Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Aiseee, nasikia kizungu zungu zungu halafu nguvu zinaniishia, naomba nikafungulie halafu narudi.

Msanii naomba nishikie kiti tafadhali, mwendelee hadi nitakaporudi.

Ila usichakachue, kumbuka hatuzungumzii vyama. Tunaongelea Utaifa na Uzalendo. Maslahi ya taifa Mbele.
 
Sijamuelewa huyu jamaa ana zungumzia nini, bora unge andika kwa lugha moja kuliko hivi unavyo mix swahili na ki-English, fool!
mkuu Fool ndo umesign jina lako hapo mwishoni? kumbuka siyo vema kureveal your name.
 
Mnganyizi; kwanza karibu kikaoni, haalafu lete hiyo Mic kwanza.

Tumesema maadili hayaruhusu lugha ya matusi. tuko live TBC au unataka wakate matangazo?

Sasa turudi kwenye hoja yako, nani hujamuelewa?

Wana JF tafadhali tusichakachue lugha. Tutumie kiswahili tu, lugha yetu ya taifa.
Wewe hapo sijakuelewa mkuu, una changanya lugha. nakushauri siku nyingine tumia lugha moja kuwasilisha hoja yako utaeleweka vizuri.
 
Aiseee, nasikia kizungu zungu zungu halafu nguvu zinaniishia, naomba nikafungulie halafu narudi.

Msanii naomba nishikie kiti tafadhali, mwendelee hadi nitakaporudi.

Ila usichakachue, kumbuka hatuzungumzii vyama. Tunaongelea Utaifa na Uzalendo. Maslahi ya taifa Mbele.
Nashukuru kwa kuniona, ingawa naona DC anafaa zaidi kwa nafasi hii.
pole kwa mfungo. Tupo pamoja shekhe
 
Hahaaa msanii, kuna watu wanakimbia maajukumu hapa, nadhani kwa kuwa hakuna posho. Iko hivi:
Dark City = katibu lakini inaonekana amechomoa
WoS= Mwenyekiti ya Kamati ya kuhusu utawala bora na kama wahujumu wanyongwe au la. Kachomoa na kunipigia kelele eti atanifikisha mahakamani. Alimtumia pia lugha ya matusi mazito ya kawaida na ya nguoni pamoja na kejeli na kashfa.

Habari ndo hiyo, kinachoniweka hapa ni uzalendo tu.

Sasa nasubiri warudi niwaulize kama watafanya hiyo kazi au la.


Mwenyekiti anapokuwa mzushi sijui inakuwaje!
Mkuu ukiambiwa onyesha ni wapi lugha ya M... imetumika sijui utaonyesha nini kwa kweli.Naona hata huruma kukupeleka mahakamani maana nitakufilisi!
 
Mwenyekiti anapokuwa mzushi sijui inakuwaje!
Mkuu ukiambiwa onyesha ni wapi lugha ya M... imetumika sijui utaonyesha nini kwa kweli.Naona hata huruma kukupeleka mahakamani maana nitakufilisi!
Nimeyasaka katika thread hii sijayaona hayo matusi sijayaona labda ulimPM.

Haya turudi kwenye mada sasa. Lete hoja zako hapa
 
Wewe hapo sijakuelewa mkuu, una changanya lugha. nakushauri siku nyingine tumia lugha moja kuwasilisha hoja yako utaeleweka vizuri.

Nimekusoma. Ila uneonyesha hiyo sehemu niliyochakachua ingekuwa vema zaidi. Nitajirekebisha.

Ila matusi na Kejeli uachae. Nimemwambia Kova asikupeleke sello huko Central . . . Du! Au nimechakachua tena?
 
Mkuu Superman
karibu tena kwenye kiti. Amini nakuambia amani ilitawala
 
NIna swali hapa kwa mgombea wa nafasi ya juu kabisa......"Hivi huu uchakachuaji wa rasilimali za Watansanyia hasa Ardhi na Madini utaishi lini"? Ili wananji waweze kufaidika na rasilimali zao na sio hao walitutawala enzi kama wakoloni na leo wanarudi kama wawekezaji. Naomba jibu lenye utekelezaji sitaki longolongo
 
Mwenyekiti anapokuwa mzushi sijui inakuwaje!
Mkuu ukiambiwa onyesha ni wapi lugha ya M... imetumika sijui utaonyesha nini kwa kweli.Naona hata huruma kukupeleka mahakamani maana nitakufilisi!

Ndiyo WoS umenitukana sana, tena mbele ya kadamnasi ya wana JF na nikataka kujiuzulu kama hawalaani kitendo hicho, mpaka wakati huu hakuna iliyefanya hivi. Hii issue yako imejaa harufu ya rushwa:

Hebu angalia matusi yako:

Mwenyekiti..uteuzi huu ni batili..huna mamlaka ya kujipa ujiko wa uenyekiti..kwa msingi huo huwezi kuniteua.Teuzi hizi nazo zinafanya kazi nzima iwe batili

Umeona?

Uteuzi huu ni batili
Huna mamlaka
Unajipa ujiko wa uenyekiti
Huwezi kuniteua.
Teuzi hizi nazo zinafanya kazi nzima iwe batili

Nilikusihi sana matusi hayo ni makubwa sana na mimi ni kama baba yako lakini hukujali na bado ukatishia kunipeleka mahakamani.

Mpaka nikajiimbia wimbo wa "Najiweka pembeni, Naogopa Msongamano"
 
Mwenyekiti, hatimaye nimepata Ilani ya 2005 ambayo most of ahadiz zilitoka humo.
http://www.ccmtz.org/ilani/ilani.pdf
Wajumbe waisome waichambue kisha tuangalie ilivyotekelezwa au telekezwa ndipo tujitutumue kuhoji uhalali wa ahadi mpya za ilani iliyopo.
Naomba kutoa hoja
 
Mkuu Superman
Nimefanikiwa kwa ombi lako kusaka kwenye net na kukuta hii kitu itakayotuongoza kuchambua ahadi za Kikwete 2005. Nimeweka ilani kwanza kama walivyoiweka wenyewe kisha nasaka ahadi ambazo hazikuwekwa kwenye ilani

Mkuu nataka niwe na Uhakika, una maaana Agenda Kuu za JF 2010 ziwe hizi?

12. Jitihada pia zimefanyika na zinaendelea kufanyika za kukabiliana na umasikini wa kipato, yaani kuwafikishia wananchi manufaa ya kukua kwa uchumi kwa wao kufaidika mmoja mmoja. Hili ndilo hasa eneo ambalo sera ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi inahusika nalo. Agenda kuu katika eneo hili ni:-
(a) uwezeshaji
(b) Kupambana na umasikini
(c) Kushiriki katika uchumi wa nchi, na
(d) Ajira.
13. Eneo hili la kuyafikisha kwa wananchi manufaa ya kukua kwa uchumi wa nchi ndilo agenda kuu na changamoto ya msingi ya Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005. Na mbinu kuu za kuikabili changamoto hii ni pamoja na zifuatazo ambazo zote ni sehemu ya MKUKUTA:-
(a) Kuendelea kukua kwa uchumi wa nchi kwa kasi kubwa zaidi (kufikia asilimia 10 ifikapo mwaka 2010).
(b) Kuongezeka kunakoendelea, kwa wingi na ubora wa huduma za jamii hasa elimu, afya, maji n.k. na miundombinu hasa barabara, madaraja, mawasiliano, umeme n.k.
(c) Modenaizesheni ya harakati mbalimbali za kiuchumi zinazowapatia ajira za kujiajiri na kipato wananchi, hjasa kilimo, ufugaji, viwanda vidogo, uvuvi, uchimbaji madini, n.k.
(d) Kuzipa uhai rasilimali mfu za wananchi ili ziweze kutumika kama dhamana za kujipatia mikopo, kwa kutumia mkakati wa kurasimisha rasilimali na biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA). Mkakati huu utachangamsha ajira za wananchi za kujiajiri wenyewe.
(e) Kuwawezesha wananchi kutumia fursa mbalimbali za maendeleo zilizopo kujiongezea kipato na kushiriki katika uchumi wa nchi, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kumiliki hisa katika makampuni mbalimbali, kama ilivyokwishaanza kwa mfuko wa umoja.
(f) Mkakati wa uanzishaji wa maeneo maalumu ya uchumi ( Special Economic Zones Strategy) kama unaotumiwa na nchi Asia ambao utazalisha ajira nyingi za kuajiriwa katika sekta rasmi, na za kujiajiri. Kwa jina jingine, mkakati huo unaitwa The Tanzania Mini-Tiger Plan.
(g) Kuimarisha taasisi zinazotoa mikopo kwa wananchi.
14. Kwa vile lengo la juhudi zote hizi zinazobainishwa na ilani ni kuyafanya maisha ya watanzania wawe bora zaidi, CCM imebuni kaulimbiu mbili zifuatazo.:-
(a) "Maisha bora kwa kila Mtanzania",
(b) "Kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya, Tanzania yenye neema tele inawezekana."
 
Ndiyo WoS umenitukana sana, tena mbele ya kadamnasi ya wana JF na nikataka kujiuzulu kama hawalaani kitendo hicho, mpaka wakati huu hakuna iliyefanya hivi. Hii issue yako imejaa harufu ya rushwa:

Hebu angalia matusi yako:



Umeona?

Uteuzi huu ni batili
Huna mamlaka
Unajipa ujiko wa uenyekiti
Huwezi kuniteua.
Teuzi hizi nazo zinafanya kazi nzima iwe batili

Nilikusihi sana matusi hayo ni makubwa sana na mimi ni kama baba yako lakini hukujali na bado ukatishia kunipeleka mahakamani.

Mpaka nikajiimbia wimbo wa "Najiweka pembeni, Naogopa Msongamano"

HII KALI! Wiki hii sijacheka kama nilivyocheka baada ya kusoma post ya mwenyekiti wangu wa mkutano!
Jamani...kiswahili chaenda kikiwa kigumu.Kama haya ni matusi ya nguoni, je yale yenyewe ya nguoni yatakuwa nini?
 
Ndiyo WoS umenitukana sana, tena mbele ya kadamnasi ya wana JF na nikataka kujiuzulu kama hawalaani kitendo hicho, mpaka wakati huu hakuna iliyefanya hivi. Hii issue yako imejaa harufu ya rushwa:

Hebu angalia matusi yako:



Umeona?

Uteuzi huu ni batili
Huna mamlaka
Unajipa ujiko wa uenyekiti
Huwezi kuniteua.
Teuzi hizi nazo zinafanya kazi nzima iwe batili

Nilikusihi sana matusi hayo ni makubwa sana na mimi ni kama baba yako lakini hukujali na bado ukatishia kunipeleka mahakamani.

Mpaka nikajiimbia wimbo wa "Najiweka pembeni, Naogopa Msongamano"
Aisee
kweli hiyo inampasa WOS kukuomba radhi walah.
Mwenyekiti rudi kwenye hoja uendeshe kikao
mie naenda kutabaruku kidogo, ugoro unaiita nje
 
Ndg M/Kiti,Ktb, na wajumbe wote mlikoko kwa kikoa hiki napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa michango yenu kwa dhati, bila kupoteza muda nina yangu machache kwa kuanzia tu kwa leo hii.


  1. Katiba ya nchi ile ndio ya kwanza kufanyiwa marekebisho
  2. Baaada ya kuundwa katiba ya nchi kuwepo na mustakabali wa nchi hii ni katika kusimamia kila sector za serikali na umma katka uwajibikaji wao katika nchii.
  3. Elimu- kuwepo na mustakabali wa nchi ndipo kutaisimamia mfumo mpya wa elimu kama wenzangu waliotangulia wakiitaji mfumo mpya wa elimu na itatuondolea ile hali ya kila waziri aingiapo wizara hiyo na kujiwekea mfumo wake wa kuiongoza wizara kwa kuifanya kama sarakasi
  4. Afya
  5. Miundombinu na mawasiliano
  6. Viwanda


Mkuu, tuko paamoja sana No.1 hadi 3 na tumeyakubali kimsingi.

Hayyo 3 ya mwisho unaweza kuyatolea ufafanuzi wa kina ili wana JF wayaelewe kwa uwazi zaidi?
 
Wiki hii sijacheka kama nilivyocheka baada ya kusoma post ya mwenyekiti wangu wa mkutano!
Jamani...kiswahili chaenda kikiwa kigumu.Kama haya ni matusi ya nguoni, je yale yenyewe ya nguoni yatakuwa nini?
WOS
mie nimecheka kuliko. ila ndo hivyo tena kama Mwenyewe kasema hizo ni tusiz za nguoni. dawa ni kusema sorry tu kisha tuendelee.
 
Mkuu Superman
karibu tena kwenye kiti. Amini nakuambia amani ilitawala

Asante sana Msanii, tuko pamoja. Kwa kuwa amani ilitawala, hii inatoa picha kuwa umekubalika. naomba tafadhali uendelee. Mimi niko hapa jukwaani.
 
Back
Top Bottom