Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

PHP:
Akizungumzia Zanzibar alisema bado kuna kazi ya kufanya kutokana haki ya kupiga kura katika uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, wabunge na serikali za mitaa kupewa watu walioishi katika jimbo husika kwa kipindi cha miaka mitatu kitendo ambacho ni kinyume cha demokrasia.

Hivi huu ni ubaguzi au lengo ni kuhakikisha nchi haitoi viongozi mamluki?
 
PHP:
Kwa Upande wa Shirikisho la Afrika Mashariki alibainisha kwamba kinachokwamisha juhudi hizo ni viongozi wa nchi wanachama kung'ang'ania nafasi zao za kisiasa wanazoshikilia.

Boloney...............................tatizo kuu la EAC ni hao viongozi wamechaguliwa na nani na mbona hakuna kura ya maoni katika maamuzi yote ambayo yamefanyika hadi sasa?

EAC ni ya viongozi tu siyo ya raia.............................................
 
Udhaifu wa Muungano haujaletwa na mabadiliko ya Katiba ya Z'bar Send to a friend Tuesday, 01 March 2011 20:42

Na Awadh Ali Said

FEBRUARI 9, gazeti moja la kila wiki lilitoa makala iliyosema "Muungano wa Tanzania sasa umekuwa dhaifu zaidi'' iliyoandikwa na Tundu Lissu.

Mwandishi amejaribu kujenga hoja inayotoa taswira kuwa Muungano wa Tanzania umezidi kuwa dhaifu kutokana na Mabadiliko ya Kumi ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 ambayo yeye anaamini kuwa mabadiliko hayo

"yamemong'onyoa misingi karibu yote ya muungano … yamebadili sura ya muungano wenyewe, mipaka yake na muundo wake" na kwamba anakhofu kuwa mabadiliko hayo "yanaweza kuwa chanzo kikuu cha kubomoka kwa Muungano na hata tishio kwa usalama wa mipaka ya Taifa".

Hoja ya kwanza ni kuwa Mabadiliko ya Kumi ya Katiba ya Zanzibar yaliitangaza Zanzibar '‘kuwa nchi yenye mipaka kamili." Anaendela kueleza kuwa "Rais anajua kuwa kabla ya mabadiliko hayo kufanyika, Zanzibar haikuwa nchi na wala mipaka yake haikutajwa." Anaegemeza hayo akirudia kifungu cha kwanza cha Katiba ya Zanzibar 1984 (kabla ya marekebisho) kinachosema '' Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."

Katika hoja hii ya kwanza kuna mambo mawili; la kwanza kuwa Mabadiliko hayo ya kumi ndio yaliyoitangaza Zanzibar kuwa nchi, na la pili ni kuwa mabadiliko hayo ndiyo yaliyobainisha mipaka ya Zanzibar ambayo mwanzo haikutajwa. Yote mawili katika hoja hii siyo ya kweli. Tuanze na la kwanza la Zanzibar kuwa nchi.

Zanzibar ilikuwa na Katiba yake ya kwanza mwaka 1979 ambayo baadaye ilifutwa na kuandikwa upya mwaka 1984, na hadi leo hii Zanzibar inaongozwa na Katiba yake hiyo ya 1984 ambayo imeshafanyiwa marekebisho mara 10. Sasa tujiulize je, Katiba ya Zanzibar ya 1984 haikutaja Zanzibar kama nchi ila baada ya hayo marekebisho ya kumi yanayolalamikiwa?
Ni kweli Katiba ya Zanzibar ya 1984 kabla ya marekebisho ya kumi ilieleza katika kifungu cha 1 kuwa " Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." Lakini ukiwacha kifungu hicho cha kwanza vifungu kadhaa wa kadhaa au tuseme katiba yote ya Zanzibar (kabla ya hayo marekebisho ya kumi) yakiitaja Zanzibar kuwa ni nchi. Angalia vifungu (baadhi tu) ili tuweke sawa hili:

(9)(i) Zanzibar itakuwa ni NCHI ya kidemokrasia na haki za kijamii.

(9)(2)(a) Mamlaka ya kuendesha NCHI ni ya wananchi wenyewe …

Pia vipo vifungu kadhaa katika Katiba ya Zanzibar vinavyoeleza kina ubaga kwamba Zanzibar ni nchi ambayo ina dhamana kwa wananchi wake.

Msingi mkuu katika kanuni za kutafsiri sheria (Statutory Interpretation ) ni kuwa ili uweze kupata tafsiri sahihi kwa waraka wowote (iwe ni Katiba, Sheria, Mkataba n.k.) ni kuwa unatakiwa uusome waraka wote ndipo uweze kufahamu maana, tafsiri au dhamira inayopatikana kwa ujumla katika waraka huo kuhusiana na jambo husika. Sio kuchopoa kifungu kimoja tu ukaegemeza hoja yako hapo hapo tu.

Lakini bila ya kuangalia vifungu vyengine vya katiba hiyo ya kabla ya marekebisho ya 10,tuangalie hicho kifungu kimoja tu, cha kwanza, kama alivyofanya mwandishi kinachosema '‘Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano" Sasa tujiulize Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri Ya Muungano inasimama katika utambulisho upi? Sawa ni sehemu ya Jamhuri, lakini utambulisho wake ni upi? Ni sehemu kama Mkoa, Wilaya, Tarafa, Jimbo, Kata au kitongoji?

Zanzibar ina katiba yake, ina Rais wake, ina Mahkama zake, ina mawaziri wake, ina Baraza lake la kutunga sheria, ina watu wake (tena wana ID zao), ina bendera yake, ina wimbo wake wa Taifa, ina Mamlaka yake ya Serikali za mitaa, ina magereza yake (vyuo vya mafunzo), ina vikosi vyake vya ulinzi, ina mapato yake na bajeti yake n.k. Je, kuna Mkoa au Wilaya yenye yote hayo? Na yote hayo yapo kabla ya hayo mabadiliko ya kumi ya katiba ya Zanzibar. Hivyo hakuna ukweli wowote kuwa Zanzibar imetangazwa kuwa ni nchi kwa mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar 1984.

Mwandishi anasema:

"Rais anajua kuwa kabla ya mabadiliko hayo kufanyika, Zanzibar haikuwa nchi na wala mipaka yake haikutajwa". Je, ni kweli mipaka ya Zanzibar haikutajwa kabla ya marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ? Tuangalie katiba ya Zanzibar 1984 kabla ya mabadiliko ya 10 kifungu cha 2(i) kinasemaje:

2(i) "Eneo la Zanzibar ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba na visiwa vidogo vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano ikiitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar."

Na baada ya marekebisho ya kumi kifungu hicho kinaendelea kuwapo kama kilivyo kuhusiana na suala la mipaka.

"1) Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo vilivyoizunguka bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar".

Hoja ya pili ya mwandishi ni kuwa marekebisho haya yanadhoofisha Muungano kwa vile yameondoa mamlaka ya kuigawa Zanzibar katika mikoa kutoka mikononi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na kuweka mamlaka hayo kwa Rais wa Zanzibar. Hili ni kweli limefanyika katika marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar. Lakini tujiulize ni kwa nini limefanyika? Inaeleweka wazi kuwa ni Rais wa Zanzibar ambaye kipindi chote tokea huo Muungano wa Tanzania uasisiwe 1964, ndiye anayeigawa Zanzibar katika mikoa na wilaya.

Hakuna kumbukumbu inayoonyesha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano amewahi kuigawa Zanzibar katika Mikoa au Wilaya. Sasa kwa takriban miaka 47 mamlaka hayo yalikuwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kikatiba lakini kiutendaji na kiutekelezaji aliyekuwa anatekeleza mamlaka hayo ni Rais wa Zanzibar; hivyo hiyo ilikuwa ni kasoro na ilistahiki kurekebishwa, na ndicho kilichofanyika. Haiwezekani tukadumisha vifungu ndani ya katiba ambavyo vinaonekana ni pambo tu. Hili litoshe kuonyesha mkanganyiko uliomo katika katiba zetu.

Hoja ya tatu ya mwandishi ni kuwa mabadiliko ya kumi yamepunguza mamlaka ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania. Anasema:

"Mabadiliko ya katiba yaliyofanyiwa yamekiuka katiba kwa kuinyang'anya Mahakama ya Rufani ya Tanzania mamlaka ya kusikiliza rufani zote zinazotoka katika Mahakama Kuu ya Zanzibar"

Kwa ufupi haijawahi kutokea kwa Mahakama ya Rufani kuwa na mamlaka ya kusikiliza rufaa zote zinazotoka katika Mahakama Kuu ya Zanzibar tokea ianzishwe.

Hoja ya nne ya mwandishi ni kuwa mabadikilo ya 10 ya katiba ya Zanzibar yamekiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano na kudhoofisha Muungano kwa vile sasa Zanzibar "imehalalisha uwepo wa vikosi vya Jeshi vya SMZ vinavyoviita Idara maalum" Ama kuhusu hili la "Vikosi vya kijeshi" kama alivyoviita mwandishi au '‘Idara Maalum" kama vinavyoitwa na katiba ya Zanzibar, hata kabla ya hayo mabadiliko ya kumi inaeleza kuwepo kwa Idara Maalum na ambazo ni Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU), Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM), Chuo cha Mafunzo na kifungu hichi hakikubadilishwa hata nukta.

Hizi ni Idara kongwe zipo Zanzibar na wala hazijaundwa na mabadiliko ya kumi na hayo mabadiliko ya kumi hata hayakugusa chochote kuhusu Idara hizi. Sijui haya yametokea wapi?

Mwisho nikubaliane na mwandishi kuwa Muungano wa Tanzania umezidi na unazidi kuwa dhaifu kila uchao na sababu za hayo zipo na ziko wazi lakini kamwe sio mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar.

Samahani: Makala ya Hoja kutoka Zanzibar ya Ally Saleh, wiki hii hatukuweza kuitoa kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
 
Profesa Shivji: Bado Watanzania hawajawa huru kumiliki rasilimali zao Send to a friend Tuesday, 01 March 2011 20:39

Elias Msuya
MOJA kati ya malengo ya kupigania uhuru kwa nchi zilizokuwa chini ya utumwa wa kikoloni ni kujiamulia mambo yao katika matumizi ya rasilimali zao.

Tanzania ni moja kati ya nchi za Afrika zilizopata uhuru mwanzoni mwa mika ya 1960 ikiwa na matumaini mapya ya kutumia rasilimali zake katika kujiletea maebndeleo.

Lakini hadi leo ni miaka 50 baada ya uhuru huo, matumaini hayo yamepotea. Kiwango cha umasikini kwa wananchi kimeongezeka, huku wananchi wachache wakifaidi keki ya taifa.

Ardhi ambayo ndiyo rasilimali kubwa kwa wananchi inamilikiwa na watu wenye uwezo kifedha. Baada ya serikali kupitisha sera ya uwekezaji, kumekuwa na uporaji wa ardhi ya kijiji na wawekezaji - mafisadi wa ndani na nje kwa visingizio mbalimbali ikiwa ni pamoja na uzalishaji wa mafuta kwa kutumia mimea (bio-fuels) na ulimaji wa mazao ya chakula kwa ajli ya masoko ya kimataifa na uchimbaji wa madini.

Kumekuwa na upanukaji wa miji huku wenye fedha wakijenga maghorofa kwa kumeza ardhi ya mila ya wenyeji ambao hurundikwa kwenye maeneo yasiyo na rutuba wala mipango miji "slums".

Hali hiyo imesababisha wananchi wengi kukosa makazi ya uhakika. Kwa mfano asilimia 70 ya wakaazi wa jiji la Dar es Salaam wanaishi kwenye makazi yasiyo na mipango miji.

Mbali na ardhi, rasilimali nyingine kama vile wanyamapori, madini, maji na misitu, zinamilikiwa na matajiri huku masikini walio wengi wakivipata kwa taabu.
Kwa jumla, wavuja jasho wa mijini na vijijini wamepoteza matumaini ya maisha kutokana na kushindwa kufaidika na rasilimali zao.

Profesa wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Issa Shivji anatathmini hali hiyo na kushauri ushirikishwaji wa wananchi katika Katiba ili kuitengeneza nchi kama watakavyo.

Akijadili mchakato wa Utungaji Katiba mpya na upana wa Mjadala wake, Profesa Shivji anasema kuwa, ardhi na ulinzi wa rasilimali unapaswa kuangaliwa upya katika Katiba

"Katiba mpya iwe kielelezo kwa maandishi katika lugha ya utalaamu wa mwafaka wa wananchi kuhusu "Tanzania tunayoitaka; dira, maadili na malengo ya jamii na taifa letu" anasema.

Anasema kuwa wananchi wanapaswa kujadili upya mfumo wa uzalishaji, mfumo wa Dola na Utawala, uhuru wa nchi na jamii wa kujiamulia mambo yao wenyewe, mfumo wa uwezo, upana na mipaka ya matumizi ya madaraka, mfumo wa haki na wajibu wa wananchi na jamii zao, mashirika yaom na maungano yao kwa ujumla wao.
Katiba ni nini?
Kumekuwa na dhana iliyojengeka miongoni mwa wananchi kuwa Katiba ni mkataba kati ya wananchi na viongozi wao katika kutekeleza yale wanayohitaji.

Lakini kwa mujibu wa Profesa Shivji, Katiba siyo mkataba bali ni mwafaka wanaofikia wananchi kutokana na mahitaji waliyonayo na jinsi ya kuyafikia.

"Katiba siyo mkataba, mkataba huhusisha bidhaa na katiba siyo bidhaa, ni mwafaka wa wananchi katika kuishi maisha wayatakayo," anasema na kuongeza,
"Kwa kuwa Katiba ni mwafaka, jambo lolote lile ambalo wananchi huona muhimu kwao huwekwa katika Katiba".

Wananchi na rasilimali
Katika Tanzania ya leo na miaka mingi ijayo, hakuna jambo lolote muhimu kwa wanajamii kuliko ardhi na rasilimali zao.

Rasilimali hizo ni chanzo cha uhai, kielelezo cha utamaduni, utambulisho wa ubinadamu, tegemeo la kuishi maisha ya kujitegemea, ya heshima na ya kifahari.

Kwa mujibu wa Profesa Shivji, bado wananchi hawajapa haki ya kumiliki rasilimali ikiwamo haki ya kumiliki mali na hifadhi yake na haki ya upatikanaji wa ardhi.

Misingi ya Azimio la Arusha
Kwa mujibu wa Profesa Shivji, Misingi ya Azimio la Arusha ililenga kujenga siasa ya Ujamaa na Kujitegemea huku ikielekeza njia kuu za uchumi zimilikiwe na serikali.
Anatoa mfano wa Katiba ya sasa Ibara ya 9(j) ambayo imekataza uendeshaji wa uchumi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali. Hata hivyo Katiba hiyo imetofautiana na misingi ya Azimio la Arusha ambapo miiko ya viongozi ya kutokujilimbikizia mali imeondolewa na tafsiri ya Ujamaa na Kujitegemea imechakachuliwa (ibara ya 151)

"Miiko ya uongozi ilikuwa na masharti kwa kiongozi na asipoyatekeleza anakabiliwa na adhabu. Lakini maadili ya viongozi wa umma hayana masharti. Kiongozi anajaza fomu ya mali zake tena wengi hawasemi ukweli na mwananchi wa kawaida hawezi kwenda kuona kiongozi amejaza nini," anasema.

Taratibu za kusimamia haki ya kumili rasilimali
Profesa Shivji anashauri kuwe na mifumo mipya kwa ajili ya umilikaji wa ardhi, muundo wa udhibiti wa ardhi, taratibu za ugawaji na kanuni za utumiaji.

Licha ya Katiba ya sasa Ibara ya 24, kutoa haki ya watu kumiliki mali, bado kumekuwa na changamoto kadhaa za jinsi ya kumiliki mali kwamfano, haki ya mtu mmoja mmoja, haki ya usawa katika upatikanaji wa ardhi bila ubaguzi kama vile ubaguzi wa jinsia.
Suala la haki ya wananchi kuwa na haki za kiuchumi na kijamii bado limebaki na utata.

Hata hivyo Profesa Shivji anatoa angalizo kuwa na haki bila kujali mfumo wa uchumi ni dhana tu bila uhalisia.
"Mfumo bora ni lazima utoe mwafaka juu ya njia ya maendeleo, tunataka maendeleo endelevu ya walio wengi, au wachache, nani ni gurudumu la maendeleo; wazalishaji au wawekezaji? Nani au ni matabaka yapi ni walengwa wa maendeleo: wavuja jasho wa mjini na vijijini au wavuna jasho, matabaka ya kibwanyeye?" anasema Shivji.

Nini kifanyike?
Kutokana na upungufu uliomo katika Katiba ya sasa, Profesa Shivji anashauri kuwa wananchi wapewe kipaumbele katika madai na matakwa yao kuhusu ardhi na rasilimali zao yawe mstari wa mbele katika mjadala wa kitaifa kuhusu katiba mpya

Anashauri pia misingi ya mfumo wa uchumi na uzalishaji na vyombo shirikishi vya kudhibiti na kusimamia ardhi na rasilimali za nchi iwekwe katika Katiba.
"Wakaazi walio wengi wa miji wahakikishiwe ardhi ya kujenga na ugawaji ardhi ushirikishe wananchi kupitia vyombo shirikishi".

Anashauri pia kuwepo na uwazi katika mikataba mikuu kuhusu rasilimali za madini, mafuta, maji, mito, milima, mapori na ardhi.

"Ichapishwe magezetini kwa kuhabarisha wananchi kwa jumla na wananchi wa eneo husika washiriki katika mijadala ya mikataba na iridhiwe na Bunge kitaifa kabla ya utekelezaji," anasema.
 
Jaji Mkuu: Bajeti finyu chanzo cha mlundikano wa kesi Send to a friend Tuesday, 01 March 2011 20:37

Fidelis Butahe

NI jambo la kwaida kusikia watuhumiwa wa kesi mbalimbali nchini wakilalamika kuwa wamekaa muda mrefu bila kesi zao kusikilizwa.

Zimekuwa zikitolewa sababu mbalimbali za kuchelewa kusikilizwa kwa kesi hizo ikiwa ni pamoja na kutomalizika kwa upelelezi wa tuhuma zinazowakabili washitakiwa.

pamoja na hayo inawezekana kauli ya Jaji Mkuu aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria jijini Dar es Salaam ikawa ndio jibu sahihi ya wale wanaolalamika kukaa muda mrefu bika kusikilizwa kwa kesi zao.
Maadhimisho hayo yaliyofanyika nje ya Mahakama Kuu hivi karibuni yaliwakutanisha wanasheria mbalimbali ambapo Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman anasema uwelewa wa wananchi kuhusu mahakama na sheria ni mdogo.

Anasema elimu juu ya mahakama itamuwezesha mwananchi kutetea haki zake kikamilifu ndani na nje ya mahakama.

Anasema mahakama imefanya mambo kadhaa kuelimisha wananchi ikiwa ni pamoja na kushiriki katika maonesho mbalimbali na kuandika vipeperushi.

Jaji Othman anaeleza hofu yake kuwa elimu juu ya mahakama inaweza kuzua mzigo kwani shauku ya wananchi kudai haki zao itaongeza idadi ya migogoro mahakamani na kwamba hadi sasa bado kuna mrundikano wa mashauri katika mahakama mbalimbali.

Changamoto zinazoikabili Mahakama

Anasema changamoto zinazoikabili Mahakama ni pamoja na bajeti finyu isiyolingana wala kuzingatia mahitaji ya Mahakama jambo ambalo ni chanzo cha ulimbikizaji wa kesi.

Anasema kiwango cha bajeti ambacho wamekuwa wakiomba kimekuwa kikipunguzwa na kwamba hata kiwango kinachopitishwa na serikali huwa hakitolewi kwa wakati jambo ambalo hufanya mahakama ishindwe kufanya vikao vyake kama ilivyopangwa.

Anasisitiza kuiomba serikali ifikilie kuitengea Mahakama bajeti ya asilimia mbili kama kianzio katika mfuko wa mahakama.

Anasema changamoto nyingine ni upungufu wa mahakimu katika mahakama za mwanzo pamoja na majengo ya Mahakama hizo huku akisema kuwa majengo mengi ya mahakama hizo ni chakavu.

Anasema vituo vingi vya Mahakama za mwanzo viko mbali kiasi kwamba wananchi hutembea umbali mrefu kutafuta haki zao huku mahakimu wengine nao wakitembea umbali wa zaidi ya kilomita 100 kuhudumia mahakama hizo.

Changamoto zajibiwa

Akijibu hoja ya changamoto mbalimbali zinazoikabili mahakama, Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwepo katika sherehe hizo anaitaka Mahakama kuongeza kasi katika Programu ya Maboresho ya Sekta ya Sheria.

"Ongezeni kasi ya maboresho ya sekta ya umma. Kwa sasa kasi iliyopo ni ndogo kwani hata wabia huwa wanalalamika kwa kukaa na pesa kwa muda mrefu na wakati mwingine wanalazimika hata kuzirudisha. Pengine hata haya malalamiko mengine yasingekuwepo sasa," anasema Rais Kikwete.


Rais Kikwete anaitaka Mahakama kuongeza juhudi na hata kubuni maarifa mapya ya kupambana na tatizo la uadilifu kwa baadhi ya watoa uamuzi (mahakimu na majaji).

Anasema bado kuna hisia kwa baadhi ya watoa uamuzi kuwa ni watu wasiokuwa na pesa ni vigumu kuweza kupata haki.

"Uwezo wa kuondoa hisia hizi uko mikononi mwenu. Mafanikio yatarejesha imani kwa wananchi na kwa jamii za kimataifa," anasisitiza Rais Kikwete.

Kuhusu tatizo la uhaba wa majaji Rais Kikwete anasema kwake si tatizo kuwateua hivyo akaitaka mahakama impelekee tu mapendekezo ya majina ya watumishi wanaostahili kuwa majaji ili yeye aweze kufanya uteuzi.

Mfuko wa Mahakama

Kuhusu mfuko huo anasema mchakato uko katika hatua za mwisho na kwamba kilichobakia ni kuandika tu mswada ili kuuepeleka bungeni na kupitishwa, anaongeza kwamba ni matarajio yake kuwa utaanza katika mwaka wa fedha ujao.

Rais Kikwete anaahidi kuendelea kuongeza bajeti ya Mahakama ikiwa ni pamoja na kuendelea kujenga vituo vya Mahakama Kuu kila mkoa na kuahidi kuendelea kujenga Mahakama za Mwanzo.

"Tengenezeni mpango wa uendelezaji wa mahakama za mwanzo gharama zijulikane tuweze kuandaa bajeti ili kurudisha hadhi ya mahakama hizo ambazo ni mahakama za wananchi," anasema Rais Kikwete.

Uelewa wa wananchi juu ya sheria

Rais Kikwete anasema baadhi ya wananchi wamekosa imani naye kutokana na msimamo wake wa kukataa kuingilia uhuru wa mahakama wanapomtaka atengue uamuzi mbalimbali unaotolewa na mahakama.

Rais Kikwete anatoa wito kwa Mahakama kushirikiana na wadau mbalimbali vikiwamo vyombo vya habari katika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sheria na nafasi ya mahakama, akieleza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kutoa elimu hiyo kwa umma.

Anasema watu wasiokuwa na elimu kuhusu mfumo wa utekelezaji wa sheria ni rahisi kuonewa na kudhulumiwa haki zao na kwamba wakijua jinsi zinavyofanya kazi na kwamba ziko kwa ajili ya kuwahudumia wao, watakuwa na imani nazo.

"Hii itanipunguzia hata taabu ninayoipata kuwa jambo likishaamuliwa na Mahakama mimi sina uwezo wa kulitengua. Mara nyingi kuna watu huwa wanakuja kwangu wakitaka nitengue uamuzi uliotolewa na Mahakama.

"Nikiwaambia kuwa mimi sina uwezo huo huwa wananishangaa sana na kuona kama ninakwepa wajibu wangu na kusema ni bora tumchague mwingine na kwamba ndio maana wanataka Katiba mpya."
 
na Lucy Ngowi




MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally, amewataka vijana kutumia fursa walizonazo ili waweze kujadili Katiba kuhusu elimu.

Ally alitoa ushauri huo jana, katika mjadala ulioandaliwa na Shirika la HakiElimu jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mhadhiri huyo, kumekuwepo na ubaguzi wa dhahiri katika mfumo wa elimu hapa nchini, jambo ambalo ni hatari kwa masilahi ya taifa.

"Hivi sasa kuna shule nzuri na zile ambazo zipo taabani. Zile zilizopo taabani ndizo zinazohudumia watoto wengi zaidi hapa nchini. Je, kwa jinsi hii tunatarajia kujenga taifa la namna gani?," alihoji mhadhiri huyo.

Alisema uvumbuzi pekee wa suala hilo ni Watanzania wote kwa umoja wao kuamua kusomesha watoto ili shule za umma ziwe za mazingira mazuri ya kutoa elimu bora, ili kusiwe na tofauti kubwa kati ya shule binafsi na zile za umma.

Katika hatua nyingine, mwanaharakati wa haki za binadamu, Deus Kibamba, amewataka vijana kushiriki katika mjadala wa kutaka Katiba mpya, ili kuondoa mfumo wa ubadhirifu na wizi uliojengeka miongoni mwa viongozi.



juu
 
Alisema uvumbuzi pekee wa suala hilo ni Watanzania wote kwa umoja wao kuamua kusomesha watoto ili shule za umma ziwe za mazingira mazuri ya kutoa elimu bora, ili kusiwe na tofauti kubwa kati ya shule binafsi na zile za umma.

The correlation between school performance and with placing our children in public school is entirely flimsy...................
 
CCM imevunja Katiba ya nchi
ban.blank.jpg


Bakari M. Mohamed​

amka2.gif
KATIBA ni mkusanyiko wa kanuni na sera ya serikali juu ya utawala wa nchi (Kamusi ya Maana na Matumizi, 2005 ukurasa wa 144); na vilevile katiba ni jumla ya kanuni ambazo kwazo huwezesha serikali itawale au chama au kampuni iendeshe shughuli zake (Kamusi ya Kiswahili Sanifu, TUKI, toleo la pili, ukurasa wa 149).
Kwa ujumla, katiba ya nchi ni mwongozo wa kuendesha mambo yote ya menejimenti na utawala wa nchi kama ilivyokubaliwa na wananchi.
Ukiachilia mbali ukuukuu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (JMT) ya 1977 (iliyofanyiwa urekebu mwaka 2005) bado mamlaka ya nchi katika Tanzania inapaswa kuifuata katiba hiyo. Kwa jinsi yoyote iwayo; hakuna mtu, kikundi cha watu na au chama cha siasa kinachopewa dhamana ya kuongoza serikali kwa mujibu wa katiba na kikaamua kufanya kinyume na utashi wa Katiba ya JMT ya 1977 (2005).
Pamoja na ukweli huu, Chama Cha Mapinguzi (CCM) kimekuwa kwa nyakati na mazingira tofauti kikivunja katiba ya nchi ilhali wenye dhamana ya kuilinda katiba hiyo, yaani wananchi, wakizidiwa ujanja na au nguvu na mfumo kwa kutokujua haki za msingi za kikatiba!
Huu ndio mwendo uliyojengwa tangu uhuru hata sasa kwamba sehemu kubwa ya wananchi wa Tanzania hawaijui katiba yao na hawana uelewa wa haki na wajibu wao kama raia.
Inawezekana, hali ya kutowashirikisha wananchi katika kupata uelewa wa wajibu na haki zao za kikatiba, kulifanywa kwa makusudi na au kwa bahati mbaya! Tuchukue dhana ya kwanza kwamba kulifanywa kwa makusudi maalumu. Dhamira ya lengo la kuwafanya wananchi mbumbumbu wa mwongozo (sheria mama) ni matokeo ya kujenga mazingira ya kutumia fursa hiyo katika kutawala fikra nyepesi za raia wasiye na uelewa wa haki, uhuru, usawa na wajibu wao kama wananchi wenye dhamana ya kuendesha serikali yao.
Kwa kulijua hili, CCM ilitumia mwanya huo katika kuficha mambo mengi yaliyotakiwa yawe wazi kwa raia juu ya uhuru wao, haki zao, na wajibu wao katika kuendesha mustakabali wa nchi yao. CCM, kama chama-dola, na kilichotawala satwa zote za uongozi wa nchi kama ilivyoainishwa kwenye Ibara ya 10 ya Katiba ya JMT ya 1977 kwa Sheria Namba 15, 1984 Ibara ya 6 iliyofutwa na Sheria Namba 4, 1992. Kwa ujumla, CCM ilishika hatamu (wengine wanauita ukiritimba) kwa muda mrefu na hata baada ya mfumo wa demokrasi ya vyama vingi vya siasa bado wenye dhamana ya chama hicho wamebaki na kasumba ileile.
Munasaba wa kuandika makala hii umekuja baada ya kuichunguza, kuipembua na kuisasambua Katiba ya JMT ya 1977 (2005) juu ya nukta muhimu zihusuzo mamlaka ya nchi na hususan juu ya uendeshaji wa shughuli za serikali inayotokana na chama kinachounda serikali.
Kwa mujibu wa Ibara ya 8(1), Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (JMT) ni nchi inayotakiwa kufuata misingi ya demokrasi na haki ya kijamii ambapo: wananchi ndio msingi wa mamlaka yote; lengo kuu la serikali linatakiwa liwe ustawi wa wananchi; serikali inatakiwa iwajibike kwa wananchi; na kwa jinsi yake wananchi wanatakiwa washiriki kwenye shughuli za serikali yao!
Bila kujali ukweli huu wa kikatiba, CCM kwa nyakati tofauti imekuwa ikipora mamlaka ya wananchi kwa kisingizio kwamba ni chama cha wananchi!
Na kwa jinsi hii makala haya yatajaribu kufanya udondozi wa nukta muhimu na nyeti juu ya malengo mahususi kumi na moja juu ya lengo kuu moja linaloainishwa kwenye Ibara ya 9 ya Katiba ya JMT ya 1977 (2005). Na kwa jinsi hiyo, tuweke mkazo kwenye kila nukta ya lengo mahsusi litakaloainishwa na jinsi CCM inavyofanya na mazingira yalivyo sasa.
Ukiachilia mbali juu ya kuheshimu na kuthamini utu na haki nyinginezo za binadamu, haki ya kufanya kazi halali, haki sawa kwa raia wote bila ubaguzi, na nchi kutawaliwa kwa misingi ya demokrasi na ujamaa kama ilivyo kwenye Ibara 9(a), 9(e), 9(g), na 9(k) bado kuna kusuasua kwa utekelezaji wa ujamaa kwa misingi ya mazingira ya Tanzania.
CCM imeacha siasa ya "Ujamaa na Kujitegemea" na inaendesha siasa za soko huria la siasa. CCM imepoteza maadili ya kiitikadi juu ya "kujenga jamii ya watu waliyo sawa na huru;" sasa inajenga matabaka ya watawala na watawaliwa, walio nacho na wasio nacho.
Sasa tugeukie nukta za muktadha wa makala hii ambazo kwa mtazamo wa jicho la uchunguzi na mantiki (hoja za kisayansi) CCM imezivunja kwa jinsi ya kushindwa kutekeleza haki na wajibu kama chama kinachounda serikali.
Tahadhari juu ya kupupia kusoma nukta hizi inatolewa na kwa jinsi hiyo ni vema msomaji akaweka kielelezo cha Katiba ya JMT ya 1977 (2005) ili kutoa nafasi ya kuziona nukta hizo.
Nukta ya kwanza ni ulinzi na utekelezaji wa sheria za nchi kama ilivyo kwa Ibara 9(b). Hadi sasa serikali ya CCM imeshindwa kulinda na kutekeleza baadhi ya sheria muhimu kwa maslahi ya taifa. Mfano wa karibuni ni kuvunjwa kwa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya 2004 na Kanuni zake za 2005; ambapo kuvunjwa kwake ndiko kulikopelekea Tanzania kuingia kwenye zabuni tata ya ufuaji wa umeme wa dharura uliyoipa mkataba ghushi Richmond Development Company LLC uliyohaulishwa kwa Dowans inayoidai TANESCO shilingi bilioni 94 za Tanzania.
Katika mazingira yasiyozoeleka, Waziri Mkuu wa JMT amemzuia Waziri wa Ujenzi, Dakta John Pombe Magufuli kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Barabara ya 2007; na kibaya zaidi, kusimamishwa utekelezaji wa sheria hiyo si kunaweza kujenga kiburi kwa wavunja sheria bali kunaweza kuleta sintofahamu na au vuta-ni-kuvute itakayovuruga utekelezaji wa sheria.
Kama wananchi wataachwa wavunje sheria ilhali kwa jinsi moja na au nyingine serikali inawaacha waendelee na uvunjifu kwa sababu za kisiasa kuna hatari ya sheria nyingi zaidi kuvunjwa.
Ibara ya 9(c) inaitaka serikali kuhakikisha kwamba shughuli zake zinahakikisha kwamba utajiri wa taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote na kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine! Cha kusikitisha, CCM imeshindwa kuendeleza sehemu kubwa ya utajiri wa Tanzania na badala yake imewaachia wageni na waporaji wa rasilimali na mali ya asili.
Kwa sehemu kubwa serikali imeshindwa kuhifadhi utajiri wa Tanzania na kuutumia kwa manufaa ya wananchi wengi wa Tanzania; badala yake serikali imeendelea kuwaachia wanyonyaji wachache wanaovuna holela.
Ubinafsishaji umefanywa kuwa unyonyaji kwa jinsi ya aina ya uwekezaji holela. Kama alivyowahi kunukuliwa Mwalimu Nyerere kwamba, "ubinafsishaji ni unyang'anyi;" na ni kweli wananchi wa Tanzania wamenyang'anywa utajiri wao na wanyonyaji wachache wenye choyo, uroho na uchu wa kinyonyaji.
Watanzania wamekuwa wakinyang'anywa ilhali CCM ikitoa usaidizi wa sera na usimamizi wa unyang'anyi huo. Utajiri wa nchi, kama madini, mawe ya thamani na vito unavunwa kwa gharama nafuu na faida kubwa inayopatikana inawatajirisha wanyonyaji wachache wenye kumiliki fursa za uwekezaji kutoka nje.
Maendeleo ya Tanzania yamekuwa yakipangwa kwa mtindo wa zimamoto juu ya menejimenti ya vurugu. Hakuna uwiano wa mizania ya mipango juu ya matumizi endelevu ya rasilimali watu na vitu katika kufikia lengo la ujenzi wa jamii ya watu waliyo sawa na huru katika kuondoa umasikini, ujinga na maradhi.
Mipango ya Tanzania imekuwa haizingatii uwiano wa upatikanaji wa rasilimali na matokeo halisi ya utumizi wake bila ya kuathiri mazingira ya uchumi, jamii na siasa.
Japokuwa Ibara ya 9(f) inatamka juu ya kuhifadhi na kudumisha heshima ya binadamu kwa mujibu wa Tangazo la Dunia la Haki za Binadamu bado kuna dalili mbaya ya ukosefu wa heshima juu ya binadamu na haki zake. Kumekuwa na uvunjifu wa moja kwa moja na au kwa taathira yake juu ya heshima ya binadamu.
CCM imeshindwa kutambulisha heshima ya binadamu juu ya haki ya kila mtu kufanya kazi yenye kulinda utu na heshima yake na juu yake kupata malipo yenye kujenga heshima ya kibinadamu.
Wakati huu sehemu fulani ya wananchi wa Tanzania wanajihusisha na kazi haramu na zinazotweza utu na heshima ya binadamu kama vile ukahaba, usafirishaji wa binadamu, uuzaji wa viungo vya binadamu (hususan vya albino), dawa za kulevya na ufuaji wa fedha haramu.
Ibara ya 9(h) imekuwa ikivunjwa kwa nyakati tofauti; hata hivyo kwenye Awamu ya Nne, CCM imebeba mzigo mzito wa lawama juu yake. Serikali ya CCM kwa mujibu wa ibara iliyotajwa inawajibika kuhakikisha kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini.
Ushahidi uliopo unaonyesha kwamba CCM imeshindwa kuzuia dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu na upendeleo! Kwa ujumla, kumeibuka uharibifu mukubwa wa mfumo na wa ndani ya mfumo (ufisadi) unaohanikizwa na ujambazi wa kiserikali unaotishia mustakabali wa uongozi wa CCM.
Kama ilivyobainishwa kwenye Ibara ya 9(c), Ibara ya 9(i) inasisitiza juu ya matumizi ya utajiri wa taifa juu ya mkazo wa maendeleo ya wananchi na hususan kwenye kuondoa umasikini, ujinga na maradhi. Hali ya matumizi ya utajiri wa nchi inakatisha tamaa na maadui hawa watatu wa taifa waliyotangazwa baada ya uhuru bado wanawasumbua wananchi. Serikali ya CCM imekuwa ikitumia nadharia zaidi juu ya utumizi wa utajiri wa taifa katika kuleta maendeleo kinyume chake chama hicho kimekuwa kikiahidi (ahadi za kinafiki zisizotekelezeka) na kuwaacha wananchi kwenye msongo wa kungojea miujiza ilhali utajiri wa taifa unavunwa na wanyonyaji wachache wenye uchu wa kunyonya kwa mtindo wa kunyang'anya!
Hali halisi ambayo CCM imeijenga kwa nyakati hizi ni knyume kabisa na Ibara ya 9(j) inayoelekeza kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi. Ukweli usiyokuwa na shaka ni kwamba CCM baada ya kulitupa Azimio la Arusha na kuruhusu uchumi huria imesababisha njia za uchumi kumilikiwa na wanyonyaji wachache ambao kwa sehemu kubwa wamehodhi mali na utajiri wa Tanzania.
Na hii inaonekana hata ndani ya CCM ambayo imesheheni matajiri wenye satwa hata yakucheza kifisadi juu ya maamuzi nyeti yenye taathira za moja kwa moja kwa uchumi wa Tanzania.
Tazama mfano wa "mgawo wa umeme" na madhara yake kiuchumi! Haya ni matokeo ya mtu mmoja na au kundi la watu wachache wenye nguvu ya kiuchumi (wafanyabiashara) waliyoimeza CCM na kukifanya chama hicho kiwe kama kampuni badala ya kuwa taasisi ya watu (wakulima na wafanyakazi) kama ilivyokuwa wakati kilipoasisiwa tarehe 5 Februari, 1977.
Kwa kuzisanifu nukta zilizoonyeshwa, kujadiliwa na kuwekwa bayana kwa jinsi CCM inavyoshiriki kwa njia moja na au nyingine ni wazi chama hicho kimevunja malengo mahsusi ya Katiba ya JMT ya 1977 (2005) na kwa vyovyote vile hakuna jinsi ya kurekebisha hali hiyo iliyovuruga mwenendo wa uchumi, jamii na siasa.
Wananchi wengi wasiojua nini kinaendelea ndani ya mzingo wa ndani (Kamati Kuu ya CCM) na wapambe wa karibu wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wamebaki vinywa wazi huku wakisubiri hatima ya uongozi wa CCM.
Kama chama kilichopoteza kada ya uongozi wa kisiasa wa kijasiri kama ilivyokuwa enzi za "jeuri ya chama" ambapo wanyonyaji na wahujumu uchumi walikuwa wakiogopa kunyonya au kuhujumu kwa kuwa uongozi wa chama ulikuwa madhubuti (ngangari) na wenye kuzingatia uhuru, haki, usawa na uadilifu kwa minajili ya kuwatumikia wananchi wa Tanzania; CCM imesheheni "mitandao" ya watu wenye choyo, uchu na uroho wa kutawala kwa utumizi mkubwa ya ujambazi wa kiserikali na utumizi endelevu ya ufisadi wa kimfumo na wa ndani ya mfumo.
CCM imekuwa chama kilichopoteza itikadi ya kuwatetea wanyonge badala yake kimekuwa chama cha kuwalinda wanyonyaji na wanyag'anyi wa utajiri wa taifa.
Mwisho, tumalizie na uvunjaji wa Ibara ya 105(1) juu ya "Muafaka wa CCM na CUF Zanzibar". Kwanza ieleweke hapa kwamba muafaka uliosababisha serikali ya umoja wa kitaifa (SUK) ya Zanzibar ni jambo la kupongezwa na kupigiwa mfano.
Hata hivyo, kufanyika kwa muafaka huo kumesababisha kuvunjwa kwa Ibara ya 105(1) (b) inayotambua kuwapo kwa Waziri Kiongozi wa SMZ.
Utashi wa kisiasa uliosababisha kufanyika kwa mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 ungetumika kufanya mabadiliko ya msingi kwenye Katiba ya JMT ya 1977 (2005) ungekuwa muafaka juu ya kujenga umoja na undugu katika kudumisha muungano.
Kwa jinsi hii, na kwa kuwa CCM imeyaacha malengo mahsusi yaliyoanishwa kwenye Katiba ya JMT ya 1977 (2005) sidhani kama bado CCM ina uhalali wa kuwa chama kinachoweza kuongoza mapambano dhidi ya kuondoa umasikini, maradhi na ujinga. CCM inaonyesha wazi kukosa dhamira ya kuendeleza mapambano ya moja kwa moja katika kuondoa aina zote za ufisadi hususan ufisadi wa kimfumo wa ndani ya mfumo na ujambazi wa kiserikali. Vilevile, hakuna dalili njema na za waziwazi kwamba CCM ina dhamira nzuri juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Hivyo basi, na kwa kuwa CCM ni chama kinachotumia sana mikutano katika kujadili na kutengeneza programu za utekelezaji ni wakati muafaka kwa chama hicho kuanza maandalizi ya kurekebisha makosa makubwa ya kimfumo na ya kiutendaji ili kulinasua taifa kwenye mkwamo wa kiuchumi, kijamii na kisiasa. Au kinyume chake Msajili wa vyama vya siasa Mheshimiwa John Tendwa, kama anaweza, achukue hatua za kisheria dhidi ya chama hicho kilichovunja Katiba ya JMT ya 1977 (2005).
Na kwa wananchi kwa ujumla, ni wajibu wetu wa kikatiba kutumia nafasi yetu katika kuhakikisha kwamba CCM, kwa kuwa ndicho chama kinachoongoza serikali, kinawajibishwa katika yale yanayokwenda kinyume na Katiba ya JMT ya 1977 (2005).
Hatujachelewa, elimu kwa umma ni muhimu. Kwa hiyo, vyama vya siasa vya kidemokrasi huu ni wakati muafaka kutumia fursa iliyopo katika kujenga jukwaa la kuishitaki CCM kwa wananchi.



h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii ni Mhadhiri Msaidizi
Kitivo cha Biashara, Chuo Kikuu Mzumbe, anapatikana kwa simu namba 0713593347 au
Barua pepe: maligwa1968@yahoo.com, bakari.mohamed@mzumbe.ac.tz

juu
blank.gif
 
Ijue Katiba ya Tanzania 1977
ban.sheria.jpg


Allan Kajembe​

amka2.gif
WIKI iliyopita tulisema Katiba ni msingi mkuu wa uendeshaji wa nchi au kikundi cha watu, baada ya wao wenyewe kuamua kuhusu mambo yao ya msingi yaendeshweje. Sasa endelea.
Wajibu uliowekwa na katiba hii ni ule wa mwananchi kuitii na kufuata Katiba na sheria za nchi.
Hii ni pamoja na wajibu wa kulinda maliasili ya nchi, kuhifadhi na kudumisha uhuru.
Ikumbukwe kwamba haya ni majukumu/wajibu wa kila raia wa nchi hii.
Hata hivyo, Katiba yetu imeweka mipaka katika haki za binadamu, kama ambavyo katiba hiyohiyo imezitambua.
Kwa mujibu wa ibara ya 30, haki hizi za msingi za binadamu zitamnufaisha mwananchi huyo kama tu hazitasababisha kuingiliwa kwa haki na uhuru wa watu wengine.
Kwa maneno mepesi, haki za raia mmoja zitalindwa na katiba iwapo tu haki hizo haziingilii haki na uhuru wa mtu/watu wengine kama unavyotambuliwa na katiba pamoja na sheria zingine za nchi.
Pia kwa muktadha huohuo, haki za wananchi hazitakiwi kuingilia maslahi ya umma, ingawa neno "Maslahi ya umma" halijatafsiriwa mahali popote kuonesha maana yake haswa.
Na mara nyingi, neno hili, limetumika vibaya(hasa na vyombo vya dola) katika kuminya na kukandamiza haki na uhuru wa watu wengine/wananchi.
Kwa mtazamo wa wanasheria wengi, huu ni mojawapo wa mwanya mkubwa kati ya mingi iliyokuwepo katika katiba inayotoa haki kwa upande mmoja na kuichukua haki hiyohiyo kwa upande mwingine.
Suala lingine la msingi katika Katiba hii ni ile inayopatikana katika sura ya tano ya katiba hii.
Hii ni sehemu inayozungumzia mahakama kama mhimili wa dola, pamoja na uhuru wake. Katika sura hii hususan kuanzia ibara ya 107A hadi ibara ya 128, suala la utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano ambalo kimsingi limewekwa mikononi mwa mahakama, linazungumzia kwa ujumla masuala yote yanayohusu Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano, Mahakama Kuu ya Zanzibar, haki katika Jamhuri ya Muungano, Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano, miongoni mwa mengi.
Katika sura hii, pia tunapata kuona Mahakama maalumu ya Katiba. Katika ibara ya 107A(1) inayozungumza kwamba mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano imewekwa katika Idara ya Mahakama na kwamba hakuna chombo chochote cha serikali wala Bunge au Baraza la Wawakilishi, kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji wa haki.
Katika hili, mahakama ndiyo iliyopewa mamlaka yote juu ya mambo yote yanayohusiana na utoaji haki hapa nchini.
Na msingi utakaoiongoza mahakama katika kufanya hivyo ni kwa kuzingati kanuni ya kisheria kwamba mahakama ni lazima ziwe huru na hivyo kutoa haki pasipo na woga wala upendeleo.
Kwa upande wa mahakama maalumu ya katiba ambayo ni mahakama inayoonekana kuwachanganya watu wengi, ni mahakama ambayo kimsingi imeanzishwa na Katiba hii katika Ibara ya 1226(1).
Katika ibara hii, mahakama hii imeanzishwa kwa minajili ya kusikiliza shauri lolote lililoletwa mbele ikiwa shauri hilo litakuwa linahusu tafsiri ya katiba hii iwapo tafsiri hiyo au utekelezaji wake umesababisha mabishano baina ya serikali za Jamhuri ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar.
Mahakama hii itatakiwa kutoa uamuzi wa usuluhishi juu ya shauri hilo. Kwa hiyo, mahakama ina jukumu hilo tu kwa mujibu wa katiba hii, na si kujadili suala lolote la kikatiba kama ambavyo wengi wamekuwa wakidhani.
Kwa msingi huo basi ‘wateja' wa mahakama hii ni serikali hizo mbili tu, na si vinginevyo.
Hata hivyo, kitu cha kushangaza zaidi katika mahakama hii ni kile kinachoelezwa na ibara ya 127(1), kwamba mahakama hii itaundwa na wajumbe ambao nusu yake watateuliwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano na nusu iliyobaki itateuliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Katika hili, utashangaa kwamba kama kila upande katika shauri mbele ya mahakama hii utakuwa na nusu ya wajumbe, sasa uamuzi utafikiwa vipi? Hii ni mojawapo ya changamoto kubwa inayoikabili Katiba yetu.
Katiba hii pia imegusia kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao umezaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Suala jingine muhimu katika Katiba hii ni la Bunge la Jamhuri ya Muungano, ambalo limeelezwa katika sura ya tatu.
Sura hii inazungumzia aina ya wabunge watakounda Bunge ambao ni pamoja na wabunge wa kuchaguliwa majimboni, viti maalumu na wale wa kuteuliwa na rais ambaye amepewa mamlaka hiyo kupitia mabadiliko ya 13 ya Katiba hii.
 
Mchakato wa katiba mpya waiva


Na Tumaini Makene

MCHAKATO wa safari ya upatikanaji wa katiba mpya ya nchi sasa unaonekana kuiva ambapo mswada wa sheria itakayoweka utaratibu mzima, uko katika hatua ya
kuchapwa kabla ya kuwasilishwa bungeni kwa ajili ya kuridhiwa na kupitishwa.

"Mheshimiwa Mwenyekiti nitaanza na suala la katiba...kama unavyojua katiba ni mchakato mrefu. Suala hili lilianza mara baada ya wananchi walipoanza kulizungumzia. Pia rais katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka mwaka jana alilizungumzia.

"Kilichokuwa kikitakiwa ni kuandaa sheria ya mabadiliko ya katiba, waraka tayari ulishaandaliwa, ukapelekwa kwenye technical committee ya makatibu wakuu wa wizara, kisha ukapelekwa kujadiliwa katika baraza la mawaziri. Sasa uko kwa printer (mchapishaji) kwa ajili ya kuchapwa tayari kwa mchakato wa bungeni ambao unaujua jinsi ulivyo."

Hayo yalisemwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Bw. Oliver Mhaiki alipokuwa akijibu baadhi ya hoja zilizoibuliwa na baadhi ya wabunge wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala, ambao jana, chini ya Mwenyekiti wake, Bi. Pindi Chana walikutana na watendaji wa wizara hiyo.

Mapema wakati wakichangia na kuuliza maswali kutokana na taarifa ya Waziri wa Sheria na katiba, Bi. Celina Kombani, baadhi ya wabunge walitaka kujua pamoja na masuala mengine, maendeleo ya mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya, kama ambavyo tayari serikali imeshaweka wazi, kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete.

Mmoja wa wabunge hao waliotaka kujua mwenendo wa mchakato wa uandaaji wa mswada kwa ajili ya sheria ya mabadiliko ya katiba, umefikia hatua gani, alikuwa ni Bi. Angellah Kairuki (Viti Maalum, CCM) ambaye pia alihoji masuala kadhaa ya utendaji wa wizara hiyo, ikiwemo kuzorota katika upandishaji vyeo wafanyakazi na ulipaji wa posho.

Mbunge wa Mbulu (CHADEMA), Bw. Mustapha Akunaay, alihoji umuhimu wa nchi kuwa na wataalamu au wanasheria wanaohusika wa mikataba lakini bado taifa limetumbukizwa katika mikataba mibovu, inayoligharimu hasara, tangu mwaka 1994.

"Nchi hii imekuwa imekumbwa na tatizo la mikataba mibovu tangu mwaka 1994, kila mkataba unaotiwa saini ni mbovu, basi kama ndivyo hivyo hakuna haja ya kuwa na idara hiyo, ni bora tukaifunga, kisha tuka-outsource (tukatoa nje ya nchi)...kitakuwa si kitu kigeni, nafikiri huko nyuma tuliwahi kufanya hivyo," alisema Bw. Akunaay.

Mbunge huyo pia alizungumzia matatizo ya wanafunzi wa Shule ya Sheria, ambapo alisema kuwa hawathaminiwi ipasavyo na kuwa hawasomi kwa vitendo, hivyo hakuna tofauti na masomo ya nadharia waliyofundishwa wakingali chuoni wakichukua shahada zao za sheria.

Mchangiaji mwingine, mmoja wa mawakili maarufu nchini, Bw. Nimrod Mkono (Mbunge wa Msoma Vijijini, CCM) naye alionekana kuunga mkono hoja ya 'kubinafsisha' baadhi ya maeneo katika mfumo wa mahakama nchini, ili kuwa na tija katika utendaji wake.

Akichangia kwa hoja yenye mifano, akidhihirisha uzoefu wake katika fani ya sheria, Bw. Mkono alionekana kusikitishwa na namna mhimili wa mahakama unavyotendewa na mihimili mingine ya serikali yaani bunge na dola, hususan katika suala la udogo wa bajeti.

Aliongeza kuwa kusema kuwa anajiandaa kuondoa 'shilingi moja' wakati wizara hiyo itakapokuwa ikiwasilisha bajeti ijayo, mpaka apate majibu ya kukithiri kwa rushwa na kucheleweshwa kwa hukumu katika mhimili huo, akisema kuwa kuchelewa kwake kumekuwa kukitengeneza mianya ya uovu huo.

Alisema mahakama imekuwa haitendewi haki na kujengewa mazingira mazuri ya kufanya kazi kama ilivyo kwa mihimili hiyo mingine, akisema kuwa serikali imekuwa haitaki kusikia juu ya suala la kujali mahakama.

"Mwenyekiti...mambo mengi hapa yanajirudia rudia tu, tangu nilipoanza kuwa mjumbe wa kamati hii, miaka kumi na moja sasa...tuwe fair kwa mahakama, hatuwatendei haki, wapewe mazingira mazuri kama ilivyo mihimili mingine, things are not okay (mambo hayako sawa), ndiyo maana kuna rushwa huku. Serikali haitaki kusikia hili.

Mapema akiwasilisha taarifa yake kwa kamati hiyo ya kudumu ya bunge, Bi. Kombani alisema kuwa moja ya changamoto inayoikabili wizara hiyo ni ufinyu wa bajeti, ambayo unasababisha haki kuchekeweshwa na hivyo kuonekana haijatendeka.

Alisema kuwa mpaka sasa mahakimu wa mahakama mbalimbali nchini hawatoshelezi mahitaji, ambapo wale wa mahakama za mwanzo wamekuwa wakilazimika kusafiri kutoka kata moja au tarafa, kwenda nyingine kusikiliza kesi na kutoa hukumu, kutokana na uhaba, akitaja takwimu kuwa kuna mahakama za mwanzo 1,105, mahakimu wakiwa ni 759.
 
SERIKALI YATAMKA: Katiba mpya 2014
• SERIKALI imesema mchakato wa mabadiliko ya Katiba utaanza hivi karibuni na itahakikisha kuwa Katiba mpya inapatikana mwaka 2014.

na Bakari Kimwanga


amka2.gif
SERIKALI imesema mchakato wa mabadiliko ya Katiba utaanza hivi karibuni na itahakikisha kuwa Katiba mpya inapatikana mwaka 2014.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Oliver Mhaiki, alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala inayoongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana, iliyotaka kufahamu jinsi serikali ilivyojipanga kwa mchakato huo.
Alisema maandalizi ya kuanza kwa mchakato huo yamekamilika na tayari muswada wake umeshapita katika vikao husika na kwamba kinachosubiriwa kwa sasa ni kufikishwa bungeni.
"Mchakato wa katiba itakayotokana na ridhaa ya wananchi utakamilika baada ya miaka miwili kutoka sasa. Wizara ilishaandaa waraka kuhusu suala hilo na ulishafikishwa katika kikao cha kamati ya ufundi ya serikali inayoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, kwa hatua zaidi.
"Kamati ya Luhanjo ilishaujadili waraka na iliupeleka katika kikao cha baraza la mawaziri ambalo lilishaketi na kuupitisha waraka huo…hatua inayofuatia sasa ni waraka huo kupitiwa kama muswada kwa ajili ya kuwasilishwa kati ya mwezi Juni au lile Bunge la Novemba," alisema Mhaiki.
Ufafanuzi huo ulitokana na maswali yaliyoulizwa na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Angellah Kairuki na Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi), ambao kimsingi walitaka kujua Katiba mpya itapatikana lini na kutaka kujua nini kinaendelea tangu Rais Jakaya Kikwete atoe tamko lake kuhusu suala hilo.
Baada ya ufafanuzi huo, kamati hiyo iliipongeza serikali kwa maandalizi iliyoyafanya mpaka sasa na kuitaka iendelee kufanya maandalizi ya uhakika zaidi bila kubahatisha, kwani wanatekeleza agizo la rais.
Kwa upande wake Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, alisema wizara yake imejipanga vizuri ingawa imekuwa ikikabiliwa na changamoto hasa katika Idara ya Mahakama, kwa kuwa na upungufu wa mahakimu katika mahakama za mwanzo na wilaya nchini.
Kombani, alisema hivi sasa serikali imefanikiwa kuajiri mahakimu wa mahakama za mwanzo ambao ni 750 huku kukiwa na upungufu wa mahakimu 350, hali inayofanya mashauri ya kesi kuchelewa kusikilizwa kwa wakati.
"Naiomba kamati hii itambue wilaya zote 12 zilizoanzishwa katika Serikali ya Awamu ya Tatu hazina majengo ya mahakama ya wilaya, hali inayopelekea wananchi kutembea umbali mrefu kuzifuata mahakama zilipo na zaidi ya wilaya 30 hazina mahakimu," alisema Waziri Kombani.
Alisema hali hiyo inasababishwa na ufinyu wa bajeti ya wizara hiyo pamoja na idara zake, ambapo kwa mwaka huu wa fedha unaoisha Juni mwaka huu walitengewa sh bilioni 499.4, ikiwa sambamba na idara zote.
Hata hivyo, Kombani alitoa wito kwa kamati hiyo kuhakikisha wanaunga mkono ombi lao la kutaka kuongezewa fedha katika bajeti ya mwaka huu ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na kuboresha huduma kwa wananchi.
Hoja na shinikizo la kutaka kuandikwa kwa Katiba mpya viliibuliwa kwa kasi mwishoni mwa mwaka jana na tamko la viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mara baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010.
 
Waraka wa kuandaa sheria ya marekebisho ya katiba uko tayari Send to a friend Wednesday, 23 March 2011 21:11

Fidelis Butahe
WIZARA ya Katiba na Sheria, imesema Waraka wa kuandaa sheria ya Marekebisho ya Katiba umekamilika na kwamba, upo hatua za mwisho za uchapaji tayari kupelekwa Bungeni kujadiliwa.

Kauli hiyo ya wizara imekuja ikiwa zimepita siku 83 tangu Rais Jakaya Kikwete kutangazia umma kuanza kwa mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Rais Kikwete alisema ameamua kuunda Tume maalum ya Katiba, ambayo itakayoongozwa na mwanasheria aliyebobea, itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali katika jamii kutoka pande mbili za Muungano.

Alisema jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato utakaowashirikisha wananchi wote, vikiwamo vyama vya siasa, wanasiasa, wafanyabiashara, asasi za kiraia, mashirika ya dini, wanataaluma na makundi mbalimbali ya watu wote.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Oliver Muhaiki, baada ya kutakiwa kujibu swali hilo na Waziri wa wizara hiyo, Celina Kombani, wakati wajumbe wa Kamati ya ya Katiba, Sheria na Utawala kutaka kujua hatua ulipofikia mchakato huo.

Wabunge hao walitaka kufahamu mchakato wa kubadili katiba na sababu zinazochangia mlundikano wa kesi mahakamani.
"Hivi sasa waraka huo uko hatua za uchapaji tu kwa ajili ya kupelekwa bungeni, ila umeshapita kamati ya ufundi makatibu wakuu wa wizara na Baraza la Mawaziri," alisema Muhaiki.

Kuhusu mlundikano wa kesi mahakamani, Waziri Kombani alisema wingi wa mahabusu kwenye magereza mbalimbali nchini, unachangiwa na bajeti ndogo inayotengewa wizara.

"Wizara hii ina ufinyu wa bajeti, ni jambo lililo wazi kwamba haki ikitendeka na mipango mingine itakwenda vizuri, kuna kesi zinashindwa kufikia tamati kutokana na uhaba wa fedha," alisema Kombani.
 
Ukweli ni kuwa katiba mpya haihitaji muda wote.......huo wa hadi 2014...................................

Athari zake ni kuwa.............................

1) Zipo sheria nyingi ambazo itabidi zitungwe na muda hautoshi wa mwaka mmoja 2015 hadi uchaguzi wa 2015

2) Miaka 3 kuandika katiba mpya ni kupoteza muda ili twende uchaguzi ujao na katiba hii mbovu kwa visingizio vya ya kuwa zipo sheria ambazo zinatakiwa kufnayiwa marekebisho na muda hautoshi.......................hiyo ni janja ya nyani....................
 
Serikali: Muda wa Katiba mpya utaamuliwa na Bunge


na Mwandishi wetu


amka2.gif
WIZARA ya Katiba na sheria imetoa ufafanuzi juu ya kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko ya Katiba utakaopelekea kupatikana kwa Katiba nyingine na kusema haina uhakika ni lini mchakato huo utakamilika kwani wenye mamlaka ya kuamua hilo ni Bunge la Jamhuri.
Ufafanuzi huo mpya unatokana na habari iliyochapishwa na gazeti hili jana ikimnukuu katibu mkuu wa wizara hiyo, Oliver Mhaiki, alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala iliyokutana na watendaji wa wizara hiyo wakiongozwa na waziri wake, Celina Kombani.
"Kimsingi alichozungumzia katibu mkuu ni mchakato wa ndani wa serikali uliojumuisha kuandaa waraka uliojadiliwa na makatibu wakuu na Baraza la Mawaziri kabla ya kupelekwa kwa muswada bungeni, suala la muda na mengineyo yataamuliwa na Bunge," alisema Omega Ngole, msemaji wa Wizara hiyo alipotembelea ofisi za gazeti hili jana.
"Suala la kuupitisha muswada kuwa sheria lina taratibu zake zikiwemo kujadiliwa na Bunge ambacho ni chombo huru," aliongeza Ngole ambaye alikuwepo katika kikao hicho na kamati ya Bunge.
Ngole alisema kuwa katibu mkuu huyo aliwaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa kilichotakiwa kufanywa na serikali ni kuandaa muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba.
Aliongeza kuwa waraka wa Baraza la Mawaziri kwa ajili ya muswada wa sheria hiyo umeandaliwa na kupitiwa na Kamati ya Ufundi inayojumuisha makatibu wakuu na tayari umeshajadiliwa na Baraza la Mawaziri.
"Ninavyofahamu, kwa sasa taratibu za kuupiga chapa muswada huo zinaendelea kwa ajili ya kuuwasilishwa bungeni," aliongeza.
Majibu ya Mhaiki yalifuatia maswali ya Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Angela Kairuki, na Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali, waliotaka kujua hatua iliyofikiwa katika kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete la kuanzisha mchakato wa kutazama upya Katiba ya nchi.
Katika salamu zake za mwaka mpya wa 2011 kwa Watanzania alizozitoa 31 Desemba, mwaka jana, Rais Kikwete alisema serikali itaanzisha mchakato wa kutazama upya Katiba kwa lengo la kuihuisha ili iendane na taifa lenye nusu karne.
 
Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya Send to a friend Tuesday, 29 March 2011 21:20

katiba.jpg
Mwandishi Wetu
MUSWADA maalumu wa kuunda Tume ya kukusanya maoni na kupendekeza muundo wa Katiba mpya ya Tanzania, unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la Aprili, mwaka huu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa muundo wa tume hiyo hautawashirikisha wabunge, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Madiwani wala kiongozi yeyote wa kisiasa.

Tume hiyo inayotarajiwa kuwa na wajumbe 30, itaundwa na Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na wajumbe wake watakuwa ni wanataaluma, hususan wanasheria na kwamba suala la jinsia litazingatiwa.

Taarifa hizo zinaeleza pia kuwa Tume itaundwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na Visiwani na inatarajiwa kuwa na majukumu mbalimbali ikiwamo kuwahamasisha watu kujua maana na muundo wa Katiba.

Majukumu mengine ya tume hiyo yaliyotajwa kwenye muswada huo ni kukusanya maoni kutoka kwa wananchi, kuchunguza na kuainisha muundo wa Katiba kulingana na mifumo ya kisiasa, kidemokrasia, uongozi, sheria za kiutawala na Serikali.

Mara baada ya Bunge kupitisha muswada huo, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuusaini na kuiunda haraka iwezekanavyo tume hiyo ili ifikapo Juni mwaka huu ianze kazi yake.Kamati hiyo itatoa rasimu ya katiba hiyo mpya ikipendekeza pia muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano utakavyokuwa.

Mchakato wa kuunda tume hiyo unakuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wananchi kuwa watulivu akisema suala hilo litaratibiwa kwa umakini ili kuwa na katiba bora ambayo itawasaidia Watanzania kwa muda mrefu.

Tamko la Rais Kikwete la kuunda tume hiyo ndilo lililozima wimbi la madai ya Katiba mpya lililoshika kasi miongoni mwa watu wa kada mbalimbali ikiwamo wanasiasa, wasomi na wananchi wa kawaida.Katika mijadala hiyo, Katiba iliyopo imeelezewa kuwa imepitwa na wakati na haiendani na mahitaji ya mazingira ya sasa ya nchi.

Vuguvugu hilo lilianza mara baada ya Uchaguzi Mkuu, Novemba mwaka jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kudai kuwa Katiba ya sasa haitoi haki ya kidemokrasia kwenye uchaguzi.
 
Comments




+1 #5 Wakudata 2011-03-30 11:49 Tume hiyo itakuwa ni tume ya kuchakachua maoni ya Wadanganyika, huo ndiyo mtizamo wangu. Raisi aliyechakachua matokeo ya uchaguzi na kung'ang'ania madarakani! tusitegemee jipya kwani maoni ya masikini waliyowengi yatatupya kwenya dust bin ikibidi hata kuchomwa moto. Tutakachoshuhud ia ni maoni yakina ROSTAM, LOWASSA, JK MCHAKACHUWAJI, UVCCM-UOZO, Tume feki ya uchaguzi 2010 ndiyo watakao pewa kipaumbele kwa sababu ya pesa yao. Itakuwa ni katiba ya kulinda DOWANS. Watakaoteuliwa na RAISI hawatakwenda kinyume na matakwa ya JK Mchakachuaji. Mungu uinusuru Tanzania na watu wake.
Quote









0 #4 Robert 2011-03-30 11:25 ]
Hivi wakati mabadiliko ya katiba z'bar, wajumbe wangapi wa bara walihusishwa? Je katiba mpya ikikinzana na ile ya z'bar, wazenji watafuata ipi? Mfano sasa katiba ya zbar inatamka kwamba zbar ni nchi kamili, wakati ya muungano inasema zbar ni sehemu tu ya nchi ya Tz.
Quote









0 #3 jalome 2011-03-30 11:07 Suala la katiba bado liko tete kwa nchi mbili zilizoungana na kupatikana Jamuhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
ukiangalia mtazamo wa mchakato wa katiba utaona kuna utata mkubwa na ikiwa upande moja u[NENO BAYA]sa haki mwengine unaweza kusema urafiki wetu basi.
angalia hivi sasa Wtanganyika wao wanataka katiba mpya, Wzanzibar wao wanasema makubaliano halali ya Muungano yamebuzwa kwa hio kujadiliwe Muungano na laumuhimu ni kurudishwa mshirika wa Muungano yani Tanganyika na katiba ya Tanganyika kwa mambo yasio ya Muungano.
Quote









+1 #2 kp 2011-03-30 10:15 Quoting Ujenzi bora:
Hili la kuwa na wajumbe wa tume sawa sawa kutoka Tanzania bara na Zanzibar sio sahihi. Mimi nafikiri kama issue ni uwakilishi wa kila sehemu ya muungano basi proportion ya wabunge ndiyo itumike kupata hao wajumbe. Tanzania bara kuna zaidi ya watu milioni 40 wakati Zanzibar hawafiki milioni 5.

Na hiyo katiba lazima ije ipigiwe kura na watanzania wote kama refurandamu kabla ya kupitishwa kuwa katiba kamili. Wakati huo wapiga kura wengi watakuwa wakazi wa bara, sasa sijui huo uwakilishi wa idadi sawa ya wajumbe itasaidia nini wakati huo.​
Maoni yako si sahihi. Zanzibar ni nchi na kama hakuna makubaliano wanaweza kujitenga. Hata kura ya maoni nategemea kuwa kila nchi itapiga kivyake yaani Watanganyika peke yao na Wazanzibari peke yao. Utaratibu huu nadhani utaleta muafaka.
Quote









0 #1 Ujenzi bora 2011-03-30 10:03 Hili la kuwa na wajumbe wa tume sawa sawa kutoka Tanzania bara na Zanzibar sio sahihi. Mimi nafikiri kama issue ni uwakilishi wa kila sehemu ya muungano basi proportion ya wabunge ndiyo itumike kupata hao wajumbe. Tanzania bara kuna zaidi ya watu milioni 40 wakati Zanzibar hawafiki milioni 5.

Na hiyo katiba lazima ije ipigiwe kura na watanzania wote kama refurandamu kabla ya kupitishwa kuwa katiba kamili. Wakati huo wapiga kura wengi watakuwa wakazi wa bara, sasa sijui huo uwakilishi wa idadi sawa ya wajumbe itasaidia nini wakati huo.
Quote
 
Wanasiasa ni kina nani?
nani atabaki?
manake Tanzania wote ni wanasiasa, wabunge wote, wanachama wote, wakereketwa wote,
wanaharakati wote,
je wataondoa watu wote wenye kadi za vyama?
au watu wenye cheo chochote kwenye chama,
au wafadhili wa vyama
au viongozi wakuu wa nchi kwenye chama.
Mie sijaelewa wanasiasa Tanzania ni kina nani, au wasio wanasiasa ni kina nani?
 
Udasa kuchambua muswada Katiba Mpya Jumamosi Send to a friend Wednesday, 30 March 2011 21:18

Fredy Azzah
JUMUIYA ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa), imeandaa kongamano la pili la Katiba ambalo pamoja na mambo mengine, litajadili muswada maalumu wa sheria unaopendekeza mabadiliko ya katiba ya Tanzania. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Udasa na Mratibu wa Kongamano hilo, Dk Kitila Mkumbo, alisema muswada huo una upungufu mwingi ambao lazima uangaliwe kwa umakini.

“Kwanza ni kwanini suala la tume apewe Rais, kwanini shughuli hii isifanywe na Bunge? Katika nchi za wenzetu kama Kenya, Ghana na Afrika kusini Bunge ndio limefanya hiyo shughuli,” alisema Dk Kitila na kuongeza: “Muswada unapendekeza tume iwe na watu 30, Kenya walikuwa na watu tisa tu, wakati mwingine mambo mazuri lazima tuyachukue kutoka kwa wenzetu, halafu haina ukomo wa kukusanya maoni na haiainishi moja kwa moja sifa za watu wanaotakiwa kuteuliwa kwenye tume.”

Kutokana na hali hiyo, alisema upungufu huo na mwingine, utachambuliwa siku hiyo kuwapa wananchi uelewa kilichopo kwenye muswada huo. Kwenye kongamano hilo, wananchi na watoa mada watajikita zaidi kueleza maudhui ambayo yanatakiwa kubebwa kwenye katiba na kuainisha mambo yanatakiwa kuchukuliwa kutoka katiba ya sasa.

Naye Mwenyekiti wa Udasa, Dk Mshumbuzi Kibogoya, alisema watoa mada wakuu kwenye kongamano hilo litakalofanyika Jumamosi hii, ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samata na Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Francis Kiwanga.

Pia, vyama vya siasa vyenye wawakilishi Bungeni vimelikwa na vimethibitisha ushiriki wake, CCM kitawakilishwa na Makamu mwenyekiti wake, Pius Msekwa na Chadema kitawakilishwa na Mwanasheria wake, Mabele Marando. “Kila chama kitapewa dakika kumi kutoa maoni yake na wananchi wengine watakaoshiriki wataruhusiwa kutoa maoni yao,” alisema Dk Kibogoya.
 
CHADEMA yagundua madudu Katiba Mpya
• Serikali yawapindua wananchi katika mchakato

na Edward Kinabo na Lucy Ngowi


amka2.gif
KAMA vile imeshindwa kusoma alama za nyakati, serikali imeamua kuchakachua mchakato wa marekebisho ya katiba mpya kwa kuandaa muswada ambao unapinga yote yanayopendekezwa na wananchi.
Badala yake, serikali inarejesha yote yanayokataliwa na wadau, hali ambayo inaweza kuhatarisha amani ya nchi na hatimaye kusababisha mchakato mzima kurudiwa huko mbele.
Mabadiliko ya katiba ni madai ya msingi na matakwa ya lazima kama nchi hii inataka kujenga na kudumisha amani ya kweli na kuleta maendeleo kwa watu wake.
Katika mazingira ambamo wananchi wamekuwa wanalalamikia mamlaka yaliyopitiliza ya rais, kama kikwazo cha maendeleo na badiliko la msingi katika katiba, muswada wa sasa unaoletwa na serikali, unalenga kuendelea kusimika mamlaka hayo.
Uchambuzi uliofanywa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), ambaye awali ndiye alidhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu mchakato wa katiba mpya, unaonyesha kuwa muswada huo uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11, Machi 2011, unataka kumpa rais mamlaka ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi.
Wakati wanaharakati na wananchi kwa ujumla wamekuwa wanasisitiza wananchi wawe na mamlaka ya mwisho katika kuamua hatima ya katiba yao, muswada huu wa serikali unarejesha mamlaka hayo kwa rais.
Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011 unatarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni, na CCM kwa kutumia wingi wa wabunge wao, wanaoiunga mkono serikali hata kwa masuala wasiyokubaliana nayo, wanatarajiwa kuunga mkono muswada huo, kuhujumu mabadiliko makubwa ambayo taifa lingefanya baada ya miaka 50 ya uhuru.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, ambayo gazeti hili lina nakala yake, mbunge huyo wa Ubungo anasema:
"Maudhui ya muswada huu yamedhihirisha tahadhari niliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya.
"Muswada huo umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali; sasa yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na Bunge kupitia muswada huo.
"Muswada huo unataka kumpa mamlaka rais ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi. Muswada huo pia utaka kumpa rais mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yeyote isipokuwa Rais wa Zanzibar.
"Muswada huo unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe, rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake, hivyo kuacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa rais.
"Muswada huo unataka kumpa rais mamlaka ya kutengeneza hadidu rejea za tume, jambo ambalo lilipaswa kufanywa na Bunge kwa kuwa sehemu ya sheria husika ama kufanywa na mkutano mkuu wa kikatiba. Kwa kutoa mamlaka ya kuunda hadidu rejea kwa rais, mwanya umetolewa kwa mtu mmoja kuweka mipaka ya nini kinastahili kufanywa na tume wakati wa mchakato wa katiba mpya, hivyo kuminya wigo wa mabadiliko.
"Muswada huo unataka tume iwasilishe ripoti yake kwa rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka yale atakayoamua rais bungeni. Muswada huu kwa kuwa na kifungu hiki utaendeleza yaliyofanywa na marais waliopita kuhusu ripoti na mapendekezo ya tume nyingine, hivyo kukwamisha mabadiliko ya kweli.
"Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa tume itakayoundwa kuitisha jukwaa (fora) ambalo litaundwa kwa ajili ya kupata maoni pekee (ad hoc) badala ya kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa Katiba (National Conference/congress) kama wadau walivyohitaji.
"Aidha, uwakilishi katika jukwaa hilo umetajwa tu kuwa ni wa kijiografia na kimakundi bila kuweka bayana mnyumbuliko wa uwakilishi. Muswada huo unataka kutoa mamlaka finyu kwa jukwaa hilo kuwa ni kutoa ushauri kuhusiana na muswada; tofauti na mkutano mkuu wa kikatiba ambao ungekuwa na mamlaka zaidi katika mchakato husika.
"Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa rais kuitisha Bunge la katiba (constituent assembly) ikiwemo kuteua wajumbe wa Bunge husika. Muswada huo unataka kutoa mamlaka makubwa kwa rais kuteua wawakilishi wa chombo kikuu zaidi katika mchakato wa katiba bila kushauriana na kundi lolote ama wananchi kuhusika katika uteuzi ama kuwa na wawakilishi walioteuliwa na makundi yenyewe, mathalani vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama vya wakulima, vyama vya wanafunzi, vyama wa wafanyakazi nk.
"Muswada huo unataka rais ashauriane na Rais wa Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pekee. Muswada huo unatoa mamlaka makubwa zaidi ya rais kuamua hata kufanya Bunge la kawaida kuwa ndilo Bunge la Katiba, jambo ambalo linaweza kurejesha udhaifu uliofanywa katika mchakato wa katiba inayotumika sasa ambapo umma uliporwa wajibu na mamlaka yake ya kushiriki moja kwa moja katika kupitisha katiba.
"Muswada huo kwa ujumla haujaeleza muda wa mchakato wa katiba na vipindi vitakavyotumiwa na vyombo mbalimbali katika hatua mbalimbali za mchakato wa katiba; ama kutoa mamlaka ya kuwekwa kwa muda huo kwa chombo chenye uwakilishi mpana wa umma kama mkutano wa katiba au Bunge, hivyo kutoa mwanya kwa mchakato mzima kucheleweshwa.
"Haya ni baadhi ya maudhui ndani ya muswada husika ambayo yamenishtusha na kunifanya nitoe tamko hili la awali wakati nikiendelea kufanya uchambuzi wa kina ambao nitautolea kauli katika hatua za baadaye."
Mnyika alitoa wito kwa vyama vya siasa, asasi za kiraia, vyombo vya habari, taasisi za dini na Watanzania kwa ujumla kufuatilia na kupata nakala ya muswada huo ama maudhui yake kwa ajili ya kuujadili kwa dharura na kutoa matamko.
Sanjari na hilo, alitoa wito kwa serikali itoe taarifa kwa umma namna ambavyo wananchi wanaweza kupata nakala za muswada huo nyeti na sababu za serikali kupuuza maoni mengi ya wadau yaliyotolewa kabla ya kuandaliwa kwa muswada huo kuhusu mchakato unaofaa kuongoza mabadiliko ya katiba katika taifa letu.
Mara kwa mara mbunge huyo amekuwa akisisitiza kuwa ipo haja kwa mchakato wa katiba mpya kupata uhalali wa umma kwa kurejea ibara 8 ambayo inatamka kwamba, "madaraka na mamlaka ni umma na serikali inafanya kazi kwa niaba na Bunge ndicho chombo kikuu cha kusimamia wajibu huo kwa kutokana na mamlaka ya kikatiba yaliyopo kwenye ibara ya 63(2) na (3) na ibara ya 98 inayohusika na mabadiliko ya katiba."
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika hotuba yake bungeni Februari 8 mwaka huu, pamoja na mambo mengine, alieleza kwamba muswada kuhusu mchakato wa katiba utawasilishwa kwenye mkutano wa tatu wa Bunge mwezi Aprili mwaka huu na kwamba utahusu kuundwa kwa tume.
Makongamano, mikutano na midahalo imekuwa ikifanyika kujadili suala la mabadiliko ya katiba na wanazuoni wamesisitiza mara kadhaa kuwa katiba isiyotokana na matakwa ya wananchi, na isiyopitishwa na wananchi, si ya wananchi.
Iwapo serikali itapuuza wito huu, itakuwa inalielekeza taifa katika machafuko ya kisiasa, na italazimika kufanya mchakato mpya ili kukidhi matakwa haya ya kisheria katika uundwaji wa katiba mpya.
Hatua hii ya serikali kuchakachua mchakato wa katiba imedhihirisha pia kwamba Rais Jakaya Kikwete alidandia hoja asiyoijua mapana na marefu yake alipokiri kwamba nchi inahitaji katiba mpya, baada ya wimbo na joto la kisiasa lililoibuliwa na aliyekuwa mgombea urais kupitia CHADEMA, Dk. Willibrord Slaa.
Dk. Slaa aliahidi kuwa angeanzisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku 100 za utawala wake. Rais Kikwete hakuwahi kuahidi wakati wa kampeni kwamba angerekebisha katiba.
Hata hivyo, baada ya wananchi kudai katiba, huku Mnyika akiahidi kupeleka hoja binafsi bungeni kwa ajili hiyo, ghafla Rais Kikwete alitekeleza ahadi hiyo ndani ya siku 100 za utawala wake – hatua ambayo wachambuzi walisema ililenga kuwanyamazisha wananchi na kuipokonya CHADEMA ajenda.
Hata hivyo, wananchi wanaendelea na mijadala kuhusu katiba mpya; na sasa linaandaliwa kongamano la pili lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), lenye lengo la kuwapa wananchi uelewa wa kutosha ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa katiba mpya.
Mwenyekiti wa UDASA, Dk. Mushumbusi Kibogoya, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, alisema mada kuu katika kongamano hilo ni ‘Maudhui na Misingi ya Katiba Mpya.'
"Safari hii tunataka watu waweze kujua zaidi kuhusu katiba, wawe tayari kutoa mawazo ili tume au kamati itakapowatembelea wawe na kitu cha kusema, watakapoachwa hivi hivi hawatakuwa na cha kuzungumza," alisema Dk. Mushumbusi.
Watoa mada katika kongamano hilo litakalofanyika keshokutwa ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga.
 
This shames JK in totality.....................................where are TZ people in all this mess?????????????????????????

PHP:
Uchambuzi uliofanywa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA),  ambaye  awali ndiye alidhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu   mchakato wa katiba mpya, unaonyesha kuwa muswada huo uliochapwa katika   gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11, Machi 2011, unataka    kumpa rais mamlaka ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa  katiba  bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi.
 
Back
Top Bottom