Tetesi: Mkutano mkuu CCM tarehe 7.7.2016; Mangula kuwa katibu mkuu, Bulembo naibu katibu mkuu

Status
Not open for further replies.
Mzee mangula abaki kuwa mshauri wa chama otherwise kumpa nafasi ya uongozi ni kumtafutia jipu.
 
Ukawa wanaacha kutibu chama chao kilichojifia, wanaanza kufanya utabiri wa mambo ya ccm
 

Bulembo hivi ameshajifunza kusoma na kuandika,?
 
Lusinde duuh! darasa la saba, yaani CCM au Dr Magu kakosa msomi ndio aweke a primary school leaver!!! you the commentator, are just joking. Bulembo na Mangula wote safi
 
Hapa ndipo mimi hubaki hoi kwa siasa za nchi yetu. Na hasa sisi tusio wafia vyama tunachanganyikiwa kidogo.

CCM wanapochagua mtu ambaye wapinzani wake wanaamini mtu huyo ni dhaifu, ilitakiwa wapinzani wa CCM wakae kimya hadi mtu achaguliwe kisha aboronge. Kuboronga huko ndiko kuwe ahueni kwa kambi nyingine na kutumike kama turufu. Ninachokiona hapa ni wapinzani wa CCM kuanza kukosoa ili kukiokoa chama dhidi ya mtu huyo "dhaifu" as if wana mapenzi na CCM yenyewe.

Vilevile UKAWA nao wakitaka kuchagua mtu wao awaongoze, utaona CCM wanakuja na hoja za kumpinga mteule wakianika udhaifu wake hata kabla ya kukamata cheo as if wana machungu na UKAWA, badala ya kuwaachia wenyewe wachaguane na wavurugane watakavyo, jambo ambalo ilibidi walifurahie.

Sijui kama ule usemi wa wahenga waliposema "adui muombee njaa" tunaujua.
 
Inabidi rais apewe tu icho cheo ili kuepuka maneno yao zidi ya chadema kudai tatizo la mgombea kutokua mwenyekiti ndo sababu ya lowassa kugombea na slaa sasa zamu ya ccm kuiga na rais kutokua mwenyekit wa chama
 
Itakuwa "bunge live"
 
CCM, katibu Mkuu mpeni Bollen Ngetti kama mnataka kuua upinzani nchi hii na mtalaaniwa.
 
Bulembo ndo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na ndiye aliyefanikisha mikakati ya ushindi wa CCM. Ndiye alikuwa msemaji wa Mgombea wetu wakati wa kampeni. Kibajaji ni Mbunge wa Mtera. Mnafahamu pia muziki wake anaowahenyesha pale Bungeni
Kibajaj ana kipaji cha kuongea ila Mara nyingi reasoning yake huwa ndogo.Hafikirii logically.
 
Apite Lusinde katika U-Naipe!
 
Mhe. Mangula kutoka Umakamu Mwenyekiti kuwa Katibu Mkuu ni kama kushushwa chini au mimi ndo sifahamu itifaki.
Kapandishwa cheo, maana umakamu mwenyekiti ni busara za mwenyekiti na sio compulsory.... Hila KM wa chama si ndio engine ya chama.
 
Safi sana CCM haifanyi mambo yake gizani. Mfanye vivyo hivyo kwa bunge liwe live; lisiendeshwe gizani.
 
Vipi kuhusu Lusinde unaonaje kwenye nafasi ya uenezi?
 
Bulembo ndo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na ndiye aliyefanikisha mikakati ya ushindi wa CCM. Ndiye alikuwa msemaji wa Mgombea wetu wakati wa kampeni. Kibajaji ni Mbunge wa Mtera. Mnafahamu pia muziki wake anaowahenyesha pale Bungen

Mtu asikudanganye, strategist katika ccm ni mzee Mangulla bila huyu mzee magamba wangekuwa hoi sana!! They will make a strategic mistake if they leave him out of their new line up!!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…