Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande asema pamoja na kukamilika kwa mradi wa Bwawa la Nyerere, watanzania tutegemee migao zaidi!

Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande asema pamoja na kukamilika kwa mradi wa Bwawa la Nyerere, watanzania tutegemee migao zaidi!

South Africa TU na uchumi wao mkubwa.
Kwa uzalishaji umeme niya 20 kidunia,
Na ya kwanza bara zima la Africa ila hata hizo megawatt 60,000 hawajafikisha.

Nchi nzima Wanazalisha megawatt 58,095
Itakua sisi uku ulimwengu wa tatu?[emoji848]

Bw.maharage arudi TU kwny ving'amuzi,
Haya mambo ya umeme Ni mweupe kabisa
Screenshot_20221225-043000.jpg
 
Huyu maharage sijui kala maharagwe ya wapi. Namshauri arudi dstv akaendee kuuza ving'amuzi
Shida ni madaraka makubwa aliyopewa Rais ndani ya Katiba yetu, bila hata kuhojiwa, ni vigezo gani ametumia katika uteuzi wake!

Tukumbuke kuwa Rais Samia, ndiye aliyemteua Maharage Chande, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO.

Bila Katiba mpya, itakayompunguzia madaraka makubwa ya ki-mungu mtu, Rais wetu, basi tutegemee, nchi yetu itaendelea kuwa masikini wa kutupa, Hadi mwisho wa Dunia hii😎
 
Ukweli lazima usemwe, nchi inaendelea kwa kasi sana, Megawatt 5000,haziwezi kutosha,, tunahitaji Gigawatt, sio megawatt
 
Mkuu Ulimuelewa Vibaya Ndugu Maharage Chande, Ukipitia Power Master Plan ya Nchi ndio utajua kuna Short term, Medium term na Long term ya mahitaji ya Nishati ya umeme iyo 60K ni Long term na nadhani ni miaka 25 ijayo ila katika short term MW 3000MW zinatosha nchi hii
Kwa sasa Total Installed Capacity ni 1605MW
Hawaoni Africa kusini, walijisahau kuweka long term plan za kuzalisha umeme, sasa wana mgao hatari, ndo wanakurupuka kuanzisha nuclear power plants
 
Nilishangazwa Sana na kauli aliyoitoa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande, eti pamoja na mradi wa Umeme wa Bwawa la Nyerere, kukaribia kukamilika, watanzania tutegemee mgao zaidi wa Umeme, Kwa kuwa mahitaji ya Umeme wa nchi hii ni Megawatt 60,000😎

Maneno hayo aliyatoa katika mjadala maalum, ulioandaliwa na Mwananchi Twitter Space.

Hivi Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, anatufanya watanzania wote hatuna akili, tusiokumbuka maneno yaliyotolewa na viongozi wetu wakuu wa nchi, kabla ya kukamilika Kwa mradi huo mkubwa kabisa wa nchi, ambao watanzania tumekamuliwa zaidi ya shilingi trillion 7 kuwa mradi huo ndiyo utakaokuwa mkombozi Kwa nchi yetu, Kwa kuwa mradi huo unategemea kuzalisha Umeme wa Megawatt 2,115 na tutazalisha Umeme wa "surplus" ambao kama nchi tunategemea kuwauzia Umeme nchi za jirani, na hivyo kutengeneza pesa nyingi za kigeni.

Hivi Hawa viongozi wetu wanatuonaje watanzania, kiasi cha kupenda kutuongopea watakavyo?

Inavyoelekea huyo Maharage Chande, anatuandaa watanzania kisaikolojia, Ili tutakapoona mgao unaendelea, basi tujue kuwa KAZI INAENDELEA, ya kuuza majenereta yao😞

Mimi naona muarobaini wa tatizo hili sugu la kuongopewa watanzania wakati wote na viongozi waandamizi wa serikali hii ya CCM, ni kuwapiga chini watawala Hawa wa CCM na kukiingoza chama kingine Ili kiingoze nchi.

Bila hivyo matatizo ya watanzania hayatakuja kutatuliwa na watawala hawa wa CCM Hadi mwisho wa Dunia hii😎

====

Chande: Bado kuna safari ndefu kufikia umeme wa viwanda

Muktasari:

Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Maharage Chande amesema mradi wa Bwawa la Umeme la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP) ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha kunakuwa na umeme wa kuendesha uchumi wa viwanda.

Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Maharage Chande amesema, licha ya juhudi za Serikali kuongeza vyanzo vya umeme likiwemo Bwawa la Umeme la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP), bado kuna safari ndefu kufikia umeme wa uchumi wa viwanda.

Ameyasema hayo leo Desemba 21 katika mjadala wa Mwananchi- Twitter Space unaoendeshwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited.

Amesema Mradi wa Bwawa wa Kufua Umeme la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP) unaotarajiwa kukamilika mwaka 2024 ni sehemu ya hatua za kupunguza changamoto hizo.

“Mradi huu utaleta umeme mwingi kwenye gridi, lakini mradi huu ni moja kati ya hatua ya safari ndegu ambayo tunayo kama nchi ya kuzalishaji kusafirisha na kusambaza umeme,” amesema Chadema leo Desemba 21, 2022 wakati wa mjadala.

Katika ufafanuzi wake, Chande amesema utafiti uliofanyika katika majarida mbalimbali unaonyesha ili uwewe na umeme wa kutosha kwa ajili ya viwanda na kukuza uchumi kila watu milioni moja wanahutaji megawati 1,000.

“Kwa idadi ya watu milioni 60, utaona tunahitaji umeme megawati 60,000 lakini kwa sasa tuna megawati 1500, tukileta hii 2115 tutakua na takribani megawati 3,800. Tunakazi kubwa ya kuongeza uzalishaji wa umeme,” amesema Chande.

Katika hatua nyingine, Chande amesema kama hakutakuwa na changamoto, ratiba ya kukamilisha mradi huo inabaki kuwa mwaka 2024.

“Hakuna aliyetegema Covid19, utaona pia kama bwawa hilo ikitokea changamoto tutatoa taarifa lakini mambo yakienda vizuri Juni mwaka 2023 tutakuwa tumemaliza,” amesema

Kesho Desemba 22, 2022 Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua hatua ya kuanza kujaza maji katika bwawa hilo lililokamilika asilimia 79 ikiwa ni matokeo ya uwekezaji wa Sh6.5trilioni zitakazokata kero kabla ya 2025.

Bwawa hilo lenye uwezo wa kuhifadhi lita bilioni 33.2 za maji eneo la Mto Rufiji mkoani Pwani, lilianza kujengwa 2019.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Yote hayo ni maandalizi kuleta mskampuni binafsi ya kipigaji aina ya iptl na yale mengine yaliyozalisha umeme kwa gesi aliyoyatimua jpm. Njia nzuri ni uwekezaji wa umma mradi udhibitiwe vizuri gharama za ujenzi. Wahuni walioko sasa lao ni kutafuta miradi ambayo watapiga hela ya umma.
Lengo liwe kushusha bei ya umeme kwa mteja kufikia viwango vya ulaya na marekani.
 
Back
Top Bottom