Mkurugenzi abanwa kwa kugoma kumlipia Makamu wa Rais malazi

Maoni ya Celina Kombani kwenye Magazeti ya Tanzania leo kuhusu nani hasa wa kulaumiwa kwenye suala hili yanaonyesha dhahiri namna anavyokiri kwamba tunajua namna serikali yetu inavyoendeshwa. Hongera wana JF. Lakini baada ya kukiri asingeishia hapo. Kwani Katibu Mkuu Kiongozi Bw Luhanjoa hajaachia ngazi hadi leo. Huyu kwa mujibu Sheria ya utumishiwa Umma Na. 8 ya 2002 ndiye Mkuu wa Utumishi wa Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri. Na isitoshe masuala ya usalama na uendeshaji wa ofisi binafsi za viongozi wakuu wa nchi yetu yako chini yake. Haya yanatokea hataki hata kuwaomba radhi wananchi waliomchagua Rais (Makamu aligombea kwa tiketi moja na Rais wetu). Hivi leo kweli Kamati za Maadili alizounda zitamwadhibu nani ikiwa kama yeye mwenyewe na timu yake wanatenda dhambi kama hii halafu wanamlaumu DED. Kama hataadhibiwa kwa hili basi tuamini kuwa nchi yetu haiendeshwi kwa misingi ya utawala bora. Nashindwa kuelewa hivi makamu kafanyiwa hivi kwa sababu ni mkimya sana au kwa sababu ni Mzanzibari? Puuh!
 
Bluray,
Mkuu shukran sana kwa maelezo yenye mwanga na kina cha uhakika..
Kitu kimoja tu ambacho napenda unifahamu. naelewa sana sheria na taratibu zinazotakiwa ktk sifa za tawala zetu kimaandishi lakini kilichonipa shida mimi zaidi ni kuelewa taratibu zinazotumika ziku zote..
Ikiwa Kiwete anapotembelea wilaya hulipiwa na wilaya husika, ikiwa Makamu wa rais anapotembelea wilaya hulipiwa gharama hizo... Je, nini matokeo ya mfarakano huu! Kumbukeni tu nchi yetu inaongozwa kiholela, kuna mambo mengi sana nchini yanafanyika bila hata aibu, acha kutembelea wilaya hata huku Ulaya wanapokuja ni kutumbua tu, hakuna hata mtu mmoja mwenye fikra za maslahi ya Taifa. Utaonekana mjinga na mwenye wazimu kwani sheria ya nchi yetu iko mikononi mwa watu...
Hivyo swala zima ni lazima litazamwe kwa mapana yake...Fedha inaliwa vibaya sana tena pengine na baadhi ya watu ambao wamo humu humu JF wanapo kwenda mikoani..Swala sio nani analipa isipokuwa ufujaji wa mfuko wetu iwe bajeti ni ya wilaya au taifa bado ni fedha za wananchi..Hizo millioni kwa msafara wa siku moja umekataliwa na mkurugenzi huyu lakini ukweli ni kwamba bado zitalipwa from somewhere..Ukiacha kutoa fedha mfuko wa nyuma ukatoa toka mfuko wa mbele au ktk shati lako bado maumivu ya matumizi mabaya ni yale yale...Ndizo guards nazotaka tuziweke..
 

Nashindwa kuelewa hivi makamu kafanyiwa hivi kwa sababu ni mkimya sana au kwa sababu ni Mzanzibari? Puuh!

"Makamu kafanyiwa hivi," kafanyiwa na nani?

Yeye VP Shein ndio kawafanyia wenzake vibaya. Yeye ndio alitakiwa kulipa. Waziri wa TAMISEMI, ofisi ya Waziri Mkuu, kasema: "Ndiyo maana rais anapokuwa kwenye ziara huenda na vyakula vyake," alisema Kombani.

Kwa hiyo, ni Shein mwenyewe ndio kala, kalala, na msafara wake, wamekunywa, wamekula, labda wakafungiwa na kufungiwa take-out, wakaondoka bila kulipa.

Halafu hii inakuonyesha kwamba, Mkuu wa Wilaya hajui taratibu za matumizi ya pesa, Makamu wa Rais hajui taratibu za fedha, au anajua lakini hajali (si ziara yake ya kwanza hii). Yeye huwa anakwenda tu sehemu na misafara mirefu, analala, anahutubia, anakula, anaondoka, hajui, hajali, haimuhusu, nani atalipa. Mpaka Waziri anakupa ujumbe hadharani, Makamu wa Rais beba chakula chako? Shame on Shein.
 

Jamani ninavyoelewa safari za makamu na viongozi wa serikali kuu zinagaramiwa na serikali kuu, kwani makamu alialikwa na halmashauri ya karatu? Hivi Tanzania tuna viongozi au ndo maana hata wenye ubongo wana hamia kwenye SIHASA(SIASA).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…