Mkurugenzi TET, Dkt. Aneth: Zaidi ya Bilioni 297 zinatarajiwa kutumika kuchapisha vitabu vya kiada takribani Milioni 54

Mkurugenzi TET, Dkt. Aneth: Zaidi ya Bilioni 297 zinatarajiwa kutumika kuchapisha vitabu vya kiada takribani Milioni 54

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Anselmo Komba amesema kwamba wanakusudia kufanikisha kupandisha wiano wa vitabu vya kiada ili kufikia kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja yaani (1:1) kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita, ambapo mpango huo utarajia kugharimu zaidi ya Bilioni 297 kwa kuchapisha vitabu takribani milioni 54.

Akizungumza na waandishi wa habari Dkt. Aneth amesema kwamba katika kufanikisha hilo watakuwa kwenye maadhimidho miaka 50 ya TET wameandaa kampeni ya 'Kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja' ambayo itachochewa na hamasa na wadau mbalimbali.
photo_2025-02-20_14-18-34.jpg
"Lengo la kampeni hii ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuchapa na kusambaza Vitabu vya Kiada kuanzia Ngazi ya Elimu ya Awali, Darasa la Kwanza hadi la Saba na Kidato cha Kwanza hadi cha Sita ili kufikia uwiano wa kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja yaani (1:1)." amesema

Amesema kuwa maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi hiyo yatafanyika Machi 7, 2025, ambapo yataambatana na matembezi ya Hisani ya Kilomita tano (5), ambapo ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia na kushiriki matembezi hayo.

"Ili kufikia lengo hili, TET inawaalika wadau wote wa elimu chini ikiwemo serikali, sekta binafsi, mashirika ya dini, mashirika ya kimataifa na watu binafsi katika kuchangia na kushiriki katika Matembezi ya Hisani ya Kilomita tano (5) yatakayofanyika tarehe 07 Machi, 2025 kuanzia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Maktaba Mpya kupitia Chuo cha Maji, Mlimani City, Mwenge na kuishia Ofisi za TET Makao Makuu."amesema

Aidha imeelezwa kwamba Mgeni Rasmi katika matembezi hayo anatarajiwa kuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim M. Majaliwa, ambapo Matembezi yataanza saa 12.00 alfajiri hadi saa 2.00 asubuhi na baadaye yatafuatia na hafla ya uzinduzi wa sherehe za Miaka 50 ya TET itakayoanza saa 3:00 asubuhi katika viwanja vya TET Makao Makuu.

Lakini Dkt. Aneth ametoa utaratibu kwa wadau ambao wanataka kushiriki matembezi hayo, kwamba wanatakiwa kujisajili na kuchangia TSH. 50,000 (Fulana) au 150,000 (Trakisuti).

"Fedha hizi zitaelekezwa moja kwa moja katika uchapaji na usambazaji wa Vitabu vya Kiada kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Tanzania Bara na Zanzibar. Taratibu za kuchangia na kujisajili zimebainishwa katika mitandao ya kijamii ya TET ya X, instagram na facebook inayopatikana kwa anwani ya taasisiyaelimutanzania. Karibu tutembee pamoja kufanikisha lengo la Kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja."

Vilevile ameweka bayana utaratibu ambao wadau wanaweza kutumia kwa ajili kuchangia kampeni ya kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja kwa kutumia namba ya malipo ya serikali ambayo ni 994040118259. Ambapo amesema kwamba Kampeni hiyo ni endelevu, kuwa tayari michango imekwishaanza kupokelewa na itaendelea kupokelewa
mpaka siku ya kilele cha maadhimisho hayo Mwezi Juni, 2025.

Hata hivyo amefafanua hali ya upatikanaji wa vitabu kwa sasa kwamba tayari umefikiwa wiano kitambu kimoja Mwanafunzi mmoja kwa baadhi ya masomo, ametolea mfano kwamba masomo ya sayasi wiano ni kitabu kimoja Mwanafunzi mmoja na masomo mengi ya sanaa wiano ni kitabu kimoja Wanafunzi watu. Lakini pia amedokeza kwamba zinaendelea kufanyika tafiti kuona namna wanavyoweza kuhusisha zaidi matumizi ya vifaa vya tehama katika mazingira mbalimbali.

Ikumbukwe Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ni Taasisi ya Umma iliyo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Tenolojia. Taasisi hii ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 13 ya Mwaka 1975. Hivyo, Mwezi Juni, 2025, TET inatimiza Miaka 50 toka kuanzishwa kwake.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Anselmo Komba amesema kwamba wanakusudia kufanikisha kupandisha wiano wa vitabu vya kiada ili kufikia kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja yaani (1:1) kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita, ambapo mpango huo utarajia kugharimu zaidi ya Bilioni 297 kwa kuchapisha vitabu takribani milioni 54.

Akizungumza na waandishi wa habari Dkt. Aneth amesema kwamba katika kufanikisha hilo watakuwa kwenye maadhimidho miaka 50 ya TET wameandaa kampeni ya 'Kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja' ambayo itachochewa na hamasa na wadau mbalimbali.
"Lengo la kampeni hii ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuchapa na kusambaza Vitabu vya Kiada kuanzia Ngazi ya Elimu ya Awali, Darasa la Kwanza hadi la Saba na Kidato cha Kwanza hadi cha Sita ili kufikia uwiano wa kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja yaani (1:1)." amesema

Amesema kuwa maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi hiyo yatafanyika Machi 7, 2025, ambapo yataambatana na matembezi ya Hisani ya Kilomita tano (5), ambapo ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia na kushiriki matembezi hayo.

"Ili kufikia lengo hili, TET inawaalika wadau wote wa elimu chini ikiwemo serikali, sekta binafsi, mashirika ya dini, mashirika ya kimataifa na watu binafsi katika kuchangia na kushiriki katika Matembezi ya Hisani ya Kilomita tano (5) yatakayofanyika tarehe 07 Machi, 2025 kuanzia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Maktaba Mpya kupitia Chuo cha Maji, Mlimani City, Mwenge na kuishia Ofisi za TET Makao Makuu."amesema

Aidha imeelezwa kwamba Mgeni Rasmi katika matembezi hayo anatarajiwa kuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim M. Majaliwa, ambapo Matembezi yataanza saa 12.00 alfajiri hadi saa 2.00 asubuhi na baadaye yatafuatia na hafla ya uzinduzi wa sherehe za Miaka 50 ya TET itakayoanza saa 3:00 asubuhi katika viwanja vya TET Makao Makuu.

Lakini Dkt. Aneth ametoa utaratibu kwa wadau ambao wanataka kushiriki matembezi hayo, kwamba wanatakiwa kujisajili na kuchangia TSH. 50,000 (Fulana) au 150,000 (Trakisuti).

"Fedha hizi zitaelekezwa moja kwa moja katika uchapaji na usambazaji wa Vitabu vya Kiada kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Tanzania Bara na Zanzibar. Taratibu za kuchangia na kujisajili zimebainishwa katika mitandao ya kijamii ya TET ya X, instagram na facebook inayopatikana kwa anwani ya taasisiyaelimutanzania. Karibu tutembee pamoja kufanikisha lengo la Kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja."

Vilevile ameweka bayana utaratibu ambao wadau wanaweza kutumia kwa ajili kuchangia kampeni ya kitabu Kimoja kwa Mwanafunzi Mmoja kwa kutumia namba ya malipo ya serikali ambayo ni 994040118259. Ambapo amesema kwamba Kampeni hiyo ni endelevu, kuwa tayari michango imekwishaanza kupokelewa na itaendelea kupokelewa
mpaka siku ya kilele cha maadhimisho hayo Mwezi Juni, 2025.

Hata hivyo amefafanua hali ya upatikanaji wa vitabu kwa sasa kwamba tayari umefikiwa wiano kitambu kimoja Mwanafunzi mmoja kwa baadhi ya masomo, ametolea mfano kwamba masomo ya sayasi wiano ni kitabu kimoja Mwanafunzi mmoja na masomo mengi ya sanaa wiano ni kitabu kimoja Wanafunzi watu. Lakini pia amedokeza kwamba zinaendelea kufanyika tafiti kuona namna wanavyoweza kuhusisha zaidi matumizi ya vifaa vya tehama katika mazingira mbalimbali.

Ikumbukwe Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ni Taasisi ya Umma iliyo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Tenolojia. Taasisi hii ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 13 ya Mwaka 1975. Hivyo, Mwezi Juni, 2025, TET inatimiza Miaka 50 toka kuanzishwa kwake.
huo ndio uzalendo sasa! hiyo Bei ni bei nzuri sana kwa kweli! labda kama vitabu havitafkia hiyo idadi! hope vitabu vitagawiwa Bure hadi kwa private schools!
 
Back
Top Bottom