Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Hata kama wameropoka ni kifungu gani cha Sheria Kilichosema Waropokaji wakamatwe?

Rais yyt anaweza kutukanwa, akakshfiwa na akasemwa kwa kebehi vile vile.
Hayo ni mambo ya kawaida ktk NCHI ZOTE ZENYE DEMOKRASIA YA KWELI.
Tazama Obama na Marais wote w Ulaya. Wanachorwa mpk Wamevaa vichupi tu.
Wanatukanwa na Kukebehiwa kila siku. Nani umeskia Kakamatwa?

Ingia Face book, Twitter and so on uone matusi wanayotukanwa Viongozi wa Nchi za wenzetu. Umeshawahi kusikia Wamekamatwa.?

Magufuli anatawala Nchi KIBEBERU.
Wakati wa Mzee wetu Kikwete Watu walikuwa wanasema wapendavyo.

Na Mzee wa Watu wala habari hana.
Leo KIKWETE anakumbukwa.
Na Huyu Magufuli Pia atapita tu.

Hizi ni Jazba za kisukuma.
Zina mwisho wake.

Walitokea kina King Arthur and Ferrous walitawala EMPIRE wacha nchi ndogo km Tz. Leo hii WAKO WAPI?
Kwisha maneno yao.
Hata mifupa yao Hakuna.
Maelezo yako ni mazuri kwako. ukabila wako hauna nafasi Tanzania. Tunaweza kuendelea kama taifa hata tusipozingatia haya mawazo yako yako ya Kikabila.
Ukweli uko palepale kuna tofauti kati ya kuropoka na Freedom of speech.
Max yuko ndani kukutea watu kama wewe.

Be peacefully, obey laws.
 
Non sense sometimes fikiria kabla ujacomment jamamiiforums anahaki yakulinda wateja wake police wanatakiwa wanaposika jambo waishirikiane na jamiiforums kufanya upelelezi je swallinalozungumziwa linaukweli nakuchukua hatua nasikutumia nguvu kksawao polisi kulinda wapugadili
IMG_20161214_044351.jpg
 
Melo yuko salama..wala hakuna jambo jipya kaitwa kuhojiwa tuu.
Lakini walio sababisha kuitwa kuhojiwa ni wale waleta habari za uzushi ambazo serikali inalazimika kuhangaika kuzikanusha kila leo...
sheria ile ya mitandao ina ipa mamlaka polisi kupata taarifa za mtu kutoka kwa mtu na inawezekana hata kuchukua vifaa husika...
Melo yuko salama salimini.
Better
 
Nawashauri jamiiforums wafungue company USA then hii JF iwe chini ya hiyo company ili iwe inaoperate kwa sheria za huko America. Ila pia vijana mkiwa nyuma ya keyboard muwe na staha, mtaiponza hii forum, No Freedom With No Limit. Tujifunze kwa Snowden, amekuwa mtumwa kwasababu ya kuongea ukweli tena kwenye nchi tunayoamini ni ya kidemokrasia. Mwisho kwa kila mtumiaji wa JF tuwe tunasoma privacy policy kabla ya kutoa taarifa zetu itatusaidia pia kujua kipi cha kuchangia na kipi ambacho sicho. Gob bless Jamiiforums, Gob Bless Maxence Melo.
 
Ilianza kidogo kidogo kabla ya kufikiwa gazeti la mbunge wa Ubungo Kubenea, yakafuatia mazuio ya UKUTA baadhi yetu tukabeza. Ikaja Lema wengine wakasema ni mkorofi na sasa ni Maxence, ni nani atafuata ...who'll be next!?
Kwa hiyo mawazo huru yasiwepo au wanataka sote tuwe kama wa redio ya wafu!
Yaani hadi sasa hawajamfikisha Maxence mahakamani! Huyu ndugu hatafanyiwa kama G. Lema kweli?
 
Kulikuwa na ulazima gani wa kumkamata na kumnyima dhamana mtu ambaye mamlaka ikimhitaji atakwenda mwenyewe? Ni bahati mbaya kubwa inayojitokeza kuwa mahabusu kunatumiwa kukomoa baadhi ya makundi kinyume cha matumizi ya mahabusu ambayo yalikuwa ni mahali pa kuhifadhia wachache walio na madhara kwa jamii au wale ambao watakuwa huru watakuwa na athari au kuathiriwa na jamii.

Ni muendelezo wa mikomoano kama hii ambapo mahabusu na magereza zinaendelea kujaa watu pomoni wasio na hatia bali waliowekwa huko kwa ajili ya kukomolewa.

Pole zenu bwana Melo, poleni Lema, na poleni wapigania haki wote mnaoathirika na matumizi mabovu ya madaraka tunayoyaona kila uchwao wakati ambao wangekuwa huko wakiendelea kudunda mtaani Kijecha jecha.
 
Vigezo na masharti inabidi kuzingatiwa ili twende na sheria mpya ya magazeti na ile ya mitandao
kusema ukweli humu JF mazombi tupo wengi mno inabidi uongozi ili ujichomoe na kadhia hii ni muhimu wote kuwa verify our names na adress kwa ujumla wake
kama kweli hatuna nia mbaya,

Ni kweli nadhani Jamiiforums yenyewe itabidi wajilaumu, wameruhusu siasa zitawale zaidi kuliko chochote kile, Watu wanaamini wanaweza kuongea chochote kile bila hata kuchukuliwa hatua na mbaya zaidi watu wamehamisha propaganda kutoka kwenye social networks wamezileta huku, hii pia imefanya watu kuona JF ni kama jukwaa la siasa au sehemu ya kufanya propaganda tu kumbe siyo hivyo, JF ni zaidi ya shule hapa, watu wamejifunza na kufanikiwa kibiashara kupitia JF na kuna benefits nyingi sana watu wamepata kupitia hii Forum, sasa mtu mmoja au jukwaa moja tu la siasa linaweza kuigharimu jamiiforums nzima.
 
View attachment 445795
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

=====================

MKURUGENZI Mtendaji wa Jamii Media na mwanzilishi wa mtandao maarufu wa JamiiForums, anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kuu cha polisi, Dar es Salaam, kwa madai ya kugomea agizo la muda mrefu la jeshi hilo.

Polisi wamekuwa wakiagiza na kuamuru kupewa taarifa za watumiaji wa JamiiForums bila mafanikio.

Maxence alipigiwa simu leo akiwa ofisini kwake asubuhi akitakiwa kufika kituoni hapo na alitekeleza mwito huo.

Baada ya kufika polisi kati, akiwa ameongozana na mhariri na mwanaharakati wa uhuru wa mawasiliano, Simon Mkina na mwanasheria, Nakazael Tenga, Maxence alinyimwa dhamana ya polisi.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa Maxence atafikishwa makahamani kesho asubuhi kujibu mashitaka ya kuzuia upelelezi wa polisi dhidi ya makosa ya mtandao.

JamiiForums imekuwa na msimamo wa kutotoa habari za wachangiaji wake kwa yeyote, kwani kufanya hivyo ni kuingialia uhuru na faragha ya wateja wake.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, msingi mkuu wa mtandao wa JamiiForums umekuwa kulinda faragha ya watumiaji wake.

Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Kampuni ya Jamii Media, inayoendesha mitandao ya JamiiForums.com na FikraPevu.com imejijengea heshima na umaarufu kwa muda mrefu kutokana na namna inavyoendesha na kusimamia shughuli zake ambazo kwa kiwango kikubwa ni za kimtandao.

Mtandao wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 2.5 kwa mwezi ambapo kwa mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.

Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya waliofundwa na wanajumuia ya JamiiForums.

Pamoja na kuendelea kutoa huduma hata katika nyakati ngumu, mtandao wa JamiiForums unakumbana mara kwa mara na changamoto nyingi zinazosababisha waanzilishi na waendeshaji wake kuwa katika misukosuko mara kwa mara, hasa na polisi.

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Jeshi la Polisi limekuwa likiushinikiza mtandao wa JamiiForums (kwa njia ya barua rasmi) kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake.

JamiiForums katika kuhakikisha inasimamia usiri wa wateja wake, imekuwa ikihoji shinikizo kutoka Polisi yanazingatia sheria gani na kutaka kujua ni vifungu gani vya sheria ambavyo wadau wa mtandao huo wamevivunja bila kupewa maelezo yanayoridhisha zaidi ya kuelezwa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa kama ushirikiano hautatolewa kwa Jeshi la Polisi.

Tayari Jamii Media imefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania (Kesi namba 9 ya mwaka 2016); kutaka Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa kuwa vinapelekea kuvunjwa kwa haki za msingi za watanzania watumiao mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na 30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.




Baada ya kufungua kesi hiyo Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliweka mapingamizi sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Lakini mnamo tarehe 4, Agosti 2016 Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuzipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media iliamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi hiyo ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Chanzo: FikraPevu
=====

Taarifa zaidi..

Maxence Melo alitarajiwa kufikishwa mahakamani leo(Jumatano) asubuhi lakini hilo halikufanyika.

Wakili wa Bw. Melo anatafakari uwezekano wa kuwasilisha ombi kortini kupinga kuzuiliwa kwa mteja wake kwa zaidi ya saa 24 bila kufikishwa kortini.

Kwenye audio hapo chini, Mike Mushi ambaye ni Mwanzilishi mwenza wa mtandao wa JamiiForums, anaelezea mwanzo wa kesi hiyo.

Hongera Max, naamini Tanzania umebaki wewe tu ambaye unaweza kusimama na kuwatetea watanzania wote na sio watumiaji wa jamiiforums tu. Mungu azidi kukusimamia. watanzania tunaamini utatoka soon. Tunataka watu wanaojitambua kama wewe Max
 
Taarifa zaidi..

Maxence Melo alitarajiwa kufikishwa mahakamani leo(Jumatano) asubuhi lakini hilo halikufanyika.

Wakili wa Bw. Melo anatafakari uwezekano wa kuwasilisha ombi kortini kupinga kuzuiliwa kwa mteja wake kwa zaidi ya saa 24 bila kufikishwa kortini.

Kwenye audio hapo chini, Mike Mushi ambaye ni Mwanzilishi mwenza wa mtandao wa JamiiForums, anaelezea mwanzo wa kesi hiyo.

Nadhani ni sahihi wakachukua hatua hiyo ,maana dhamana ni haki ya Mtuhumiwa. Lakini kwa bahati mbaya Polisi wamekuwa wakitumiwa kuwaumiza watuhumiwa Kisaikolojia.

Ni muda sasa Mawakili kuweza kuiangalia Sheria ikiwezekana kufungua Kesi ya Madai dhidi ya Jeshi la Polisi kwa hivi Vitendo vya kuwanyima Dhamana watuhumiwa.
 
Lakini serikali ikihitaji information zozote toka Jf wanashindwaje kudukua ktk server za Jf mpaka wamkamate jamaa
 
Wakurugenzi wa Mitandao kama Watsaap, Facebook, Weakleaks na mingineyo duniani wanaishi vipi kama mmiliki wa kimtandao kidogo tu cha JF kinachotumiwa zaidi na wasomi anahenyeka kiasi hicho?

Katika mitandao kama ya weakleaks watu mashuhuri duniani huchafuliwa,hutajwa Wazi kwa sifa zao na anayechukia huambiwa akashtaki.Lakini hatujawahi kusikia hata siku moja DG wa mtandao huo akihenyeka kama anavyohenye kama alivyo Max.
 
Nawashauri jamiiforums wafungue company USA then hii JF iwe chini ya hiyo company ili iwe inaoperate kwa sheria za huko America. Ila pia vijana mkiwa nyuma ya keyboard muwe na staha, mtaiponza hii forum, No Freedom With No Limit. Tujifunze kwa Snowden, amekuwa mtumwa kwasababu ya kuongea ukweli tena kwenye nchi tunayoamini ni ya kidemokrasia. Mwisho kwa kila mtumiaji wa JF tuwe tunasoma privacy policy kabla ya kutoa taarifa zetu itatusaidia pia kujua kipi cha kuchangia na kipi ambacho sicho. Gob bless Jamiiforums, Gob Bless Maxence Melo.
Hivi haujui kama serikali inaweza kuzuia facebook,instagram,etc... kutokuwa hewani kwenye ardhi ya Tanzania sembuse ije iwe jf?
 
Hivi kweli Max akipewa taarifa uje Polisi tarehe kadhaa ili tukufikishe mahakamani hatakwenda kweli mpaka mpaka awekwe ndani kama jambazi?
 
Back
Top Bottom