Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 86
‘Bado mmoja ..’
Kiukweli ushahidi niliokuwa nao ulikuwa unatosha kabisa, kufanya lolote, lakini kuna baadhi ya mambo nilihitajika kuyafuatilia, ili kuhakiki, na sikutaka kutumia nguvu, sana, ni hekima ndogo tu....
Tuendelee na kisa chetu.
*********
Docta alisafiri kwenda kijijini kuonana na mke wake!
Wakati nipo nyumbani nikijiandaa kwenda kumtembelea mume wangu hospitalini, mara nikasikia kuwa nina mgeni, nilipouliza ni nani wakasema ni Inspekta wa polisi, nikajua kuwa sasa mambo yameanza kuvuja, sikutaka mambo haya yaharakishe sana kabla sijamalizana na uchunguzi wangu.
Ukisikia polisi kaja kwako hata kama huna kosa utakuwa na wasiwasi tu…
Nikatoka nje kwa kupitia mlango wa nyuma, hadi bustanini, nikaagiza huyo mgeni aletwe huko , kwani likuwa kakaribishwa chumba cha maongezi, sikutaka niongee naye ndani, nilitaka sehemu huru ambayo kila mtu anaweza kuona.
Mkuu huyo akaja huko bustanini, akiwa kashikilia mkoba wake, kuonyesha yupo kazini. Alikuwa mtu wa makamo, na hali yake kiafya ilionyesha sio haba, kitambi kidogo, japokuwa ukakamavu wa kiaskari bado ulikuwa kwenye damu, akasogea hadi pale nilipokuwa nimesimama, na mimi nikamsogelea na kunyosha mkono kusalimiana.
‘Samahani kwa ujio huu wa ghafla, unafahamu kazi zetu tena, pale unapopata taarifa unatakiwa uifuatilie kwa haraka , maana tuna kazi nyingi sana za kufanya,…kwa hili sikupenda kuwatuma vijana wangu, namuheshimu sana baba yako,...’akaaza kujieleza.
‘Nashukuru kwa hilo pia nashkuru kwa kunitembelea japokuwa nilikuwa na ratiba zangu nyingine kiukweli,..,kwani sasa hivi natakiwa kwenda kumuona mgonjwa...huko alipolazwa..’nikasema
‘Oh, kwani mume wako anaendeleaje?’ akauliza
‘Hajambo kidogo, unajua matatizo yake sio yale ya kusema kapona, anahitajia muda wa kuchunguzwa, itokee hiyo hali ndio unaweza kufanya jambo, lakini hajambo, sasa hivi yupo kwenye mazoezi tu ya kawaida...’nikasema
‘Kwahiyo kumbe tunaweza kumtembelea na kuongea naye?’ akauliza
‘Mhh, hayo anayeweza kuyajibu ni dakitari wake,…kwani kuna jambo mnahitaji kuongea naye,?’ nikamuuliza
‘Ni maswali ya kawaida tu....lakini kama bado hali yake haijawa sawa hakuna haraka sana, ....’akasema
‘Haya niambie ujio wako kwangu una makusudio gani na mimi, maana nyie watu hamji kwa mtu bila lengo maalumu, na mkionekana kwa mtu ujue kuna jambo...’nikasema.
‘Ni kweli, nimekuja kwa lengo maalum, lakini sio kwa ubaya,....’akasema na kutoa makabrasha yake, halafu akasema;
‘Katika uchunguzi wetu, tumegundua kuwa yule kijana mdogo wa mume wako alikuwepo siku ile Makabrasha alipouwawa, na alionekana akiranda randa eneo la lile jengo, na baadaye akaondoka na mtu siyefahamika, ..’akatulia
‘Sasa tulitaka kuongea naye, lakini hayupo, na watu wangu wamejaribu kumtafuta bila mafanikio, hata kazini kwake hawajui huyo mdogo wake mume wako kaenda wapi, je unafahamu huyu kijana wenu kaenda wapi, maana ni muhimu sana..?’ akaniuliza
‘Kwakweli hata mimi sijui kaenda wapi, na nilishamwambia kuwa asiondoke bila ya kuwasiliana na mimi…’nikasema na yeye akaniangalia kwa mashaka.
‘Haiwezekani, ina maana hata nyie, hata …mke wake naye hayupo…sasa inatupa mashaka kidogo, ....Je hata mume wako hafahamu wapi kijana wenu alipokwenda...? ‘ akauliza
‘Hafahamu kabisa, maana jana nilipofika kumuona mgonjwa, yeye mwenyewe ndiye aliniulizia kama nimewahi kuonana na mdogo wake, kwani anaona ajabu siku mbili kupita bila mdogo wake kufika kumuona,.... sio kawaida yake..’akasema
‘Ina maana katoroka basi…, au kuna kitu kimemtokea, maana msije mkakaa kimiya kumbe yupo kwenye matatizo?’ akaniuliza
‘Kwanini atoroke, hilo la kutoroka halipo…na sizani kama yupo kwenye matatizo, huenda ni katika kuhangaika na mishe mishe za kutafuta riziki…huenda kuna jambo alilifuatilia, akakwama mahali, na hataki kusema wapi alipo, unafahamu tena vijana...lakini kauli yako hiyo ya kusema katoroka, ina nitia mashaka, kwanini unasema hivyo?’ nikamuuliza
‘Sisi katokana na uchunguzi wetu, tuna mambo tulitaka kumuuliza, tunahisi kuna mambo anayafahamu, unajua bado tunafuatilia ile kesi ya mauaji ya Makabrasha.....’akasema
‘Kwahiyo mnamshuku kwa msingi gani, kuwa anafahamu muuaji, au yeye kashiriki, au ni kutaka kufahamu mambo ambayo huenda yatawasaidia kumpata huyo muuaji?’ nikamuuliza.
‘Tunahisi yeye anaweza kutusaidia, ....kumpata huyo muuaji, ‘akasema.
‘Mhh, kama angelikuwa anafahamu hilo, angelisema, maana ukumbuke Makabrasha alikuwa ndiye wakili wao, na alikuwa hajafanikisha malengo yao, wasingeliweza kukaa kimiya kama wanamfahamu huyo muuaji...’ nikasema
‘Kiukweli Mkabrasha alikuwa haaminiki, inawezekana, huyo kijana anamfahamu huyo muaaji, lakini hana uhakika kuwa kweli huyo jamaa kafanya hivyo, akiogopa kujiingiza kwenye matatizi ya ushahidi.., au pia inawezekana alishirikiana na huyo muaaji, ,....’akasema.
‘Hilo la kushirikiana na huyo muuaji, nalipinga, kama nilivyokuambia, Makabrasha alikuwa ni kama ndugu yao, pili alikuwa ni wakili wao .....’nikasema.
‘Yote yawezekana, ndio maana nilitaka niongee naye mimi mwenyewe uso kwa uso, na sisi ni wataalamu wa mambo hayo, nikiongea naye tu, ninaweza kuhakiki hayo ninayotaka kuyafahamu, kama hahusiki hatutamlazimisha,...’akasema
‘Nakumbuka mara ya kwanza ulisema aliyefanya hivyo, atakuwa mtu wa ndani, anaweza akawa mfanyakazi wa mule mule,..akishirikiana na watu wa nje, ina maana mnahisi kuwa huyo aliyekuwa nje ni huyo kijana?’ nikamuuliza.
‘Ni moja ya mambo ambayo tunayafuatilia, kuhakiki, ndio maana tunataka kumuhoji yeye binafsi,…kuna ushahidi huo kuwa huenda ni yeye aliyekuwa nje,...lakini kama ulivyosema , ni kwanini wamuue mtu kama huyo,..hata sisi tunashindwa kuunganisha huo ukweli, mpaka tumuone, ila tunahisi huyo kijana atakuwa anahusika, kwa namna moja au nyingine,...sasa kinachotufanya tuzidi kumweka kwenye kundi la wahusika, ni huko kutoweke kwake kwa ghafla...’akasema
‘Mimi sijui kama kweli katoweka , hiyo kauli bado sijakubaliana nayo, kwani sio mara ya kwanza kufanya hivyo, nilishawahi kumkanya kuhusu hiyo tabia yake ya kuondoka bila kuaga, na kukaa kimiya,....’nikasema.
‘Kwahiyo hiyo sio mara ya kwanza kuondoka ghafla hivyo…?’ akauliza
‘Sio mara ya kwanza, ..ni tabia yake, na mwenyewe hujitetea akisema kazi zake zinamfanya awe hivyo, anaweza kuitwa mahali, akajikuta hana mawasiliano, au hataki kufahamika yupo wapi, kwasababu ya ushindani wa kibiashara..ndivyo anavyojietetea....’nikasema.
‘Hiyo sio kawaida kabisa, kama ni hivyo kwanini kazini kwake wasifahamu wapi alipo…ina maana kuondoka huko ni kwa kibinafsi, au sio…?’akauliza
‘Ndivyo anavyofanya hivyo, ....sio jambo geni kwetu...akirudi nitamfahamisha kuwa nyie mnamtafuta....’nikasema
‘Ni bora ufanye hivyo, kwasababu wanafamilia wa Makabrasha wanataka hiyo kesi ikamilike haraka iwezekanavyo…, na wanadai kuwa kuna njama za kuficha ukweli, na wameshapeleka malalamiko yao ngazi za juu...’akasema
‘Ni nani kafanya hivyo?’ nikauliza
‘Ni mwafamilia wao mmoja ambaye ni mwanasheria, ni mmoja wa watoto wake, acha yule mkubwa, yule mkubwa tuliongea naye tukamalizana, lakini kuna huyo mwanasheria, ni mkorofi kidogo…,anajifanya anafahamu sana sheria,....’akasema
‘Kazi ipo…kam ni huyo eeh,…haya hilo ni jukumu lenu,..na , kwahiyo mkaamua kuanza tena upelelezi au sio kutokana na shinikizo hilo.....?’nikamuuliza
‘Sio kuanza upelelezi, mbona upelelezi ulikuwa unaendelea, japokuwa sio ule wa haraka haraka, maana tulifika mahali tukasema muuaji ni mmoja wa maadui za marehemu, lakini sio kwamba tulishafunga jalada lake,..hapana,bado tunachunguza....’akasema.
‘Mimi niwatakie kila-laheri, maana mauaji hayo, yalinitia doa, kwahiyo akipatikana huyo muuaji, hata mimi nitakuwa katika wakati mzuri hata ikibidi kuwashitaki nyie polisi kwa kunisingizia mambo nisiyohusika nayo...’nikasema.
‘Huwezi kutushitaki, sisi ni moja ya kazi zetu...’akasema akijiandaa kuondoka.
‘Haya nashukuru kwa hilo, nitafanya kama ulivyoniomba, na inaonekana huyo muaaji ni mjanja sana, kafanya mauaji na imeshindikana kumfahamu ni nani, isije ikawa ni mmoja wa watu wenu...’nikasema
‘Hiyo haipo, sio watu wangu...ni tetesi za mitaani tu, hilo nakuhakikishia, ni mmoja wa maadui za marehemu, na tutampata tu....ni swala la muda...’akasema.
‘Lakini nahisi sasa hivi mnafanya hivyo kwa shinikizo la wanafamilia, nyie mlishakata tamaa..’nikasema.
‘Hapana hatukuwa tumekata tamaa, ila ushirikiana wa wananchi umekuwa mdogo, ni kama vile watu walitaka mtu huyo afe tu. Sisi bado tupo kazini, tutapambana na hawo watu,na kama kuna watu wanafahamu muuaji watuambie, sisi hatuwezi kuwashika watu kama hakuna ushahidi…’akasema
‘Nakuelewa afande..’nikasema
‘Tuliwaambia hao wanafamilia, kama kuna watu wanaowahisi watufahamishe,...maana mzazi wao, alikuwa kajijengea maisha ya kuwa na maadui wengi, hata ndani ya familia yake mwenyewe, hata marafiki zake, sasa ni nani unaweza kumhisi, hiyo sio kazi rahisi....’akasema
‘Lakini ni moja ya kazi zenu, msikwepe majukumu...’nikasema
‘Hilo silikatai, lakini ili tufanikiwe, tunahitajia ushirikiane wenu,...na nilikuwa nataka kukuuliza swali…kuna tetesi kuwa kuna vitu viliibiwa kwako, na sasa umevipata ni kweli au si kweli?’ akaniuliza
‘Vitu gani hivyo…?’ nikamuuliza.
‘Nimesikia kuwa kuna mikataba yako ilipotea, ..na umeshaipata, je ni nani aliichukua?’ akaniuliza
‘Mimi sijafika kwenu kulalamika kuhusu kuibiwa,..ila nilisema kuna vitu vyangu havionekani, … je ulishawahi kuniona kuja kwako kulalamika kuhusu kuibiwa?’ nikamuuliza
‘Hujashitakia hilo...lakini unaweza ukaacha kutokana na shinikizo, na tunahisi uliogopa, kufanya hivyo kwa sababu ya ujanja wa Makabrasha,..na ndio maana kipindi kile tulikushikilia, tukijua huenda uliamua kumuondoa kwa tabia yake hiyo..’akasema
‘Hapana sio hivyo…’nikasema
‘Kuna tetesi hizo…,hebu niambie ukweli, maana huenda ikatusaidia katika uchunguzi wetu..’akasema
‘Mkuu mimi sina cha kukuambia,...kama ningelikuwa na tatizo hilo ningelishawaambia, na kwanini niogope kuwaambia kwa shinikio la mtu kama Makabrasha, mimi simuogopi yoyote inapohusu sheria, na nikiwa nimesimamia kweli ukweli na haki, mimi nina wanasheria wangu, wangelifanyia hilo kazi...’nikasema.
‘Sawa, lakini kama kuna lolote unalifahamu, tueleze, na ukimuona huyo kijana mwambie aje kituoni, asije akasubiri tukatumia nguvu, kwani hata kama atajificha wapi sisi tutampata tu....na kama kuna lolote wewe unahisi litatusaidia kuimaliza hiyo kesi kama raia mwema, tunakuhitajia ushirikiane wako,...’akasema akiondoka.
‘Nikimuona nitamshauri hivyo afande....’nikasema
************
Nilipomaliza kuongea na mkuu wa upelelezi, niliondoka hadi hospitalini , na nilimkuta mume wangu akiwa kwenye mapumziko baada ya mazoezi, alionekana kuchoka kidogo, sikutaka kuongea naye sana, kwani alitakiwa kupumzika, ila yeye akaanza kuongea;
‘Mdogo wangu yupo wapi, ,mbona haji kuniona....?’ akauliza
‘Nafikiri kazi zimekuwa nyingi, nitamwambia nikimuona’nikasema
‘Nasikia kuwa polisi wanamtafuta, kwani ana kosa gani?’ akaniuliza
‘Kwakweli mimi sijui,...na inaonekana una vyanzo vingi vya habari, kwanini unajihanganisha na wewe hustahili kufanya hivyo, unatakiwa kujali afya yako kwanza’nikasema
‘Mimi nazungumza kuhusu mdogo wangu...’akasema kwa ukali, na mimi nikakaa kimiya nikimsikiliza.
‘Mke wangu nilishakuambia kuwa mdogo wangu ni mtu muhimu sana kwangu,sitafurahia kama ananyanyaswa, au kusingiziwa mambo ambayo hajafanya,nilikuambia kuwa umlinde , sasa wewe unasema hujui lolote..mbona mimi nimefahamu kuwa polisi wanamtafuta’akasema
‘Yule sio mtoto mdogo anafahamu ni nini anachokifanya, ...na kutafutwa na polisi ni jambo la kawaida, kama hana hatia unafikiri watamfanya nini, au unafahamu lolote kuhusu yeye, kuwa huenda ana jambo kalifanya?’ nikamuuliza.
‘Hajafanya kitu bwana....kama kuna tatizo lolote waje waniulize mimi..’akasema kwa kujiamini
‘Wakuulize wewe kuhusu nini?’ nikamuuliza
‘Kama wanahisi kafanya kosa, waje waniulize mimi, kwasababu yule ni mdogo wangu...’akasema
‘Ina maana akifanya kosa lolote huko alipo, waje wakuulize wewe kwani yule ni mtoto mdogo, yeye umri wake, uanastahili kushitakiwa, na hata kuhukumiwa, kama kafanya kosa, ...’nikasema.
‘Mke wangu mimi nimeshakuhisi kuwa una jambo dhidi ya mdogo wangu, nimeshakushitukia unamtafuta nimi mdogo wangu, kama kuna lolote dhidi yangu pambana na mimi, usimshinikize mdogo wangu kwenye mambo yanayonihusu mimi, nikuambia ukweli, kama kuna lolote unalifahamu ambalo linamfanya mdogo wangu ashindwe kuja kuniona, naomba unifahamishe, ...maana kama nikifahamu kuna jambo baya dhidi yake, ambalo wewe unalifahamu, ukanificha, mke wanguhatutaelewana...’akasema akiniangalia na kwa kujiamini sana.
‘Mimi sijui lolote, kama ningelifahamu hilo, ningelishakuambia, ukumbuke yeye alikuwa kama mtoto wangu, mdogo wangu wa damu, nimemuhangaikia hadi hapo alipofika, sasa kwanini nishindwe kumfuatilia hilo....labda kama kafanya makosa, na kaamua kuyakimbia, mimi siwezi kujua...’nikasema.
‘Huwezi kujua..hahaha huwezi kujua lakini mengine unafuatilia na kujua…hilo kwa vile sio damu yako, unalipuuza, kama kweli angelikuwa ni mdogo wako ungelifanya hivyo, upuuzie hivyo.....!?’ akaniuliza kwa mshangao.
‘Nikuulize kitu ili tusaidiane kwa hilo, je yeye kwa mara ya mwisho kuonana naye, ilikuwa lini, alifika lini kukuona kwa mara ya mwisho..na mliongea nini, au ulimuagiza nini..?’ nikamuuliza na yeye akatulia kidogo, na baadaye akasema;
‘Kuna vitu nilimtuma, akasema kabati halifunguki, na akasema huenda wewe umebadili kitasa, na akaniambia mambo yamekuwa mabaya, hawezi tena kuendelea na mimi, ...sikumuelewa, na hatukupata muda wa kuongea naye kwa undani maana nilikuwa kwenye ratiba maalumu, ambayo haikutakiwa kusubiria...’akasema
‘Ulimtuma nini, kwanini hukuniambia mimi, au kumtuma kwangu ili niweze kukupatia hivyo vitu ..kuna siri gani kati yako na mdogo wako?’ nikamuuliza
‘Hicho nilichomtuma ni mambo yangu mimi na yeye, kuna mambo mengine yanahusu maswala yangu, mimi na yeye, sikutaka kukusumbua, kama ningelikuhitajia wewe, ningelikuambia tu, kwanini niogope kukuambia eeh…’akasema
‘Bado hujanirizisha kwa jibu lako…’nikasema
‘Sikiliza mke wangu, unajua mimi mume wako nimebadilika, wewe hulioni hilo,…matatizo haya yamenibadili, mimi sio yule mume wako wa wa…ok, ngoja nikirudi nyumbani tutaongea hapa sio mahali salama kwa mazungumzo hayo, unanielewa mke wangu…’akasema
‘Nona kweli umebadilika, …na kubadilika huko ujiandae vyema, maana kunaweza kukubadili kweli…’nikasema
‘Mke wangu niamini…nataka tuwe mke na mume kweli…na mimi niwajibike kama mume, hivi hutaki kunisaidia kwa hilo,..na na… kuna mambo mengi nahitajia kuyaweka sawa, ili nitimize dhamira yangu hiyo...na kwa hilo ni lazima tuwe na makubaliano,ya kimsingi, bila hivyo mambo hayatakwenda vyema, na sioni kwanini, ufunge kabati langu, ...’akasema kama analalamika.
‘Nilifunga hilo kabati,kwasababu kuna vitu vilipotea, na hatujajua ni nani alivichukua, wewe ulisema hujavichukua, kwahiyo nikaona ili kulinda usalama wa vitu vyetu, ni muhimu kubadili kila kitu. Nitakupa ufungua wa kabati lako, ukitoka,kwa hivi sasa ninao, hili ni kwa usalama wa vitu vyote mle ndani...’nikasema
‘Kuna vitu nahitajika kuvichukua mara kwa mara, hata nikiwemo humu.., na mara nyingi ndio namtuma mdogo wangu, huoni itakuwa vigumu kuvipata, na utafanya nifanye majukumu yangu kwa shida,…nielewe hapo, ni kwa masilahi ta familia, unanielewa mke wangu?’ akaniuliza
‘Ukihitajia vitu vyako, niambie mimi, au mtume mdogo wako kwangu mimi, na kwa vile mimi nipo nitampatia, au mimi sio mke wako, huniamini, unamuamini mdogo wako zaidi yangu, huoni hilo ni kosa...’nikasema.
‘Mhh, haya,....nikitoka hapa tutayaweka sawa,....mimi ni mume wako, nahitajia kujua kila kitu, na ilitakiwa mimi ndiye nifanya hivyo, lakini naona wewe umejiamulia wewe mwenyewe tu, ...nikitoka hapa ni lazima niweke haya mambo sawa, itakuwa sio vyema kila mtu anafanya anavyotaka...’akasema
‘Hamna shida ukitoka tutayamaliza, na usiseme ‘sio kila mtu..’, aliyefanya hivyo ni mke wako, na nimefanya hivyo kwa nia njema, na nitashukuru sana ukirudi nyumbani...maana sasa hivi kila kitu kipo sawa, usijali ...’nikasema na yeye akaniangalia, na kusema;
‘Mke wangu, nikuulize tena hili swali, ni nini mliongea na mdogo wangu ambacho kimefanya awe hivyo, alipofika siku ile alikuwa hana amani,…namfahamu sana, kuna kitu kimemtokea, mpaka akakimbia…na ni wewe unayeweza kumfanya awe hivyo…?’ akaniuliza
‘Ina maana kakimbia?’ nikamuuliza kwa mshangao
‘Sio kawaida yake, nahisi kuna kitu,....kama unahusika na jambo baya, au ….kuna kitu anajishuku, au..hata sielewi,…..ni bora uniambie mapema, sitaweza kuvumilia, kama kweli unahusika na hilo..’akasema
‘Mimi sijakuelewa, ...mume wangu, hebu kwanza nikuulize, uniambie kwa uhakika wako, je umeshapona na kuweza kukumbuka yote yaliyotokea nyuma, maana docta kaniambia sasa hivi umeshaanza kujijua na kukumbuka mambo yaliyopita,..je ni kweli?’ nikamuuliza.
‘Usikwepe swali...nimekuuliza kuhusu mdogo wangu...’akasema
‘Ndio maana nataka niwe na uhakika na hilo kabla sijakujibu swali lako..na kabla sijakuambia lolote, maana kuna mengi ya kuongea,…lakini siwezi kukiuka mkataba wetu,..sasa niambie ukweli je umeshapona, kiukweli, isije ikatokea jambo ukaja kunilaumu….’nikasema
‘Nimeshapona….unataka kuniuliza swali gani…’akasema
‘Una uhakika umeshapona, docta kaniambia umepona, lakini nataka uhakika wako, usije kujifany aumepona ukaharibikiwa tena, ukafanya mambo ya ajabu tena…una uhakika umepona…?’ nikauliza.
‘Swali gani unataka kuniuliza, nikujibu?’ akauliza, kwanza akajibaragua kama anatabasamu, ile ya kuonyesha ananijali.
‘Unakumbuka siku alipouwawa Makabrasha..?’ nikamuuliza hapo akashtuka, na akageuka kuangalia nje, halafu akasema
‘Mhh…kwanini unaiuliza hivyo…?’ akaniuliza bila kuniangalia
‘Nakuuliza hivyo ili kupima kama kweli umepona au la…’nikasema
‘Ehee…yah, nakumbuka, ..ilikuwa tarehe eeh…mmh, sina uhakika na tarehe, ila nakumbuka tu hivyo…’akasema
‘Je siku ile uliwahi kufika kwake, ukaongea naye, na ukiwa humo ndio akapigwa risasi..?’ nikamuuliza
‘Wewe…ni-ni-ni nani kakuambia hayo....?’ akauliza akionyesha mshituko fulani, nikamkagua kuhakikisha kama yupo sawa.
‘Nimekuuliza swali nikiwa na maana, je ulikuwepo au hukuwepo, ndio au hapana, sitaki maelezo, nisije nikakuchosha?’ nikamuuliza
‘Hapana, sikuwepo mimi nilikuwa naumwa, .’akasema sasa akijituliza.
‘Hapo sasa inaonyesha umepona, unakumbuka, kama unafahamu kuwa siku hiyo ulikuwa unaumwa, ndio maana hukuweza kwenda huko, basi inaonyesha unakumbuka vyema, ...’ nikasema na hapo akainua uso kuniangalia.
‘Kuna nini mke wangu kimetokea…?’ akaniuliza
‘Ni bora ukumbuke vyema, maana watu wanaweza kukudhania kuwa ulikuwa unajifanya unaumwa, kutokana na kuonekana sehemu mbali mbali, wakati ulitakiwa uwe hospitalini, ..’nikasema na yeye akabakia kimiya, na baadaye akasema;
‘Mke wangu sikiliza nikuambia kitu,..na hili ni muhimu sana kwako, hayo maswala ya mauaji ya Makabrasha yaache kama yalivyo, mimi nimeshaongea na wakili, anayashughulikia, usijitumbukize kwenye maswala yasiyokuhusu, utajitakia matatizo ambayo sipendi wewe uyapate, wewe ni mke wangu, ninajali sana usalama wako, hayo mambo mengine uwaachie wanaume...’akasema kwa kujiamini
‘Una uhakika na hilo, kuwa hukumbuki kilichotokea, ....maana kama ulionekana huko, ujue polisi wanasubiri upone wakuulize hilo swali, ni bora ukaniambia ukweli ili nijue jinsi gani ya kuwasaidia,...’nikasema.
‘Mimi sikumbuki bwana, hayo sijui umeyapata wapi, ina mana ndilo lililomfanya mdogo wangu akimbie, kama ni hilo, umemshinikiza mdogo wangu mpaka akakuambia mambo ambayo hutakiwi kuyafahamu, utaniweka mahali ambapo sitakuelewa, ....’akasema kwa hasira.
‘Utanielewa tu , siku ikifika, maana sio mimi tu ninayehitajia huo ukweli, hata mkuu wa upelelezi anahitajia huo ukweli, hata watoto wa Makabrasha wanahitajia huo ukweli, na hata huyo docta anayekuhudumia hapa atapenda kujua ukweli, kuwa kweli muda wote huo ulikuwa unaumwa au ulikuwa na mambo yako, isije ikawa ulipona, ukawa unasingizia, ili kufanikisha mambo yako...’nikasema
‘Unasema nini,.! yaani wewe umdiriki kusema hivyo mke wangu kuwa mimi siumwi, hivi wewe mwanamke una ubinadamu kweli, siwezi kuamini haya...’akasema kwa sauti ya unyonge.
‘Kuumwa ulikuwa unaumwa kweli, lakini matendo yako yananitia mashaka, nahisi kuna muda ulikuwa umepona, ukaamua kutumia kama ulivyoshawishika…, ili kuweza kukamilisha mambo yako, sasa mimi sijui, ...’nikasema
‘Siamini masikio yangu…’akasema
‘Naongelea uhalisia….kama ulipona lini mimi sijui…, je ulipona baada ya Makabrasha kuuwawa, au kabla ya hapo, ....hilo litakuwa juu yako na docta anayekuhudumia, cha muhimu ni ukweli...nausubiria sana huo ukweli, siku utapoona umepona kweli, uwe tayari kuelezea hayo na kila kitu....na wote wanaohusika, na tukimalizana, huenda Inspekta naye atakuwa akikusubiria ......’nikasema
‘Inspecta!!!...wa nini…huyo mzee atulie ..ndiye kaanza tena, hajakoma ubishi eeh, wewe ubiria, kasema nini huyo mzee…?’ akauliza
‘Anatimiza wajibu wake…’nikasema
‘Wewe mwanamke, usijifanye upo juu...nakuonya kwa hilo, usijiingize kwenye matatizo, unakumbuka mkataba wetu unasema nini, mume ndiye nani...’akataka kuongea na mimi nikasema.
‘Huo ulikuwa mkataba wako sio na marehemu sio.., ...ongea kuhusu mkataba wetu, je mkataba wetu unasema nini, hilo ndilo la muhimu, ama kuhusu maswala ya mkataba usiwe na shaka nayo, mimi ninachokihitajia ni afya yako, ...ukipona mambo ya mkataba yatajielezea yenyewe, utahukumu haki kwa haki, au sio, si ndio unautegemea huo..’nikasema
‘Sio mimi, ni wewe uliyeutengeneza au sio…’akasema
‘Halafu nimesahau jambo....’nikasema na yeye akaniangalia kwa mashaka sasa, ...nikamsogelea kama kumnong’oneza;
‘Eksi, wako, mpenzi wako yule wa kujifunzia, si unamkumbuka…enzi kabla hatujaona…na yeye kakimbilia kwao...nahisi kafahamu kuwa mliyoyafanya yameshagundulikana...sasa sijui, huenda wapo na mdogo wako huko, au ndio mumepanga iwe hivyo, mimi sijui, na docta....’nikakatiza maana mlango ulifunguliwa
*************
Mlango ulipofunguliwa…mume wangu bado alikuwa kashikwa na butwaa, mdomo unamcheza cheza akitaka kuongea jambo…uso ukajenga chuki…lakini alipomuona docta akatabasamu kidogo, akakunjua uso, uliokwisha kuanza kuharibika kwa chuki fulani,...halafu akasema;
‘Mke wangu hayo hatujamaliza, ngoja nirudi nyumbani tutapambana huko huko, ....siogopi lolote, ...nafikiri ulikuwa hujanitambua,mimi sio yule mume wako wa zamani , mume bwege, nimeshajitambua, nikuambie ukweli, mimi siogopi polisi au yoyote yule, hilo nimeshajipanga vyema tu....’akasema na docta akawa keshaingia,
Docta akawa anamuangalia mume wangu kwa uso wa kujiuliza aliona jinsi mume wangu alivyobadilika usoni...
‘Karibu sana docta, nimeshapona unaonaeeh, naongea na mke wangu....’akasema akijibaragua kwangu;
‘Hajapona huyu anajifanyiza tu kupona…’nikasema na yeye akageuka kuniangalia, na mimi sikumjali, na docta akasema
‘Leo tutalithibitisha hilo..maana hata polisi wananisumbua, wanataka kuongea nay eye..’akasema docta
‘Polisi..!!’akasema hivyo docta
`Bado mmoja...’ nikasema kwa sauti iliyowafanya wote waniangalie.
Nb Je ni kweli kuwa mume wa huyo mdada alikuwa akisingizia kuumwa, je ni kweli anahusika na hayo yote, na swali kubwa hadi sasa, ni nani aliyemuua Makabrasha, ...?
WAZO LA LEO: Maisha ya ndoa sio kuonyeshana ubabe, kuwa ni nani zaidi, maisha ya ndoa ni makubaliano , yenye lengo jema, la kila mtu kufahamu nafasi yake na wajibu wake, kwani wanandoa ni kitu kimoja, ili mfanikiwe kwenye safari yenu ya upendo na furaha, ni vyema kila mmoja akajiona ni muhusika mkuu, kwa nafasi yake. Kila mmoja amjali mwenzake,amuonee huruma, na hekima, busara na upendo viwe ndivyo dira ya kila mmojawapo.
‘Bado mmoja ..’
Kiukweli ushahidi niliokuwa nao ulikuwa unatosha kabisa, kufanya lolote, lakini kuna baadhi ya mambo nilihitajika kuyafuatilia, ili kuhakiki, na sikutaka kutumia nguvu, sana, ni hekima ndogo tu....
Tuendelee na kisa chetu.
*********
Docta alisafiri kwenda kijijini kuonana na mke wake!
Wakati nipo nyumbani nikijiandaa kwenda kumtembelea mume wangu hospitalini, mara nikasikia kuwa nina mgeni, nilipouliza ni nani wakasema ni Inspekta wa polisi, nikajua kuwa sasa mambo yameanza kuvuja, sikutaka mambo haya yaharakishe sana kabla sijamalizana na uchunguzi wangu.
Ukisikia polisi kaja kwako hata kama huna kosa utakuwa na wasiwasi tu…
Nikatoka nje kwa kupitia mlango wa nyuma, hadi bustanini, nikaagiza huyo mgeni aletwe huko , kwani likuwa kakaribishwa chumba cha maongezi, sikutaka niongee naye ndani, nilitaka sehemu huru ambayo kila mtu anaweza kuona.
Mkuu huyo akaja huko bustanini, akiwa kashikilia mkoba wake, kuonyesha yupo kazini. Alikuwa mtu wa makamo, na hali yake kiafya ilionyesha sio haba, kitambi kidogo, japokuwa ukakamavu wa kiaskari bado ulikuwa kwenye damu, akasogea hadi pale nilipokuwa nimesimama, na mimi nikamsogelea na kunyosha mkono kusalimiana.
‘Samahani kwa ujio huu wa ghafla, unafahamu kazi zetu tena, pale unapopata taarifa unatakiwa uifuatilie kwa haraka , maana tuna kazi nyingi sana za kufanya,…kwa hili sikupenda kuwatuma vijana wangu, namuheshimu sana baba yako,...’akaaza kujieleza.
‘Nashukuru kwa hilo pia nashkuru kwa kunitembelea japokuwa nilikuwa na ratiba zangu nyingine kiukweli,..,kwani sasa hivi natakiwa kwenda kumuona mgonjwa...huko alipolazwa..’nikasema
‘Oh, kwani mume wako anaendeleaje?’ akauliza
‘Hajambo kidogo, unajua matatizo yake sio yale ya kusema kapona, anahitajia muda wa kuchunguzwa, itokee hiyo hali ndio unaweza kufanya jambo, lakini hajambo, sasa hivi yupo kwenye mazoezi tu ya kawaida...’nikasema
‘Kwahiyo kumbe tunaweza kumtembelea na kuongea naye?’ akauliza
‘Mhh, hayo anayeweza kuyajibu ni dakitari wake,…kwani kuna jambo mnahitaji kuongea naye,?’ nikamuuliza
‘Ni maswali ya kawaida tu....lakini kama bado hali yake haijawa sawa hakuna haraka sana, ....’akasema
‘Haya niambie ujio wako kwangu una makusudio gani na mimi, maana nyie watu hamji kwa mtu bila lengo maalumu, na mkionekana kwa mtu ujue kuna jambo...’nikasema.
‘Ni kweli, nimekuja kwa lengo maalum, lakini sio kwa ubaya,....’akasema na kutoa makabrasha yake, halafu akasema;
‘Katika uchunguzi wetu, tumegundua kuwa yule kijana mdogo wa mume wako alikuwepo siku ile Makabrasha alipouwawa, na alionekana akiranda randa eneo la lile jengo, na baadaye akaondoka na mtu siyefahamika, ..’akatulia
‘Sasa tulitaka kuongea naye, lakini hayupo, na watu wangu wamejaribu kumtafuta bila mafanikio, hata kazini kwake hawajui huyo mdogo wake mume wako kaenda wapi, je unafahamu huyu kijana wenu kaenda wapi, maana ni muhimu sana..?’ akaniuliza
‘Kwakweli hata mimi sijui kaenda wapi, na nilishamwambia kuwa asiondoke bila ya kuwasiliana na mimi…’nikasema na yeye akaniangalia kwa mashaka.
‘Haiwezekani, ina maana hata nyie, hata …mke wake naye hayupo…sasa inatupa mashaka kidogo, ....Je hata mume wako hafahamu wapi kijana wenu alipokwenda...? ‘ akauliza
‘Hafahamu kabisa, maana jana nilipofika kumuona mgonjwa, yeye mwenyewe ndiye aliniulizia kama nimewahi kuonana na mdogo wake, kwani anaona ajabu siku mbili kupita bila mdogo wake kufika kumuona,.... sio kawaida yake..’akasema
‘Ina maana katoroka basi…, au kuna kitu kimemtokea, maana msije mkakaa kimiya kumbe yupo kwenye matatizo?’ akaniuliza
‘Kwanini atoroke, hilo la kutoroka halipo…na sizani kama yupo kwenye matatizo, huenda ni katika kuhangaika na mishe mishe za kutafuta riziki…huenda kuna jambo alilifuatilia, akakwama mahali, na hataki kusema wapi alipo, unafahamu tena vijana...lakini kauli yako hiyo ya kusema katoroka, ina nitia mashaka, kwanini unasema hivyo?’ nikamuuliza
‘Sisi katokana na uchunguzi wetu, tuna mambo tulitaka kumuuliza, tunahisi kuna mambo anayafahamu, unajua bado tunafuatilia ile kesi ya mauaji ya Makabrasha.....’akasema
‘Kwahiyo mnamshuku kwa msingi gani, kuwa anafahamu muuaji, au yeye kashiriki, au ni kutaka kufahamu mambo ambayo huenda yatawasaidia kumpata huyo muuaji?’ nikamuuliza.
‘Tunahisi yeye anaweza kutusaidia, ....kumpata huyo muuaji, ‘akasema.
‘Mhh, kama angelikuwa anafahamu hilo, angelisema, maana ukumbuke Makabrasha alikuwa ndiye wakili wao, na alikuwa hajafanikisha malengo yao, wasingeliweza kukaa kimiya kama wanamfahamu huyo muuaji...’ nikasema
‘Kiukweli Mkabrasha alikuwa haaminiki, inawezekana, huyo kijana anamfahamu huyo muaaji, lakini hana uhakika kuwa kweli huyo jamaa kafanya hivyo, akiogopa kujiingiza kwenye matatizi ya ushahidi.., au pia inawezekana alishirikiana na huyo muaaji, ,....’akasema.
‘Hilo la kushirikiana na huyo muuaji, nalipinga, kama nilivyokuambia, Makabrasha alikuwa ni kama ndugu yao, pili alikuwa ni wakili wao .....’nikasema.
‘Yote yawezekana, ndio maana nilitaka niongee naye mimi mwenyewe uso kwa uso, na sisi ni wataalamu wa mambo hayo, nikiongea naye tu, ninaweza kuhakiki hayo ninayotaka kuyafahamu, kama hahusiki hatutamlazimisha,...’akasema
‘Nakumbuka mara ya kwanza ulisema aliyefanya hivyo, atakuwa mtu wa ndani, anaweza akawa mfanyakazi wa mule mule,..akishirikiana na watu wa nje, ina maana mnahisi kuwa huyo aliyekuwa nje ni huyo kijana?’ nikamuuliza.
‘Ni moja ya mambo ambayo tunayafuatilia, kuhakiki, ndio maana tunataka kumuhoji yeye binafsi,…kuna ushahidi huo kuwa huenda ni yeye aliyekuwa nje,...lakini kama ulivyosema , ni kwanini wamuue mtu kama huyo,..hata sisi tunashindwa kuunganisha huo ukweli, mpaka tumuone, ila tunahisi huyo kijana atakuwa anahusika, kwa namna moja au nyingine,...sasa kinachotufanya tuzidi kumweka kwenye kundi la wahusika, ni huko kutoweke kwake kwa ghafla...’akasema
‘Mimi sijui kama kweli katoweka , hiyo kauli bado sijakubaliana nayo, kwani sio mara ya kwanza kufanya hivyo, nilishawahi kumkanya kuhusu hiyo tabia yake ya kuondoka bila kuaga, na kukaa kimiya,....’nikasema.
‘Kwahiyo hiyo sio mara ya kwanza kuondoka ghafla hivyo…?’ akauliza
‘Sio mara ya kwanza, ..ni tabia yake, na mwenyewe hujitetea akisema kazi zake zinamfanya awe hivyo, anaweza kuitwa mahali, akajikuta hana mawasiliano, au hataki kufahamika yupo wapi, kwasababu ya ushindani wa kibiashara..ndivyo anavyojietetea....’nikasema.
‘Hiyo sio kawaida kabisa, kama ni hivyo kwanini kazini kwake wasifahamu wapi alipo…ina maana kuondoka huko ni kwa kibinafsi, au sio…?’akauliza
‘Ndivyo anavyofanya hivyo, ....sio jambo geni kwetu...akirudi nitamfahamisha kuwa nyie mnamtafuta....’nikasema
‘Ni bora ufanye hivyo, kwasababu wanafamilia wa Makabrasha wanataka hiyo kesi ikamilike haraka iwezekanavyo…, na wanadai kuwa kuna njama za kuficha ukweli, na wameshapeleka malalamiko yao ngazi za juu...’akasema
‘Ni nani kafanya hivyo?’ nikauliza
‘Ni mwafamilia wao mmoja ambaye ni mwanasheria, ni mmoja wa watoto wake, acha yule mkubwa, yule mkubwa tuliongea naye tukamalizana, lakini kuna huyo mwanasheria, ni mkorofi kidogo…,anajifanya anafahamu sana sheria,....’akasema
‘Kazi ipo…kam ni huyo eeh,…haya hilo ni jukumu lenu,..na , kwahiyo mkaamua kuanza tena upelelezi au sio kutokana na shinikizo hilo.....?’nikamuuliza
‘Sio kuanza upelelezi, mbona upelelezi ulikuwa unaendelea, japokuwa sio ule wa haraka haraka, maana tulifika mahali tukasema muuaji ni mmoja wa maadui za marehemu, lakini sio kwamba tulishafunga jalada lake,..hapana,bado tunachunguza....’akasema.
‘Mimi niwatakie kila-laheri, maana mauaji hayo, yalinitia doa, kwahiyo akipatikana huyo muuaji, hata mimi nitakuwa katika wakati mzuri hata ikibidi kuwashitaki nyie polisi kwa kunisingizia mambo nisiyohusika nayo...’nikasema.
‘Huwezi kutushitaki, sisi ni moja ya kazi zetu...’akasema akijiandaa kuondoka.
‘Haya nashukuru kwa hilo, nitafanya kama ulivyoniomba, na inaonekana huyo muaaji ni mjanja sana, kafanya mauaji na imeshindikana kumfahamu ni nani, isije ikawa ni mmoja wa watu wenu...’nikasema
‘Hiyo haipo, sio watu wangu...ni tetesi za mitaani tu, hilo nakuhakikishia, ni mmoja wa maadui za marehemu, na tutampata tu....ni swala la muda...’akasema.
‘Lakini nahisi sasa hivi mnafanya hivyo kwa shinikizo la wanafamilia, nyie mlishakata tamaa..’nikasema.
‘Hapana hatukuwa tumekata tamaa, ila ushirikiana wa wananchi umekuwa mdogo, ni kama vile watu walitaka mtu huyo afe tu. Sisi bado tupo kazini, tutapambana na hawo watu,na kama kuna watu wanafahamu muuaji watuambie, sisi hatuwezi kuwashika watu kama hakuna ushahidi…’akasema
‘Nakuelewa afande..’nikasema
‘Tuliwaambia hao wanafamilia, kama kuna watu wanaowahisi watufahamishe,...maana mzazi wao, alikuwa kajijengea maisha ya kuwa na maadui wengi, hata ndani ya familia yake mwenyewe, hata marafiki zake, sasa ni nani unaweza kumhisi, hiyo sio kazi rahisi....’akasema
‘Lakini ni moja ya kazi zenu, msikwepe majukumu...’nikasema
‘Hilo silikatai, lakini ili tufanikiwe, tunahitajia ushirikiane wenu,...na nilikuwa nataka kukuuliza swali…kuna tetesi kuwa kuna vitu viliibiwa kwako, na sasa umevipata ni kweli au si kweli?’ akaniuliza
‘Vitu gani hivyo…?’ nikamuuliza.
‘Nimesikia kuwa kuna mikataba yako ilipotea, ..na umeshaipata, je ni nani aliichukua?’ akaniuliza
‘Mimi sijafika kwenu kulalamika kuhusu kuibiwa,..ila nilisema kuna vitu vyangu havionekani, … je ulishawahi kuniona kuja kwako kulalamika kuhusu kuibiwa?’ nikamuuliza
‘Hujashitakia hilo...lakini unaweza ukaacha kutokana na shinikizo, na tunahisi uliogopa, kufanya hivyo kwa sababu ya ujanja wa Makabrasha,..na ndio maana kipindi kile tulikushikilia, tukijua huenda uliamua kumuondoa kwa tabia yake hiyo..’akasema
‘Hapana sio hivyo…’nikasema
‘Kuna tetesi hizo…,hebu niambie ukweli, maana huenda ikatusaidia katika uchunguzi wetu..’akasema
‘Mkuu mimi sina cha kukuambia,...kama ningelikuwa na tatizo hilo ningelishawaambia, na kwanini niogope kuwaambia kwa shinikio la mtu kama Makabrasha, mimi simuogopi yoyote inapohusu sheria, na nikiwa nimesimamia kweli ukweli na haki, mimi nina wanasheria wangu, wangelifanyia hilo kazi...’nikasema.
‘Sawa, lakini kama kuna lolote unalifahamu, tueleze, na ukimuona huyo kijana mwambie aje kituoni, asije akasubiri tukatumia nguvu, kwani hata kama atajificha wapi sisi tutampata tu....na kama kuna lolote wewe unahisi litatusaidia kuimaliza hiyo kesi kama raia mwema, tunakuhitajia ushirikiane wako,...’akasema akiondoka.
‘Nikimuona nitamshauri hivyo afande....’nikasema
************
Nilipomaliza kuongea na mkuu wa upelelezi, niliondoka hadi hospitalini , na nilimkuta mume wangu akiwa kwenye mapumziko baada ya mazoezi, alionekana kuchoka kidogo, sikutaka kuongea naye sana, kwani alitakiwa kupumzika, ila yeye akaanza kuongea;
‘Mdogo wangu yupo wapi, ,mbona haji kuniona....?’ akauliza
‘Nafikiri kazi zimekuwa nyingi, nitamwambia nikimuona’nikasema
‘Nasikia kuwa polisi wanamtafuta, kwani ana kosa gani?’ akaniuliza
‘Kwakweli mimi sijui,...na inaonekana una vyanzo vingi vya habari, kwanini unajihanganisha na wewe hustahili kufanya hivyo, unatakiwa kujali afya yako kwanza’nikasema
‘Mimi nazungumza kuhusu mdogo wangu...’akasema kwa ukali, na mimi nikakaa kimiya nikimsikiliza.
‘Mke wangu nilishakuambia kuwa mdogo wangu ni mtu muhimu sana kwangu,sitafurahia kama ananyanyaswa, au kusingiziwa mambo ambayo hajafanya,nilikuambia kuwa umlinde , sasa wewe unasema hujui lolote..mbona mimi nimefahamu kuwa polisi wanamtafuta’akasema
‘Yule sio mtoto mdogo anafahamu ni nini anachokifanya, ...na kutafutwa na polisi ni jambo la kawaida, kama hana hatia unafikiri watamfanya nini, au unafahamu lolote kuhusu yeye, kuwa huenda ana jambo kalifanya?’ nikamuuliza.
‘Hajafanya kitu bwana....kama kuna tatizo lolote waje waniulize mimi..’akasema kwa kujiamini
‘Wakuulize wewe kuhusu nini?’ nikamuuliza
‘Kama wanahisi kafanya kosa, waje waniulize mimi, kwasababu yule ni mdogo wangu...’akasema
‘Ina maana akifanya kosa lolote huko alipo, waje wakuulize wewe kwani yule ni mtoto mdogo, yeye umri wake, uanastahili kushitakiwa, na hata kuhukumiwa, kama kafanya kosa, ...’nikasema.
‘Mke wangu mimi nimeshakuhisi kuwa una jambo dhidi ya mdogo wangu, nimeshakushitukia unamtafuta nimi mdogo wangu, kama kuna lolote dhidi yangu pambana na mimi, usimshinikize mdogo wangu kwenye mambo yanayonihusu mimi, nikuambia ukweli, kama kuna lolote unalifahamu ambalo linamfanya mdogo wangu ashindwe kuja kuniona, naomba unifahamishe, ...maana kama nikifahamu kuna jambo baya dhidi yake, ambalo wewe unalifahamu, ukanificha, mke wanguhatutaelewana...’akasema akiniangalia na kwa kujiamini sana.
‘Mimi sijui lolote, kama ningelifahamu hilo, ningelishakuambia, ukumbuke yeye alikuwa kama mtoto wangu, mdogo wangu wa damu, nimemuhangaikia hadi hapo alipofika, sasa kwanini nishindwe kumfuatilia hilo....labda kama kafanya makosa, na kaamua kuyakimbia, mimi siwezi kujua...’nikasema.
‘Huwezi kujua..hahaha huwezi kujua lakini mengine unafuatilia na kujua…hilo kwa vile sio damu yako, unalipuuza, kama kweli angelikuwa ni mdogo wako ungelifanya hivyo, upuuzie hivyo.....!?’ akaniuliza kwa mshangao.
‘Nikuulize kitu ili tusaidiane kwa hilo, je yeye kwa mara ya mwisho kuonana naye, ilikuwa lini, alifika lini kukuona kwa mara ya mwisho..na mliongea nini, au ulimuagiza nini..?’ nikamuuliza na yeye akatulia kidogo, na baadaye akasema;
‘Kuna vitu nilimtuma, akasema kabati halifunguki, na akasema huenda wewe umebadili kitasa, na akaniambia mambo yamekuwa mabaya, hawezi tena kuendelea na mimi, ...sikumuelewa, na hatukupata muda wa kuongea naye kwa undani maana nilikuwa kwenye ratiba maalumu, ambayo haikutakiwa kusubiria...’akasema
‘Ulimtuma nini, kwanini hukuniambia mimi, au kumtuma kwangu ili niweze kukupatia hivyo vitu ..kuna siri gani kati yako na mdogo wako?’ nikamuuliza
‘Hicho nilichomtuma ni mambo yangu mimi na yeye, kuna mambo mengine yanahusu maswala yangu, mimi na yeye, sikutaka kukusumbua, kama ningelikuhitajia wewe, ningelikuambia tu, kwanini niogope kukuambia eeh…’akasema
‘Bado hujanirizisha kwa jibu lako…’nikasema
‘Sikiliza mke wangu, unajua mimi mume wako nimebadilika, wewe hulioni hilo,…matatizo haya yamenibadili, mimi sio yule mume wako wa wa…ok, ngoja nikirudi nyumbani tutaongea hapa sio mahali salama kwa mazungumzo hayo, unanielewa mke wangu…’akasema
‘Nona kweli umebadilika, …na kubadilika huko ujiandae vyema, maana kunaweza kukubadili kweli…’nikasema
‘Mke wangu niamini…nataka tuwe mke na mume kweli…na mimi niwajibike kama mume, hivi hutaki kunisaidia kwa hilo,..na na… kuna mambo mengi nahitajia kuyaweka sawa, ili nitimize dhamira yangu hiyo...na kwa hilo ni lazima tuwe na makubaliano,ya kimsingi, bila hivyo mambo hayatakwenda vyema, na sioni kwanini, ufunge kabati langu, ...’akasema kama analalamika.
‘Nilifunga hilo kabati,kwasababu kuna vitu vilipotea, na hatujajua ni nani alivichukua, wewe ulisema hujavichukua, kwahiyo nikaona ili kulinda usalama wa vitu vyetu, ni muhimu kubadili kila kitu. Nitakupa ufungua wa kabati lako, ukitoka,kwa hivi sasa ninao, hili ni kwa usalama wa vitu vyote mle ndani...’nikasema
‘Kuna vitu nahitajika kuvichukua mara kwa mara, hata nikiwemo humu.., na mara nyingi ndio namtuma mdogo wangu, huoni itakuwa vigumu kuvipata, na utafanya nifanye majukumu yangu kwa shida,…nielewe hapo, ni kwa masilahi ta familia, unanielewa mke wangu?’ akaniuliza
‘Ukihitajia vitu vyako, niambie mimi, au mtume mdogo wako kwangu mimi, na kwa vile mimi nipo nitampatia, au mimi sio mke wako, huniamini, unamuamini mdogo wako zaidi yangu, huoni hilo ni kosa...’nikasema.
‘Mhh, haya,....nikitoka hapa tutayaweka sawa,....mimi ni mume wako, nahitajia kujua kila kitu, na ilitakiwa mimi ndiye nifanya hivyo, lakini naona wewe umejiamulia wewe mwenyewe tu, ...nikitoka hapa ni lazima niweke haya mambo sawa, itakuwa sio vyema kila mtu anafanya anavyotaka...’akasema
‘Hamna shida ukitoka tutayamaliza, na usiseme ‘sio kila mtu..’, aliyefanya hivyo ni mke wako, na nimefanya hivyo kwa nia njema, na nitashukuru sana ukirudi nyumbani...maana sasa hivi kila kitu kipo sawa, usijali ...’nikasema na yeye akaniangalia, na kusema;
‘Mke wangu, nikuulize tena hili swali, ni nini mliongea na mdogo wangu ambacho kimefanya awe hivyo, alipofika siku ile alikuwa hana amani,…namfahamu sana, kuna kitu kimemtokea, mpaka akakimbia…na ni wewe unayeweza kumfanya awe hivyo…?’ akaniuliza
‘Ina maana kakimbia?’ nikamuuliza kwa mshangao
‘Sio kawaida yake, nahisi kuna kitu,....kama unahusika na jambo baya, au ….kuna kitu anajishuku, au..hata sielewi,…..ni bora uniambie mapema, sitaweza kuvumilia, kama kweli unahusika na hilo..’akasema
‘Mimi sijakuelewa, ...mume wangu, hebu kwanza nikuulize, uniambie kwa uhakika wako, je umeshapona na kuweza kukumbuka yote yaliyotokea nyuma, maana docta kaniambia sasa hivi umeshaanza kujijua na kukumbuka mambo yaliyopita,..je ni kweli?’ nikamuuliza.
‘Usikwepe swali...nimekuuliza kuhusu mdogo wangu...’akasema
‘Ndio maana nataka niwe na uhakika na hilo kabla sijakujibu swali lako..na kabla sijakuambia lolote, maana kuna mengi ya kuongea,…lakini siwezi kukiuka mkataba wetu,..sasa niambie ukweli je umeshapona, kiukweli, isije ikatokea jambo ukaja kunilaumu….’nikasema
‘Nimeshapona….unataka kuniuliza swali gani…’akasema
‘Una uhakika umeshapona, docta kaniambia umepona, lakini nataka uhakika wako, usije kujifany aumepona ukaharibikiwa tena, ukafanya mambo ya ajabu tena…una uhakika umepona…?’ nikauliza.
‘Swali gani unataka kuniuliza, nikujibu?’ akauliza, kwanza akajibaragua kama anatabasamu, ile ya kuonyesha ananijali.
‘Unakumbuka siku alipouwawa Makabrasha..?’ nikamuuliza hapo akashtuka, na akageuka kuangalia nje, halafu akasema
‘Mhh…kwanini unaiuliza hivyo…?’ akaniuliza bila kuniangalia
‘Nakuuliza hivyo ili kupima kama kweli umepona au la…’nikasema
‘Ehee…yah, nakumbuka, ..ilikuwa tarehe eeh…mmh, sina uhakika na tarehe, ila nakumbuka tu hivyo…’akasema
‘Je siku ile uliwahi kufika kwake, ukaongea naye, na ukiwa humo ndio akapigwa risasi..?’ nikamuuliza
‘Wewe…ni-ni-ni nani kakuambia hayo....?’ akauliza akionyesha mshituko fulani, nikamkagua kuhakikisha kama yupo sawa.
‘Nimekuuliza swali nikiwa na maana, je ulikuwepo au hukuwepo, ndio au hapana, sitaki maelezo, nisije nikakuchosha?’ nikamuuliza
‘Hapana, sikuwepo mimi nilikuwa naumwa, .’akasema sasa akijituliza.
‘Hapo sasa inaonyesha umepona, unakumbuka, kama unafahamu kuwa siku hiyo ulikuwa unaumwa, ndio maana hukuweza kwenda huko, basi inaonyesha unakumbuka vyema, ...’ nikasema na hapo akainua uso kuniangalia.
‘Kuna nini mke wangu kimetokea…?’ akaniuliza
‘Ni bora ukumbuke vyema, maana watu wanaweza kukudhania kuwa ulikuwa unajifanya unaumwa, kutokana na kuonekana sehemu mbali mbali, wakati ulitakiwa uwe hospitalini, ..’nikasema na yeye akabakia kimiya, na baadaye akasema;
‘Mke wangu sikiliza nikuambia kitu,..na hili ni muhimu sana kwako, hayo maswala ya mauaji ya Makabrasha yaache kama yalivyo, mimi nimeshaongea na wakili, anayashughulikia, usijitumbukize kwenye maswala yasiyokuhusu, utajitakia matatizo ambayo sipendi wewe uyapate, wewe ni mke wangu, ninajali sana usalama wako, hayo mambo mengine uwaachie wanaume...’akasema kwa kujiamini
‘Una uhakika na hilo, kuwa hukumbuki kilichotokea, ....maana kama ulionekana huko, ujue polisi wanasubiri upone wakuulize hilo swali, ni bora ukaniambia ukweli ili nijue jinsi gani ya kuwasaidia,...’nikasema.
‘Mimi sikumbuki bwana, hayo sijui umeyapata wapi, ina mana ndilo lililomfanya mdogo wangu akimbie, kama ni hilo, umemshinikiza mdogo wangu mpaka akakuambia mambo ambayo hutakiwi kuyafahamu, utaniweka mahali ambapo sitakuelewa, ....’akasema kwa hasira.
‘Utanielewa tu , siku ikifika, maana sio mimi tu ninayehitajia huo ukweli, hata mkuu wa upelelezi anahitajia huo ukweli, hata watoto wa Makabrasha wanahitajia huo ukweli, na hata huyo docta anayekuhudumia hapa atapenda kujua ukweli, kuwa kweli muda wote huo ulikuwa unaumwa au ulikuwa na mambo yako, isije ikawa ulipona, ukawa unasingizia, ili kufanikisha mambo yako...’nikasema
‘Unasema nini,.! yaani wewe umdiriki kusema hivyo mke wangu kuwa mimi siumwi, hivi wewe mwanamke una ubinadamu kweli, siwezi kuamini haya...’akasema kwa sauti ya unyonge.
‘Kuumwa ulikuwa unaumwa kweli, lakini matendo yako yananitia mashaka, nahisi kuna muda ulikuwa umepona, ukaamua kutumia kama ulivyoshawishika…, ili kuweza kukamilisha mambo yako, sasa mimi sijui, ...’nikasema
‘Siamini masikio yangu…’akasema
‘Naongelea uhalisia….kama ulipona lini mimi sijui…, je ulipona baada ya Makabrasha kuuwawa, au kabla ya hapo, ....hilo litakuwa juu yako na docta anayekuhudumia, cha muhimu ni ukweli...nausubiria sana huo ukweli, siku utapoona umepona kweli, uwe tayari kuelezea hayo na kila kitu....na wote wanaohusika, na tukimalizana, huenda Inspekta naye atakuwa akikusubiria ......’nikasema
‘Inspecta!!!...wa nini…huyo mzee atulie ..ndiye kaanza tena, hajakoma ubishi eeh, wewe ubiria, kasema nini huyo mzee…?’ akauliza
‘Anatimiza wajibu wake…’nikasema
‘Wewe mwanamke, usijifanye upo juu...nakuonya kwa hilo, usijiingize kwenye matatizo, unakumbuka mkataba wetu unasema nini, mume ndiye nani...’akataka kuongea na mimi nikasema.
‘Huo ulikuwa mkataba wako sio na marehemu sio.., ...ongea kuhusu mkataba wetu, je mkataba wetu unasema nini, hilo ndilo la muhimu, ama kuhusu maswala ya mkataba usiwe na shaka nayo, mimi ninachokihitajia ni afya yako, ...ukipona mambo ya mkataba yatajielezea yenyewe, utahukumu haki kwa haki, au sio, si ndio unautegemea huo..’nikasema
‘Sio mimi, ni wewe uliyeutengeneza au sio…’akasema
‘Halafu nimesahau jambo....’nikasema na yeye akaniangalia kwa mashaka sasa, ...nikamsogelea kama kumnong’oneza;
‘Eksi, wako, mpenzi wako yule wa kujifunzia, si unamkumbuka…enzi kabla hatujaona…na yeye kakimbilia kwao...nahisi kafahamu kuwa mliyoyafanya yameshagundulikana...sasa sijui, huenda wapo na mdogo wako huko, au ndio mumepanga iwe hivyo, mimi sijui, na docta....’nikakatiza maana mlango ulifunguliwa
*************
Mlango ulipofunguliwa…mume wangu bado alikuwa kashikwa na butwaa, mdomo unamcheza cheza akitaka kuongea jambo…uso ukajenga chuki…lakini alipomuona docta akatabasamu kidogo, akakunjua uso, uliokwisha kuanza kuharibika kwa chuki fulani,...halafu akasema;
‘Mke wangu hayo hatujamaliza, ngoja nirudi nyumbani tutapambana huko huko, ....siogopi lolote, ...nafikiri ulikuwa hujanitambua,mimi sio yule mume wako wa zamani , mume bwege, nimeshajitambua, nikuambie ukweli, mimi siogopi polisi au yoyote yule, hilo nimeshajipanga vyema tu....’akasema na docta akawa keshaingia,
Docta akawa anamuangalia mume wangu kwa uso wa kujiuliza aliona jinsi mume wangu alivyobadilika usoni...
‘Karibu sana docta, nimeshapona unaonaeeh, naongea na mke wangu....’akasema akijibaragua kwangu;
‘Hajapona huyu anajifanyiza tu kupona…’nikasema na yeye akageuka kuniangalia, na mimi sikumjali, na docta akasema
‘Leo tutalithibitisha hilo..maana hata polisi wananisumbua, wanataka kuongea nay eye..’akasema docta
‘Polisi..!!’akasema hivyo docta
`Bado mmoja...’ nikasema kwa sauti iliyowafanya wote waniangalie.
Nb Je ni kweli kuwa mume wa huyo mdada alikuwa akisingizia kuumwa, je ni kweli anahusika na hayo yote, na swali kubwa hadi sasa, ni nani aliyemuua Makabrasha, ...?
WAZO LA LEO: Maisha ya ndoa sio kuonyeshana ubabe, kuwa ni nani zaidi, maisha ya ndoa ni makubaliano , yenye lengo jema, la kila mtu kufahamu nafasi yake na wajibu wake, kwani wanandoa ni kitu kimoja, ili mfanikiwe kwenye safari yenu ya upendo na furaha, ni vyema kila mmoja akajiona ni muhusika mkuu, kwa nafasi yake. Kila mmoja amjali mwenzake,amuonee huruma, na hekima, busara na upendo viwe ndivyo dira ya kila mmojawapo.