf umeibomoa kwa ajili ya sifa za kijinga.

Sijui haya majungu yanawasaidia nini
 
Back
Top Bottom