Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, kwanini usijiuzulu?

Mkuu umeongea kwa uchungu sana, huu sasa ndiyo uzalendo.

Mamlaka husika kama mmepitia uzi huu chukueni hatua.

Ilifikia mahali eti mpaka vyeti vya Covid-19 navyo ni dili pale uwanjani.
 
In short wanadanga kutoka kwa abiria
 
Lango la kuingia nchini linapokosa mtu makini lawama na kudumaa Kwa huduma lazima kuwepo;
Makanjanja wapo wengi na wanazidi kueneza Kwa Kasi.

Wapo wanaojaribu kuharakisha ouvu Kwa madai kwamba ruhusa ipo ya kula kulingana na urefu wa kamba zao.

Kwa hali hizi taifa hatuwezi kupiga hatua kama Kila mmoja wetu hata kemea mambo haya🤔
 
Lango la kuingia nchini linapokosa mtu makini lawama na kudumaa Kwa huduma lazima kuwepo; Kwa kipindi kifupi toka kuzinduliwa Kwa terminal 3 madhaifu yafuatayo yapo wazi na
Story yako imejaa hisia kuliko uhalisia.

1. Mkurugenzi - Uwanja wa ndege ajiuzulu kwa ishu za Air Tanzania? Precision Air?

2. Precision Air hawatumii Terminal 3

3. Eti wafanyakazi wa ndege watafute abiria ambae hajacheck-in? Umewahi kufika JF Kennedy International Airport (NY), Dubai (DXB), Los Angeles International Airport (LAX) au New Delhi ukaona abiria anatafuta mpaka nje?

***New Delhi Airport hakuna matangazo sijui spika ww fuatilia screens tu.
 
Ni terminal ipi hiyo unayoongelea?
 
Kwa kweli nimesoma yote lakini lazima niseme ukweli haya yote sijawahi kukutana nayo na mimi ni msafiri sana na natumia sana airport sijawahi ku experiance kitu kibaya sasa siwezi kusema kitu sijakiona, lakini nataka ni comment kitu kimoja mtoa mada kaongelea suala la mtu kuitwa hapa sio kweli system haifanyi kazi hivyo.

Ukiwa umefanya booking ya ndege lakini hukutokea airport ile inaitwa No show na kuna penalty unapigwa sio kazi yao kukupigia uko njiani au home eti bro jina lako liko hapa mbona hujatokea halafu ahh unajuwa nime cancel au niko njiani nakuja hapana hakuna kitu kama hicho ndio maana ukiwa na booking unaweza kuchange date kwa gharama ndogo,

wake wanaoitwa ni wale wamesha fanya check in wana boarding pass lakini hajatokea kwenye gate wale ndio wanaitwa sababu kuu ni za kisalama huyu mtu ka check in ina maana yuko ndani kisha ingia yuko wapi? watakutafuta mpaka wakupate na kama hawajakupata basi mzigo wako lazima ushushwe kiusalama na wewe utatafutwa kiusalama hizo nchi zingine zote duniani wanataitwa majina watu walio check in tayari sio booking.
 
Hawa ndiyo wale viongozi waliozoea kufanya kazi kwa mazoea, utashangaa rais yupo na viongozi wa kumtumbua huyu kilaza wapo lakini kwa kuwa ni mwana CCM mwenzao wanamuacha tu aendelee kulitia taifa hasara. Mtu kama huyu inabidi atumbuliwe tu, mbona kuna wengine wenye uwezo wa kufanya hii kazi kwa weledi wako benchi?
 
Mkuu ukifika International Airports eg. Schiphol hawanaga huo muda. Kama haupo utajipanga. Nilishawahi kuachwa na ndege huko Schiphol nikiwa na boarding pass tayari.
NB: ndege inabeba watu 400 wakatafute mzigo wako wakaushushe kisa umecheck-in?
 
Jamaa kachemka waoitwa ni wale waliokuwa tayari na boarding pass basi kwa ajili ya usalama ndege haiondoki mpaka apatikane kama hajapatikana kwa muda mzigo wake lazima ushushwe basi hakuna kuitana sababu una booking.
 
Jamaa kachemka waoitwa ni wale waliokuwa tayari na boarding pass basi kwa ajili ya usalama ndege haiondoki mpaka apatikane kama hajapatikana kwa muda mzigo wake lazima ushushwe basi hakuna kuitana sababu una booking.
Boarding pass si kigezo cha kutafutwa.
 
Mkuu ukifika International Airports eg. Schiphol hawanaga huo muda. Kama haupo utajipanga. Nilishawahi kuachwa na ndege huko Schiphol nikiwa na boarding pass tayari
Mkuu utaitwa labda kama hukusikia hasa ukiwa na boarding pass au labda hukuwa na mzigo uliopakiwa kwenye ndege vinginevyo ndege haiondoki na mzigo wa mtu na yeye haja board ndege wakati ka check in hio ni serious security breach
 
Boarding pass si kigezo cha kutafutwa.
Naoma tuelewane kidogo sababu za kiusalama jina lako litaitwa sio kutafutwa na usipotokea ndege haitoki mpaka mzigo wako uwe off loaded kama huna mzigo unaachwa airport ufanye mchakato mwingine kama ulipitiwa shauri yako kuna gharama utaingia au utalala airport mpaka wapate connection ila sasa swali wewe mpaka una boarding pass ndege inakuacha unafanya nini humo airport?
 
wale front desk wakifunga check In wanajuwa number ya watu wanaenda kwenye gate na list wana scan boarding zote zikitimia number zao ndege inapewa green light kama mtu kakosekana katika ile list ya pili jina litaitwa au tangazo final call gate fulani hujatokea umelala huko wanatizama ana mzigo kwenye ndege yes basi ndege hairuki mpaka mzigo wako utafuatwe utolewe kwenye ndege, hata siku moja ndege haiondoki na mzigo na mwenye mzigo kabaki hakuna.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…