Jamani msianze kusifia wakati mnashusha guard zetu..
Kusifia hapa si kushusha guard, actually ni kupandisha guard, kupandisha guard ya fiscal responsibility, kupandisha guard ya accountability, kupandisha guard ya ethics, kupandisha guard ya fairness, kupandisha guard ya mipaka kati ya central and local governments, kupandisha guard na attention kuhusu issues zinazohitaji civil disobedience, kupandisha guard kuhusu taratibu zetu....
kuweni makini sana na swala hili laweza kuwa zito kuliko tunavyofikiria.
Ogah kauliza swali zuri sana.. Je ni utaratibu gani hufanyika wakati wa misafara ya viongozi kama hii..
Swali zuri sana, lakini regardless ya jibu, makamu wa rais (mwenye resources nyingi sana) kuji impose kwenye local governments zimlipie siyo fair, siyo fiscally responsible, siyo ethical, haionyeshi leadership.Ni kama baba tajiri anayejipeleka kwa mtoto wake asiye na uwezo na kumtaka mtoto wake amhudumie kwa malazi ya hali ya juu sana ambayo yataharibu bajeti ya mwanae ambayo ingeweza kutumika kwa vitu vingi vinavyohitaji fedha hizi.
Kwa hiyo kama kwa kawaida fedha hizi hulipwa na ofisi ya makamu wa rais, then madiwani na mkurugenzi wamefanya vizuri kutotaka kulipa.Kama kwa kawaida gharama hizi hulipwa na serikali za mitaa/ halmashauri, then this is wrong and unfair and should be changed, and this act is good as a precedent for civil disobedience.
Tuachane na maswala ya bajeti kwa sababu Tanzania ni nchi inayoongozwa kiholela..
Kwa hiyo mkuu unatetea uholela? The way forward ni kuachana na bajeti na kuendelea kiholela? hivi ndivyo tutatoka kwenye umasikini wetu? then unategemea maendeleo kweli?
Tuna hakika Ofisi ya Makamu wa rais ina bajeti inayo cover misafara kama hii tena humegewa allowance juu kwa siku kinachotakiwa ni (receipt) supporting document ziwakilishwe wizarani...
Sasa nachoshindwa kuelewa ni utaratibu gani umetangulia kwani yawezekana Makamu wa rais amealikwa na wilaya na utaratibu unasema ukimwalika kiongozi unalipia gharama!
Wilaya ingemualika kwa kufuata utaratibu na kuwashirikisha madiwani na mkurugenzi sidhani kama wangekataa kulipia.Watanzania ni wakarimu peer to peer, sembuse kwa makamu wa rais? Kama mkuu wa wilaya kamkaribisha makamu wa rais wakati hana bajeti ya kumkirimu halafu akaingiza mkono katika mifuko ya halmashauri ku cover expenses, bila kuwashirikisha madiwani na mkurugenzi then mkurugenzi na madiwani wana haki ya kukataa gharama.
who knows utaratibu ktk nchi ya Wadanganyika..
Even the more reason ku demand accountability na transparency, na ku encourage vitendo vya mkurugenzi. katika nchi isiyo na utaratibu kama Tanzania, mtu yeyote anayeelekea kuongozwa na utaratibu kama mkurugenzi huyu ni wa kusikilizwa na kuigwa, inawezekana utaratibu haupo na kesi kama hii ndiyo ikawa precedent ya kuanzisha utaratibu.
Inawezekana kuna wakurugenzi kibao wa wilaya wamefurahi sana kwa sababu ziara hizi zinawatia gharama ila hawana courage ya kuzikataa gharama hizi.Huyu mkurugenzi kamwe si mtu wa kupuzwa.
Je, ktk maswala ya mwaliko ni nani anachukua dhamana ya matumizi?..
Hili limejibiwa hapo juu, sitegemei madiwani wote na mkurugenzi wao wakakosa uungwana kiasi cha kumuadhiri makamu wa rais waliyemualika na kuelewa kuwa watapata gharama, inaonekana wamebambikiwa gharama bila kujua.
kuna maswali mengi sana inabidi tufahamu kilichotokea na zaidi ya yote tuwe tayari kumlinda mkurugenzi huyu..
Na msimamo wa mkurugenzi unasaidia kutoa mwanga kumulika hapa kuona maswali zaidi na kupata majibu.Mkurugenzi angekubali kulipa wala tusingejua makamu wa rais anajichana vipi kwa siku, all the more reason to encourage this guy
Je, akifukuzwa kazi tutafanya nini?
Huyu mkuu anaonekana ana fiscal responsibility, akifukuzwa kazi itakuwa loss ya halmashauri na watu wanaojua principles za fiscal responsibility na concept ya "profiles in courage" hawawezi kumuacha huyu.hata hapa tunaweza kumpigia kampeni kama symbol of hope in the midst of timid and corrupt leaders.
Mkuu unanipa impression kwamba uko concerned kuhusu kibarua kuota majani na kitumbua kuingia mchanga kwa mtu mmoja kuliko maslahi ya taifa na trend nzima ya fiscal responsibility bongo. This is worrying if not disappointing.