Pre GE2025 Mkutano Maalum wa Baraza la vyama vya siasa na wadau wa Demokrasia, January 4, 2024

Pre GE2025 Mkutano Maalum wa Baraza la vyama vya siasa na wadau wa Demokrasia, January 4, 2024

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mgeni rasmi anasema ni muhimu sana kuwa jasiri katika kutoa maoni na zaidi kuwa jasiri katika kusikiliza.
Halafu tuwe na utamaduni wa kuaminiana.
 
Mgeni Rasmi anakaribishwa. Kwaheshima sana Mheshimiwa Jenista Mhagama anapiga goti.
Tapeli katika maigizo. Toka lini jizi la kura likawa na unyenyekevu huo? Na Bado Kuna vyama vinaamini kwenye mikutano ya kupotezeana muda!
 
Wito wa mgeni rasmi ni kulitendea haki taifa hili. Amewaona wazee wenye maarifa mengi sana. Ni muhimu kutoa maoni ili mswada ukienda bungeni uwe na maslahi mapana ya nchi hii.
 
Tunapotoa maoni tutoe maoni ambayo yataleta kutungwa kwa sheria itakayodumu kwa muda mrefu.
 
Kama utazifuatilia kwa makini 4R utakuja kugundua kuwa huu ndio wakati mwafaka wa kujenga nchi katika msingi imara.
4R ni Nini boss, au unadhani Bado watu tunapotezwa na hizo mbwembwe za kisanii?
 
Msisitizo maalum; wakati watu wanatoa maoni na wale wanaochokoza mada. Tuwe makini na tuwe wawazi tuwe wa kujenga na siyo kufarakana.
 
4R ni Nini boss, au unadhani Bado watu tunapotezwa na hizo mbwembwe za kisanii?
Check hapa ndugu yangu
R1.jpg
R2.jpg
R3.jpg
R4.jpg
 
Tumeanza unafki mapeeema MWAKA bado mbichi. Katika hali tuliyo nayo ya uhuni katika demokrasia na chaguzichafu ni sahihi kusema hiki ni "KIKAO CHA AIBU"
Watu na akili zao hawawezi kukaa pamoja kujadili na wanyang'anyi na wadhulmati wasio tayari kuacha dhulma hizo... SIFUATILIAGI UJINGA!!!
 
Mkutano umefunguliwa Rasmi.
Kaa mkao wakula
 
Zamu ya makatibu wa vyama vya siasa inafuata sasa.
 
Mshereheshaji amependeza kweli kweli. Na sauti yake inajaa kwenye mic. Anawaita viongozi wengine wa vyama vya siasa na picha ya viongozi wa dini itakuwa ya mwisho.
 
Wakimaliza viongozi wa dini picha ya upendeleo viongozi wanawake wanafuata.
 
Ukifuatilia kwa umakini sana kuhusu 4R utagundua kuwa tupo kwenye mwanzo mpya. Sasa basi ni kujikita katika kujenga nchi yetu. Kwa kutumia falsafa ya 4R tutajenga nchi kwenye msingi imara.
Tukijikite katika kujenga nchi yetu???? Ni nchi gani hiyo??
Napenda kukukumbusha tu kwamba "Ujenzi wa Taifa Imara huanza na hatua ya Ujenzi wa Msingi Imara, ambao ni Katiba ya Nchi." Kamwe, nyumba haiwezi kuwa Imara na bora endapo kama msingi wake siyo Imara na wala siyo bora.
Endapo kama kweli tupo serious tunataka kujenga nchi yetu kuwa imara kwa kutumia Falsafa ya 4R, basi ni lazima Sharti kuu la kwanza kabisa ni Kutunga Katiba Mpya itakayotokana na Maoni, Mawazo na Fikra za wananchi wengi zaidi wa nchi hii ya Tanzania. No any other way around.
 
Tunapotoa maoni tutoe maoni ambayo yataleta kutungwa kwa sheria itakayodumu kwa muda mrefu.
Hakuna kitu kama hicho, Sheria nchi hii zinatungwa kwa Hila na genge la kiongozi aliye madarakani na wapambe wake. Hao mliowaita hapo ni Ili kuhadaa umma na Dunia kuwa mna Nia njema, lakini ki ukweli maoni yenu tayari mnayo mfukoni, na ndio Sheria itatungwa kuendana nayo, na wala sio hayo maoni ya hao mnaowapotezea muda hapo.
 
Mgeni Rasmi na meza kuu wanatoka sasa ukumbini. Sasa kazi inaanza. Muda wa kusikiliza na kutoa maoni
 
Bakari Machumu ndiye mwenyekiti sasa wa Mjadala unaofuata
 
Back
Top Bottom