Mkude ndiye kiungo bora wa chini kuwahi kutokea nchini?

Mkude huyu ambaye hata Timu ya Taifa hafurukuti? Ulizia wanawajua akina Ali Maumba(Coastal Union). Hussein Masha(Pamba & Simba). Isa Athumani( Yanga). Au Michael Paul "Nylon" ( Simba)
Umemuona juzi taifa akikichafua ,narudia tena hakuna kama mkude Tanzania

National team wanamuonea tu
 
Daaah mtoa mada kuna viungo bora kbsaa hujawatendea haki

Mf : Issa Athuman.. Ramadhan Lenny.. Athuman Abdalah china.. Hussen Marsha.. Salvatory Edward... Niko Bambaga... Michael Paul... Hamis Gaga.. Wazir Mahadhi.. Godfrey Bonny Mwandanje...kiukweli Mkude ni mzr sio kwa ulivyompamba mkuu...
 
Japo namkubali Huyu Fundi Jonas Gerald Mkude,Lakini huu uchambuzi wako wa Kitaalam nimeupenda na nimeukubali.
 
Kwa nafasi yake ya holding mildifielder, anaitendea haki.
Mkude kwa mimi nimuonavyo, hapaki rangi mpira, anatimiza tu jukumu lake, nyang'anya mpira kisha toa pasi, mkude yeye ni mtu wa kuangalia mbele tu, pasi zake nyingi ni forwards sio za nyuma vinginevyo imemlazimu sana. Ana pasi ambazo nyingi ni accurate na diagonal, kwa uchezaji wake na vision aliyo nayo, ana uwezo wa kugeuza defense kuwa offense ndani ya muda mchache sana.
 
Mkude huyu ambaye hata Timu ya Taifa hafurukuti? Ulizia wanawajua akina Ali Maumba(Coastal Union). Hussein Masha(Pamba & Simba). Isa Athumani( Yanga). Au Michael Paul "Nylon" ( Simba)
Anayefurukuta taifa stars hii ni nani??
 
Uliwahi kumuona ATHUMANI CHINA? na HAMISI GAGA? hawa watu ni hatari sana,, hyo mkude anajaribu tu.... Sio FUNDI wa muda wote
Kila kizazi na watu wake, ndio maana messi halinganishwi na pele.
 
Kila kizazi na watu wake, ndio maana messi halinganishwi na pele.
Ndy hajawahi kutokea? ,,wakati walikuwapo akina NICO NJOHOLE,,CHINA,,GAGA,ISSA ATHUMANI,,ALLY MAUMBA,, LENY,,MASHA,,nk.,, SEMA kwa SASA UTAELEWEKA
 
Ndy hajawahi kutokea? ,,wakati walikuwapo akina NICO NJOHOLE,,CHINA,,GAGA,ISSA ATHUMANI,,ALLY MAUMBA,, LENY,,MASHA,,nk.,, SEMA kwa SASA UTAELEWEKA
Sasa kina Masha, Ramadhani Lenny (mapafu ya mbwa) ndio kizazi cha Mkude?? Hao wa miaka ya 90 na 2000 mwanzo. Mkude mlinganishe na wale wa 2010 mpaka sasa. Naongelea kizazi, sio mamba anayocheza tu.
 
Sasa kina Masha, Ramadhani Lenny (mapafu ya mbwa) ndio kizazi cha Mkude?? Hao wa miaka ya 90 na 2000 mwanzo. Mkude mlinganishe na wale wa 2010 mpaka sasa. Naongelea kizazi, sio mamba anayocheza tu.
UZI unasema mkude ndiyo kiungo wa BORA ambaye hajawahi kutokea,,sasa unajuwa KISWAHILI cha KUSOMA au kuandika?kama hajawahi tokea hao akina NJOHOLE walikuwa wa NCHI GN?
 
Athuman Iddi Chuji
Shaban Nditi
Seleman Matola

Hawa wachache ni wachezaji bora kuliko Mkude,kwenye list ya viungo wote Mkude hata kwenye 50 bora hawezi kuwepo
 
Athuman Iddi Chuji
Shaban Nditi
Seleman Matola

Hawa wachache ni wachezaji bora kuliko Mkude,kwenye list ya viungo wote Mkude hata kwenye 50 bora hawezi kuwepo
Yaani hata Simba tu hawezi kuwa kiungo mkabaji bora wa wakati wote...

Mleta mada huenda umri wake ungali mdogo...
 
Hata Marehemu Godfrey Bonny tu hamfikii huko kwa akina Lenny mmeenda mbali
 
UZI unasema mkude ndiyo kiungo wa BORA ambaye hajawahi kutokea,,sasa unajuwa KISWAHILI cha KUSOMA au kuandika?kama hajawahi tokea hao akina NJOHOLE walikuwa wa NCHI GN?
Ndio maana nami kabla ya kusema hivyo nilisema kila kizazi kina watu wake.
 

Huu ni uongo. Mpira wa tanzania haukuwahi kuwa wa tofauti na sasa.... Hayo maneno eti zaman ndo kulikuwa na mpira ni uongo ambao unapaswa kutumika kuwadanganya watoto wadogo.i was there. Miaka ile ya beki hasifiwi kazi yake ni kuondoa mpira nyuma na wachezaji wengine kukimbia na mpira anao anao.... Unakuja kudanganya watu hapa... Si afadhali miaka hii hata pasi zipo na mashambulizi yanapangwa... Acheni uongo mkidhni wote ni kizazi za 90s humu ndani.
 
Kwanza mleta mada amesema "Kwa muda wote", unadhani kwanza ametafiti kujua kuwa akina Abdulrahman Lukongo walikuwa wanachezaje!
Mtemi Ramadhani? Hamis Gagarino? Juma Mkambi? Charles Bornface? Athumani China? Khalid Abeid? Abdulrahman Juma?Hivi Sunday Manara alikuwa mshambuliaji au kiungo mshambuliaji?
Mpira wa mabeki kubutua? Upi huo?
Method Mogella uliwahi kumsikia? Samli Ayubu"beki mstaarabu", Jumanne Ayubu "kwasakwasa" Mohamed Chuma nk. Mleta mada aliwahi kuwasikia hawa? Tuepuke kauli jumuifu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…