Nsaji Mpoki
JF-Expert Member
- Nov 5, 2007
- 396
- 68
Maoni ya Celina Kombani kwenye Magazeti ya Tanzania leo kuhusu nani hasa wa kulaumiwa kwenye suala hili yanaonyesha dhahiri namna anavyokiri kwamba tunajua namna serikali yetu inavyoendeshwa. Hongera wana JF. Lakini baada ya kukiri asingeishia hapo. Kwani Katibu Mkuu Kiongozi Bw Luhanjoa hajaachia ngazi hadi leo. Huyu kwa mujibu Sheria ya utumishiwa Umma Na. 8 ya 2002 ndiye Mkuu wa Utumishi wa Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri. Na isitoshe masuala ya usalama na uendeshaji wa ofisi binafsi za viongozi wakuu wa nchi yetu yako chini yake. Haya yanatokea hataki hata kuwaomba radhi wananchi waliomchagua Rais (Makamu aligombea kwa tiketi moja na Rais wetu). Hivi leo kweli Kamati za Maadili alizounda zitamwadhibu nani ikiwa kama yeye mwenyewe na timu yake wanatenda dhambi kama hii halafu wanamlaumu DED. Kama hataadhibiwa kwa hili basi tuamini kuwa nchi yetu haiendeshwi kwa misingi ya utawala bora. Nashindwa kuelewa hivi makamu kafanyiwa hivi kwa sababu ni mkimya sana au kwa sababu ni Mzanzibari? Puuh!