Mkurugenzi wa Moshi Manispaa kujenga bweni la wavulana 80 kwa Tsh 150,000,000/= Ni upigaji mkubwa

Mkurugenzi wa Moshi Manispaa kujenga bweni la wavulana 80 kwa Tsh 150,000,000/= Ni upigaji mkubwa

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949
mwananchi.co.tz

Moshi kujenga bweni la watoto wa kiume kukabiliana na ukatili


Mbunge wa Moshi Mjini, Priscus Tarimo akizungumzia ujenzi wa bweni la wavulana linalojengwa katika shule ya kutwa ya Msandaka iliyopo Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro mara baada ya kulikagua. Picha na Janeth Joseph
Muktasari:

Katika kukabiliana na matukio ya ukatili kwenye jamii, ikiwemo vitendo vya ulawiti kwa watoto wa kiume, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, imelazimika kujenga bweni la wanafunzi wa kiume katika shule ya kutwa ya Sekondari ya Msandaka iliyopo katika Kata ya Msaranga, Wilaya ya Moshi ili kukabiliana na vitendo hivyo.

Moshi. Katika kukabiliana na matukio ya ukatili kwenye jamii, ikiwemo vitendo vya ulawiti kwa watoto wa kiume, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro imelazimika kujenga bweni la wanafunzi wa kiume katika shule ya kutwa ya Sekondari ya Msandaka iliyopo Kata ya Msaranga, Wilaya ya Moshi ili kukabiliana na vitendo hivyo.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa bweni hilo, mkurugenzi wa manispaa hiyo, Mwajuma Nasombe amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kushamiri kwa matukio ya ukatili kwa watoto wa kiume.

“Hili bweni tumejenga makusudi kwa ajili ya kusaidia watoto wa kiume kwenye eneo letu, tukiangalia takwimu za ukatili kwa watoto wetu wa kiume, ukatili uko juu, kwa hiyo kupitia kamati ya fedha na mipango ya halmashauri, tukakubaliana tujenge bweni hili ili tuwe na uhakika wa kutengeneza baba bora baadaye,” amesemea Nasombe.

Bweni hilo ambalo ujenzi wake umeshaanza, linatarajiwa kukamilika Desemba 2024 ambapo litagharimu zaidi ya Sh150 milioni hadi kukamilika kwake na litakuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 80 kwa wakati mmoja.

Akizungumzia ujenzi wa bweni hilo, mbunge wa Moshi Mjini, Priscus Tarimo amesema kujengwa kwa bweni la wavulana katika shule hiyo ni chachu ya kumlinda mtoto wa kiume kwa kuwa wamesahaulika katika jamii.

Tarimo amesema ujenzi wa bweni hilo, utapunguza matukio ya ukatili na unyanyapaa kwa watoto wa kiume kwa kuwa tayari jitihada za Serikali na taasisi za kimataifa za kumsaidia mtoto wa kike zimeshafanikiwa na hivyo mtoto wa kiume kusahaulika.

“Ukiangalia matukio mengi ya unyanyapaa yanayotokea hivi sasa dhidi ya watoto wa kiume madhara makubwa sio kwa mtoto wa kike kama ilivyo kwa mtoto wa kiume, kwa hiyo sisi tumekuwa wa kwanza kufanya hivyo, kuhakikisha watoto wetu wa kiume wanakula salama.

“Jitihada za kiserikali za ndani na za taasisi za kimataifa za kumsaidia mtoto wa kike zimeshafanikiwa kiasi kwamba kwenye jamii tunachokiona mtoto wa kiume amesahaulika, mtoto wa kike amewekewa mazingira mazuri sana, hivyo ujenzi wa bweni hili utasaidia kwa kiasi kikubwa kumsaidia mtoto wa kiume asikutane na madhila,” amesema Tarimo.

Tarimo amesema serikali imewekeza kwenye shule za wasichana kila mkoa, hivyo mtoto wa kike tayari ameshajengewa mazingira mazuri ya kumlinda na kwamba changamoto iliyopo kwa sasa ni kwa watoto wa kiume.

“Kwa hiyo, sisi tumechukua hatua sasa, kwamba tunapomlinda mtoto wa kike na mtoto wa kiume naye tumlinde, hivyo tunashukuru serikali yetu kwa kutoka fedha hizi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hii ya maendeleo inayoendelea kwenye maeneo yetu,” amesema mbunge Tarimo.

Pamoja na mambo mengine, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo jimboni kwake ikiwemo shule ya sekondari Mawenzi ambayo serikali imetoa zaidi ya Sh234 milioni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa tisa ambao ujenzi wake umekamilika.

Akiishukuru serikali wa niaba ya wananchi, diwani wa kata hiyo, Charles Lyimo amesema ujenzi wa bweni hilo utakuwa ni mwarobaini wa kukomesha matukio ya ukatili kwa watoto wa kiume ambao walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda shuleni.

“Tunashukuru sana Serikali Kwa kuona umuhimu wa kujenga bweni hili hapa, maana shule hii iko mbali sana na makazi ya wannachi, kwa hiyo watoto wetu wa kiume walikuwa wakikumbana na matukio mengi ya ukatili huko njiani,” amesema diwani huyo.
 
Ni sawa ujenzi ni gharama ila bweni ni hall Tu halina nakshi zozote m 150 ni upigaji
 
H
Ujenzi ni gharama ndugu

Sishangai tena kajibana mnoo Kwa bweni la kisasa bado yuko vizuri
Tunaomba mchoro WA Hilo bweni!!

Cha kushangaza, kutakuwa hakuna vitanda Wala makabati Wala vyoo.

Mkandarasi aliyekuwa anajenga majengo ya serikali bila kiwango, kule mwanga DC , wakati bibi huyo akiwa DED, ndiye amehama naye anajenga tena soko la mbuyuni huko Moshi manispaa.
 
Yaani wewe chuki uliyonayo kwa mkurungezi wa moshi ni kubwa sana ambapo usipokaa sawa ni lazima UFE Mwaka huu.maana umejitahidi na kufanya kila njia kutaka kumchafua Mkurugenzi lakini umegonga Mwamba. Utahangaika sana lakini hutaweza kumchafua mkurugenzi.kila mtu humu jukwaani ameshuhudia namna ambavyo umekuwa ukianzisha vibandiko vya uongo na uzushi kutaka kumpaka matope na kumchafua mkurungenzi.

Una roho mbaya kama shetani au linyoka. Utakufa na wivu wako.umasikini wako wa akili utafukiwa nao udongoni. Aliyepata kapata tu .wewe endelea kuhangaika na kuteseka tu huku mkurungenzi akiendelea kuchapa kazi na kusonga mbele.wewe moyo wako hauna tofauti na lichawi.
 
Acha wizi wewe chawa, wewe ni sawa na yule wa tra bil 7 nyumbani! Mbwa nyie!
Kama hujuwi masuala ya ujenzi ni bora ukae kimya tu.ujenzi wa madarasa au mabweni ni gharama na kuna hatua mbalimbali katika ujenzi wake ili kujenga kwa ubora na kuweza kudumu kwa Muda mrefu pasipo kufanyiwa marekebisho yatakayo hitaji pesa nyingine .usifikiri vinajengwa tu kama nyumba ya kulala mbuzi au ng'ombe.
 
Kiwanja ni Bure
Maji ni Bure,
Shule ina umeme
Shile ipo mjini na sio kijijini ambako vifaa viko karibu.
Hiyo milioni 150, ni upigaji mkubwa.

Huyo mkurugenzi alimteua mkuu wa idara ya kilimo kusimamia ujenzi wa hospital ya wilaya ya mwanga.

Tunataka tumsikie Engineer aliongealea bei sio Ded. Huyo mama ninmpigaki mkubwa.

 
Bweni 1 Lina beba vitanda 20 vya double deki hvyo n wavula 40 Kwa bweni Moja,hvyo hapo yanatakiwa yajengwe mabwen mawiliii ...
 
Kama Mili 150 Ina gharama za vifaa, ghama za ufudi, Kodi (SDL na VAT)na faida ya mkandarasi ni sawa tu hakuna upigaji hapo

Wabongo acheni ushamba wa hela
 
Kama Mili 150 Ina gharama za vifaa, ghama za ufudi, Kodi (SDL na VAT)na faida ya mkandarasi ni sawa tu hakuna upigaji hapo

Wabongo acheni ushamba wa hela
Huyu ded ndiye aliyefanya haya madudu, akapandishwa cheo
 
Mil 150 kwa bweni ni gharama ya kawaida sana...Mleta mada usikurupuke ni vema ungekuja na Details za Mchoro,BOQ alafu ndio useme kuna ubadhirifu ila 150m ni hela ya kawaida kwenye ujenzi wa bweni.

Ukute mleta mada hajawah kujenga hata choo ila wabongo.
 
Hapo bweni Moja litakuwa na double deck 40 SAWA na wavulana 80 kwaTsh 150 milioni.

Ukumbuke,wazazi watakija kuchangishwa vitanda
Laymen Wakiona 150 mil wanapagawa ni hela ndogo

Ukidadavua kitaaalamu hakuna hela hapo

Huwa namshangaa kasimu majaliwa kuingizwa mkenge kwenye hizi issue za kitaalam

kama vile ujenzi hufanywa na majini sio binadamu wanaotakiwa kulipwa na kupata faida pia
 
Back
Top Bottom